On Thursday, 30 September 2007, Roots Marketing Communications, the advertising agent for Zantel and others, celebrated its first Birthday at its offices in Masaki, Dar es salaam. Our Chief Photography, Abdallah Mrisho was there to capture the event........
Kikundi maarufu cha sanaa za uchekeshaji kijulikanacho kwa jina la Ze Comedy cha jijini Dar es Salaam kiko matatani baada ya kudhihaki maadiko takatifu ya dini ya kiislamu (kurani), hivyo kuwatibua waislamu nchini.
Aidha wasanii hao wametakiwa kuwaomba radhi waislamu kabla hawajachukuliwa hatua kali ambayo huenda ikawadhuru.
Onyo hilo limetolewa na Sheikh Hashim Ruseganya wa Msikiti wa Mtambani jijini Dar es Salaam wakati wa hotuba ya swala ya Ijumaa aliyoitoa msikini hapo hivi karibuni.
Wakati Fainali ya Miss Tanzania 2007-08 ikitarajiwa kufanyika leo kwenye Viwanja vya Leaders Club, Kinondoni, Dar es Salaam, imebainika kuwa Miss Ilala, Latifa Warioba, ameundiwa zengwe ili abwagwe.
Latifa ameundiwa zengwe na baadhi ya warembo washiriki pamoja na waandaaji wa mashindano hayo katika ngazi ya vitongoji na kanda mbalimbali, kutokana na kubainika kuwa na sifa nyingi za kuibuka mshindi.
Habari zilizolifikia dawati gazeti hili, zinasema kuwa tayari kumeshazuka hali ya kumkatisha tamaa mrembo huyo kama vile kumtenga na warembo wenzake ili kumuathiri kisaikolojia na hatimaye ashindwe kushindana sawia.
Siri ya kuachwa nyumbani mwanamuziki maarufu wa Bendi ya African Stars International ‘Twanga pepeta’, Kamarada Ally Choki huku wenzake wakipaa kwenda Uingereza, imefichuka.
Kuachwa huko kwa Choki kunatokana na kupigwa marufuku nguli huyo wa muziki wa kibongo kukanyaga ardhi ya Uingereza kutokana na madai ya kushitukiwa dili lake la kuingiza watu wasio wanamuziki nchini humo.
Ndoa na mabadiliko yake Habari za leo msomaji wangu mpendwa wa kona hii pendwa, nikukaribishe kwa wiki nyingine tuweze kulonga kama ‘kawa’ kuhusiana na mambo yanayotuhusu hususan katika suala zima la mapenzi, si unajua mambo yangu Anti Liz? Jumamosi hii, nikiwa na ari, nguvu na kasi ya kutisha, kwa raha zangu nitachambua hii kama inavyojitambulisha hapo juu, napenda ufahamu kuwa nimeiteua baada ya kupata mapendekezo mengi kutoka kwa wasomaji.
Wakati dalili za ushindi katika kesi ya mauaji inayomkabili Nyakutengwa zimeanza kuonekana, Wakili Dk. Ishengoma anayemtetea Nyakutengwa katika kesi hiyo ameingiwa na tamaa! Anampenda mke wa Nyakutengwa Samantha, mrithi wa utajiri mkubwa wa marehemu baba yake mzee Davis Mosha aliyeuawa na Nyakutengwa.
Ishengoma anaamini akimpata Samantha tayari atakuwa ameuweka utajiri wake wote mikononi mwake, mawazo hayo ndio yanamfanya abadilishe msimamo katika kumtetea Nyakutengwa! Hivi sasa anataka kijana huyo afungwe maisha au anyongwe ili yeye abaki na Samantha akiponda maisha.