Tembelea... |
 |
Kalenda |
 |

Marafiki wetu |
 |
Habari Zilizopita |
 |



| |
 |
|
|
 |
 |
|
 |
Na Khadija Mngwai SHIRIKISHO la Soka nchini, TFF, limeitaka klabu ya Yanga kutoa taarifa za kuthibitisha kushiriki ama kutoshiriki katika michuano ya Kombe la Tusker linalotarajiwa kuanza kutimia vumbi Desemba 15 katika Uwanja wa Taifa jijini Dar es salaam... |
|
 |
 |
|
 |
Na George Kayala MSIBA wa aliyekuwa Makamu Mwenyekiti wa Klabu ya Yanga mzee Ngozoma Matunda umewagonganisha wagombea mbalimbali wanaowania nyadhifa tofauti katika Shirikisho la Soka nchini, TFF, huku wengine wakikwepa kuhudhuria katika msiba huo kwa hofu ya kukutana na wapinzani wao... |
|
 |
 |
|
 |
Baada ya kuua watu wengi katika upasuaji wa moyo, hatimaye Dk. Terrence anaamua kuhama Tanzania na kwenda Sudan katika jiji la Khartoum ambako ameajiriwa na hospitali iitwayo Khartoum Heart Institute kama daktari bingwa wa upasuaji wa moyo! Ujio wake katika jiji hili umemfurahisha kila mtu, anaonekana ni mkombozi na anashangiliwa kila mahali alikopita jambo ambalo halikudumu kwa muda mrefu sana kwani miezi michache baadaye, alianza kuua tena na kama ilivyokuwa alipokuwa Mwanza, baada ya upasuaji ulioua mtu, alikimbia uwanja wa ndege na kukabidhi kisanduku kwa rubani wa ndege zilizoleta misaada kwa wakimbizi wa Darfur.
Watu wa Khartoum hawakuweza kulivumilia sana jambo hilo kama ilivyokuwa huko Mwanza ambako pamoja na watu kufa bado Dk. Terrence hakufanywa chochote, vitisho vya kumuua vikaanza kama asingeondolewa katika nchi hiyo. Badala ya kuogopa Dk. Terrence hakushtuka, badala yake aliendelea kuua watu kama kawaida hatimaye siku ikafika, akakutwa akiwa amekatwa vipande vipande na kichwa kuondolewa, kilichofanya atambulike ni koti lake la kazi lililoandikwa jina pamoja na miwani!
Hakuna aliyesikitishwa sana na tukio hilo kwani watu tayari walishamchoka, akazikwa na Halmashauri ya jiji la Khartoum kwani hakuwa na ndugu katika nchi hiyo. Taarifa baada ya hapo zilipelekwa Tanzania ambako watu walishtushwa sana na kifo chake, miongoni mwao akiwa ni Greyson, kijana aliye mahabusu kwa kosa la mauaji ambayo hakuyafanya lakini kila mtu anaamini alishiriki! Alikamatwa nyumbani kwake na kukutwa na bunduki aina ya SMG na kuunganishwa katika kesi utekaji wa gari la benki lililokuwa likisafirisha fedha kwenda wilayani Geita kutoka Mwanza, watu wawili wakauawa.
Yote hayo yalitokea muda mfupi tu baada ya Greyson kuanza kuchunguza kifo cha Sato, mchumba wake waliyetarajia kufunga naye ndoa wiki chache baadaye ambaye alikufa akiwa chumba cha upasuaji, Dk. Terrence akimpasua moyo baada ya kudai ulikuwa na tundu jambo ambalo Sato hakuwahi kulilalamikia kabla! Hicho ndicho kilichotokea kwa msichana aitwaye Michelle.
Mchumba wa msichana huyo aitwaye Denis naye pia alifia chumba cha upasuaji katika tukio la kufanana na hilo, Michelle akaamua kusitisha masomo yake chuo Kikuu cha St. Augustine kilichopo mjini Mwanza ili apate nafasi ya kuchunguza vizuri kifo cha mpenzi wake, hakufanya chochote, kwani siku hiyo hiyo aliyoacha shule aligongwa na katapila akiwa ndani ya bajaj na kupelekwa chumba cha kuhifadhia maiti akiaminika amekufa, lakini baadaye alikohoa na kupelekwa chumba cha upasuaji kupasuliwa kichwa kuondoa damu iliyovujia chini ya fuvu.
Akiwa chumba cha upasuaji, Dk. Gasper aliyekuwa akifanya upasuaji huo, anapokea maelekezo kutoka kwa Dk. Terrence kwamba ahakikishe Michelle anakufa, anabisha kwa muda lakini baadaye anakubali na kuamua kulitekeleza jambo hilo la kinyama! Wiki chache baadaye ndipo Dk. Terrence ndio alihama Tanzania kwenda Sudan akiwa amemwachia Dk. Gasper vitisho vya kutofungua mdomo pamoja na rushwa ya dola elfu hamsini.
Je, nini kitaendelea baada ya kifo cha Dk. Terrence? Je, Greyson atatoka gerezani au atanyongwa? Je, siku moja itathibitika kwamba Michelle aliuawa chumba cha upasuaji? SONGA NAYO... |
|
 |

 |
|
 |
MTOTO KIKOJOZIMtoto mmoja alikuwa na tabia ya kukojoa kitandani kila siku na mama yake akaweka utaratibu kwamba kila akiamka kama mtoto huyo amekojoa anamchapa. Basi siku moja mtoto huyo alikojoa mpaka akaloanisha shuka lote. Mama alipoamka kama kawaida siku hiyo alimchapa sana hadi yule mtoto akawa ameumia matakoni. Usiku yule mtoto ambaye hulala chumba kimoja na wazazi wake, akakosa usingizi kabisa ndipo alipomsikia mama yake akimwambia baba yake akojoe. Mtoto kusikia vile akainuka na kusema, hata sikubali, mimi nikikojoa unanichapa lakini baba unamwambia aachie kojo. Duh! Mama kusikia vile alijisikia aibu na kuanzia siku hiyo mtoto akawa analala ‘sitting room’ |
|
 |
|
|
 |
Kura Yako / Poll |
 |
Habari Katika Picha |
|
 |

Nani Yupo / Alikuwepo |
 |
|