Chuo cha Usimamizi wa fedha cha IFM cha jijini Dar, kimeibuka kidedea katika Shindano la kumsaka mlimbwende wa Vyuo Vikuu nchini, Miss Higher Learning, baada ya Mwanafunzi wa chuo hicho, Betrice Lukindo, kutwaa taji hilo usiku wa kuamkia leo. Wakati Betrice akibatizwa umalkia wa Vyuo Vikuu nchini, Linda Mzinga kutoka Chuo cha Ustawi wa Jamii, Kijitonyama amechukua nafasi ya pili na Doris Donatus kutoka Dar es Salaam Institute of Technology (DIT) akiibuka mshindi wa tatu. Kwa ushindi huo, Magreth amepata tiketi ya moja kwa moja ya kujiunga na Kambi ya Miss Tanzania msimu huu, tayari kwa kuwania taji la Miss Tanzania, 2009/10. Shindano hilo lilifanyika ndani ya viunga vya Karimjee katikati ya jiji la Dar es Salaam, lililosababishwa kwa udhamini mkubwa wa Mtandao wa simu za mkononi wa Vodacom, Global Publishers Ltd, Clouds FM, Ndege Insuarance, kinywaji cha Overmeer na wadhamini wengine kibao.
Miss Vodacom Higher Learning 2009/10, Betrice Lukindo (katikati) akiwa katika picha ya pozi na mshindi wa pili, Linda Mzinga (kulia) na kushoto ni Doris Donatus, mshindi wa tatu.
Hii ndiyo ilikuwa Top 5.
Majaji, kutoka kushoto ni Miss Tanzania mwaka juzi , Jokate Mwegelo, Mwenyekiti wa Kamati ya Miss Tanzania, Hashimu Lundenga ‘Anko’ na Miss Tz mwaka jana, Nasreen Mohamed, wakiwa makini kutazama warembo (hawapo pichani).
Warembo wakicheza staili ya Mugongo Mugongo jukwaani baada ya kupanda kwa mara ya kwanza.
Kundi la sanaa la International Youth Ferowship, likikonga nyoyo za wadau wa urembo kwa ngoma ya kichina kabla ya mrembo kutangazwa.
Wanenguaji wa bendi ya muziki wa dansi ya African Stars ‘Twanga Pepeta’ wakivamia jukwaa wakati wa shindano hilo.
Nani amesema wanenguaji siyo masister Duu? Hawa mamiss ila ni wanenguaji wa Twanga wakiwa chobingo wakijipodoa kwa ‘Mapouda’
Staa wa Kundi la ucheshi la Orijino Komed ‘Masanja Mkandamizaji” akiinama kukwepa kamera baada ya kubambwa ukumbini hapo akishuhudia mchuano mkali wa walimbwende hao. PICHA:CHRISTOPHER LISSA/GPL
Usiku wa kuamkia leo mkongwe wa muziki kutoka Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo (DRC), Mbili Abel alifanya makamuzi ya kufa mtu katika onesho lililofanyika Ukumbi wa Police Oficers Mess Oysterbay, jijini Dar es Salaam. Katika onesho hilo mwanamuziki huyo alisindikizwa na ‘Wazee Sugu’ The Akapitale Band chini ya mkongwe, Kikumbi Mwanza Mpango 'King Kikii'
Mbili Abel akifanya majambozi jukwaani
Hapa akiserebuka na wacheza shoo wake
Mashabiki wakichizika na vibao vilivyowahi kutamba enzi hizo
Wazee Sugu wakipagawisha na kitambaa cheupeee... Ishara ya upendo
Mashabiki wakichizika kwa kibao cha Wazee Sugu, ‘kitambaa cheupe’ PICHA: RICHARD BUKOS /GPL
Sakata la mchekeshaji mwenye uwezo mkubwa nchini kulawitiwa, sasa linaweza kuchambuliwa na Risasi Jumamosi baada ya kupata ÔdataÕ za uhakika kutoka kwa vyanzo vyake...
Ni maajabu makubwa, maziko ya Mfalme wa muziki wa Pop duniani, Michael Jackson ambapo inasemekana yatahudhuriwa na watu wapatao milioni 1 huku wengine milioni 750 wataangalia kwa njia ya runinga...
Katika mapenzi, kila mmoja huwa na hisia zake moyoni, kwa bahati mbaya hisia hizo haziwezi kuonekana kwa macho na ni vigumu sana mtu kutoa hisia zake za siri. Mara nyingi imekuwa ikitokea wapenzi kuzungumza kwa vitendo zaidi kuonesha kilichopo moyoni mwao...
Jacob ametoka gerezani baada ya msamaha wa Rais, alinusurika na kifo cha kunyongwa Rais aliposoma kitabu chake kiitwacho Give me another chance Êalichokiandika akiwa gerezani! Hukumu yake ikabadilishwa kuwa kifungo cha maisha ambacho nacho kimefutwa baada ya kuugua kifua Kikuu akiwa gerezani.
