Timu ya Uwazi Giant, inayoshiriki michuano ya NSSF, imetoa onyo kwa timu nyingine katika michuano hiyo baada ya kuishushia gharika ya mabao 10-0 timu ya IPP, katika mchezo uliofanyika jana kwenye Uwanja wa Sigara Chang’ombe.
Mabao ya Uwazi Giant, yalipachikwa na mshambuliaji hatari Julius Kihampa, Festo Anan na Nuru James.
Kipigo hicho cha mwaka kilisabisha Kocha wa IPP Sebo, kuingia mitini kabla ya mchezo huo kumalizika na alipoulizwa kulikoni alikana kuifahamu IPP na kusema kuwa iliyokuwa inacheza si timu yake.
Kichapo hicho cha aibu kwa timu ya IPP, kiliwafanya wachezaji wake mahili kama Maulid Baraka Kitenge, Jimmy Charles na wengine wengi kupotea kwenye mazingira ya kutatanisha.
Naye mkurugenzi wa Global Publishers ambaye ndiye mdhamini mkuu wa Uwazi Giant, Eric Shigongo alisema kuwa kama vijana wake watatwaa kombe hilo atatoa zaidi kiasi cha shilingi milioni mbili na nusu zinazotolewa na mdhamini wa mashindano hayo yaani NSSF, ambacho aliahidi kutoa hapo awali.

Kikosi cha Uwazi Giants, kikijiandaa kuvaana na IPP FC jana.

Kikosi cha IPP FC, wakiwa katika ukaguzi kabla ya kuvaa na Uwazi Giants, katika Uwanja wa TCC Chang’ombe jana.

Uwazi Giants wakimalizia hatua ya ukaguzi mbele ya mmoja wa wana kamati ya mashindano ya NSSF Cup, Taji Liundi (mwenye miwani).

Wachezaji wa IPP FC (wenye jezi za njano) wakiwa katika picha ya pamoja na wachezaji wa Uwazi Giants, mara baada ya kumalizika kwa pambano lao jana.

Benchi la wachezaji wa akiba wa Uwazi Giants wakifuatilia kwa makini mpambano huo.

Mlinzi wa pembeni wa Uwazi Giants, Elius Kambili akitolewa nje mara baada ya kuchezewa rafu.

Mpiga picha wa Global Publishers, Issa Mnally akishangilia kwa furaha ushindi wa timu yao.

Mpiga picha wa IPP, akiwa amechoshwa na magoli waliyofungwa timu yao ya IPP FC.
PICHA: MUSA MATEJA NA ISSA MNALLY /GPL