Wanenguaji wa bendi ya FM Academia, ‘Wazee wa Ngwasuma’ leo alfajiri walinaswa na kamera yetu wakiwajibika jukwaani katika onesho la bendi hiyo lililofanyika kwenye Ukumbi wa Msasani Club jijini Dar, onesho hilo lilikwenda sambamba na promosheni ya Jishindie Pajero inayoendeshwa na kampuni ya Global Publishers.
VIUNO VYA WATOTO WA DIAMOND BALAA TUPU Wanenguaji wa Bendi ya Diamond Musica, ‘Vijana Classic, Moto mara 3’ wakitikisa viuno kama walivyonaswa na kamera yetu Ukumbi wa Mango Garden leo alfajiri. PICHA :RICHARD BUKOS/ GPL.
Wataalam wa masuala ya umeme wakifunga mataa katika mnara uliopo viwanja vya mnazi mmoja jijini Dar es Salaam, kwaajili ya maandalizi ya mkesha wa Maulidi unaotarajiwa kufanyika kesho katika viwanja hivyo. PICHA :RICHARD BUKOS/ GPL.
Mwenyekiti wa CCM, Rais Jakaya Kikwete akifungua Mkutano wa Halmashauri Kuu ya Taifa ya CCM Mjini Dodoma March 7, 2009. Kulia ni Katibu Mkuu wa CCM, Yusuf Makamba.
Mwenyekiti wa CCM, Rais Jakaya Kikwete, Makamu Mwenyekiti wa CCM (Bara), Pius Msekwa (wapili kulia), Katibu Mkuu wa CCM, Yusuf Makamba (wapili kushoto) na Katibu Mkuu wa CCM Mstaafu, Rashidi Kawawa (kulia) wakiimba wimbo wa Chama cha Mapinduzi kabla ya kuanza kwa Kikao cha Halmashauri Kuu ya Taifa ya CCM Mjini Dodoma, March 7,2009.
Wajumbe wa Halmashauri Kuu ya Taifa ya CCM, Waziri Mkuu, Mizengo Pinda na Katibu Mwenezi wa CCM na Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makaazi, Capt.John Chiligati wakiteta katika kikao kilichoongozwa na Mwenyekiti wa CCM, Rais Jakaya Kikwete Mjini Dodoma , March 7, 2009. (Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu)
Mke wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Jakaya Mrisho Kikwete, Mama Salma, Jana(6.3.2009) alizindua sherehe za maadhimisho ya Sikukuu ya Wanawake Duniani, ambayo hapa nchini yalifanyika katika Viwanja vya Mnazi Mmoja jijini Dar es Salaam. Katika sherehe hizo, kundi la vichekesho la Orijino Komedi lilizua balaa bada ya kuibukia uwanjani hapo na kusababisha watu kukanyagana katika kutaka kuwaona.
Mama Kikwete, akiwasalimia akimama wajasiriamali.
Kikundi cha walemavu, kikiimba shairi katika maadhimisho hayo.
Kikundi cha Sanaa cha Maalbino, kikicheza ngoma ya kimakonde uwanjani hapo.
Mama JK akisoma hotuba.
Umati ukisikiliza hotuba ya Mama JK.
Baada ya Mama Salma, kumaliza hotuba, msanii wa Orijino Komedi, Isaya Mwakirasa ‘Wakuvwanga’ akapanda jukwaani kumuiga kwa kurudia akiyozungumza na sauti yake.
Kundi zima la Orijino Komedi, lilipanda jukwaani kufanya vitu vyake.
Joti wa Orijino Komedi, akiwavuja mbavu waliohidhuria wakati akicheza sebene la FM Academia. PICHA: RICHARD BUKOS NA CHRISTOPHER LISSA /GPL.
Mwenyekiti wa CCM, Rais Jakaya Kikwete akisalimiana na Mjumbe wa Kamati Kuu, Waziri Mkuu, Mizengo Pinda baada ya kuwasili kwenye uwanja wa ndege wa Dodoma March 6,2009.
Wajumbe wa Kamati Kuu ya CCM, Waziri Mkuu, Mizengo Pinda na Katibu Mkuu wa CCM, Yusufu Makamba wakiteta kabla ya kuanza kwa kikao cha Kamati hiyo, Mjini Dodoma, March 6,2009.
Mwenyekiti wa CCM, Rais , Jakaya Kikwete akizungumza wakati alipofungua mkutano wa Kamati Kuu ya CCM Mjini Dodoma, March 6, 2009.Kushoto ni Makamu Mwenyekiti wa CCM ( VISIWA), Amaan Karume, wakwanza kulia ni Makamu Mwenyekiti wa CCM (Bara), Pius Msekwa na watatu kushoto ni Katibu Mkuu wa CCM, Yusuf Makamba. (Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu)