Dk. Othman anaokoka katika mikono ya sheria, ni rafiki yake mpendwa Dk. Ringo ndiye aliyefanya mipango ya kumtoa Dk. Othman. Baada ya kujitundika katika chumba cha mahabusu, anaokolewa na Musa ambaye aliandaliwa na Mkuu wa Kituo Mwakatego. Hatimaye Musa anaachiwa huru baada ya kutimiza makubaliano aliyotakiwa kuyafanya! Othman anapelekwa mochwari, akiwa humo mlango unagongwa, mambo yanaharika, Gebeshi anashauri aingie kwenye jeneza la kusafirishia maiti, hakubisha akafanya hivyo, lakini hatimaye wakagundua kuwa aliyekuwa akigonga mlango alikuwa ni Dk. Ringo.
Baada ya kutoka huko wakaondoka kwenda Masaki kwa Dk. Ringo, huko mipango ya safari ya Uingereza ikaendelea kupangwa! Siku iliyofuata magazeti yote yaliandika habari za kujinyongwa kwa Dk. Othman, kila gazeti liliandika kwa kichwa chake, ingawa picha iliyoonyesha akiwa amening’inia ilitumiwa na kila gazeti.
Wakiwa barabarani kuelekea Uwanja wa Ndege tayari kwa safari ya kwenda Uingereza, wakasimamishwa na maaskari waliokuwa katika taa za Karume. Dk. Ringo akachanganyikiwa!
Alijua kila kitu kilishaharibika! Nini kitaendelea? SONGA NAYO…... |