"Tulimualika Richard kupitia M-Net, tuliona yeye ni mmoja wa vijana jasiri kufuatia kitendo chake cha kukaa ndani ya jumba la Big Brother kwa siku 98 bila kufanya ngono licha ya vishawishi vingi, cha ajabu hatujapata jibu lolote na wala Richard mwenyewe hakuonekana,"alisema mmoja wa waratibu hao.
Kitendo cha Richard kukacha tamasha hilo kwasababu tu M-Net hawakumruhusu kimewaudhi wengi, huku baadhi wakisema kuwa, kwa kitendo hicho ushindi wake hauna faida yoyote kwa Taifa.
"Hivi ushindi wake utakuwa na faida gani kwa jamii kama kuwepo kwake tu kwenye shughuli kama hiyo ya kijamii kunakuwa na ugumu kiasi hicho.
"Asijione lulu kwa umaarufu alioupata, ni vyema kutovimba kichwa na kuanza kujihusisha katika shughuli za kijamii,"alisema Fred Leonard wa Magomeni jijini Dar es Salaam.
Naye Judica Limo wa Kurasini aliliambia Amani kuwa, licha ya kwamba watu wamekuwa wakimsema Richard kwa vitendo vichafu alivyokuwa akifanya ndani ya jumba la Big Brorher,bado kuhudhuria kwake katika tamasha hilo kulikuwa na umuhimu.
Mpaka tunakwenda mtamboni hatukufanikiwa kupata taarifa zozote rasmi za kwanini mshindi huyo wa BBA hakuweza kuhudhuria tamasha hilo na mpaka sasa kijana huyo ameendelea kukaa mafichoni akila raha na mkewe.
|