Tembelea... |
 |
Kalenda |
 |

Marafiki wetu |
 |
Habari Zilizopita |
 |



|
|
 |
|
|
 |
 |
|
 |
Mrembo huyo alitiwa katika mkono wa dola pamoja na wifi yake aitwaye Asha Jumbe walipokuwa nyumbani kwa mpenzi wake wa sasa aliyetambulika kwa jina moja la Jumbe, maeneo ya Tabata jijini Dar es Salaam. Kwa mujibu wa shuhuda wetu, juzi majira ya saa 5:00 asubuhi, zilifika defenda mbili nyumbani kwa akina Jumbe ambapo walifanikiwa kuwatia nguvuni Wema na wifi yake huyo kisha kuwapeleka katika Kituo cha Polisi, Magomeni. Ikadaiwa kwamba, wakati mlimbwende huyo ambaye katika siku za hivi karibuni amekuwa hakauki magazetini akipandishwa kwenye gari la polisi, alionekana akitokwa na machozi huku mwenzake (Asha) akionekana kutokuwa na wasiwasi wowote. Amani lilifika katika Kituo cha Polisi Magomeni majira ya saa 6:00 usiku na kuwakuta ndugu zake Wema na Asha wakihaha kuwawekea dhamana ambapo mpaka linaondoka eneo hilo, hakukuwa na dalili zozote za kuweza kutolewa. Aidha, alikuwepo pia mpenzi wake wa sasa akijaribu kufanya ‘mandingo’ ili akalale nyumbani na mpenzi wake huyo lakini juhudi zake ziligonga mwamba kwani taarifa tulizozipata wakati tunakwenda mtamboni zilidai kuwa, watuhumiwa hao walilala selo. Hivi karibuni, Kanumba alifungua jalada la kesi katika Kituo Polisi Magomeni kwa madai kuwa, alivamiwa na Wema akiwa na shoga zake kisha kupigwa na kuharibiwa vibaya gari lake.
|
|
 |
|
|
 |
Kura Yako / Poll |
 |
Habari Katika Picha |
|
 |

Nani Yupo / Alikuwepo |
 |
|