Mwendesha baiskeli akiwa amesimama mbele ya magari kwenye mataa ya makutano ya Barabara ya Ally Hassan Mwinyi na Kawawa eneo la Morocco, jijini Dar es Salaam. Wapanda baiskeli wengi hupoteza maisha kwa kujichanganya na magari sehemu kama hizi na kwa kutojua sheria za usalama barabarani.
KWA MMACHINGA POPOTE DUKA Wafanyabiashara za kutembeza maarufu ‘wamachinga’ hawana hiyana, wao popote pale wanaweza kufungua duka. Pichani, kijana huyu alinaswa na kamera yetu, leo mchana, akiendelea na biashara zake katikati ya Barabara ya Ally Hassan Mwinyi maeneo ya Namanga, jijini Dar. PICHA ZOTE NA RICHARD BUKOS /GPL
Katika Nani Zaid, wiki hii tunao mastaa wanaong’ara katika filamu nchini, Haji Adamu na Adam Kuambiana. Wasanii hawa hawajawahi kushiriki katika Tamthilia za Luninga, lakini wametokea kujitwalia umaarufu baada ya kuingia katika Tasnia ya Filamu nchini Tanzania. Baadhi ya sinema ambazo wawili hawa wameonyesha cheche zao ni pamoja na Fake Pastors, Sauti ya Manka na Regina (Adamu Kuambina) na Jeraha la Ndoa, Miss Bongo na Quick Money (Haji Adamu). Je, kwa maoni yako, nani zaidi? Piga kura yako sasa!.
MABINGWA wa Ligi Daraja la Kwanza ya Marekani ya Kaskazini, Vancouver Whitecaps FC, leo wanashuka katika Uwanja Mkuu wa Taifa jijini Dar es Salaam kukipiga na mabingwa wa hapa, Yanga kwenye mchezo wa kimataifa wa kirafiki...
Licha ya leo kuwa siku ya kazi lakini nyomi la watu alfajili hii lilinaswa na kamera yetu likiselebuka katika Bonanza la Akudo Impact, lililofanyika ufukwe wa Msasani Beach Club jijini Dar es Salaam.
Viongozi wa Bendi ya TOT Respect, Badi Bakule (kulia) na Abdul Misambano walinaswa wakikomaa wenyewe jukwaani katika onyesho la bendi hiyo, lililofanyika Ukumbi wa Mango Garden leo alfajili.
Wanenguaji wa Bendi ya Msondo Music Band, Nacho Said, ‘Mama Nzawisa’ na Queen Emmy wakiwa wamejipumzisha baada ya kazi nzito ya kutikisa kiuno katika onesho la bendi yao lililofanyika Africentre jijini Dar, usiku wa kuamkia leo. PICHA: RICHARD BUKOS /GPL
Mc wa aliyekuwa akisherehesha katika onyesho la pamoja kati ya Kanda Bongomani na FM Academia, ambalo lilifanyika katika ukumbi wa Msasani Club, akiwa amekaa huku akishindwa kuamini kwamba mwanamuziki huyo kutoka Kongo kaingia mitini.
KIUNO CHAKO HICHO….. Lilian Intarnet mnenguaji mahiri wa bendi ya African Stars, ‘Twanga pepeta, akinengua sambamba na mwimbaji wa bendi hiyo Ferguson, katika onyesho lililofanyika jana katika ukumbi wa TCC Chang’ombe jijini Dar. Picha: Issa Mnally/ GPL.
Maskini Tanzania! Sifa mbaya ya wawekezaji wa Kichina nchini, imeendelea kuchukua nafasi pana, baada ya hivi karibuni Ijumaa Wikienda kubaini biashara ya ngono, inayoendeshwa kama duka ndani ya hoteli ya kifahari jijini...
Kijana mmoja ambaye jina lake halikuweza kupatikana mara moja, mwishoni mwa wiki iliyopita alitunukiwa kichapo cha nguvu kutoka kwa mwanamke mmoja mwenye hasira kali baada ya kubaini kuwa, alikuwa akimfanyia vitendo vya uasherati...
Upelelezi wa mauaji ya mwanamke mwendawazimu yaliendelea, polisi wakafanikiwa kukutana na mtu aitwaye James Ngalo ambaye alishuhudia mtu akitupa koti daraja la salenda usiku wa manane, walipokwenda eneo hilo walilikuta koti pamoja na panga!
Wote wakafahamu aliyetupa koti hilo ndiye aliyemuua mwanamke mwendawazimu, upelelezi ukaendelea. James Ngalo na mkewe Rachel Msangi ni Wanasheria wanaomiliki kampuni yao binafsi iitwayo James & Rachel Advocates, ni familia yenye watoto wawili mapacha Dana mwenye mtindio wa ubongo na Dona. Walianzia shughuli zao mjini Arusha na baadaye kuhamia Dar es Salaam ambako walifungua ofisi nyingine kubwa zaidi ya Uwakili, wakiwa na mtoto wao Dana, Dona alibaki Arusha akisoma shule ya Kimataifa Arusha.
Masaa machache tu baada ya James kutoa taarifa kwa polisi, mzee aitwaye Badru Mohamed anamtembelea ofisini kwake na kudai yeye ni mfanyabiashara wa mafuta na alikuwa akihitaji ushauri wake wa kisheria, kwa sababu James alikuwa na haraka ya kwenda kumpokea mtoto wake Dona ambaye siku hiyo alikuwa akirejea kutoka shule alitaka wakutane siku nyingine lakini mzee huyo akaomba hata kama ni nyumbani amfuate usiku maana alikuwa na shida ya haraka, kwa jinsi alivyoonekana, James hakukataa, akamkaribisha nyumbani kwa chakula cha usiku.
