arrowSet HomePage |arrowBookMark Us
right
lines

Global Publishers Tanzania- Uwazi

Tafuta  

Tembelea...

Kalenda

Gazeti la Ijumaa

Marafiki wetu

Habari Zilizopita

Soma Magazeti Yetu...

Gazeti la Risasi Mchanganyiko
Amani
Gazeti la Ijumaa Wikienda

Bongo Celebrities ...

 
Habari Zinazotamba Habari Mchanganyiko
» Ray C: Mabuzi wa nje mwisho ...
» RICHARD: AKINA NANIHII WANA ...
» Nakaaya mzinzi?
» JOHARI: Mwili wake umepotez ...
» TUMEWABAMBA!
» KUtafuta maisha kumenifanya ...
» REDIHENDED!
» The assasination mauaji ...
» Yanga SC laini kama ina ...
» MY GHOSTS (MIZIMU YANGU ...
» waziri mkuu
» warembo wapanda jukwaan ...
» WAGONJWA WA MOYO PRESHA ...
» JIMAMA FUSKA LANASWA

 

DAR KILA SIKU CHRISTMAS

photos  
DAR KILA SIKU CHRISTMAS
Mpiga besi gitaa wa kundi moja la taarabu akiwapagawisha mashabiki wake katika onesho lililofanyika ukumbi wa Mango Garden jijini Dar es Salaam usiku wa kuamkia leo.
PICHA NA RICHARD BUKOS /GPL
    (21 November 2008)
Views: 14 | Maoni (1) |

 

ZIPOMPA: MIMI SIJAOA JAMANI,NIMEOLEWA

ijumaa  
ZIPOMPA: MIMI SIJAOA JAMANI,NIMEOLEWA

Wiki hii katika safu hii makini ya Ten Questions ‘maswali kumi’ tutakuwa na MC maarufu nchini, Gladys Chiduo almaarufu kwa jina la Zipompapoma au Zipo!...
    (21 November 2008)
Views: 305 | Maoni (6) | Soma Zaidi

 

MPAKANJIA: Nimechoshwa na Aisha Bui

ijumaa  
MPAKANJIA: Nimechoshwa na Aisha Bui
Na Waandishi Wetu

Aliyekuwa mume wa Mbunge wa CCM, marehemu Amina Chifupa, Mohamed Mpakanjia, ambaye pia ni mfanyabiashara maarufu jijini Dar es Salaam, ametoboa siri iliyokuwa moyoni mwake kwa miaka kadhaa sasa...
    (21 November 2008)
Views: 802 | Maoni (8) | Soma Zaidi

 

GADNER ATOKA NA MISS TABATA

ijumaa  
GADNER ATOKA NA MISS TABATA
Na Waandishi wetu

ikiwa zimepita siku kadhaa toka iliporipotiwa kuwa, mke wa ndoa wa ‘Mr no Comment’, Gadner G. Habash, Lady Jaydee ameonekana hana pete ya ndoa, kuna habari kuwa, Gadner sasa yupo ndani ya uhusiano wa kimapenzi na aliyekuwa Miss Tabata, 2007, Alfonsina Michael...
    (21 November 2008)
Views: 762 | Maoni (17) | Soma Zaidi

 

GAMBOSHI(15)

hadithi za Shigongo  
Mwandishi maarufu duniani Richard Massawe, ambaye ni Raia wa Tanzania anajishindia Tuzo ya Boldness Award iliyoambatana na kitita cha dola milioni moja hivyo kuamua kurejea nyumbani kumuoa Mwanamitindo Anitha Nicholson! Baada ya harusi watu hawa wanapata ajali na kufa hapo hapo kisha kuzikwa kijijini kwao na Richard huko Kibosho.
Wakati katika ulimwengu unaonekana kwa macho Richard na Anitha wamekufa, kwenye ulimwengu mwingine usioonekana uitwao Gamboshi ambako watu hao wamepelekwa kugeuzwa Misukule ili wafanye kazi watakazopewa huko, Anitha kuimba na Richard kuwa Mwandishi wa gazeti la kichawi liitwalo Gamboshi Leo!

