arrowSet HomePage |arrowBookMark Us
right
lines

Global Publishers Tanzania- Uwazi » Articles for September 2007 Year

Tafuta  

Tembelea...

Kalenda

Gazeti la Ijumaa

Marafiki wetu

Habari Zilizopita

Soma Magazeti Yetu...

Gazeti la Risasi Mchanganyiko
Amani
Gazeti la Ijumaa Wikienda

Bongo Celebrities ...

 
Habari Zinazotamba Habari Mchanganyiko
» Mpenzi mwenye tabia hizi m ...
» (SIMULIZI ZA CHUMBANI) MDUA ...
» Mduara wa Mahaba (19)
» (SIMULIZI ZA CHUMBANI) MDUA ...
» Aisha Madinda: NGONO INANIU ...
» JACKLINE AMUANIKA ALIYEMTOA ...
» KANUMBA: NARGIS ALINITESA ...
» Wazee wa Tarime waapa k ...
» Silaha mahakamani
» Wawakilishi CUF wagoma ...
» AHSANTENI SANA KWA KUWA ...
» Stars tupeni raha kesho
» MTOTO ALIYEISHI
» Yanga: Leo chereko

 

Irene uwoya anadatisha

ijumaa wikienda  
Irene uwoya anadatishaNa Hamida Hassan
Miss Tanzania namba tano, mwaka 2006, Irene Uwoya, ameonekana kuwadatisha wanaume wengi wakware kutokana na umbo lake lenye mvuto wa aina yake. Wanaume hao ambao wamekuwa wakilipigia simu gazeti hili kwa muda mrefu, walisema kuwa mbali ya kudatishwa na umbo, pia sura ya mrembo huyo ni alama nyingine ‘inayowakong’oli’ kupita kiasi.
    (30 September 2007)
Views: 1790 | Maoni (8) | Soma Zaidi

 

Kapuya, Mudhihir Why?

ijumaa wikienda  
Kapuya, Mudhihir Why?Fatma Amri na Rehema Sapali
P amoja na dua za kuwatakia heri Waziri wa Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa, Juma Kapuya na Mbunge wa Mchinga (CCM), Mudhihir Mudhihir kuendelea kumiminika, fikra za Watanzania bado zinauliza kwanini (why), juu ya ajali zilizowakumba viongozi hao...
    (30 September 2007)
Views: 568 | Maoni (0) | Soma Zaidi

 

Wema Sepetu

ijumaa wikienda  
Wema SepetuNa Issa Mnally
Sherehe ya kutimiza umri wa miaka 19 ya Miss Tanzania 2006, Wema Isaac Sepetu, ilikuwa kufuru, kutokana na kutawaliwa na vituko kemu kemu, wakati wa kipindi hiki cha Mwezi Mtukufu wa Ramadhani...
    (30 September 2007)
Views: 2530 | Maoni (4) | Soma Zaidi

 

Ze Comedy waua!

ijumaa wikienda  
Na Richard Bukos
Kundi la vichekesho la Ze Comedy, mwishoni mwa wiki iliyopita liliua sherehe ya uzinduzi wa mfuko wa Uadilifu, Uwajibikaji na Uwazi, zilizofanyika katika Viwanja vya Mnazi Mmoja, Dar- es Salaam.

Ze Comedy ambalo huonesha vichekesho vyao kupitia Luninga ya EATV, liliua uzinduzi huo muda mfupi baada ya kupanda jukwaani kutokana na kusababisha vurugu kubwa iliyohatarisha maisha ya watu......
    (30 September 2007)
Views: 1399 | Maoni (2) | Soma Zaidi

 

Njia makini za kukabiliana na upweke

Mahaba  
Njia makini za kukabiliana na upwekeNajisikia furaha sana moyoni mwangu, furaha hiyo inatokana na uzima niliojaliwa na Mungu. Karibuni tujifunze jinsi ya kuwa bora zaidi katika uhusiano wetu na wachumba ama ndoa zetu. Kila kitu kinawezekana tukikubali kujifunza.
Kama kuna kitu kinachouma zaidi katika uhusiano ni kuachwa, hasa kama ulikuwa una mapenzi mazito juu ya mwandani wako........
    (30 September 2007)
Views: 680 | Maoni (0) | Soma Zaidi

 

