arrowSet HomePage |arrowBookMark Us
right
lines

Global Publishers Tanzania- Uwazi » Articles for August 2008 Year

Tafuta  

Tembelea...

Kalenda

Gazeti la Ijumaa

Marafiki wetu

Habari Zilizopita

Soma Magazeti Yetu...

Gazeti la Risasi Mchanganyiko
Amani
Gazeti la Ijumaa Wikienda

Bongo Celebrities ...

 
Habari Zinazotamba Habari Mchanganyiko
» Mpenzi mwenye tabia hizi m ...
» (SIMULIZI ZA CHUMBANI) MDUA ...
» Mduara wa Mahaba (19)
» (SIMULIZI ZA CHUMBANI) MDUA ...
» Aisha Madinda: NGONO INANIU ...
» JACKLINE AMUANIKA ALIYEMTOA ...
» KANUMBA: NARGIS ALINITESA ...
» MIHELA YOTE HII!!
» Niliona kitu cha ajabu ...
» MUWAKUMBUKE WENZENU
» MAMA KAVUNJA UCHUMBA W ...
» Mateso ni lazima unapot ...
» MWISHO ATOA TAMKO
» THE BLOOD DEAL! -10

 

MEDIA BONANZA

photos  
MEDIA BONANZA
Mbunge wa Kinondoni Iddi Azan akisalimiana na mwandaaji wa Bonanza la Waandishi
wa Habari Mkurugenzi wa ASET Asha Baraka kabla ya kuanza kwa mchezo wa
kuvuta kamba kati ya waandishi kike na Mamisi Utalii leo katika viwanja vya Leaders

MEDIA BONANZA
Warembo wa Miss Utalii 2008 wakivuta kamba kushindana na waandishi wa
habari (hawapo pichani) katika shindano la kuvuta kamba katika Bonanza
la Wanahabari, Ma-mis hao walishinda raundi zote mbili

MEDIA BONANZA
Pamboja na Mkurugenzi wa Aset kuwapiga tafu waadhishi wa habari wa
kike katika mchezo wa kuvuta kamba haikusaidia kitu, kwani walishindwa!

MEDIA BONANZA
Ma-misi Utalii wakishangilia kwa furaha mara baada ya kuwashinda wandishi
wa habari wa kike wa vyombo mbalimbali katika mchezo wa kuvuta kamba.
Media Bonanza hufanyika kila mwaka na huwakutanisha waandishi wa habari wote nchini.
PICHA: Issa Mnally GPL
    (31 August 2008)
Views: 90 | Maoni (0) |

 

P- SQUARE WALIVYOWASHA MOTO DAR!

photos  
Usiku wa kuamkia leo kulifanyika onesho la muziki wa wasanii kutoka Nigeria wanaojiita P-SQUARE
ambao wanatamba hivi sasa ni kabao chao kikali cha DO ME. Wasanii hao, Peter na Paul Okoye
ambao ni pacha, walipagawisha vilivyo mashabiki waliofurika kwenye viwanja vya LEADERS CLUB
usiku wa kuamkia leo. Onesho hilo la kufana liliandaliwa na EAST AFRICA RADIO/CHANNEL 5 za
jijini Dar es salaam. Picha zifuatazo zilizopigwa na mpiga picha mkuu wa GPL, RICHARD BUKOS
zinajieleza zenyewe...

P- SQUARE WALIVYOWASHA MOTO DAR!

P- SQUARE WALIVYOWASHA MOTO DAR!

P- SQUARE WALIVYOWASHA MOTO DAR!

P- SQUARE WALIVYOWASHA MOTO DAR!

P- SQUARE WALIVYOWASHA MOTO DAR!

P- SQUARE WALIVYOWASHA MOTO DAR!
P-SQUARE katika picha ya pozi
    (31 August 2008)
Views: 488 | Maoni (2) |

 

MZEE WA PAMBA

photos  
VUNJA JUNGU DAR, BALAA
MZEE WA PAMBA
Mdau maarufu wa bendi ya Akudo Impact Pius Luta maarufu kama Mzee wa Pamba akiyarudi
na mashabiki waliofika katika Ukumbi wa Vatican City jijini Dar es Salaam usiku wa kuamkia
leo katika onesho la maalum la vunja jungu.
PICHA : RICHARD BUKOS NA CHRISTOPHER LISSA / GPL
    (30 August 2008)
Views: 210 | Maoni (2) |

 

KINGA YAZUA BALAA!

risasi jumamosi  
KINGA YAZUA BALAA! Baadhi ya wanafunzi wa Shule ya Msingi Mwembesonga iliyopo Morogoro mjini wakimkimbiza hospitalini mwenzao Happiness Gaitani wa Darasa la 4 A baada ya kulegea na kupoteza fahamu muda mfupi alipopewa dawa za kinga ya kichocho na minyoo
PICHA NA DUSTAN SHEKIDELE/ GPL
    (30 August 2008)
Views: 137 | Maoni (0) |

 

