Ni wiki nyingine tulivu kabisa tunakutana kupitia safu hii maridhawa kabisa ambapo pamoja na mambo mengine tunazungumzia mada mbalimbali zinazogusa uhusiano wa kimapenzi...
Mpenzi msomaji, kijana Beka anaendelea kusimulia mkasa uliomkuta huko Bububu Zanzibar ambapo babu mmoja aliyetokea kumpenda alimfundisha uchawi. Wiki iliyopita nilielezea alivyokwenda na babu yake wa Zanzibar kwa bibi ambaye aliwahi kuishi naye aliyekuwa akimtesa na kumdhulumu pesa zake. Lengo lao lilikuwa ni kulipiza kisasi kwa bibi huyo na kumdai fidia kwa mambo aliyomfanyia kijana Beka kabla hajafundishwa uchawi na uganga. Walipofika kwa bibi, uliona jinsi walivyomtesa ambapo bibi huyo aliomba msamaha na kumpatia Beka mkia wa Taa kama fidia ya mambo yote aliyomtendea, mkia ambao alisema utamsaidia katika mambo yake ya kichawi na uganga. Leo anaendelea kusimulia kuhusu mtu wa kwanza kumtibia baada ya kufundishwa uganga. Hebu ungana na Mwandishi wako KULWA MWAIBALE katika kisa hiki cha kweli…
Ni watu wachache wanaofahamu umuhimu wa kuwa na rafiki katika maisha yao. Wengi kati yao wanajikuta katika makundi ya watu bila kujua faida ya kuwa na ushirikiano na wengine...
Jeshi la Polisi Jijini Dar es Salaam linaendelea kutoa elimu ya bure kwa madereva Taxi ikiwa ni hatua ya kuboresha huduma ya usafiri huo jijini hapa ambapo Polisi hupita katika vituo vya Taxi na kukusanya madereva kisha kuanza kuwapa somo. Pichani afisa huyu wa Polisi aliyenaswa leo mtaa wa Azikiwe Jijini akitoa elimu hiyo ambapo jana, kamera yetu pia iliwanasa Trafiki wakitoa somo kwa madereva mtaa wa Samora.
JAMANI SIYO NJAA TUNASHUSHIA TU! Katika hali ambayo haikujulikana mara moja kama ni njaa au hamu, kundi hili la watu lilinaswa na kamera yetu mtaa wa Samora Jijini Dar es Salaam likigombania kununua madafu majira ya saa saba mchana wakati wa muda wa Lunch. Hata hivyo baadhi yao walimwambia mpiga picha wetu kuwa walikuwa wanashushia baada ya kupata mlo wa mchana.
Kama utakuwa na kumbukumbu za kutosha katika masuala ya michezo ya Luninga ndani ya Bongo, basi bila shaka utamkumbuka Bwana mdogo aliyesifika sana kwa jina la Kibakuli, akiigiza kama mtoto wa mzee Muhogo Mchungu wakati huo wakiwa katika kundi la Kaole Sanaa Group! Basi huyu kidume aliyeko pichani ndiye Kibakuli ambaye hivi sasa kawa jibaba la maana na si bwana mdogo tena, ingawa aliuambia mtandao huu kuwa hivi sasa anakuja kivingine katika Movie za ukweli na si kuigiza kitoto kitoto.
Timu ya Taifa Stars imerejea leo asubuhi kambini the Atriums Hotel ikitokea Abidjan, Ivory Coast, ilipokwenda kushiriki michuano ya CHAN ambayo inaendelea kutimua vumbi huko Afrika Magharibi. Taifa Stars wamerejea baada ya kutoka sare ya bao 1-1 na Chipolopolo ya Zambia. Pichani: Kipa wa akiba Deo Mushi akiteremka kutoka katika gari lililowaleta kambini The Atriums Hotel iliyopo Sinza jijini Dar.
...Nadir Haroub (Kanavaro) akikagua mabegi yake kama yapo salama mara baada ya kuwasili.
...Kocha Maximo akibadilishana mawazo na Daktari wa Timu hiyo.
...Kanavaro akipiwapigia simu ndugu, jamaa na marafiki, kuwataharifu kuwa amewasili salama nyumbani
'Thanks for your Support'... ndivyo anavyoonekana kusema kocha Maximo wakati akisalimiana na Mkurugenzi wa Zizzou Fashion Store, Athuman Tippo mara baada ya kuwasili kambini leo asubuhi. PICHA: ISSA MNALLY/GPL
Kampuni ya Global Publishers jana ilichezesha Bahati Nasibu ndogo ya JISHINDIE PAJERO na jumla ya washindi 10 walijinyakulia zawadi za Stand Fan na simu za mkononi katika droo iliyochezeshwa viwanja vya Bakhresa, Manzese jijni Dar es salaam. Baada ya droo hii, itakayofuata ni droo kubwa ambapo msomaji mmoja wa magazeti ya Global Publishers atajinyakulia gari aina ya Mistubish Pajero yenye thamani ya shilingi milioni 12 na itakuwa ya pili kutolewa baada ya ile ya Mercedes Benz iliyotolewa Desemba mwaka jana. Pichani ni baadhi ya wasanii waliokuwepo kutoa burudani kwa wasomaji waliohudhuria Maofisa kutoka Bodi ya Michezo ya Kubahatisha Tanzania, Bw. Emmanuel Ndaki (kulia), Bw. Humud Abdulhussein (anayemfuatia) na Meneja Mkuu wa Global Publishers Bw. Abdallah Mrisho (mwenye tai) na Ofisa Masoko wake Bw. Mahmoud Omari wakifurahia burudani iliyokuwa ikitolewa uwanjani hapo.