Huko wanapata mateso makubwa, Richard anakatwa ulimi wake lakini Anitha anafanikiwa kutoroka na kukimbia akimwacha mume wake amefungwa kwenye jiwe akipewa mateso sababu ya ukorofi wake. Baadaye Richard anapuliziwa dawa iitwayo Pumbazo na kuwa zezeta na kukubaliana na maisha ya Gamboshi, akifanya kazi zote alizopewa.
Je, nini kitaendelea? Anitha yuko wapi? Nini kitampata Richard baada ya hapo? Watakuja kuungana? SONGA NAYO…
    (21 November 2008)
Views: 268 | Maoni (4) | Soma Zaidi

 

Mwanamke anavyoweza kudumisha/kubomoa penzi lake

Mahaba  
Mwanamke anavyoweza kudumisha/kubomoa penzi lake

Ninayo kila sababu ya kumshukuru Mungu wangu wa Mbinguni kutokana na upendo wake kwangu, kunishindia katika majaribu na kunipa faraja niwapo matatizoni. Hakika sioni wa kufanana na yeye, kwangu ni kila kitu na ataendelea kubaki kiongozi wa maisha yangu milele na milele...
    (21 November 2008)
Views: 99 | Maoni (1) | Soma Zaidi

 

Ngasa, Tegete, Owino kuikiNgasa, Tegete, Owino kuikimbia mbia

champion ijumaa  
Ngasa, Tegete, Owino kuikiNgasa, Tegete, Owino kuikimbia mbia

WACHEZAJI wa Yanga Jerry Tegete, Mrisho Ngassa(Pichani katikati) na George Owino wako mbioni kutimka nchini kwa ajili ya kucheza soka la kulipwa katika nchi tofauti walikotakiwa kwa majaribio...
    (21 November 2008)
Views: 151 | Maoni (0) | Soma Zaidi

 

TFF: Yanga mtacheza Tusker?

champion ijumaa  
Na Khadija Mngwai

SHIRIKISHO la Soka nchini, TFF, limeitaka klabu ya Yanga kutoa taarifa za kuthibitisha kushiriki ama kutoshiriki katika michuano ya Kombe la Tusker linalotarajiwa kuanza kutimia vumbi Desemba 15 katika Uwanja wa Taifa jijini Dar es salaam...
    (21 November 2008)
Views: 34 | Maoni (0) | Soma Zaidi

 

Michael Wambura, Malinzi wakwepa kusalimiana msibani

champion ijumaa  
Na George Kayala

MSIBA wa aliyekuwa Makamu Mwenyekiti wa Klabu ya Yanga mzee Ngozoma Matunda umewagonganisha wagombea mbalimbali wanaowania nyadhifa tofauti katika Shirikisho la Soka nchini, TFF, huku wengine wakikwepa kuhudhuria katika msiba huo kwa hofu ya kukutana na wapinzani wao...
    (21 November 2008)
Views: 58 | Maoni (0) | Soma Zaidi

 

THE LAST HOPE (tumaini la mwisho) 14

hadithi za Shigongo  
Baada ya kuua watu wengi katika upasuaji wa moyo, hatimaye Dk. Terrence anaamua kuhama Tanzania na kwenda Sudan katika jiji la Khartoum ambako ameajiriwa na hospitali iitwayo Khartoum Heart Institute kama daktari bingwa wa upasuaji wa moyo! Ujio wake katika jiji hili umemfurahisha kila mtu, anaonekana ni mkombozi na anashangiliwa kila mahali alikopita jambo ambalo halikudumu kwa muda mrefu sana kwani miezi michache baadaye, alianza kuua tena na kama ilivyokuwa alipokuwa Mwanza, baada ya upasuaji ulioua mtu, alikimbia uwanja wa ndege na kukabidhi kisanduku kwa rubani wa ndege zilizoleta misaada kwa wakimbizi wa Darfur.