Badala ya saa mbili usiku mzee Badru aliwasili saa tatu usiku na kufunguliwa mlango, mtoto Dona alikuwa chumbani amelala, sebuleni alikuwepo Rachel akiwa amembeba mtoto wao mwenye mtindio (Dana).
Katika hali ambayo James na Rachel hawakuitegemea kwani walishatayarisha chakula cha mgeni, walishangaa kumwona mzee Badru akichomoa bastola kwenye koti na kuanza kuwamiminia wote watatu!
Dona alisikia kelele akiwa chumbani, akanyanyuka na kuanza kutembea kwenda sebuleni, akamwona mzee mwenye bastola mkononi, taratibu akakimbia na kujificha kwenye kona pembeni kabisa ya nyumba.
Badala ya kwenda chumbani ambako mzee Badru alikwenda na kumsaka kila sehemu bila mafanikio. Dona akatoka hadi nje na kukimbia kwenye bustani ambako alijificha katikati ya migomba, baadaye akasikia hatua za mtu zikielekea eneo hilo na tochi ikimulika, alikuwa ni mzee Badru akimtafuta ili ammalizie, akafika mpaka kwenye migomba na kusimama kando yake, Dona alisikia mwili ukifa ganzi, hata sauti ya kuhema kwake aliisikia ni kubwa, kiasi kwamba mzee huyo angegeuka tu nyuma lazima angemwona na kummiminia risasi. Je, nini kitaendelea? SONGA NAYO…
Ni wiki nyingine tofauti kabisa na wiki iliyopita ambapo tunakutana tena kupitia safu hii nikiamini kwamba umzima na unaendelea vyema na majukumu yako ya kila siku kama kawaida...
Zubeda Ruvanga, mwanamke mwenye umri wa miaka 38, anasimulia mateso aliyokumbana nayo tangu akiwa mtoto. Wachawi walianza kumpa tabu za maisha tangu akiwa darasa la tatu kwenye Shule ya Msingi Mwandiga Kigoma. Wiki iliyopita alikomea pale alipoangua kilio mbele ya kundi la wachawi waliokuwa kwenye sherehe ya kumpokea kuwa malkia wao, hivyo kumchanganya Mfalme Dajani aliyewanyamazisha wachawi wote na kumuuliza Zubeda kilichokuwa kinamliza. Endelea kusoma sehemu ya pili ya mkasa huu wa kusikitisha...
HUKU wadau mbalimbali wa soka wakidai Kocha wa Taifa Stars, Mbrazil Marcio Maximo hafai kuendelea kukinoa kikosi hicho kutokana na kuwatenga wachezaji wake, akiwemo kiungo wa Simba Haruna Moshi ‘Boban’ na wa Yanga, Athuman Idd ‘Chuji’, makocha wa klabu hizo nao wameunga mkono...
KOCHA Mkuu wa Timu ya Simba, Mzambia Patrick Phiri, ameshusha tambo zake Ligi Kuu ya Vodacom kwa kudai kuwa, hakuna timu itakayoweza kukizuia kikosi chake kushika nafasi ya pili kwa kuwa anaiandaa kwa kazi hiyo...
KLABU ya Al Ahly ya Misri inazidi kubanwa mbavu na kuurahisisha mchezo wao dhidi ya Yanga baada ya kwenda sare ya bila kufungana na Timu ya Polisi ya huko ikiwa katika Uwanja wa Kimataifa wa Cairo juzi huku kiungo wao wa kutumainiwa Mohammed Barakat akilimwa kadi nyekundu...
Padri anaamua kumsaidia Adrian kusoma kwani amegundua kilichomo ndani yake, hakuwa mtoto wa kawaida! Msaada wake unakuwa ni kumpeleka kwenye Shule ya Seminari iitwayo Kiparato ambako anaanza darasa la kwanza, huko anakutana na watoto wengi wa matajiri kwani shule hiyo inaheshimika na watu wenye uwezo pamoja na viongozi hupeleka watoto wao hapo kupata elimu bora.
Miongoni mwa watoto aliokutana nao kwenye shule hiyo, tena kwenye darasa lake ni Edward, huyu ni mtoto wa mfanyabiashara aitwaye Lonjino ambaye kwake fedha ni kila kitu! Mtoto huyu amelelewa katika mazingira ya fedha, mazungumzo nyumbani kwao kila siku yanahusu fedha na wazazi wake kumwambia kabisa akikua ni lazima atafute utajiri na mbegu hiyo imepandikizwa ndani ya kichwa cha Edward.
Mtoto mwingine ambaye Adrian amekutana naye kwenye darasa lake ni Paul Kitumbi, pia mtoto wa tajiri, naye fedha maishani mwake ni kila kitu, anafahamu amekuja shuleni kusoma ili akimaliza Chuo Kikuu arejee nyumbani kusimamia shughuli za baba yake kwani yeye pekee ndiye mtoto wa kiume kwenye familia hiyo!
Adrian amezungukwa na matajiri, anajisikia mnyonge mbele ya wenzake na hana rafiki hata mmoja, ni aidha anatengwa au anajitenga mwenyewe. Hii inamfanya kila siku awakumbuke mama na dada yake Adventina aliowaacha kwenye dhiki kubwa, anaapa kusoma mpaka afanikiwe na kuikomboa familia yake. Je, nini kinaendelea? SONGA NAYO…