Na Mariam Mndeme Watangazaji maarufu wa kipindi pendwa cha Afro-Beat kinachorushwa na kituo cha Televisheni cha East Africa (EATV) Maimartha Jesse na Benny Kinyaiya hivi karibuni walibambwa live kwenye ukumbi wa Mango Garden ulioko Kinondoni jijini Da es Salaam, wakipeana raha kiaina.....
Na Catherine Kassally Mademu (wasichana) wawili ambao ni walinzi wa kampuni moja binafsi (majina yao na kampuni yao haikufahamika) hivi karibuni walimshikisha adabu brazameni (kijana wa kileo) anayedaiwa kuwa ni kibaka kwa kumpiga kipigo kikali nusura ya kumtoa roho......
Na Mwandishi Wetu Msichana mmoja aliyefahamika kwa jina la Suleha Jacob a.k.a Queen Sully ambaye ni mnenguaji maarufu kwenye kumbi mbalimbali za burudani jijini Dar es Salaam, ameonja joto ya jiwe baada ya kuvamiwa na wanaume watano kisha kumfanyia kitu mbaya.....
Dotto Mwaibale na Mwandishi Wetu, Urambo Ajali ya gari iliyompata Waziri wa Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa, Prof. Juma Kapuya hivi karibuni mjini Tabora na kusababisha vifo vya watu watatu na wengine kujeruhiwa, imeelezewa kwamba ilikuwa mbaya na ingemuwia vigumu mtu yeyote kupona.....
Ilipotimu saa sita kamili mchana nilifuatwa na wazee watatu ambao walinifungua kamba kisha niliongozana nao hadi sehemu ya wazi iliyokuwa na majini wengi waliokuwa wamefurahi.
Majini hao waliponiona walishangilia na kusema; “Mau! Mau!” ndipo niliongozwa na kwenda kukalisha kwenye jamvi ambapo haukupita muda mrefu aliletwa Husna na kuja kuketishwa upande wangu wa kushoto......
Tunakutana tena katika muendelezo wa makala ya wiki iliyopita iliyokuwa inahusu dondoo kumi za kumdatisha mpenzi wako. Kimsingi kuna mambo mbalimbali ambayo unatakiwa kuwa makini nayo katika maisha yako ya kila siku ili kulifanya penzi lenu lizidi kushamiri kadiri siku zinavyozidi kusogea....
Kama nilivyosema katika mahojiano yangu na televisheni ya Chanel Ten, Jumamosi iliyopita kwamba, ili filamu ya Fake Pastors ambayo inatokana na hadithi hii, iweze kuuzwa kwa bei ambayo kila Mtanzania ataimudu, nililazimisha kusafiri hadi China ambako tulifanya uzalishaji wake. Mategemeo yetu yalikuwa, filamu hii iwe hapa nchini tarehe 15 Septemba na kuanza kuuzwa tarehe 20.....
Mzee wa Kanisa la Kiinjili la Kilutheri Tanzania (KKKT) Mvuti, jijini Dar es Salaam Phares Kweka aliyefumaniwa na mke wa mtu wiki iliyopita, Buguruni jijini Dar es Salaam, sasa ametoweka nyumbani kwake.
Habari za uhakika kutoka kwa rafiki wa karibu wa mzee huyo, (jina tunalihifadhi), Kweka alitoweka mara baada ya kuchapishwa kwa habari zake za fumanizi kwenye gazeti letu la Risasi la wiki iliyopita.
Kweka alifumaniwa na kijana mmoja wa eneo hilo aitwaye Marc Tibber akiwa na mke wake katika nyumba ya kulala wageni ya Mremi’s Annex Jumatatu ya Septemba 17, mwaka huu.......