MAKAKATI WAO ULIANZA IKULU DESEMBA 2004
NYARAKA zilizopatikana kwa uchunguzi zinabainisha mbinu zilizotumiwa na Rais Mstaafu Benjamini Mkapa kwa kushirikiana na aliyekuwa Waziri wa Nishati na Madini, Daniel Yona kunyakua kifisadi Mgodi wa Makaa ya mawe wa Kiwira wakati ukiwa mali ya umma chini ya Shirika la Taifa na Maendeleo (NDC).

Nyaraka zimethibitisha wazi kwamba viongozi hao wawili wa serikali ya Awamu ya tatu ya Tanzania (1995-2005) walikula njama wakiwa Ikulu na kuunda kampeni yao binafsi iitwayo Tanpower Resources na kisha kuisajili rasmi Desemba 29, 2004, kabla ya kujinyakulia hisa binafsi nono katika Mgodi wa makaa ya Mawe wa Kiwira Mechi 2005.
Mgodi huo ulioko mkoani Mbeya hivi sasa unakamilisha mradi wenye thamani ya Dola za Marekani milioni 27.8 (takribani bilioini 340/-) wa kuzalisha umeme utakaouziwa Shirika la Taifa la Ugavi wa Umeme (Tanesco).
Kilikuwa ni kipindi kisichozidi miezi mitatu tu (Desemba 2004 hadi Mechi 2005) wao na kuwa matajiri wakubwa kwa kutumia Ikulu na nyadhifa walizodhaminiwa na umma wa wapiga-kura na walipa-Kodi wa Tanzania. Katka kutekeleza hatua hiyo Mkapa na Yona walihakikisha kampeni yao waliyosajili, inakuwa na wanahisa ambao ni familia zao, jamaa au marafiki wa karibu sana.
Nyaraka zinaonyesha kwamba mambo yalianza moto-moto kwa Daniel Yona kuandika barua akiwa Waziri wa Nishati na Madini mnamo Machi 24, 2005 kwa Evans Mpundi aliyepewa ukurugenzi katika kampuni yao – Tanpower Resources (T) Ltd. Namba CDA 48/171/01,
Yona anasema kwa Kiingereza “I am glad to inform you that the government has agreed to go into joint venture partnership with TanPower Resources (T) Ltd in managing and operating Kiwira Coal Mines Ltd, as outlined in your writen proposal.” Tafsiri yake: “Nina furaha kukuarifu kwamba Serikali imekubali kuwa na ubia na TanPower Resources (T) Ltd. Katika kumeneji na kuendesha kampuni ya Mgodi wa Kiwira.”
Yona anaendelea kwa Kiingereza katika barua yake akisema “As you are fully aware, ital and its expatriate as well as loal staff need to be paid and reassured of the future of the company,” Tafsiri yake: kama unavyofahamu fika KCML inahitaji mtaji, utaalamu na wafanyakazi wake wanahitaji kulipwa ili kuhakikishiwa mastakabali wa baadaye wa kampuni.”
Katika barua hiyo, Yona anasema serikali imeteua timu ya kufanya majadiliano na TanPower Resources jinsi ya kufanya mchakato huo kwa haraka kisheria na kitaalamu.
Barua inataja majina ya maofisa wa serikali walioteuliwa katika timu ya majadiliano kuwa ni: Ms A. Bukuku (Mwenyekiti); kaimu kamishna wa Madini, Omari Chambo; mtaalam wa ushauri wa PSRC (Parastatal Sector Reform Comminission), J.J. Ngelime; na wakili wa Serikali, B. Sahel.
Nakala za barua hiyo zimesambazwa kwa aliyekuwa Waziri wa Fedha Basil Mramba, aliyekuwa waziri wa Mipango na Ubinafsishaji Dk. Abdallah Kigoda, aliyekuwa Mwanasheria Mkuu Andrew Chenge, aliyekuwa Waziri wa Katibu Kiongozi Ikulu, Marten Lumbanga, aliyekuwa mwenyekiti wa PSRC JohnRubambe, na aliyekuwa Mwenyekiti wa KCML Rumisha Kimambo.
Katika mkataba wa ubia TanPower Resources imenyakua asilimia 70 ya hisa (na kuwa wamiliki)KCML.
Mkataba huo wa kifisadi ulisainiwa juni 8,2005, na Mwenyekiti PSRC Rubambe, \meneja wa KCML Adam Salim Abdu, na wakurugenzi wawili wa TanPower Resources (Evans Mapundi na Wilfred Malekia). Hatimaye TanPower Resources ilijinyakulia hisa zaidi hadi kufikia asilimia 85 na kuiahi Serikali asilimia 15 tu.

Nyaraka moja inaonyesha jinsi Evans mapundi alivyomuandikia barua Yona Januari 2005, akielezea dhamira ya “kampuni yake” (TanPower Resources) kuingia ubia na serikali katika kuendesha KCML kwa kuingiza mtaji wa bilioni 40.1/- kwa mwezi kwa kampuni kubwa tatu ambazo ni IPTL, Songes, Richmond na sasa Kiwira.
Wachambuzi wa masuala ya kifedha wamebainisha kwamba Tanesco itakuwa inajimaliza kwani itakuwa haina uwezo wa kulipa kiasi hicho. Mapato ya Tanesco kwa mwezi ni chini ya dola za Marekani milioni 19.25 (takriban bilioni 25/-)
Awali TanPower Resources ilisajiliwa na majina ya wakurugenzi waasisi watano ambao ni: Anna Mkapa (mke wa rais mtaafu), Daniel Yona, Nicholas Mkapa (mtoto wa rais mstaafu); Joseph Mbuna (baba mkwe wa Nicholas Mkapa) na Evans Mapundi. Baadaye katikati ya mwaka 2005 TanPower Resources ilinyakua hisa za asilimia 85 katika kampuni ya Kiwira Coal and Power Limited (KCML), na kuingia mkataba wenye utata na Tanesco wa kuuza umeme wa megawati 200 katika gridi ya umeme ya Taifa.
Kwa mujibu wa vyanzo vya habari vya kuaminika ndani ya serikali, kuna uwezekano wa kutokea athari kubwa katika mkataba huo na mradi wenyewe unaonekana kusuasua ingawa mkataba ulifanywa zaidi ya miezi 20 iliyopita.
Hofu waliyonayo watoa habari ni kwamba huenda mkataba huo ukaliingiza taifa katika gharama kuwa kwa seriikali na hatimaye kwa watumiaji umeme kama ilivyotokea kwa mradi tata wa IPTL mwaka 1995 na Richmond 2006. wanasema Tanesco huenda itaanza kulipa Kiwira Coal and Power Limited dola za Marekani milioni sita
(takriban bilioni 8/-) kila mwezi wakati itakapoanza kununua umeme huo ghali wa megawati 200 kwa mujibu wa mkataba. Hali hiyo itasababisha Tanesco kuwa na majukumu ya kulipa madeni yanayofikia dola za Marekani milioni 20 (takriban bilioni 26/-) kwa mwezi kwa kampuni kubwa tatu ambazo ni IPTL, Songas, Richmond na sasa Kiwira.
Wachambuzi wa masuala ya kifedha wamebainisha kwamba Tanesco itakuwa inajimaliza kwani itakuwa haina uwezo wa kulipa kiasi hicho. Mapato ya Tanesco kwa mwezi ni chini ya dola za Marekani milioni 19.25 (takriban bilioni 25/-)
(Imetolewa na Kulikoni, Jumatatu Machi 31, 2008)