sehemu ya umati uliofurika kushuhudia uchezeshaji wa Bahati Nasibu hiyo.
..wasanii wa vichekesho wakifanya vitu vyao..
Mmoja wa wasomaji wa magazeti ya Global akifubgwa kitambaa usoni kabla ya kuokota kuponi ya mshindi. Aliyemsimamia nyuma ni Ofisa kutoka Bodi ya Michezo ya Kubahatisha, Bw. Humud PICHA: MUSSA MATEJA
Na Rhobi Chacha Kifo cha Mtangazaji wa Independent Television (ITV) na Radio One, Rehema Mwakangale, aliyefariki dunia jana (Jumanne), majira ya saa kumi na moja alfajiri, katika Hospitali ya Mikocheni, jijini Dar es Salaam, baada ya kuugua kwa muda mfupi, kimebua mshtuko mkubwa miongoni mwa watangazaji wenzake....
Na Mwandishi Wetu Kufuatia kuchelewesha hati ya dhamana katika Mahakama ya mwanzo Kinondoni, jijini Dar es Salaam, Miss Tanzania 2006, Wema Isaac Sepetu, jana (Jumanne), amelala mahabusu ya Segerea jijini Dar es Salaam...
Darasa la Maisha ndiyo kolamu ambayo inakujia hivi sasa na anayekupakulia uhondo wote huo siyo mwingine bali ni mimi Joseph Shaluwa ambaye ninakuambia hutajuta kupoteza muda wako kusoma mada hii, kwani itakubadilisha hakika! Kabla ya kwenda mbali zaidi, napenda kuwakumbusha kwamba kitabu changu kipya cha Secret Love kinapatikana mitaani kwa wauza magazeti wote. Kanunue usome mbinu mpya za mapenzi, Love Story nzuri pamoja na Love Messages za kumtumia umpendaye...
Mzee Muddy anarudi Zanzibar, anakuta nyumba yake imetapakaa damu kila mahali na ukimya wa ajabu umetawala. Alipofungua mlango na kuingia hapo ndipo alipobaki mdomo wazi! Akahisi mwili mzima ukisisimka! Je, nini kitatokea? Mwandishi Wetu JOSEPH SAHALUWA anaendelea...
A new fatal disease that inflames the outer layer of the Brain causing an immediate death, has attacked the third world, it is called Chinese Encephalitis, so far it has killed about one thousand two hundred people in the Eastern Congo and it is moving so fast across Lake Tanganyika towards the United Republic of Tanzania, where it is expected to kill lots of people if no steps are taken to stop it now before it is to too late. So far this disease has neither cure nor vaccine and it is spread by a mosquito called AnophelenX…
Ugonjwa mpya wa hatari uitwao Chinese Encephalitis ambao hushambulia ngozi nyembamba inayofunika ubongo na kusababisha kifo haraka, umeibuka katika ulimwengu wa tatu.
Mpaka hivi sasa ugonjwa huu umekwishaua watu elfu moja na mia mbili katika ukanda wa Kongo ya Mashariki na unasambaa kwa kasi kuvuka ziwa Tanganyika ukielekea katika Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, ambako unategemewa kuua watu wengi kama hatua za haraka hazitachukuliwa mapema. Mpaka sasa ugonjwa huu hauna tiba wala kinga na unasambazwa na Mbu aitwaye AnophelenX…
MBINU! Timu ya soka ya Yanga imepata ufundi toka kwa klabu ya Ismailia ya Misri kwa ajili ya mchezo wa dhidi ya Al Ahly utakaopigwa katika Uwanja wa Cairo Misri kati ya Machi 13-15...
Na Adolph Balingilaki FUNIKA KOMBE! Huku Taifa Stars ikitarajiwa kurejea nchini leo kutoka Ivory Coast, habari tulizozipata jana wakati tukienda mitamboni zinadai kuwa Serikali iliwaita ghafla kuwahoji viongozi wa Shirikisho la Soka Tanzania (TFF), ili kujua sakata sakata linaloendelea kati ya Marcio Maximo na baadhi ya wachezaji wa timu hiyo...
Na Chile Kasoga MCHEZAJI Ulimboka Mwakingwe wa Simba, anazidi kuipa hofu klabu hiyo kutokana na kutojulikana yuko wapi kwa sasa, huku kukiwepo na taarifa tofauti zinazomfanya kutohudhuria mazoezi....