Tembelea... |
 |
Kalenda |
 |

Marafiki wetu |
 |
Habari Zilizopita |
 |



  
| |
 |
|
|
 |
 |
|
Washindi wa Droo ndogo ya Shinda Benz wapatikana
|
photos |
|
|
 |
Washindi watatu wa droo ndogo ya kwanza katika Bahati nasibu ya Shinda Benz au Mitisubishi Pajero inayoendeshwa na Kampuni ya Global Publishers & General Enterprises Ltd wamepatikana. Washindi hao ni Bi.Zubeda Mkangumbe aliyejishindia seti ya Sofa za kisasa, Hamida Kissere aliyejishindia kabati la nguo na Iluminata V.Bunga aliyeondoka na Dressing table. Droo hiyo ilichezeshwa jana katika viwanja vya Bakhresa Manzese Jijini Dar es Salaam na kushuhudiwa na mamia ya wananchi pamoja na maofisa kutoka Bodi ya michezo ya Bahati nasibu nchini ambao ni Bakari Maggid na Emmanuel John Ndaki. Akizungumza mara baada ya kutangazwa majina ya washindi hao, Meneja Mkuu wa Global Publishers Abdalah Mrisho alitoa wito kwa wananchi kuendelea kutuma kuponi zao ili kuweza kujishindia zawadi kemkem ambazo zitapatikana katika droo zingine zinazotarajiwa kufanyika hivi karibuni. ?Pamoja na zawadi nyingi ambazo tunatarajia kutoa, lakini zawadi kubwa ni gari mbili aina ya Mercedes Benz na Mitsubish Pajero.Tunaomba wasomaji wetu waendelee kutuma kuponi kwa wingi ili kujiwekea nafasi nzuri ya kushinda?alisema Meneja huyo. Zifuatazo ni baadhi ya picha za matukio ya wakati wa uchezaji droo hiyo  Baadhi ya wananchi wakichanganya Kuponi tayari kwa kuchagua washindi.  Msanii mahiri aitwaye Wabojo alitoa burudani safi wakati wa droo hiyo  Mhariri mshauri wa gazeti la Uwazi Elvan Stambuli akimkabidhi mwanadada huyu kitabu cha hadithi ya Machozi na Damu baada ya msichana huyu kujibu swali kwa ufasaha.  Wanenguaji hawa Veronica Stepahano?Chichinaa? na Abdul Nohamed wakisindikiza droo hiyo.  Meneja Mkuu wa kampuni ya Global Publishers Abdalah Mrisho akiongea na waandishi wa habari mara baada ya kutangazwa kwa washindi katika droo hiyo. SALUNI POPOTE PALE! Vijana hawa walinaswa na kamera yetu maeneo ya Manzese Jijini Dar es Salaam wakinyoana nywele mtaani.Hali ngumu ya maisha inasababisha watu wengi kushindwa kumudu gharama ya Saluni. Picha zote na Christopher Lissa |
|
 |

 |
|
 |
Sato, binti mwenye sura ya kuvutia mfanyakazi wa kampuni ya ukaguzi wa mahesabu ya NACL, mchumba wa kijana aitwaye Greyson ambaye wanafanya kazi ofisi moja anaugua kikohozi na kuamua kwenda hospitali ambako daktari bingwa wa magonjwa ya moyo Dk. Terrence Kisendi amegundua Sato ana tatizo kwenye moyo wake na kuamua kumfanyia upasuaji. Ingawa Sato alibisha sana mwanzoni akidai hakuwa na tatizo la moyo, ushawishi wa Greyson ulimfanya akubali kupasuliwa kwani kulikuwa na siku chache tu mbele kabla hawajafunga ndoa na hakutaka siku ya harusi wapate matatizo! Kwa shingo upande Sato akakubali na kuingia chumba cha upasuaji akiamini angetoka salama lakini haikuwa hivyo, akafa akiwa juu ya meza ya upasuaji!
Baada ya kifo chake, Dk. Terrence alimkabidhi kijana mmoja aitwaye Albert kisanduku na kumwamuru akikimbize uwanja wa ndege wa Mwanza ambako alikabidhi kisanduku hicho kwa rubani wa ndege iliyokuwa imekuja mjini humo kubeba minofu ya samaki, baada ya kukabidhi naye alipewa kisanduku kingine na kuondoka nacho hadi nyumbani kwa Terrence ambaye alikipokea na kukuta kuna maburungutu ya dola, akachukua kiasi kidogo na kumkabidhi Albert ambaye aliondoka, mbele kidogo akapata ajali ya gari na kufa.
Kifo cha Sato kilipokelewa kwa mshtuko mkubwa sana familia yake, haikuwa tayari hata kidogo kukubali kwamba kilikuwa ni cha kawaida, ikabidi waombe mwili wake ufanyiwe uchunguzi ili kujua kilichomuua. Wizara ya Afya ikamteua Dk. Bernadetha Ndadayo kuifanya kazi hiyo, tayari amemaliza na anaingia kwenye chumba cha mikutano kusoma matokeo ya uchunguzi huo, alipoanza kusona kidogo kikohozi kikamshika. Je, nini kitaendelea? SONGA NAYOÖ
|
|
 |

 |
|
TWANGA WAIBUKA NA STAILI MPYA
|
photos |
|
|
 |
Bendi ya African Stars 'Twanga Pepeta International' usiku wa kuamkia leo walitambulisha staili mpya ya uchezaji hiitwayo 'kisigino' katika ukumbi wa Mango Garden jijini Dar es Salaam kama wanenguaji wa bendi hiyo wanavyoonekana pichani baada ya kunaswa na kamera yetu. MI' MTU MZIMA DOGO MOTO WANGU HUUWEZI Muimbaji wa African Stars 'Twanga Pepeta International' Saleh Kupaza licha ya utu uzima alionao lakini kiuno chake balaa, pichani akishindana na kunengua na mnenguaji wa bendi hiyo Abilahi Saleh Zungu aliye kushoto. KUPAZA UMETUKUNA MI' NA MKE WANGU Muimbaji wa Twanga Saleh kupaza akipewa 'hi' na shabiki mmoja alifika na mkewe katika ukumbi wa Mango Garden waliofika kuhudhuria onesho maalum la usiku wa Zain baada ya kuwakuna kwa minenguo yake. PICHA ZOTE NA RICHARD BUKOS / GPL |
|
 |
|
|
 |
Kura Yako / Poll |
 |
Habari Katika Picha |
|
 |

Nani Yupo / Alikuwepo |
 |
|