arrowSet HomePage |arrowBookMark Us
right
lines

Global Publishers Tanzania- Uwazi » ijumaa » Richard, mkewe full shangwe

Tafuta  

Tembelea...

Kalenda

Gazeti la Ijumaa

Marafiki wetu

Habari Zilizopita

Soma Magazeti Yetu...

Gazeti la Risasi Mchanganyiko
Amani
Gazeti la Ijumaa Wikienda

Bongo Celebrities ...

 
Habari Zinazotamba Habari Mchanganyiko
» Aunt Ezekiel alivyopigika k ...
» KIGOGO WA MURO NAYE KUKAMAT ...
» JERRY MURO AKOSWA RISASI
» Kigogo afanyiwa umafia
» ZITO LAIBUKA
» JERRY: NASAKWA NIUAWE!
» Waraka wa Papii watua kwa J ...
» Wapendwa marafiki wa Go ...
» Mpenzi wangu kapewa mim ...
» MAPAPARAZI DAR WALIVYOM ...
» (SIMULIZI ZA CHUMBANI) ...
» KIGOGO IKULU, BALOZI WA ...
» Uhusiano wa nyakati na ...
» BARUA KUTOKA KWA MAREHE ...

Richard, mkewe full shangwe

ijumaa

Richard, mkewe full shangweMara baada ya mkewe Richard kuondoka kwa hasira nyumbani kwa mzee Bezuidenhout usiku wa fainali za BBA, alikwenda kwa rafiki yake mmoja aliyesoma nae Chuo Kikuu cha Dar es Salaam (UDSM) aishiye maeneo ya Mbezi Beach ambako mumewe hakupajua hadi siku chache zilizopita.

Kwa mujibu wa chanzo chetu cha habari cha kuaminika, Richard alifanya jitihada za ziada kujua sehemu alikokimbilia mkewe na alipofanikiwa kupajua alikwenda kumuangukia na hatimaye alifanikiwa kumuhamishia kwa siri hoteli aliyofikia.

Katika uchunguzi wake na kwa kusaidiwa na chanzo chake cha habari, Ijumaa limefanikiwa kuibua maficho ya wawili hao ambapo sasa inajulikana wanaishi Holiday Inn, ambayo ni hoteli yenye hadhi ya nyota 5 iliyopo katikati ya jiji la Dar es Salaam ambako mshindi huyo wa BBA ndiko alikofikia tangu awasili nchini wiki mbili zilizopita.

Kwa mujibu wa chanzo chetu, baada ya mtafaruku uliotokea kati ya Richard na mkewe ambaye alikerwa na uhusiano wa kimapenzi uliokuwepo baina ya ‘Big Brother’ huyo na mshiriki mwenzake kutoka nchini Angola, Tatiana, hivi sasa mambo ni shwari ingawa Ricki hajamtamkia wazi Richard kuwa amemsamehe kwa yote aliyoyafanya.

Chanzo hicho kiliongeza kuwa, ingawa wanafamilia walichukizwa na kitendo cha Ricki kumuita ndugu yao Nguruwe, kauli ambayo ilimaanishi hata yeye ameolewa na nguruwe, lakini kwa sasa wamemsamehe na wamemuomba naye amsamehe mumewe na kwamba yaliyopita yamepita wagange yajayo.

“Kama Ricki aliweza kumuita Richard nguruwe, hiyo ilimaanisha nyumba nzima ni ya nguruwe na bila shaka yeye pia ameolewa na nguruwe. Lakini yote hayo tumemsamehe, hivyo tunamuomba naye amsamehe mumewe, yaliyopita yamepita, tugange yajayo,” kilisema chanzo hicho kikikariri tamko la familia.

Aidha, chanzo chetu kimeeleza kuwa wanafamilia wametoa darasa kwa wanandoa hao kuwa hawana budi kuweka pembeni tofauti zao ili kuinusuru ndoa yao changa ambayo haijaaliwa kupata mtoto hata mmoja.

