Mzee wa Kanisa la Kiinjili la Kilutheri Tanzania (KKKT) la Mvuti Wilaya ya Ilala, jijini Dar es Salaam, Phares Kweka wiki hii alikumbwa na aibu ya mwaka baada ya kufumaniwa akiwa na mke wa rafiki yake aitwaye Nasim Mohamed katika nyumba ya kulala wageni (gesti) ya Mremi’s iliyopo Buguruni jijini.
Tukio hilo lilitokea saa nne, Jumatatu ya Septemba 17, mwaka huu baada ya kuwekewa mtego na mume wa mwanamke huyo aitwaye Marc Tibber uliofanikisha kumnasa akiwa mtupu kitandani kama anavyoonekana pichani ukurasa wa mbele....
Prosper, mwanafunzi wa kidato cha sita katika shule ya sekondari ya wavulana ya Pugu, mwenye uwezo mkubwa darasani, ndoto za kuwa mtu mkubwa na mwenye mafanikio baadaye maishani mwake, asiyependa mambo ya ngono kabisa isipokuwa masomo, anarejea nyumbani kwao Mbezi baada ya kufunga shule akiwa na furaha nyingi moyoni mwake.
Nusu saa tu baada ya kurejea nyumbani mambo yanabadilika napengine yakamharibia milele! Furaha yote aliyokuwa nayo inageuka kuwa msiba baada ya mtoto mdogo aliyekuwa na baba yake ndani ya ofisi yake kupiga kelele akidai amebakwa! Muda mfupi tu baadaye watu wanajaa kuizunguka nyumba, wakitaka kumpiga baba yake Prosper, mzee Lufungulo mpaka wamuue lakini mwenyekiti wa serikali ya mtaa anawazuia lakini baadaye polisi wanawasili na kumuuliza mtoto anayedai kubakwa juu ya kilichotokea, hapo ndipo mtoto anatoa maelezo yaliyowafanya hata Prosper na nduguze John na Saimon washindwe kuamini! Mtoto amedai, mzee Lufungulo na watoto wake walimvua nguo na kumbaka kwa zamu.
Je, nini kitaendelea? SONGA NA HADITHI HII YA KUSIKITISHA.......
Nyakutengwa yuko gerezani, akishtakiwa kwa kosa la mauaji ambayo wakili Dk.Ishengoma amefanikiwa kumtetea mpaka dakika ya mwisho na dalili kuonekana kwamba kesi hiyo atashinda lakini ghafla, wakili wake amejikuta katika mapenzi na Samantha ambaye ni mke wa Nyakutengwa! Anamtaka mwanamke huyo awe mke wake, jambo la kwanza alilofanya ni kumdanganya ili akikane kitabu cha kumbukumbu kinachoenyesha kuwa Davis Mosha ndiye alifanya mauaji yote na Nyakutengwa aliua akiwa katika kujihami, lengo la kufanya hivyo ni kuhakikisha Nyakutengwa anafungwa maisha.
Jambo la pili alilofanya ni kutuma chakula chenye sumu gerezani ili Nyakutengwa akila afe. Kijana aitwaye Chacha ndiye amekipeleka na kudai mbele ya maaskari anadai ametumwa na Samantha! Nyakutengwa hakula chakula hicho ila rafiki yake aitwaye Thobias ambaye baadaye alikufa na kusababisha Samantha akamatwe na kutupwa mahabusu kwa kosa la mauaji ambayo hakuyafanya. Nyakutengwa aliposikia badaye kuwa chakula alicholetewa na mke wake kilikuwa na sumu alikasirika, hivi sasa hataki hata kumwona.
Kwa Dk. Ishengoma yanayotokea yote ni furaha tupu, anaamini atatumia nafasi hiyo kumpata Samantha ambaye hakika anahitaji msaada wake kuliko wakati mwingine wowote. Samantha alipomwomba amsaidie kuongea na Nyakutengwa, Dk. Ishengoma alikubali lakini akamuuliza kama alikuwa anampenda.