Tembelea... |
 |
Kalenda |
 |

Marafiki wetu |
 |
Habari Zilizopita |
 |



  
| |
 |
|
|
 |
 |
|
 |
 Kigogo mmoja wa Benki jijini Dar es Salaam, (jina limehifadhiwa) ameonesha kufuru ya pesa kwa kumhonga Miss Tanzania kiasi cha shilingi milioni 3 (3,000,000/=), sambamba na kumuahidi mrembo huyo kumjenge nyumba na kumnunulia gari la kifahari. Meseji na baadhi ya vielelezo vilivyotua mezani kwa Amani hivi karibuni vimefichua matumizi hayo makubwa ya fedha yanayodaiwa kufanywa na kigogo huyo kwa ajili ya kupalilia penzi la mlimbwende mwenye heshima ya Miss TZ. Kwa mujibu wa sms hiyo, kiasi hicho cha pesa alichodaiwa kupewa Miss huyo (jina lake limehifadhiwa) ni mwanzo wa huduma atakazopewa endapo atakubali kukandamiza raha na mheshimiwa huyo. |
|
 |
 |
|
 |
 Warembo wa Tanzania waliojitambulisha kwa jina moja moja la Amina, Janie na Candy wamepiga picha za utupu (x) na kuzisambaza sehemu mbalimbali za jiji la Dar es Salaam. Gazeti hili lilifanikiwa kupata picha za baadhi ya warembo hao hivi karibuni wakiwa katika mitindo mbalimbali ya mahaba. Aidha nyuma ya picha hizo warembo hao wameweka namba zao za simu za mikononi pamoja na mitandao wanayopatikana. Kufuatia kuwepo kwa mawasiliano ya mabinti hao, gazeti hili liliamua kuwapigia kwa nyakati tofauti na kufanikiwa kumpata Janie aliyedai yupo Arusha kikazi. Janie alisema kuwa, angerudi jijini baada ya siku tatu na kama kuna mtu anahitaji huduma yake aweke mihadi naye kwa sababu alikuwa na ‘oda’ nyingi jijini Dar es Salaam. |
|
 |
 |
|
Kudaadeki Walai!!!!
|
Amani |
|
|
 |
 Katika hali ya kustaajabisha dada mmoja aliyedaiwa kuwa ni mwanafunzi wa Chuo Kikuu kimoja nchini (jina tunalihifadhi) aliyetajwa kwa jina la Veronica Amos, amejikuta akifanyiwa kitu mbaya na vijana wa kihuni. Tukio hilo lilitokea hivi karibuni usiku wa saa sita eneo la Ubungo, Maziwa jijini Dar-es-Salaam kwenye kichochoro kimoja cha mtaa, ambapo vijana hao walimvamia dada huyo 'sistaduu' na kumchania nguo kisha kumpora simu. Shuhuda wetu aliyekuwepo eneo la tukio ambaye hakupenda jina lake liandikwe gazetini alidai kuwa, dada huyo alikuwa akitokea kuponda starehe ndipo alipopatwa na balaa hilo. "Yule dada ni mwanafunzi wa chuo kikuu (anataja jina) mara kwa mara amekuwa akipita maeneo ya hapa nyumbani usiku, amepanga nyumba ya tano kutoka ninapoishi, siku hiyo alipita kama kawaida yake, nadhani alikuwa anatoka kustarehe. |
|
 |

