arrowSet HomePage |arrowBookMark Us
right
lines

Global Publishers Tanzania- Uwazi » ijumaa » Ray, Kanumba watishiana uchawi!

Tafuta  

Tembelea...

Kalenda

Gazeti la Ijumaa

Marafiki wetu

Habari Zilizopita

Soma Magazeti Yetu...

Gazeti la Risasi Mchanganyiko
Amani
Gazeti la Ijumaa Wikienda

Bongo Celebrities ...

 
Habari Zinazotamba Habari Mchanganyiko
» Mpenzi mwenye tabia hizi m ...
» (SIMULIZI ZA CHUMBANI) MDUA ...
» Mduara wa Mahaba (19)
» (SIMULIZI ZA CHUMBANI) MDUA ...
» Aisha Madinda: NGONO INANIU ...
» JACKLINE AMUANIKA ALIYEMTOA ...
» KANUMBA: NARGIS ALINITESA ...
» MWINYI MKATILI
» Denti afumwa!
» Kijiji Uturuki chachinj ...
» TUNATAKA MAENDELEO
» Tumaini la mwisho - 24
» (SIMULIZI ZA CHUMBANI) ...
» Mfanyakazi auawa mgodin ...

Ray, Kanumba watishiana uchawi!

ijumaa

Ray, Kanumba watishiana uchawi!Kwa mujibu wa chanzo chetu cha habari ambacho kiliomba hifahi ya jina lake, baada ya vinara hao kujizolea umaarufu katika tasnia hiyo, hasa baada ya kufanya vizuri katika Filamu ya Johari, wamekuwa hawapikiki chungu kimoja.

Habari zaidi zinasema baada kutoa filamu zao, mmoja kati ya mastaa hao anajiona wa ghali sana kiasi cha kuamua kuanzisha chuki zisizo na sababu.

"Unajua ...(anataja jina) ni mkorofi sana, lakini mwenzake mara kadhaa amekuwa akiomba wakutane kwa ajili ya kuweka mambo sawa, na yeye hukataa," kilieleza chanzo hicho.

Inadaiwa kuwa, baada ya kuwepo kwa maneno ya chini chini kuwa wawili hao sasa ni sawa na paka na panya, waliamua kuyamaliza kisha kutangaza kwenye vyombo vya habari kuwa hawana tofauti yoyote, lakini baada ya muda mfupi 'bifu' likarudi tena upya.

Aidha kiliendelea kupasha kuwa, bifu lililorudi kwa mara ya pili, lilikuwa la kimya kimya huku wawili hao wakikosa hata mawasiliano ya kawaida kama wasanii wa tasnia moja.

"Huwezi kuamini hata kusalimiana kwao ni shida, mimi nakuambia haya kwa uhakika kwa sababu ni watu wangu wa karibu, nawajua vizuri. wanaweza hata kukutana barabarani lakini wapishane kama hawajuani, yaani hawa watu hawapatani hata kidogo," kilieleza chanzo hicho.

Katika hatua nyingine, chanzo chetu kilipasua kuwa, baada ya bifu hilo kuendelea chini kwa chini, walifikia hatua ya kutumiana meseji za matusi na kutishiana maisha.

"Kuna wakati hutambiana magari, mavazi na vito vya thamani, lakini mambo yamezidi kuwa mabaya baada ya mmoja wao kumtishia mwenzake kumwendea kwa mganga wa kienyeji, ili kumzima nyota yake," kilipasha chanzo hicho.

Hata hivyo, inadaiwa kuwa baada ya mmoja wa wasanii hao kutishiwa uchawi, hakuonyesha kujali, badala yake alijibu mapigo kwa kumwambia kuwa angemwendea kwa mtaalam mkali zaidi yake.

"...(anamtaja jina) hakukubali kushindwa, alimwambia kuwa yeye ana mtaalam mzuri zaidi Bagamoyo na kuahidi kupambana naye," kilisema chanzo hicho.

Baada ya gazeti hili kupata madai hayo, lilifanikiwa kumpata Ray kwa njia ya simu ambaye alikasirishwa sana na tuhuma hizo.
"Hivi una akili kweli wewe? Mimi niko ndani ya Yesu, sina mambo ya kishirikina na wala sijawahi kufikiria, kuhusu Kanumba sipo tayari kuzungumza chochote," Ray alisema kwa ukali kisha akakata simu.

Akizungumza na Ijumaa kwa njia ya simu, Kanumba alisema hana muda wa kuzungumzia mambo ya Ray na kwamba ushirikina anausikia kwa watu.

