Na Fatma Amri Siku chache baada ya Juma Kassim ‘Nature’ kuoa imebainika kuwa yule demu aliyemuoa alikuwa ni mwanamke wa mwanamuziki mwenzake wa muziki wa kizazi kipya, Saidi Juma ‘Chege’.
Akizungumza na mwandishi wetu katikati ya wiki hii, Chege alisema kuwa ameshangazwa na hatua ya Nature kumchukulia kimwana wake licha ya kufahamu kuwa alikuwa na uhusiano naye kimapenzi.
“Nashangaa sana Nature kumuoa demu ambaye alikuwa wangu wakati kuna wanawake wengi ambao angeweza kuchagua mmoja na kumuoa,” alisema Chege.
Kijana Prosper ambaye ni mwanafunzi wa kidato cha tano katika shule ya sekondari Pugu anarejea nyumbani likizo akiwa amejawa na furaha pamoja na matumaini makubwa maishani mwake kwa sababu amefanya vizuri kwenye mitihani yake, furaha yake yote inafutika na kugeuka kuwa msiba kwani muda mfupi tu baada ya kuwasili nyumbani na kusalimiana na kaka zake kabla hajaingia ofisini kwa baba yake pia kumsalimia, kelele inasikika ndani ya ofisi hiyo iliyopo nyumbani kwao ambako baba yake anajishughulisha na biashara ya kuuza vifaa vya ujenzi, msichana mdogo analia akidai amebakwa!
Muda mfupi baadae, majirani wanakusanyika na kufuatiwa na polisi! Hapo hapo mtoto anabadilisha maelezo yake na kudai amebakwa na familia nzima kwa zamu, hii inawafanya Prosper na ndugu zake pamoja na baba yao wakamatwe na kupelekwa polisi na hatimaye mahabusu! Mama yao ambaye ni mwalimu hakuwepo wakati hayo yanatokea, aliporejea nyumbani na kuambiwa alianguka chini na kufa hapo hapo.
Akiwa gerezani mzee Lufungulo ameamua kugoma kula ili afe, kwa siku nane mfululizo hajatia kitu mdomoni, mwisho ameanguka chini na kupoteza fahamu! Maaskari waliokuwa wakipuuza, wanambeba na kumpeleka Zahanati ya gereza.
Nyakutengwa ameachiwa huru na kwenda nyumbani kwake ambako anamchukua mwanae Davis na kuondoka bila kumuaga mfanyakazi wa ndani na kusafiri kwa ndege hadi Mwanza ambako kwa hasira ameamua kutokomea maporini, hataki kuonana na Samantha maishani mwake, anaamini alituma chakula chenye sumu gerezani kwa lengo la kumuua bahati mbaya akafa rafiki yake Thobias. Amekwishaapa hawezi kumsamehe kwa kosa hilo, Nyakutengwa haelewi kulichotokea mpaka chakula hicho kikafika gerezani, hakuna wa kumwambia kuwa ni Wakili Ishengoma aliyefanya kitendo hicho.
Je, nini kitaendelea? Samantha atatoka gerezani au atahukumiwa kunyongwa kwa kosa la mauaji? Je, huko anakokwenda Nyakutengwa na mtoto wake kutatokea nini? SONGA NAYO.....
Hii ni siku ya 17 katika mfungo wa Ramadhani, mwezi mtukufu ndiyo huo unayoyoma, tuombeane kheri ili kumaliza salama ibada hii muhimu kwa waumini wa Dini ya Kiislamu.
Wiki iliyopita kulitokea na matatizo, hivyo ukashindwa kupata makala haya ya Uwanja wa Huba, hata hivyo ulishaombwa radhi na mhariri wa gazeti kwakuwa kilichotokea ni makosa ya kiufundi........
Duh, mke wa mtu mdebwedo! Mwanamke mmoja mkazi wa Morogoro mjini ambaye jina lake halikuweza kupatikana mara moja aliyefahamika kama ni mke wa mtu, hivi karibu alitekwa na wahuni kisha kumpeleka msituni na kumfanyia kitu mbaya.
Tukio hilo ambalo lilishuhudiwa na mwandishi wetu, lilitokea wiki iliyopita katika eneo la karibu na Kiwanja cha Shule ya Msingi Uwanja wa Ndege mkoani hapa.......