Khadija Kopa apigwa ndoa

risasi jumamosi  
Khadija Kopa apigwa ndoa Na Christopher Lissa
Malikia wa muziki wa taarabu nchini Khadija Kopa amefunga ndoa ya tatu na mwanaume aliyefahamika kwa jina moja la Jafari ambaye anaonekana kuwa mdogo kiumri yaani “Kiserengeti boy’...
    (30 August 2008)
Views: 1771 | Maoni (21) | Soma Zaidi

 

Spika Sitta amzimikia K-Lyin

risasi jumamosi  
Spika Sitta amzimikia K-Lyin Na Hawa Mkombozi
Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Samweli Sitta, Jumanne, Agosti 26, mwaka huu, alisema kuwa anamzimikia sana mwanadada Jacqueline Ntuyabaliwe maarufu kama ‘K-lyin’ kwa mashairi na sauti yake tamu ya kuvutia...

    (30 August 2008)
Views: 572 | Maoni (5) | Soma Zaidi

 

Mzee Yusuf kuongeza wake wawili

risasi jumamosi  
Mzee Yusuf kuongeza wake wawili Na Christopher Lissa
Nguli wa muziki wa mipasho nchini wa Kundi la Jahazi Modern Taarab ‘Wana wa nakshi nakshi’ Mzee Yusuf ameibuka na kudai kuwa ana uwezo wa kuongeza wanawake wawili zaidi kwani bado ana uwezo wa kuwamudu...
    (30 August 2008)
Views: 568 | Maoni (7) | Soma Zaidi

 

Wasanii Jumba la dhahabu wasakwa

risasi jumamosi  
Wasanii Jumba la dhahabu wasakwa Na Rhobi Chacha
Baadhi ya wasanii wa Kundi la Fukuto Arts Promotion lililokuwa likirusha mchezo wake kwenye Kituo cha luninga cha TBC1 uliojulikana kwa jina la Jumba la dhahabu, wanasakwa na Polisi kwa kumtapeli kijana Moriss Lucas anayejulikana kwa jina la ‘Young Bilionaire’...

    (30 August 2008)
Views: 361 | Maoni (1) | Soma Zaidi

 

Mtumwa wa ngono (24)

hadithi za Shigongo  
Kutoka utumwa wa ngono hadi kuwa nguli wa masuala ya Mitindo nchini Uingereza, haikuwa kazi ndogo. Dina amepita kwenye milima mingi lakini hatimaye akafanikiwa maishani, pato lake la kwanza baada ya kuingia mkataba na kampuni iliyomwibua ya England Modelling Agency (EMA) ilikuwa ni paundi milioni mbili, zaidi ya shilingi milioni mianne za Kitanzania. Kitu cha kwanza alichokifanya baada ya kupata mkabata huo, ni kuamua kusafiri kwenda Afrika Kusini kwenye mji wa Johannesburg alikokuwa akiishi kabla ya kwenda Uingereza. Anataka kwenda kutoa shukrani zake lakini pia kumtafuta John Kamau, mpenzi wake waliyepotezana muda mrefu.

Nje ya uwanja wa ndege, anakutana na Madame Modesta, mwanamke aliyeishi naye ndani akimtesa na kumfanya mtumwa wa ngono akiwa amefungwa minyororo! Hasira zinampanda Dina na kujikuta akitamani hata kumpiga risasi. Baadaye wanaongea na kusameheana, ndipo mwanamke huyo huyo akampa siri ya mahali John Kamau alipo, kwamba yupo kwenye gereza la Posmo katika Jiji la Capetown.

Dina anasafiri hadi kufika mbele ya gereza hilo lakini wakati anatembea kwa miguu kuelekea sehemu ya kuingilia, maaskari walijitokeza na kumweka chini ya ulinzi wakimwambia anashtakiwa kwa kosa la mauaji! Kichwani mwake hana kumbukumbu kabisa kama amewahi kuua akiwa nchini humo, amekosa kitu cha kujibu. Je, nini kitaendelea? SONGA NAYO…
    (30 August 2008)
Views: 599 | Maoni (4) | Soma Zaidi

 

Unakufa Nikikuona-2

Mikasa ya kusisimus  
Msako mkali wa kumtafuta Patrick au Patii kama alivyojulikana na wengi unaendelea. Pamoja na Wapelelezi wenye uzoefu wa muda mrefu kumfuatilia, hakuna aliyefanikiwa kumtia mikononi zaidi ya kuambulia kifo! Tayari ameshaua Wapelelezi wanne; Peter, James, Anna na Mabesha.