Watu wa Khartoum hawakuweza kulivumilia sana jambo hilo kama ilivyokuwa huko Mwanza ambako pamoja na watu kufa bado Dk. Terrence hakufanywa chochote, vitisho vya kumuua vikaanza kama asingeondolewa katika nchi hiyo. Badala ya kuogopa Dk. Terrence hakushtuka, badala yake aliendelea kuua watu kama kawaida hatimaye siku ikafika, akakutwa akiwa amekatwa vipande vipande na kichwa kuondolewa, kilichofanya atambulike ni koti lake la kazi lililoandikwa jina pamoja na miwani!

Hakuna aliyesikitishwa sana na tukio hilo kwani watu tayari walishamchoka, akazikwa na Halmashauri ya jiji la Khartoum kwani hakuwa na ndugu katika nchi hiyo. Taarifa baada ya hapo zilipelekwa Tanzania ambako watu walishtushwa sana na kifo chake, miongoni mwao akiwa ni Greyson, kijana aliye mahabusu kwa kosa la mauaji ambayo hakuyafanya lakini kila mtu anaamini alishiriki! Alikamatwa nyumbani kwake na kukutwa na bunduki aina ya SMG na kuunganishwa katika kesi utekaji wa gari la benki lililokuwa likisafirisha fedha kwenda wilayani Geita kutoka Mwanza, watu wawili wakauawa.

Yote hayo yalitokea muda mfupi tu baada ya Greyson kuanza kuchunguza kifo cha Sato, mchumba wake waliyetarajia kufunga naye ndoa wiki chache baadaye ambaye alikufa akiwa chumba cha upasuaji, Dk. Terrence akimpasua moyo baada ya kudai ulikuwa na tundu jambo ambalo Sato hakuwahi kulilalamikia kabla! Hicho ndicho kilichotokea kwa msichana aitwaye Michelle.

Mchumba wa msichana huyo aitwaye Denis naye pia alifia chumba cha upasuaji katika tukio la kufanana na hilo, Michelle akaamua kusitisha masomo yake chuo Kikuu cha St. Augustine kilichopo mjini Mwanza ili apate nafasi ya kuchunguza vizuri kifo cha mpenzi wake, hakufanya chochote, kwani siku hiyo hiyo aliyoacha shule aligongwa na katapila akiwa ndani ya bajaj na kupelekwa chumba cha kuhifadhia maiti akiaminika amekufa, lakini baadaye alikohoa na kupelekwa chumba cha upasuaji kupasuliwa kichwa kuondoa damu iliyovujia chini ya fuvu.

Akiwa chumba cha upasuaji, Dk. Gasper aliyekuwa akifanya upasuaji huo, anapokea maelekezo kutoka kwa Dk. Terrence kwamba ahakikishe Michelle anakufa, anabisha kwa muda lakini baadaye anakubali na kuamua kulitekeleza jambo hilo la kinyama! Wiki chache baadaye ndipo Dk. Terrence ndio alihama Tanzania kwenda Sudan akiwa amemwachia Dk. Gasper vitisho vya kutofungua mdomo pamoja na rushwa ya dola elfu hamsini.

Je, nini kitaendelea baada ya kifo cha Dk. Terrence? Je, Greyson atatoka gerezani au atanyongwa? Je, siku moja itathibitika kwamba Michelle aliuawa chumba cha upasuaji? SONGA NAYO...
    (20 November 2008)
Views: 182 | Maoni (5) | Soma Zaidi

 

KASEBA ASHINDA MPAMBANO WA MABINGWA

photos  
KASEBA ASHINDA MPAMBANO WA MABINGWA
Bingwa wa Dunia wa Kickboxing mkanda WKL Kg 79, Japhet Kaseba, hivi karibuni alitoka Japan kushiriki shindano la Mabingwa la Dunia na kufanikiwa kuwachakaza vilivyo wapinzani wake, pichani akionesha kombe alilopewa baada ya ushindi na CD iliyorekodiwa mpambano huo.

ACHENI UZUSHI, HAKUNA GOTI NILILOVUNJWA
KASEBA ASHINDA MPAMBANO WA MABINGWA
Wabongo wengine bwana, eti wamemzushia Kaseba amedundwa na kuvunjwa goti katika mpambano wa Mabingwa wa Kickboxing uliofanyika nchini Japan hivi karibuni, pichani mshikaji akiwaonesha waandishi wa habari magoti yake yote mawili baada ya kuzushiwa kuwa goti lake moja amefanyiwa oparesheni baada ya kuumizwa.