For my wife, i will die! (Nitakufa kwa ajili ya mke wangu 23

hadithi za Shigongo  
Laibon alikuwa na akili nyingi kuliko kawaida, alichokifanya alipokuwa nyumbani kwa rafiki yake Milkov katika Jiji la Moscow, Urusi ni kujifunza kuogelea baharini! Hakuwa na haja na mashindano wala umaarufu, alifanya hivyo akiwa na lengo la siku moja kuzamia hadi kwenye Meli ya St. Petersbugy, akiamini kama asingefanikiwa kuwaona ndugu zake, basi utajiri wa madini ungekuwa halali yake.........
    (30 September 2007)
Views: 582 | Maoni (4) | Soma Zaidi

 

Sir Nature ampindua Chege

risasi jumamosi  
Sir Nature ampindua Chege Na Fatma Amri
Siku chache baada ya Juma Kassim ‘Nature’ kuoa imebainika kuwa yule demu aliyemuoa alikuwa ni mwanamke wa mwanamuziki mwenzake wa muziki wa kizazi kipya, Saidi Juma ‘Chege’.

Akizungumza na mwandishi wetu katikati ya wiki hii, Chege alisema kuwa ameshangazwa na hatua ya Nature kumchukulia kimwana wake licha ya kufahamu kuwa alikuwa na uhusiano naye kimapenzi.

“Nashangaa sana Nature kumuoa demu ambaye alikuwa wangu wakati kuna wanawake wengi ambao angeweza kuchagua mmoja na kumuoa,” alisema Chege.

    (29 September 2007)
Views: 1611 | Maoni (9) | Soma Zaidi

 

NIMERUDI TOKA KUZIMU -7

hadithi za Shigongo  
Kijana Prosper ambaye ni mwanafunzi wa kidato cha tano katika shule ya sekondari Pugu anarejea nyumbani likizo akiwa amejawa na furaha pamoja na matumaini makubwa maishani mwake kwa sababu amefanya vizuri kwenye mitihani yake, furaha yake yote inafutika na kugeuka kuwa msiba kwani muda mfupi tu baada ya kuwasili nyumbani na kusalimiana na kaka zake kabla hajaingia ofisini kwa baba yake pia kumsalimia, kelele inasikika ndani ya ofisi hiyo iliyopo nyumbani kwao ambako baba yake anajishughulisha na biashara ya kuuza vifaa vya ujenzi, msichana mdogo analia akidai amebakwa!

Muda mfupi baadae, majirani wanakusanyika na kufuatiwa na polisi! Hapo hapo mtoto anabadilisha maelezo yake na kudai amebakwa na familia nzima kwa zamu, hii inawafanya Prosper na ndugu zake pamoja na baba yao wakamatwe na kupelekwa polisi na hatimaye mahabusu! Mama yao ambaye ni mwalimu hakuwepo wakati hayo yanatokea, aliporejea nyumbani na kuambiwa alianguka chini na kufa hapo hapo.

Akiwa gerezani mzee Lufungulo ameamua kugoma kula ili afe, kwa siku nane mfululizo hajatia kitu mdomoni, mwisho ameanguka chini na kupoteza fahamu! Maaskari waliokuwa wakipuuza, wanambeba na kumpeleka Zahanati ya gereza.

Je, atapona au ndio mwisho wake?......
    (29 September 2007)
Views: 561 | Maoni (1) | Soma Zaidi

 

UKWELI ULIOFICHWA -63

hadithi za Shigongo  
Nyakutengwa ameachiwa huru na kwenda nyumbani kwake ambako anamchukua mwanae Davis na kuondoka bila kumuaga mfanyakazi wa ndani na kusafiri kwa ndege hadi Mwanza ambako kwa hasira ameamua kutokomea maporini, hataki kuonana na Samantha maishani mwake, anaamini alituma chakula chenye sumu gerezani kwa lengo la kumuua bahati mbaya akafa rafiki yake Thobias. Amekwishaapa hawezi kumsamehe kwa kosa hilo, Nyakutengwa haelewi kulichotokea
mpaka chakula hicho kikafika gerezani, hakuna wa kumwambia kuwa ni Wakili Ishengoma aliyefanya kitendo hicho.

Je, nini kitaendelea? Samantha atatoka gerezani au atahukumiwa kunyongwa kwa kosa la mauaji? Je, huko anakokwenda Nyakutengwa na mtoto wake kutatokea nini? SONGA NAYO.....
    (29 September 2007)
Views: 593 | Maoni (2) | Soma Zaidi

 

Makundi ya watu na aina ya mapenzi - 2

Mahaba  
Hii ni siku ya 17 katika mfungo wa Ramadhani, mwezi mtukufu ndiyo huo unayoyoma, tuombeane kheri ili kumaliza salama ibada hii muhimu kwa waumini wa Dini ya Kiislamu.

