arrowSet HomePage |arrowBookMark Us
right
lines

Global Publishers Tanzania- Uwazi » ijumaa » MPAKANJIA: Nimechoshwa na Aisha Bui

Tafuta  

Tembelea...

Kalenda

Gazeti la Ijumaa

Marafiki wetu

Habari Zilizopita

Soma Magazeti Yetu...

Gazeti la Risasi Mchanganyiko
Amani
Gazeti la Ijumaa Wikienda

Bongo Celebrities ...

 
Habari Zinazotamba Habari Mchanganyiko
» Mpenzi mwenye tabia hizi m ...
» (SIMULIZI ZA CHUMBANI) MDUA ...
» Mduara wa Mahaba (19)
» (SIMULIZI ZA CHUMBANI) MDUA ...
» Aisha Madinda: NGONO INANIU ...
» JACKLINE AMUANIKA ALIYEMTOA ...
» KANUMBA: NARGIS ALINITESA ...
» BALLALI
» SirI 6 za kujua undani ...
» FROM CHINI WITH TRUE LO ...
» NJIA NYEPESI ZA KUTEKA ...
» MKURUGENZI ZAIN KUTOA ...
» Maximo akiri...
» Pampula

MPAKANJIA: Nimechoshwa na Aisha Bui

ijumaa

Akiongea na Ijumaa, Mpakanjia au maarufu kama ‘Meddy’, amesema kuwa, aliachana na Aisha Bui siku nyingi hata kabla Amina hajafariki dunia tofauti na baadhi ya watu wanavyofikiria kwamba aliishi naye kwa muda.

Meddy aliyasema hayo alipoulizwa na waandishi wa habari hii kuhusu tuhuma zinazomwandama kwamba, alimuoa Aisha na kumpangia nyumba Mwenge, jijini Dar na baadaye kumtelekeza huku akijua msichana huyo aliaharibu uhusiano wake na baba yake mzazi kwa sababu yake.

Aidha, Meddy aliendelea kuweka wazi kuwa, kikubwa kilichomfanya ampige chini Aisha ni tabia ya ukorofi ambayo yeye alishindwa kuitibu licha ya kumtaka kila wakati abadilike.

“Mimi sijamtelekeza Aisha, ila tabia yake ya ukorofi ndiyo iliyonifanya nitengane naye. Huyo mwanamke ni mkorofi, mkorofi balaa. Si nyinyi wenyewe mliona alivyowatoa baruti na kisu mlipokwenda kumhoji?” Alisema Mpakanjia.

Akionekana hajapendezwa na habari za kudaiwa kumtelekeza Aisha, Mwenge toka kwao Kigamboni, Meddy alisasambua kuwa, kutokana na ukorofi huo, alimtema Aisha hata kabla Amina hajafariki dunia.

Akasema kuwa, aliamua kuchukua hatua hiyo mapema ili kuepusha shari na kwamba, mpaka sasa hana mchumba na ni yeye mwenyewe atakayeamua aishi na yupi lakini siyo Aisha.

Hata hivyo, katika hali ambayo haikutegemewa, Meddy alitoa matamshi yaliyorudisha mambo nyuma pale aliposema kuwa, mpaka anammwaga chini Aisha, hakuwa amefunga naye ndoa kama wengi walivyompakazia.
“Mimi sikuwahi kufunga ndoa na Aisha, naapa! Watu walinipakazia tu,” alisema Mpakanjia ambaye katika siku za hivi karibuni ameonekana kufungua mambo yaliyofungika kuhusu maisha yake na Amina na Aisha.

Meddy aliongeza kuwa, kuna habari amekuwa akizisikia zikisemwa juu yake, pia amashasikia kwamba, Aisha ana kidume kingine chenye asili ya kiarabu ambacho kinamuua yeye kiaina, lakini yeye hataki kumjibu kitu kwa sababu anajua anataka kusafiria nyota yake au kupata umaarufu kupitia jina lake.

“Nimeshasikia mengi achilia hilo la kumtelekeza, nasikia ana jamaa huyo wa kiarabu na amekuwa akinipaka vibaya mitaani, lakini mimi sijibu kitu, kwani najua anataka kusafiria nyota yangu au kupata umaarufu kupitia jina langu,” alisema Meddy.
Aliongeza kuwa, anachokiangalia kwa sasa ni biashara zake tu na si vinginevyo.

Ijumaa lilikwenda nyumbani kwa Aisha, maeneo ya Mwenge baada ya kumkosa kwenye simu, lengo likiwa kutaka kumsikia anasema nini kuhusu madai ya kutoolewa kwa ndoa na Mpakanjia na ukorofi, lakini hakupatikana mara moja.
Aidha, Ijumaa lilimtwangia simu dingi wa Aisha, mzee Bui, lakini naye hakuwa tayari kuongelea lolote kuhusu mambo hayo akisisitiza hataki, hataki, hataki kabisa!