Hakuamini alipoambiwa yuko huru, kwa msaada wa nauli aliyopewa na Mkuu wa Gereza alisafiri hadi katikati ya jiji la Dar es Salaam ambako alipanda basi jingine lililompeleka mpaka stendi karibu na nyumba iliyowahi kuwa yake lakini akamwachia mfanyakazi wao wa ndani baada ya kuhukumiwa kifungo, sababu mke na mtoto wake walishauawa.
Kwenye nyumba hiyo anagonga, lango linafunguliwa na badala ya kumkuta Diana, aliyewahi kuwa mfanyakazi wao wa ndani, macho yake yanakutana na msichana mwingine ambaye baada ya kujitambulisha alimtukana na kuamini ni mwizi sababu taarifa alizonazo ni kwamba Jacob alikuwa gerezani akitumikia kifungo cha maisha, msichana huyo akalibamiza lango kwa nguvu na kuondoka zake akimwacha Jacob ameduwaa. Je, nini kitaendelea? SONGA NAYO...
Sueya anajikuta njia panda baada ya mganga kukataa dhamira yake ya kumdhuru wifi yake, nini kitakachofuata baada ya mganga wa kwanza kukataa kumdhuru wifi yake? ili kuyajua yote. KANYAGA TWENDE...
Kauli nzito imetolewa kuhusu kifo cha aliyekuwa Mbunge wa Viti Maalum kwa tiketi ya Umoja wa Vijana wa Chama Cha Mapinduzi (UVCCM), Marehemu Amina Chifupa Mpakanjia...
Warembo walioshiriki shindano la kumsaka mlimbwende wa Miss Dar City Centre lililofanyika Ukumbi wa Hoteli ya Lamada wiki iliyopita, jana walikabidhiwa zawadi zao ukumbini hapo. Pichani mshindi wa kinyang'anyiro hicho, Silvia Shally, akipokea kitita chake cha milioni moja.
Miss Dar City Centre, Silvia Shall, akiwa kwenye pozi na Miss Global Publishers, Nelly Kamwelu, wakati akijiandaa kupokea kitita chake.
Msanii wa maigizo, Charles Magali, leo jioni, alinaswa na kamera yetu ukumbi wa Hoteli ya Lamada akiwa kwenye mishemishe za mazoezi ya filamu mpya.
Njemba hii pichani (kushoto) ikimpodoa mmoja wa warembo wanaocheza maigizo katika kundi la Mzee Magali kama walivyonaswa katika ukumbi wa Hoteli ya Lamada leo jioni.
THABITI ABDUL AJIUNGA JAHAZI Aliyekuwa mwanamuziki wa African Stars ‘Twanga Pepeta Internationa’, Thabit Abdul, akiwapagawisha mashabiki wa Jahazi Modern Taarab katika ukumbi wa Mango Garden jijini Dar es Salaam mara mara baada ya kujiunga na kundi hilo. Picha: Richard Bukos na Christopher Lissa/ GPL
Wasanii waliochukua fomu za kushiriki kucheza filamu ya Tears on Valentine leo tena wameendelea kufurika katika Ofisi za Tollywood,zilizopo Sinza Bamaga, jijini Dar es Salaam tayari kwa kufanyiwa usaili. Mkurugenzi wa filamu hiyo, Hammie Rajab, ambaye pia ni mmoja wa majaji, amesema kuwa kila kukicha wasanii wamekuwa wakijitokeza kwa wingi hivyo kuwapa wakati mgumu wa kuwafanyia usaili kulingana na ratiba. Aliendelea kusema kwamba mbali na hilo, wamekuwa pia wakishangazwa na uwezo mkubwa wa washiriki hao kwani kila mmoja anaonekana kuwa na kipaji hicho ukizingatia kuwa, wengi wao hajawahi kucheza filamu hata mara moja.
Wasanii wakisubiri kuingia ndani ya ofisi za Tollywood kwa ajili ya usaili.
Waliokaa mezani kutoka kulia ni Hammie Rajab, Mkurugenzi wa Filamu hiyo na kushoto kwake ni Jaji Joseph Shaluwa wakiwatwanga maswali washiriki hao.
Cleopatra 3, mwenye sketi nyeupe, akiwa kwenye moja ya majaribio ya shughuli hiyo na Anither Tibigenda (anayemnyoshea kidole) Kushoto ni Debora Sanga mmoja wa majaji wa Tollywood Movies. Picha zote:Musa Mateja/GPL.
Kitendawili sasa kinaweza kuteguka, kuhusu vuta nikuvute iliyokuwepo kuhusu maisha ya galacha wa Bongo Flava, Rehema Chalamila ‘Ray C’. Katika siku za hivi karibuni, umekuwepo utata kuhusu Ray C a.k.a Kiuno bila mfupa, baada ya gazeti pendwa la Risasi kuandika kwamba anaishi gesti, habari ambayo mwanamuziki huyo aliikanusha.
Lile shindano la kumsaka Miss Higher Learning linalowashirikisha warembo kutokana vyuo mbalimbali vya juu nchini linatarajiwa kufanyika leo (Ijumaa) ndani ya Ukumbi wa Karimjee jijini Dar es salaam...