Wiki iliyopita kulitokea na matatizo, hivyo ukashindwa kupata makala haya ya Uwanja wa Huba, hata hivyo ulishaombwa radhi na mhariri wa gazeti kwakuwa kilichotokea ni makosa ya kiufundi........
    (29 September 2007)
Views: 265 | Maoni (0) | Soma Zaidi

 

Mke wa mtu mdebwedo!

risasi jumamosi  
Na Dunstan Shekidele, Morogoro

Duh, mke wa mtu mdebwedo! Mwanamke mmoja mkazi wa Morogoro mjini ambaye jina lake halikuweza kupatikana mara moja aliyefahamika kama ni mke wa mtu, hivi karibu alitekwa na wahuni kisha kumpeleka msituni na kumfanyia kitu mbaya.

Tukio hilo ambalo lilishuhudiwa na mwandishi wetu, lilitokea wiki iliyopita katika eneo la karibu na Kiwanja cha Shule ya Msingi Uwanja wa Ndege mkoani hapa.......
    (29 September 2007)
Views: 941 | Maoni (1) | Soma Zaidi

 

Simba, Yanga zagombea kocha

champion ijumaa  
Simba, Yanga zagombea kochaNA ISAAC KIJOTI
BAADA ya timu za Simba na Yanga za jijini Dar es Salaam kuanza msimu wa Ligi Kuu ya Vodacom kwa vipigo huku zikiwa na makocha wasaidizi, imeelezwa kwa sasa zimeingia katika kinyang’anyiro cha kocha.

Habari za ndani zilizolifikia gazeti hili kutoka katika vyanzo vyetu vilivyopo ndani ya uongozi wa Simba, zinasema viongozi wa Wekundu wa Msimbazi wameamua kumuwinda Sammy Timbe wa Uganda anayewaniwa na Yanga......
    (28 September 2007)
Views: 521 | Maoni (2) | Soma Zaidi

 

Hili ni bonge la sapraiziii!

Mahaba  
Karibu tena msomaji wangu, kama unazingatia hesabu ya Mwezi wa Ramadhani, leo ni swaumu ya 16, tunazidi kupunguza siku, tuombeane dua ili tuweze kumaliza mfungo huu mtukufu, Mungu yupo nasi, hilo nina uhakika nalo kwa asilimia mia moja.

Juma hili nimeamua kukufanyia ‘sapraizi’, nataka tushiriki pamoja ili tusaidiane mawazo na memba wenzetu wa safu hii pendwa, nyote ni ndugu zangu kwahiyo sote ni ndugu, hivyo hatuna budi kusaidiana......
    (28 September 2007)
Views: 616 | Maoni (1) | Soma Zaidi

 

Ashanti awashangaza Waingereza

champion ijumaa  
London, Uingereza
Msanii wa Muziki, Ashanti Douglass wa nchini Marekani, ameushangaza umma wa Waingereza baada ya kukataa fedha iliyobakia (chenji) wakati alipokwenda kufanya manunuzi kwenye mtaa maarufu kwa maduka ya nguo katikati ya Jiji la London nchini Uingereza......
    (28 September 2007)
Views: 365 | Maoni (1) | Soma Zaidi

 

Jamhuri Kocha wa wiki tatu...

champion ijumaa  
Na Immaculate Masanja
BAADA ya kuanza vibaya michuano ya Ligi Kuu ya Vodacom msimu huu, uongozi wa Klabu ya Simba umemteua Jamhuri Kihwelu ‘Julio’ kuwa Kocha Mkuu wa timu hiyo kwa muda.

Awali timu hiyo ilikuwa ikimnyatia Kocha wa Timu ya Taifa ya Vijana ya Oman, Talib Hilal, lakini kwa sasa uongozi wa Klabu ya Simba umedai hauna uwezo wa kumlipa......
    (28 September 2007)
Views: 289 | Maoni (0) | Soma Zaidi
Back  <<  1 2 3 ... 14 15 16  >>  Next Page
 

Kura Yako / Poll

Habari Katika Picha


Gazeti la Uwazi


Nani Yupo / Alikuwepo


Home Page | About Us | Regista | Picha | Bongo Celebrities | Maoni | Contact Us

hit counter

 

2008 © globalpublisherstz.com