Katika hatua nyingine, mashabiki wa Richard kutoka sehemu mbalimbali za Afrika, wamekuwa wakimtumia barua pepe kumueleza tabia za Tatiana ambaye alikuwa mpenzi wake kwenye Jumba la BBA.

Mashabiki hao wamemtaka Richard kuanchana kabisa na Tatiana kwani nchini kwao Angola anajulikana kama mwanamke ambaye hajatulia na amepachikwa jina la Kicheche!.

“Kitendo cha Richard kurejea nchini na kutoonana na mkewe, kilimkosesha raha ndiyo maana wakati akiongea na waandishi wa habari alisema atafanya kila awezalo kuhakikisha anampata na kweli amefanikiwa,”ilielezwa.

Hata hivyo, habari zaidi kutoka kwa mnyetishaji wetu zilisema kuwa baada ya Richard kumpata mkewe, ameamua kuishi naye kwa muda hotelini wakifurahia matunda ya ushindi alioupata.

“Ricki hivi sasa hana kinyongo tena na mumewe kwani amekuwa akienda kuwasalimia wakwe zake kisha kurejea hotelini, sasa roho ya Richard imetulia kwani alitueleza ushindi wake usingekuwa na maana bila kuwa na mkewe,” kilitanabahisha chanzo hicho.

Mshindi huyo wa BBA alikuwa katika mgogoro mkubwa na mkewe, kufuatia kuwa na uhusiano wa kimapenzi na Tatiana kutoka Angola ambao ulimkera Ricki ambaye inadaiwa aliamua kufungasha virago na kurudi kwao Canada.


 (Votes #: 6)
    (23 November 2007)
Soma Zaidi: 3067 | Maoni Yako (14)

Udaku Mwingine

ijumaa
 
  • Tatiana Richard mambo bado!
  • Mke wa Richard sasa asakwa
  • Ndoa ya Richard vululu vululu: Mke atoweka, Richard aweweseka.
  • Richard amuangukia mkewe
  • RICHARD TATIANA, WATESA
  •    

    #1 Author: masawengomanzito (23 November 2007 06:05)

    Nilijua watarudiana wale donge nono la BBA, mtoto wa kitasha sasa yupo kwenye hoteli ya nyota tano wakitumbua. Alipoona dalili za Rich kushinda ndio akarudi kama angetupwa asingerudi ng'o toka kwao kanada love tongue
     
    fast    

    #2 Author: jt (23 November 2007 07:15)

    plse translate us what is on the newspaper about the goldenboy the news of tanzania of today we want to hear???????????PLSE PLSE
     
    fast    

    #3 Author: UE (23 November 2007 07:18)

    Ricky, kama huyo Tatiana ni 'KICHECHE' usikubali hivi hivi mpaka mkapime ngoma, huwezi kujua labda Rich kashakanyaga grd ya taifa, ni balaa hiloo!!!
     
    fast    

    #4 Author: Solomon (23 November 2007 09:37)

    That is good to see you together again. Marriage is forever - for better for worse! It is important to be faithful among the couple anyway, Richard did stupid things and we should not remember and cling on them because he has regreted them. Good example! Others are claiming that Rick is after Rich´s money, this is absurd! Ridiculous! She married him when he had nothing, ofcourse she had something!! all was for love! Good!

     
    fast    

    #5 Author: Abdi Mkwizu (23 November 2007 11:04)

    Binafsi nimefurahishwa sana na uamuzi wa busara alioufanya Richard wa kumuomba msamaha mkewe na hivyo kufanya ndoa hiyo iendelee kama ilivyokuwa awali. Mengi yamesemwa dhidi ya Ricky. Lakini nasita kukubaliana na busara za watu wanaomlaumu Rick kuwa ni mbaguzi kwa kumwita Rich nguruwe. Tuache uswahili. Kama kweli Ricky alikuwa ni mbaguzi asingekubali kuolewa na mswahili ambaye alikuwa hana kitu. Itakuwa ni kupungukiwa busara kusema eti Ricky amerudi kwa Rich ili afaidi fedha alizoshinda.
     
