Madai dhidi ya mwanamuziki huyo, yametolewa na baadhi ya ndugu na marafiki zake ambao waliomba hifadhi ya majina yao, kufuatia kuishi na Mmarekani huyo kwa kipindi hicho.
Mwanamuziki huyo, anayetamba na wimbo wake mpya wa Sister Sister, aliomshirikisha Judith Wambura ?Lady Jaydee? alirushiwa kijembe hicho hivi karibuni.
?Kitendo cha kuishi na kuishi na bwanake huyo kwa muda wa miaka mitano bila kumuoa ni uzinzi,? alisema mtoa habari wetu huyo kutoka Arusha, alipoongea na Risasi kwa simu, kwa sharti la kutotajwa jina lake gazetini.
Kwa mujibu wa ndugu huyo, Nakaaya na huyo mwanaume wanaishi nje ya mji wa Arusha na bado hawajafanikiwa kupata watoto hadi sasa.
Chanzo hicho kilizidi kusema kuwa, licha ya bwana huyo kufahamika nyumbani kwa Nakaaya, lakini bado hajatangaza ndoa na hivyo kuwatia mashaka wanafamilia.
?Hatumkatazi Nakaaya kuishi na mwanaume wake, lakini tunachochukia ni wawili hao kuishi bila kuoana kwani ni kosa kwa dini zote,? alisema mtu huyo aliyejiita mwanafamilia.
Mwanamuziki huyo mwenye makazi halisi Arusha, hupenda kutembelea jijini Dar es Salaam kwa ajili ya kazi zake za muziki, amepanga chumba Sinza Lion ambapo hufikia akiwa na mchumba wake huyo.
Katika mahojiano maalumu aliyowahi kuyafanya siku za nyuma na mwandishi wetu, Nakaaya alisema kuwa kutamka kuhusu ndoa ni jukumu la mwanaume.
?Unajua kuwa suala la kuolewa, mwanaume ndiye anatakiwa aseme mwenyewe, hivyo kama bado hajaamua kusema sio vizuri kumlazimisha,? alisema Nakaaya.
|