Yanga ilianza kampeni za kutetea taji lake kwa kuichapa Prisons mabao 4-0, huku ikiutumia mchezo wa kesho kama mwendelezo wa furaha yao ya kuwabamiza mahasimu wao Simba bao 1-0 na kuwa timu peeke katika mzuguko huo kucheza mechi 10 na kupoteza mchezo mmoja tu dhidi ya Kagera Sugar.
Kocha wa Yanga, Dusan Kondic(Pichani chini) alisema mchezo wa kesho anauchukulia kwa uzito mkubwa pamoja na kwamba atakuwa anacheza na timu ambayo inaburuza mkia.
Kondic ambaye ameiwezesha Yanga kushinda michezo tisa kati ya 10, alisema pamoja na kwamba wataingia katika Uwanja wa Jamhuri wakiwa na kumbukumbu nzuri ya kuwabamiza watani wao Simba bao 1-0, hawatawadharau maafande hao.
Iwapo Yanga itaibwaga Polisi Moro katika mchezo wa kesho, itafikisha pointi 30 na kumaliza mzunguko wa kwanza ikiwa kileleni mwa ligi hiyo huku ikifuatiwa kwa karibu na Kagera Sugar, inayoshika nafasi ya pili kwa kuwa na pointi 22 na Mtibwa yenye pointi 17 ikiwa nafasi ya tatu.
Watoto hao wa Jangwani watajitupa uwanjani huku afya ya mfadhili wao, Yusuf Manji ikiwa tete baada ya kuugua ghafla siku chache baada ya mchezo dhidi ya watani wao wa Jadi Simba.
Mwenyekiti wa Yanga, Iman Madega aliliambia Championi Ijumaa kuwa hali ya Manji ilibadilika ghafla juzi mchana na kukimbizwa katika Hospitali ya Aga Khan ambapo taarifa zinasema kuwa muda wowote jana angepelekwa kutibiwa nje ya nchi.
Aidha uongozi wa Yanga umewaomba wanachama na wapenzi wa timu hiyo kuwa na utulivu wa hali ya juu kipindi hiki ambacho wanaendelea kufuatilia kwa
|