Tembelea... |
 |
Kalenda |
 |

Marafiki wetu |
 |
Habari Zilizopita |
 |



  
| |
 |
|
|
 |


 |
|
LUMBANGA AMRUKA PROFESA MAHALU
|
udaku |
|
|
 |
• Asema hakumtuma kuingia mikataba ununuzi wa jengo • Adai zilitengwa bilioni moja na si tatu.
ALIYEKUWA Katibu Mkuu Kiongozi, Marten Lumbanga (60), amemruka Balozi Costa Mahalu mahakamani akisema hakumtuma kuingia mikataba miwili ya ununuzi wa jengo la ubalozi wa Tanzania nchini Italia.
Lumbanga, ambaye kwa sasa ni Balozi wa Tanzania kwenye Umoja wa Mataifa nchini Uswisi, alidai hayo jana katika Mahakama ya hakimu Mkazi Kisutu, Dar es Salaam. Mbele ya Hakimu Mkazi mkuu Mfawidhi sivangilwa Mwangesi.
Madai hayo aliyatoa alipotoa ushaidi katika kesi ya kuhujumu uchumi na wizi wa zaidi ya sh. Bilioni mbili inayomkabili Profesa Mahalu, aliyekuwa Balozi wa Tanzania nchini Italia na aliyekuwa ofisa utawala wa ubalozi huo, Grace Martin,
Lumbago alidai akiwa katibu Kiongozi, alitumia nafasi hiyo kuishawishi serikali kununua jingo la ubalozi huo, baada ya Profesa Mahalu kwenda kumlalamikia kwamba anafanya kazi katika mazingira magumu.
Alidai Profesa Mahalu alimlalamikia kuwa hadi mtu afike kwenye ofisi za ubalozi, inabidi apite kwenye sebule ya nyumba ya mtu mwingine.
Lupanga alidai alichofanya yeye kutokana na malalamiko hayo ni kutoa pendekezo la kununuliwa kwa jengo la ubalozi.
Alidai hakuwahi kumpa maelekezo ya kuingia mikataba miwili katika ununuzi wa jingo hilo na hana taarifa zake, zaidi ya kesoma magazetini.
“Sikumpa maelekezo ya kuingia mikataba mwili na wala sihusiki na ununuzi wa jingo hilo.
“Nahusika kwa kuwa Mahalau alikuja ofisini kwangu kunipa habari za kusikitisha kwamba ukitaka kufika ofisini kwake lazima upite katika sebule ya mtu, nikatumia nafasi yangu kuishawishi serikali kwa kuwa kulikuwa na umuhimu wa kupata jengo, ili awe na mazingira mazuri ya kufanyia kazi,” alidai Lumbanga.
Akiongozwa na Mwendesha mashitaka wa Taasisi ya kuzuia na kupambana na Rushwa (TAKUKURU) , Joseph Hole, alidai baada ya ombi la Mahalu kukubaliwa, serikali ilitenga sh bilioni moja kwa ajili ya ununuzi wa jengo hilo, ingawa zilionekana hazitoshi kwa kuwa lilikuwa likiuzwa kwa sh. Bilioni tatu.
Balozi Lumbanga alidai baada ya kutolewa kwa fedha hizo, mwaka mmoja baadaye, Mahalu alimfuata na kumuomba amuunge mkono ili fedha ziongezwe, kwani kama angenunua jengo kwa sh. Bilioni tatu, angeweza kupata msamaha wa kodi.
Alidai alimueleza Mahalu kuwa suala la msamaha wa kodi si la serikali ya Tanzania hivyo ni vyema akawasiliana na serikali ya Italia ili asije kuvunja sheria za nchi hiyo.
Alihojiwa na wakili alex Mgongolwa anayewatetea akina Mahalu, Balozi Lumbanga alidai hakuwahi kupata taarifa zozote juu ya maandalizi ya ununuzi wa jengo hilo na mikataba miwili inayohusu ununuzi wake.
Lumbanga alizikana nakala alizokuwa akionyeshwa na Mgongolwa kwamba Novemba 11, mwaka 2005, alipata barua inayoonyesha Mahalu ameingia mikataba miwili ya ununuzi wa jengo la ubalozi kwa sh bilioni tatu.
“Hizi nakala sina kumbukumbu nazo na sijawahi kuziona wala hazijaletwa kwangu, labda kama zilipokewa na mtu mwingine, lakni si mimi,” alidai Lumbanga.
Alipoulizwa na Mgongolwa kuhusu kikao cha 39 cha Bunge kilichofanyika Agosti 3, 2004 kwamba Bunge lilithibitisha kuwa mkataba wa ununuzi wa jengo ni sh. Bilioni 2.9, Lumbanga alidai bajeti ya serikali ilikuwa ni sh bilioni moja na kama ziliongezwa zilikuwa jitihada za Maalu kutaka fedha nyingine za ununuzi wa jengo hilo.
Profesa Mahalu na Grace wanakabiliwa na mastaka sita ya kutoa taarifa za uongo ju ya ununuzi wa jengo la ubalozi mjini Roma , Italia kwa lengo la kumdanganya muajiri, kughushi, kuhujumu uchumi, wizi wa zaidi ya sh. Bilioni mbili na kusababisha hasara kwa serikali.
Kesi hiyo itaendelea kusikilizwa Machi 14, mwaka huu.
(Imetolewa na Uhuru Alhamisi, 28/2/2008)
|
|
 |
|
|
 |
Kura Yako / Poll |
 |
Habari Katika Picha |
|
 |

Nani Yupo / Alikuwepo |
 |
|