Richard Bukos na Christopher Lissa Kundi la vijana 10, limedaiwa kuibuka eneo la Manzese, Dar es Salaam na kuendesha ‘songombingo’ la kikatili kwa kuwateka mabinti kisha kuwabaka kwa zamu.
Vyanzo mbalimbali vya Ijumaa Wikienda, vilieleza kwamba vijana hao, hutumia gia ya kuwateka mabinti na kwenda kuwabaka kwa kujitambulisha kama askari wa jadi ‘sungusungu'....
Na Mwandishi Wetu Hali ya mauzauza, ilitawala kwenye tukio la kuungua hadi kuteketea kwa Hoteli ya Kitalii ya Sea Cliff, iliyopo Masaki jijini Dar es Salaam. Hoteli hiyo ilianza kuungua juzi (Jumamosi), saa 12 jioni na moto kuzimwa saa 4 usiku, ajali ambayo inadaiwa kusababishwa na ‘shoti’ ya umeme.....
Wiki hii, kupitia 'Street Version' tunapata maoni kutoka kwa baadhi ya Watanzania ambao wamekuwa wakifuatilia kwa karibu Shindano la Big Brother Afrika (BBA) linaloendelea hivi sasa huko Afrika ya Kusini.....
Kutoka Moscow Mzungu raia wa Urusi, Alexander Pichushkin, amefikishwa mahakamani kujibu mashtaka ya kuua watu 62, makosa ambayo anadaiwa kuyafanya ndani ya kipindi cha miaka kumi na tano iliyopita....
Na Mwandishi Wetu Mfanyabiashara maarufu chini,, Mohammed Mpakanjia ‘Meddy’ ambaye alikuwa hajulikani alipo, sasa amefichuliwa. Habari za kuaminika kutoka chanzo chetu cha habari zilizolifikia gazeti hili wiki hii, zinasema kuwa Mpakanjia yupo Kimara jijini Dar es Salaam anapumzika....
Nainua mikono yangu juu, kwa heshima zote, nikimrudishia Mungu wangu, sifa heshima na utukufu. Yeye ni kila kitu katika maisha yangu, bila msaada wake, hakika siwezi kuwa kama nilivyo leo! Nakusihi nawe msomaji wangu mpenzi, jenga utaratibu wa kumshukuru Mungu kwa kila jambo.....
Laibon anakamatwa ndani ya meli waliyozamia na kutupwa majini, akimwacha Tina, Bibi Khadija pamoja na mtoto aliyemwokota Hope wakiendelea na safari bila kugundulika lakini mwendo mfupi tu mbele anashuhudia ndege zikishuka na kuilipua meli hiyo.
Hii inamaanisha mpenzi wake Tina na watu wote waliokuwemo ndani ya meli hiyo wamekufa, Laibon analia lakini machozi yake yanamezwa na maji....