Tembelea... |
 |
Kalenda |
 |

Marafiki wetu |
 |
Habari Zilizopita |
 |



  
| |
 |
|
|
 |
 |
|
NEC YALIA NA UCHAGUZI KWA WANGWE!
|
photos |
|
|
 |
 Tume ya Taifa ya Uchaguzi (NEC) imeelezea kufadhaiashwa na kusikitishwa na taarifa za matukio yanayotishia amani katika kampeni za uchaguzi mdogo wa Ubunge katika Jimbo la Tarime. Mwenyekiti wa Tume hiyo Jaji Lewis Makame amewaeleza waandishi wa habari mapema hii leo Jijini Dar es Salaam kuwa, NEC imepata taarifa za kuwepo kwa matukio hayo ikiwa ni pamoja na kuumizwa kwa viongozi wa vyama vya siasa na wananchi pamoja na vitisho,uchochezi na lugha za matusi hali ambayo ameonya kuwa haitavumiliwa na Tume yake. ?Ikumbukwe kwamba vitendo hivyo ni ukiukwaji wa sheria na endapo wanaouhusika watabainika hatua za kisheria zitachukuliwa dhidi yao?alionya Jaji Makame.Pichani kushoto Jaji Makame akifafanua jambo alipokuwa anaongea katika mkutano huo na waandishi wa habari. MUFTI MKUU WA TANZANIA ABURUZWA MAHAKAMA KUU! Mufti Mkuu wa Tanzania Sheikh Issa bin Simba pamoja na baadhi ya viongozi wa Baraza Kuu la Waislam Tanzania (BAKWATA) leo wameburuzwa katika Mahakama Kuu ya Tanzania kwa tuhuma mbalimbali ikiwa ni pamoja na kuwafukuza baadhi ya viongozi waandamizi wa Baraza hilo. Hata hivyo Mufti hakufika mahakamani hapo na badala yake aliwakilishwa na Wakili wake Alhaji Said Elmaamry.Kesi hiyo Namba 592008 iko mbele ya Jaji Projesta Rugazia. Hata hivyo kesi hiyo ilikwama kidogo kutokana na hati za upande wa mashitaka zilizofikishwa mahakamani hapo kuwa na kasoro nyingi na hivyo kuilazimisha mahakama kuuamuru upande wa mashitaka kuwasilisha hati nyingine zilizo sahihishwa. Sambamba na Mufti kesi hiyo pia inaihusu Bodi ya wadhamini wa BAKWATA. ambapo Masheikh wanaomshitaki Mufti ni aliyekuwa naibu Muft Abubakar Zuberi, Sheikh Mataka, Sheikh Chizenga, Sheihk Hamid, Sheikh Abdul Yusuf na wengine ambao wanadai walitimuliwa na BAKWATA kinyume cha sheria. Pichani Wakili wa kesi hiyo El Maamry (kulia) akibadilishana mawazo na baadhi ya mashekh walalamikaji katika kesi hiyo (kushoto ni Sheikh Shaban Maaka) PICHA NA CHRISTOPHER LISSA/GPL |
|
 |

 |
|
 |
Msichana tajiri Priscilla amempenda mlemavu aitwaye Muddy. Wote wana historia zao mbaya za maisha na hawafahamiani vizuri!
MUDDY: Huyu ni yatima aliyelelewa na bibi yake aliyemtesa sana mpaka akafikia uamuzi wa kutorokea Dar es Salaam ambako alijiunga na kundi la majambazi waitwao Komandoo Yosso lililopanga kumtumia kuwa anaingia ndani ya nyumba na kufungua milango kwa sababu ya umbile lake dogo, tukio la kwanza tu kushirikishwa halikuzaa matunda, maaskari waliwazunguka na kuwakamata wenzake wote isipokuwa kiongozi wao Tom Kundea aliyefanikiwa kuondoka eneo la tukio akiwa na Muddy kwenye buti ya gari.
Eneo la Tazara gari lake lilizingirwa na maaskari, akamiminiwa risasi nyingi lakini baadaye ikagundulika alikuwa bado hajafa, hivyo akakimbizwa hospitali ya Amana. Hakuna aliyeelewa kwamba ndani ya buti kuna mtu, gari likavutwa mpaka kituo cha Polisi ambako usiku Muddy alibetua na kutoka kisha kutambaa hadi Stesheni ya Tazara, akapanda kwenye treni akiamini ni ya reli ya kati ili arudi nyumbani kwao Kilosa, baadaye akagundua alikuwa amepanda treni ielekeayo Zambia akiwa tayari amekwishavuka mpaka.
Mzee Kantalamba waliyesafiri naye anajitolea kumchukua na kwenda naye nyumbani kwake Porini kabisa, huko ndiko Muddy anagundua kwamba mzee huyo alikuwa ni mganga wa tiba za Jadi. Amelipenda eneo hilo na anaamini atajificha hapo kwa miaka mingi bila kukamatwa.
PRISCILLA. Priscilla anafiwa na mwanamke aliyeamini kwamba ni mama yake kumbe haikuwa hivyo, mama yake mzazi alikufa kwa kuvuja damu nyingi wakati wa kujifungua, lakini hakuna aliyemwambia jambo hilo. Baada ya mazishi ya bibi aliyeamini kwamba ni mama yake yaliyofanyika mjini Moshi kwa msaada wa Halmashauri ya mji, mwanamke mmoja anajitokeza kumchukua kwenda kuishi naye nyumbani kwake, huko ndiko Priscilla amegundua kwamba mwanamke huyo ni msagaji, alitaka kumgeuza mke wake. Uamuzi alioufikia ni kutoroka.
Akipita gizani usiku huo anasikia watu wakiimba kanisani, anasogea karibu na kuingia ndani kwani amegundua ni siku ya Mkesha wa Pasaka, ameketi nyuma kabisa akiwaza, mahubiri hayamwingii kichwani mwake kabisa. Ibada ilipokwisha alimfuata Mchungaji na kumsimulia historia yake, kwa huruma Mchungaji huyo alimchukua na kwenda kumtambulisha kwa mke wake, huo ndio ukawa mwanzo wa kuishi nao, wakamchukulia kama mtoto wao na kumpeleka shule.
Priscilla akaanza kufurahia maisha lakini baadaye mke wa Mchungaji alipata nafasi ya kwenda kusoma mjini Nairobi, akawaacha wawili tu ndani ya nyumba, Priscilla hakuwa na wasiwasi wowote akiamini Robert Njenga alikuwa ni mtumishi wa Mungu na alimpenda na kumchukulia kama mtoto wake hivyo asingeweza kumdhuru.
Mchungaji akaanzisha utaratibu wa kutengeneza juisi nzuri kila siku jioni lakini Priscilla alipokunywa juisi hiyo alihisi kupata usingizi wa ajabu, akalala bila hata kujiegeuza na alipoamka asubuhi kwenda kujisaidia chooni, sehemu ya haja kubwa ilikuwa ikimuuma kupita kiasi, alikuwa amechanika na hakufahamu kilichomchana kwani kabla ya kulala hakuwa na tatizo hilo. Wasiwasi mwingi ulimwingi lakini hawezi kumuuliza Mchungaji Robert. Je, nini kitaendelea katika maisha ya watu hao wawili? SONGA NAYO?
|
|
 |
|
|
 |
Kura Yako / Poll |
 |
Habari Katika Picha |
|
 |

Nani Yupo / Alikuwepo |
 |
|