"Mambo ya uchawi na mimi yametokea wapi tena? Mimi nimezaliwa katika familia yenye maadili na inayomwogopa Mungu, sina habari kabisa na mambo ya kishirikina. Kuhusu Ray, sina muda wa kuzungumza juu ya mambo yake," alisema Kanumba kabla ya kukata simu.


 (Votes #: 0)
    (20 September 2007)
Soma Zaidi: 1278 | Maoni Yako (8)

Udaku Mwingine

ijumaa
 
  • WEMA, IRENE SASA WAFIKIA PABAYA
  • WEMA SEPETU HUYU!
  • Wema amtosa kanumba
  • Irene Uwoya,Wema Sepetu Kutwangana
  • VIGOGO WA WEMA WAMTISHIA KANUMBA
  •    

    #1 Author: mkere (20 September 2007 18:09)

    Hawa watoto ndio maana wananiudhi wanaonyesha jisni gani amabvyo hawajakomaa kiakili na hizo pesa ndio zina wazuzua. Mbaya zaidi wote wanatoka katika familia zilizomtanguliza mungu mbele halafu wanajiingiza katika ushirikina. Kama kuna mtu wa kuwashauri awashuri wanaume hawatambiani kuhusu vito,nguo na magari ni upuuzi mtupu. Kama ni uigizaji wote ni wakali ninge kuwa mimi wao ninge boresha kiingereza maana wote wana accent mbaya sana na umaarufu hupotea kama upepo wasichezee maisha
     
    fast    

    #2 Author: tatu (21 September 2007 09:58)

    RAY& KANUMBA MNATISHIANA UCHAWI DUH KUMBE NYIE WAKIZAMANI SANA MABROO
     
    fast    

    #3 Author: FARIDA (21 September 2007 13:56)

    HUAGA SISI WASANII TUNAWAPENDA SANA PALE MNAPO SHIRIKIANA RAY & KANUMBA KUNA NINI TENA AU HAWA PAPA RAZI WANA MIZUSHIA KAMA WANAYO SEMA NIKWELI JIREKEBESHENI NINYI NI NDUGU WA BABA MMOJA NINA MAANA BABAYETU ALIYE MBINGUNI.MUNGU ANA WAPENDA NA ANA MAKUSUDI NA MAISHA YENU MUOMBENI.
    KANUMBA VIPI JAMANI MBONA UNATAKA KUSHUSHA UMAARUFU WAKO KUWA MAKINI KUMBUKENI SIO WOTE WAMIPENDAO.BYEE BYEE GOOD DAY FATHER LOVE THEM

     
    fast    

    #4 Author: Lameck lewi (23 September 2007 03:34)

    Kanumba acha ujinga wewenimtu wanamna gani? kila siku
    vurugu nawasani wenzako? mara una bif na Ray
    sasa hivi napo ume rukia kwa Frenk badala yakupandisha umaarufu unazidi kuudidimiza.haitoshi umeanza kutishiana ucha. think befor to do.
    by by.
     
    fast    

    #5 Author: Karoli Jackson (31 October 2007 13:38)

    SIKU ZOTE UMAARUFU PALE AMBAPO KUNA USHIRIANO BAINA MTU NA MTU,SASA IWEJE LEO KANUMBA UPATE UMAARUFU UANZE MIZENGWE NA WASANII WENZAKO ACHA UTOTO JENGA USHIRIKIANO NA WENZAKO NA MUNGU ATAKUONGEZEA UMAARUFU ZAIDI.
     
    fast    

    #6 Author: mwana (27 November 2007 23:25)

    hilo
     
    fast    

    #7 Author: faith (5 December 2007 18:24)

    jaman kanumba na ray nawaomben muombane msamaha kwani nyie niwatu wa mungu kwanini mgombane?kibaya zaidi mnatishiana kuuana maisha hayaend hivyo kaka zanguni mmoja ajishushe kwa mwenzake mungu atawasaidia, na kugombana kunawapunguzi mibaraka

    kanumba najua wewe nimtu wa mungu pls mwite ray muombane msamaha plz nitakupigia nisikie kama mumesuruhisha mungu atawasaidien katika uigizaji wenu
     
    fast    

    #8 Author: John (11 April 2008 15:55)

    Mmh, that's too much
     
    fast    

    Add comments

    Name:
    E-mail:

    Code:
    Include security image CAPCHA.
    to renew the code
    Enter Code:

     

    Kura Yako / Poll

    Habari Katika Picha


    Gazeti la Uwazi


    Nani Yupo / Alikuwepo


    Home Page | About Us | Regista | Picha | Bongo Celebrities | Maoni | Contact Us

    hit counter

     

    2008 © globalpublisherstz.com