Na Joseph Shaluwa Wahenga walinena, mafahari wawili hawakai zizi moja, usemi huo umeonekana kutimia baada ya wakali wa sanaa ya maigizo nchini, Vicent Kigosi 'Ray' na swahiba wake wa siku nyingi, Steven Kanumba 'Kanumba' kuwa na chuki 'bifu' za chini kwa chini kiasi cha kutishiana kurogana, Ijumaa limedolezwa....
Na Salum Mnette Naibu Waziri wa Kazi na Maendeleo ya Vijana, Dk. Emmanuel Nchimbi kwa mara ya tatu jana, alimgaragaza aliyekuwa mgombea Ubunge wa Jimbo la Songea mjini, Edson Mbogoro kupitia CHADEMA, baada ya kumshinda katika kesi ya kupinga ushindi wake iliyokuwa ikiunguruma katika Mahakama ya Rufaa jijini Dar es Salaam.....
Na Hamida Hassan Msanii maarufu wa Bongo Fleva nchini, Rehema Chalamila 'Ray C' amefuata nyayo za washiriki watano waliotangulia kutoka katika mpambano wa The Ijumaa Sexiest Girl baada ya kupata 9.1% ya kura zote zilizopigwa na mashabiki....
Tangu siku hiyo familia yetu na ya mpenzi wangu ziliingia kwenye vita vikali, hata hivyo mama alinifahamisha kwamba bibi yake alimueleza ukoo wetu haurogeki hivyo tusingedhuriwa na mtu yeyote.
Aliongeza kusema kuwa, ili tusirogwe tulipaswa kuishi kitakatifu (Tauwidi) ambapo tulitakiwa kuswali, kutoa zaka na kuwapenda watu wengine.....
Laibon ametoka kwenye chumba walimofungiwa na Mohamed, kiu ya maji ndiyo inayomsumbua, akiwa jikoni anakamatwa na Yuri, nahodha shoga asiye na huruma na kupelekwa juu kabisa ya meli kwenye chumba cha mateso ambako kwa siku kadhaa anateswa na baadaye kutupwa majini akiwa amevishwa boya na kufungukiwa chakula....
Sina shaka mtakuwa wazima wa afya njema na mnaendelea na majukumu yenu ya kila siku salama, mimi pia ni mzima na nina furaha ya ajabu moyoni mwangu! Unajua kwanini nina furaha? Kwa sababu naishi bila hofu, nikiwa chini ya uangalizi makini wa Mungu wangu ambaye ni muaminifu siku zote!....