    fast    

    #6 Author: meyl (23 November 2007 13:49)

    Ricki alimpenda richard alikuwa hana pesa na yeye mke wake ndo alimkubalia mke wake aende kwenye mashindano ya Big Brother sasa majungu ya nini tunafurahi wamerudiana waanze maisha mema yenye upendo zaidi nawatakia kila la kheri
     
    fast    

    #7 Author: nandy hope (23 November 2007 13:58)

    mmh, ila kama tatiana ni kicheche its better wakapima ngoma first,coz i heard walikwenda pekupeku,wapime kwanza!!!
     
    fast    

    #8 Author: kila66 (23 November 2007 18:04)

    Huyu dogo mbona mzuri sana kwa fingers... mzungu atatulia tu... Check mambo yake....
    http://www.youtube.com/watch?v=J2qEk-lZH1U
    http://www.youtube.com/watch?v=NEk1B6FfSzs
     
    fast    

    #9 Author: JULIE NAM (23 November 2007 20:11)

    SO RICHIANA FANS .. WE HAVE TO HIDE ... RICKY AND RICHARD BACK TOGETHER .. NO PHOTO OF THEM OR ANYTHING ...

    GIVE US PROOF .. WE DON'T BELIEVE IT ..THIS RUBBISH
     
    fast    

    #10 Author: cheri (23 November 2007 23:24)

    this wil never work riki is fooling herself after richi told everybody he is inlove wit tati will she be able to trust him again da housemates are going on tour soon is riki going with to keep a eye on richi boy and tati or is this just for da money riki u are a stupid fool that boy maried to young this will happen again

    julie nam
    same one 4rm BBstrap rihiana fan big time i also dont believe this bull would like some proof richi used tati he should be ashamed of himself he would never won money without our tati this will never work or is it about da money let be and let god
     
    fast    

    #11 Author: Maibob (24 November 2007 03:42)

    Richard and Ricki- Very very Exellent .Thank you guys for coming to such a conclusion.Richard bro please respect your wife.To Ricki thank you so much for taking our african boy back, i live in Canada ,Vancouver and i know that Canadians are are very good people.Sorry for what ever happened dear. Richard make us proud as we live here in Canada.
    God bless you guys.

    To you guys who are busy writing bad things, Please stop and leave them alone. Be real Africans brothers and sisters please i berg you.


    ooo thak God ,You guys belong together, Shame to the devils agents.wooooooooo.
     
    fast    

    #12 Author: UE (24 November 2007 06:58)

    Kila!! Nimeona finger Babake!! huyo mtoto wa kizungu ndio maana alichanyikiwa na Rich, maana Ofuneka hakumind hata kama tatiana alikuwa ubavuni, noma!!!!
    Jamani jimuvuzisheni kwenye hiyo glob hapo chini mtaona jinsi Rich alivyompagawisha Ofuneka wakati Tatiana yupo fofofo.
    www.youtube.com/watch?v=NEk1B6FfSzs
     
    fast    

    #13 Author: ebi (24 November 2007 18:56)

    i d like to see pix of richard and his wife together.
    If they are together, then the woman has a large heart and should come from delta state of nigeria.
    See ya rivhie boy.
    ebi Nigeria

    hi love to see richard and rickie pix

    pls get richard to write to me hear in nigeria
     
    fast    

    #14 Author: CECILIA (29 November 2007 09:49)

    Very interested to know anything concerning my favourite- Richard- unfortunately do not understand language. any english version please!!!
     
    fast    

    Add comments

    Name:
    E-mail:

    Code:
    Include security image CAPCHA.
    to renew the code
    Enter Code:

     

    Kura Yako / Poll

    Habari Katika Picha


    Gazeti la Uwazi



    Nani Yupo / Alikuwepo


    Home Page | About Us | Regista | Picha | Bongo Celebrities | Maoni | Contact Us

     hit counter

    counters

    2008 © globalpublisherstz.com