Sasa Mkuu wa Kitengo cha Upelelezi, Makao Makuu Moses Lupango, anawaagiza Wapelelezi Joel na Pius kumfuatilia kwa mara nyingine nchini Uingereza. Joe alipofika nyumbani, kabla ya kumueleza mkewe tayari alishahisi kwamba alitakiwa kusafiri, akapingana naye kwa nguvu zote. Joel akabaki njia panda! Je, Joe atamsikiliza mkewe au atatimiza majukumu yake ya kikazi? Mtunzi JOSEPH SHALUWA anaendelea...
    (30 August 2008)
Views: 516 | Maoni (2) | Soma Zaidi

 

Ndoa na changamoto zake!-2

Mahaba  
Ndoa na changamoto zake!-2 ...Wengi wanashindwa kukabiliana nazo
Sina shaka mambo yenu ni mazuri wasomaji wangu wapenzi na mnaendelea kutimiza majukumu yenu ya kila siku vyema kabisa. Kwa upande wangu mimi ni mzima wa afya njema kwa msaada wa Mungu wa Mbinguni...

    (30 August 2008)
Views: 220 | Maoni (1) | Soma Zaidi

 

NEW BBC CHANNELS!

udaku  
Good afternoon all

We are delighted to announce BBC commitment to Africa with launch of new branded channels

BBC Worldwide Channels pledged its commitment to the African market recently as plans were announced to launch a suite of BBC-branded thematic channels into the region. The channels will be available via MultiChoice’s DStv platform, Africa’s leading television provider, from 1 September 2008*

The new thematic channels - BBC Entertainment, BBC Knowledge, BBC Lifestyle and CBeebies - will replace and build on the success of existing channels BBC Food and BBC Prime, enabling viewers to access even more of the award-winning and high-quality programming from the BBC.

BBC Channels will be made available on channel 306 to all DStv Premium subscribers on the 01 September 2008 at 06:00 CAT

Regards,

Lucy Kiwhele
PUBLIC RELATION MANAGER
MULTICHOICE TANZANIA LTD
    (29 August 2008)
Views: 46 | Maoni (0) |

 

VIATU VYA CHACHA WANGWE VITANIKAA !

photos  
Job Chacha (katikati) ambaye ni Wakili wa Mahakama Kuu ya Tanzania akiongea na Waandishi wa Habari katika Ukumbi wa Idara ya Habari (MAELEZO) Jijini Dar es Salaam leo juu ya azma yake ya kuwania kiti cha ubunge Jimbo la Tarime kwa tiketi ya Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA). Kiti hicho kiko wazi kufuatia kifo cha aliyekuwa akikikalia marehemu Chacha Wangwe,kushoto kwake ni Afisa wa Idara MAELEZO Sise Mwirabi na kulia ni mpambe wake.
 VIATU VYA CHACHA  WANGWE VITANIKAA !

LAZIMA MTU AFE PALE DDC!
 VIATU VYA CHACHA  WANGWE VITANIKAA !
Mkurugenzi wa Kampuni ya Dynamite Promotions INC Shomari Kimbau (Katikati) akiwa tambulisha mabondia Ramadhani Miyeyusho (kushoto) na Selemani Said ‘tall’ ambao watatwangana Agosti 30 mwaka huu ndani ya ukumbi wa DDC Mlimani Jijini Dar es Salaam kuwania ubingwa wa Tanzania ‘Welterweight Title’

BONGO TAABU HATA KWA MAGARI
 VIATU VYA CHACHA  WANGWE VITANIKAA !
Kufuatia ubovu wa miundombinu hususan ya kupitishia maji taka, leo mchana kamera yetu iliyanasa magari yakipita kwa taabu katika Barabara ya Uhuru Jijini Dar es Salaam kutokana na mvua za rasharasha zilizoanza kunyesha.
PICHA :CHRISTOPHER LISSA NA RICHARD BUKOS / GPL
    (29 August 2008)
Views: 146 | Maoni (0) |

 

NAFASI ZA KAZI NA ZABUNI

classified ads  
POSITION: Programme assistant
QUALIFICATION: Secondary education, with a diploma/ advanced diploma in business/ public administration/ Human Resources Management. A first degree In business or public administration, edonomics, political science and social sciences would be advantageous, but not a stiff requirements. At least 3 to 5 years of progressive administrative, human resources, or programme experience
APPLY TO: Development support Serveces Unit, UNDP,
P.O.BOX 9182 Dar es Salaam
DEADLINE; 5th September 2008
PUBLICATION: 21st August 2008 Daily News....
    (29 August 2008)
Views: 0 | Maoni (0) | Soma Zaidi

 

NAFASI ZA KAZI NA ZABUNI

classified ads  
POSITION: Programme assistant
QUALIFICATION: Secondary education, with a diploma/ advanced diploma in business/ public administration/ Human Resources Management. A first degree In business or public administration, edonomics, political science and social sciences would be advantageous, but not a stiff requirements. At least 3 to 5 years of progressive administrative, human resources, or programme experience
APPLY TO: Development support Serveces Unit, UNDP,
P.O.BOX 9182 Dar es Salaam
DEADLINE; 5th September 2008
PUBLICATION: 21st August 2008 Daily News....
    (29 August 2008)
Views: 0 | Maoni (0) | Soma Zaidi
Back  <<  1 2 3 ... 21 22 23  >>  Next Page
 

Kura Yako / Poll

Habari Katika Picha


Gazeti la Uwazi


Nani Yupo / Alikuwepo


Home Page | About Us |