 |
|
 |
 Mbunge mmoja machachari na mwenye msimamo mkali bungeni, ambaye ni kijana na hana mke, amejikuta katika wakati mgumu baada ya kuona 'mgongo' wa mwanadada Ray C katika gazeti dada, Ijumaa Wikienda ya wiki hii. Tukio hili la aina yake lilitokea siku hiyo hiyo katika baa maarufu ya Chako ni Chako iliyopo Dodoma mjini ambayo wabunge wengi hukaa jioni baada ya vikao vyao ambako Mbunge huyo na mwenzake kutoka Chama cha Upinzani cha CUF ambaye pia ni kijana walikuwa wameketi wakinywa huku Mheshimiwa akisoma gazeti hilo. Mwandishi wetu wa Dodoma aliyekuwa pembeni akipata chakula chake, alifanikiwa kuyanasa mazungumzo ya wabunge hao wawili wakiongelea picha hiyo ya Ray C. "Aiseee huyu mtoto anatisha, utafikiri Beyonce, hizo ndizo figa ambazo mimi huwa nazitaka, si unajua. Mpenzi wangu wa zamani alikuwa mnene, mimi hivi sasa nataka shepu kama hizi, lazima nimpate huyu Ray C hivi nikijifanya kumtafutia tripu ya nje kimuziki atakataa?" |
|
 |
 |
|
 |
 Msanii mkongwe katika game ya muziki wa kizazi kipya, Judith Wambura 'Lady Jaydee' (pichani juu) ameiambia Abby Cool & MC George Over The Weekend kuwa kwa upande wake hana mpango wa kuachana na sanaa ya muziki hata akifikisha umri kama alionao mwanamuziki mkongwe wa taarab, Bi. Kidude. Akipiga stori zaidi na safu hii nyumbani kwake eneo la Hananasif, Kinondoni, Dar es Salaam, Jide a.k.a Komando, alisema kwamba wapo baadhi ya watu ambao huwa wanafikiria ameachana na game ya muziki pindi anapokuwa kimya, kitu ambacho siyo kweli. 'Kimya changu huwa ni kukaa na kufikiria vitu vipya vya kuimba, ndiyo maana huwa natoka na mashairi ambayo yanaigusa jamii, ambayo pia huiteka Afrika Mashariki, alisema. Akiyazungumzia mabadiliko yake katika muziki, ikiwemo staili ya kwaito ambayo anaitumia hivi sasa, Jide alisema kwamba hiyo ni kutokana na kutembelea nchi mbalimbali kisha kupata mawazo kutoka kwa wanamuziki wengine wakiwemo wale ambao wamefanikiwa kupitia staili hiyo ya kwaito. Msanii huyo ambaye anamiliki tuzo kumi na moja amesema kuwa nia yake ni kuongeza nyingine zaidi ili ndoto zake za kuwa mwanamuziki anayemiliki tuzo nyingi zitimie. Hivi sasa Jide anamiliki bendi inayojulikana kama Machozi Band ambayo ina jumla ya wasanii kumi. 'Nina mpango wa kuipeleka Machozi nje ya nchi ili kwenda kujifunza mengi zaidi' alisema. |
|
 |
 |
|
 |
 Mtangazaji wa Televisheni ya Afrika Mashariki (EATV), Irene Kiwia, ameingia katika skendo ya ngono baada ya kudaiwa kuwa na uhusiano wa kimapenzi na kigogo mmoja ambaye ni mume wa mtu. Habari toka kwa chanzo chetu cha kuaminika zimedai kuwa kutokana na uhusiano huo, ndoa ya kigogo huyo (jina tunalihifadhi) imetingishika kwa kiasi kikubwa mpaka kukaribia kusambaratika. Chanzo chetu kilifafanua kwamba ndoa ya mume huyo ambaye ni mdogo wa mmoja wa mawaziri maarufu katika Serikali ya Awamu ya Tatu, ilitingishika baada ya mke wa kigogo kubaini uwepo wa mapenzi kati ya mumewe na Irene. |
|
 |
 |
|
 |
 Kitchen Party ya aliyekuwa Miss Tanzania mwaka 1999, Hoyce Temu ilikuwa ya aina yake kufuatia watu wa Usalama wa Taifa ‘system’ kuweka ulinzi wa ‘kufa mtu’ huku mwandishi wa gazeti hili akitishiwa bastola. Shughuli hiyo ambayo ilifanyika Julai 22, mwaka huu katika Ukumbi wa Water Front jijini Dar es Salaam, ilihudhuriwa na watu maarufu lukuki akiwemo mke wa Rais mstaafu, mama Anna Mkapa. Mwandishi wetu (jina tunalihifadhi) ambaye alifanikiwa kupata mwaliko wa ‘kitchen party’ hiyo akiwa amejikoki kisawasawa, alitinga katika ukumbi huo na kuchagua meza moja iliyopangwa mahususi kwa ajili ya wageni waalikwa. Alipotulia, mwandishi huyo alianza kusoma mazingira huku akiweka sawa kamera yake ili aweze kuchukua baadhi ya matukio yaliyojiri katika ukumbi huo. |
|
 |
 |
|
Waliomuua Amina Kazi Kwao!
|
uwazi |
|
|
 |
 Kamanda wa polisi Mkoa wa Kinondoni Bw. Jamal Rwambow ametoa msimamo wa jeshi lake kuwa watawakamata na kuwahoji wale wote wanaodaiwa kumuua aliyekuwa mbunge kupitia Umoja wa Vijana wa Chama cha Mapinduzi (UVCCM) marehemu Amina Chifupa endapo watapata taarifa yenye ushahidi juu ya kifo hicho. Akizungumza na mwandishi wetu juzi kwa njia ya simu Kamanda Rwambow alisema kuwa endapo baba wa marehemu atakuwa dira kwa kuwakilisha majina ya watu wanaosadikiwa kuhusika na kifo hicho watayapokea na kuyashughulikia kisheria. "Sisi polisi mkoa wa Kinondoni hatujapokea malalamiko hayo lakini wanafamilia wakilalamika na kutuletea majina hayo tutayafanyia kazi," alisema Rwambow. |
|
 |

 |
|
Ni kwa maslahi ya UMMA au maslahi ya NYUMA?
|
--- |
|
|
 |
SAKATA la ununuzi wa rada iliyonunuliwa na Serikali ya awamu ya tatu ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, katika mazingira ya utatanishi mwaka 2002, lingali likichanja mbuga kama moto wa nyikani nyakati za kiangazi. Wengi wetu ambao tulikuwa hatujui kwa undani nini hasa kilikuwa ama kingali kimejificha ndani ya sakata hili, hivi sasa tunayajua, baada ya ukweli wake kuanza kuanikwa hadharani.
Teknolojia imetuwezesha kufunguliwa macho, Teknolojia imeonyesha tena umuhimu wake katika mchakato wa maendeleo, mchakato wa kuleta ukombozi, mchakato wa kupambana na ulafi wa baadhi ya viongozi wetu na uozo uliomo ndani ya baadhi ya serikali zetu, sio tu za kiafrika bali duniani kwa ujumla. Si hata serikali ya Uingereza ilichangia katika hili? unadhani sio uozo huo?
Bunge la Uingereza limejadili suala hili, na kukiri kuwa rushwa ilikuwemo katika manunuzi hayo, Rais wetu, mhe. Jakaya M. Kikwete, kaomba arejeshewe chenchi (cha juu kama wanavyosema vijana wa kizazi cha sasa), kutoka katika mabilioni yaliyokuwa yametolewa kwa ajili ya kununua rada hiyo. Ni kizungumkuti na mshike mshike kila kona kwa ujumla hivi sasa.
|
|
 |
|
|
 |
Kura Yako / Poll |
 |
Habari Katika Picha |
|
 |

Nani Yupo / Alikuwepo |
 |
|