Tembelea... |
 |
Kalenda |
 |

Marafiki wetu |
 |
Habari Zilizopita |
 |



  
| |
 |
|
|
 |
 |
Arsenal, Man, Barca dimbani Ulaya
|
champion |
|
 |
Wakati ambapo Arsenal itasafiri hadi Hispania kumenyana na Sevilla ndugu zao Manchester United itakuwa nyumbani ikiikaribisha Sporting Lisbon ya Ureno.
Mechi hiyo ya Man United dhidi ya Sporting inatarajiwa kupigwa saa 4:45 kwa saa za Afrika ya Mashariki. Arsenal inayonolewa na Mfaransa, Arsene Wenger na Man United, Sir Alex Ferguson hazijawahi kupoteza mchezo hata mmoja tangu zimeanza mchakato wa kuwania tiketi ya kucheza hatua ya mtoano katika ligi hiyo.
Mechi nyingine ambayo itachezwa hiyo kesho itakuwa kati ya Lyon ya Ufaransa ambayo itakuwa wenyeji wa Barcelona ya Hispania.
Wajerumani, Stuttgart watakuwa na kibarua kigumu wakati watakapoikaribisha Rangers ya Uskochi huku mchezo mwingine ukizikutanisha Dynamo Kiev ambayo itakuwa nyumbani ikipepetana na AS Roma ya Italia.
CSKA Moscow ya Urusi kesho hiyo hiyo itakuwa nyumbani ikitoana jasho na PSV Eindhoven ya Uholanzi wakati ambapo Inter Milan ya Italia ikitoana jasho katika dimba lao na Fenerbahce.
Mchezo mwingine wa Ligi ya mabingwa utakaopigwa hiyo kesho utakuwa katika Steaua ya Romania ikimenyana katika uwanja wao wa nyumbani dhidi ya Slavia. Mechi nyingine zitakazopigwa wiki hii katika mfululizo wa ligi hiyo ni:-
Kesho kutwa Jumatano: Besiktas vs Marseille Liverpool vs Porto (4:45) usiku Rosenborg vs Chelsea Valencia vs Schalke 04 Werder Bremen vs Real Madrid Lazio vs Olympiacos Benfica vs AC Milan Celtic vs Shakhtar Doneski
|
|
 |
|
|
 |
Kura Yako / Poll |
 |
Habari Katika Picha |
|
 |

Nani Yupo / Alikuwepo |
 |
|