 (Votes #: 6)
    (21 November 2008)
Soma Zaidi: 2585 | Maoni Yako (14)

Udaku Mwingine

ijumaa
 
  • MPAKANJIA AACHA MKE MWINGINE: Ni yule binti aliyemrithi Amina Chifupa
  • Baada ya kumtema Aisha Bui: MPAKANJIA AMNASA KOLETA WA KAOLE
  • MKE WA MPAKANJIA AWEHUKA
  • Mpakanjia naye achanganyikiwa
  • MPAKANJIA: Amina unanipa mateso makubwa
  •    

    #1 Author: solange (21 November 2008 01:23)

    hamkomi tu this time atawachoma kisu kikweli kweli, heee huyo mpakanjia nae eti anatafuta umaarufu kupitia jina langu, aiii umaarufu upi ulionao?ka jina kenyewe kalikuzwa na mkeo.
     
    fast    

    #2 Author: saade (21 November 2008 03:38)

    we solange sema kweli bwana mpaka njia ni mfanya biashara maarufu hapo mwanzo na marehemu alimpenda kwa pesa zake au umaarufu wake hivyo useme nyota zao zilikwenda sawa lakini habari ndio hiyo upo hapo sasa hivi meddy si meddy wa mwanzo wa enzi zile zake.
     
    fast    

    #3 Author: Babu (21 November 2008 05:03)

    We Saade acha kuongea pumba, huyo Mpakanjia mwenyewe ni Dalali (Mtu Kati) tu, hana lolote, eti mfanyabiashara maarufu, ni biashara gani anafanya kama c kivuli cha shangazi yake waziri flani ....!
     
    fast    

    #4 Author: asha (21 November 2008 06:04)

    Huyo mpakanjia amshukuru amina ndo aliye mvuta jina lake kwani umaarufu waliokuwa wanamjua labda wauza unga wenzie.. kwa hilo asitake umbea bure..
     
    fast    

    #5 Author: QT (21 November 2008 09:59)

    Kusemwa ukweli zamani wengi tulikuwa hatumjui mpkanjia mpaka alivoanza kuandikwa kwenye magazeti kwa mgongo wa amina RIP hana umaarufu wa hivyo! na huyo Aisha alimuoa actudanganye. na hivi sasa kamchumbia Anita wa kwenye wimbo wa matonya mbona anatabia ya kuwakana wanawake zake au ndio njia ya kutafutia wanawake wengine
     
    fast    

    #6 Author: walewale (21 November 2008 12:11)

    Mpakanjia umekwisha na umri umeenda tulia tu ufe kistaarabu!!!!!!!!!!!!acha ulimbukeni
     
    fast    

    #7 Author: mkuyu (21 November 2008 12:55)

    acheni ujinga watu wanaongeza sikutuuu.
     
    fast    

    #8 Author: Lupe Fiasco (21 November 2008 16:19)

    winked no recourse feel no angry sad
     
    fast    

    #9 Author: Elmish Omary (27 November 2008 03:32)

    Mpakanjia bado unaapa tu viapo vitakuzuru baba hujakomaa eeh japokuwa we bingwa wa kuapisha tunasikia ulimwapisha Amina hadi kazurika sasa hiyo ni chamtoto laana ya babake Aisha imeanza kazi bado viapo vyenu. Take care walee wanao kuna wanawake wa mapenzi na wanawake wa pesa.
     
    fast    

    #10 Author: mamawawili (27 November 2008 12:35)

    huyu ni mwongo sana mpakanjia mimi najua kabisa aisha alimuoa na alikuwa anafanya kazi ocean sandlas na ndo alosababisha aisha aache kazi mtoto wa watu alikuwa ametulia sana aisha ila ilo limpakanjia ndo limemuahalibu.aisha panga maisha yako huyo mpakanjia kazoea sana kudanganya watoto wa watu
     
    fast    

    #11 Author: magj (5 December 2008 02:28)

    Mpakanjia,Aisha kwa sasa wote wanahitaji ushauri NASIHI.KWANI WOTE WAMEKWISHAATHIRIKA KISAIKOLOJIA.

    MPAKANJIA-ANAMAJONZI YA KUFIWA NA MBUNGE
    AISHA-ANAMAJONZI YA KUACHIKA.

    jamani tusiwalaumu .KWA MSAADA KWAO KUTOKA KWANGU NI WAO KUMUGOPA MUNGU KWA YOTE WANAYOYAFANYA-WAFUATE MAELEKEZO YA DINI[/i]
     
    fast    

    #12 Author: eric (11 December 2008 03:58)

    Jamani tuwasaidiene hawa watu la sivyo mbele litakuwa balaa li no ngine
     
    fast    

    #13 Author: Dommy (14 December 2008 23:49)

    Mh hapa napata mkanganyiko wa akili. Huyu Mpakanjia si ndo yule aliyewahi kukana kuwa hajamwoa Aisha na wala hamjui??. au nakosea ah sasa asema alimwacha kitambo. makubwa

    Haya mwaya pengine umeona umesahaulika kwa muda katika ulimwengu wa habari za watu maarufu
     
    fast    

    #14 Author: Emma (18 December 2008 03:26)

    halafu nyie wajinga manomuita mpakanjia mfanyabiashara maarufu,mnajua anafanya biashara gani??au mmekariri tu maarufu,maarufu kila mtu, nyoko!!
     
    fast    

    Add comments

    Name:
    E-mail:

    Code:
    Include security image CAPCHA.
    to renew the code
    Enter Code:

     

    Kura Yako / Poll

    Habari Katika Picha


    Gazeti la Uwazi


    Nani Yupo / Alikuwepo


    Home Page | About Us | Regista | Picha | Bongo Celebrities | Maoni | Contact Us

    hit counter

     

    2008 © globalpublisherstz.com