PICHA ZOTE NA RICHARD BUKOS
    (20 November 2008)
Views: 57 | Maoni (1) |

 

KATIBU WA TAHLISO KIZIMBANI

photos  
KATIBU WA TAHLISO KIZIMBANI
Katibu Mkuu wa chama cha wanafunzi wa vyuo vikuu nchini, Bwana Julius Mtatiro jana alipandishwa kizimbani kwa tuhuma za kuhamasisha mgomo katika Chuo Kikuu Dar es Salaam cha Mlimani, kupitia chama wanafunzi wa shuleni hapo DARUSO jamaa amewekewa dhamana mpaka Dec. 2 mwaka huu.

KIGOGO WA CCM NYAPINYAPI KWA UFISADI
KATIBU WA TAHLISO KIZIMBANI
Mweka Hazina wa CCM mkoa wa Kigoma, Bw. Shabani Maranda jana ombi lake la dhamana katika kesi ya ufisadi inayomkabili katika Mahakama ya Kisutu liligonga mwamba kurudishwa rumande mpaka kesho.
PICHA ZOTE NA RICHARD BUKOS /GPL.
    (20 November 2008)
Views: 53 | Maoni (2) |

 

Vunja mbavu

Vichekesho na Udaku  
Vunja mbavu
MTOTO KIKOJOZI
Mtoto mmoja alikuwa na tabia ya kukojoa kitandani kila siku na mama yake akaweka utaratibu kwamba kila akiamka kama mtoto huyo amekojoa anamchapa.
Basi siku moja mtoto huyo alikojoa mpaka akaloanisha shuka lote. Mama alipoamka kama kawaida siku hiyo alimchapa sana hadi yule mtoto akawa ameumia matakoni.
Usiku yule mtoto ambaye hulala chumba kimoja na wazazi wake, akakosa usingizi kabisa ndipo alipomsikia mama yake akimwambia baba yake akojoe.
Mtoto kusikia vile akainuka na kusema, hata sikubali, mimi nikikojoa unanichapa lakini baba unamwambia aachie kojo.
Duh! Mama kusikia vile alijisikia aibu na kuanzia siku hiyo mtoto akawa analala ‘sitting room’
    (20 November 2008)
Views: 101 | Maoni (1) | Soma Zaidi

 

Siri imevuja!

Amani  
Siri imevuja!
Na Mwandishi Wetu

Msichana mmoja mrembo aliyetajwa kwa jina moja la Joyce, mkazi wa Mwananyamala jijini Dar es Salaam, hivi karibuni amejikuta katika wakati mgumu baada ya ‘kumegwa’ (kufanya mapenzi) na midume miwili ya kizungu katika hoteli moja maarufu iliyopo maeneo ya Oysterbay bila ridhaa yake...
    (20 November 2008)
Views: 998 | Maoni (7) | Soma Zaidi

 

Soo la Juma Nature kubaka

Amani  
Soo la Juma Nature kubaka
Christopher Lissa na Issa Mnally

Msanii nyota wa kundi la muziki la TMK Wanaume Halisi Juma Kassimu ‘Sir Nature’ jana alifikishwa katika Mahakama ya Wilaya ya Temeke akikabiliwa na tuhuma za kumbaka mwanafunzi (jina lake na la shule vinahifadhiwa).
Nature alisomewa mashitaka akiwa na mwenzake aitwaye Godwin Malima, mbele ya Hakimu mfadhiwi wa mahakama hiyo Bi. Hellen Riwa...
    (19 November 2008)
Views: 950 | Maoni (18) | Soma Zaidi
Back  <<  1 2 3 ... 316 317 318  >>  Next Page
 

Kura Yako / Poll

Habari Katika Picha


Gazeti la Uwazi


Nani Yupo / Alikuwepo


Home Page | About Us | Regista | Picha | Bongo Celebrities | Maoni | Contact Us

hit counter

 

2008 © globalpublisherstz.com