Wasanii nyota wa muziki wa kizazi kipya, Juma Kassimu,’Nature’ na Ferouz Mrisho, ‘Ferouz’ usiku wa kuamkia leo wamekonga nyoyo za wanazi wa burudani jijini Dar es Salaam, baada ya kutwanga shoo kali ya uzinduzi wa albamu zao mbili, ndani ya ukumbi wa Diamond Jubilee.Albamu ya Nature inaitwa ‘Tugawane umasikini’ ambapo albamu ya Ferouz inaitwa ‘Sauti na vyombo’.
Nature akikonga nyoyo za mashabiki.
Ferouz akiwapagawisha mashabiki,hapa anaimba wimbo wake wa Mr.Police man.
Enika alisindikiza shoo hiyo,hata hivyo kivazi chake kilionekana kuwazingua wengi.
Mbunge wa Temeke Abass Mtemvu, akiwa na mbunge wa viti maalum Bi. Al-Shaimaa Kwegyir, ambao walikuwa wageni rasmi katika shoo hiyo.
Mtangazaji mahiri wa Redio Times FM, Tayana Amri, akiwa na msanii Mbungangari Lameck, ‘Pig Black’, wakifuatilia kwa karibu makamuzi ya TMK Wanaume halisi. PICHA :CHRISTOPHER LISSA/GPL
Jana jioni wakazi wa jiji la Dar es Salaam, walishuhudia mwanamuziki mkongwe kutoka nchini DRC Kongo, aishie nchini Uingereza, Kanda Bongoman, akifanya makamuzi ya kufa mtu ambayo yalienda sambamba na kuinadi bahati Nasibu ya Jishindie Pajero, ndani ya Ukumbi wa Msasani Club. Mwanamuziki huyo leo anatarajiwa kufanya onesho lingine mkoani Morogoro.
Kanda Bongoman na wanenguaji wake wakifanya makamuzi wakati wakiitanagaza Bahati Nasibu hiyo
KAMA HANA MFUPA Bongoman akijinyonganyonga jukwaani katika kuwakumbusha mashabiki wake mambo ya enzi hizo.
HAKUHOFIA VIBAKA ALIJICHANGANYA NA MASHABIKI Baada ya kuona mashabiki wamepandwa na mzuka Bongoman aliamua kujumuika nao.
ILIKUWA NI KUJIRUSHA TU Umati wa watu ukijimwaga katika onesho hilo. PICHA: RICHARD BUKOS /GPL.
Na Mwandishi Wetu Aliyekuwa Miss na muandaaji wa mashindano ya ma-miss hapa nchini siku za nyuma, Mange Kimambi ‘MK’, amechezea kichapo, baada ya kudaiwa kuwachafua vigogo katika mtandao aliokuwa akiumiliki wa www.mangeblogspot.com, kabla ya kuufunga....
Na Rhobi Chacha Mkurugenzi wa Kampuni ya Global Publishers, inayochapisha magazeti pendwa ya Risasi, Ijumaa, Ijumaa Wikienda, Amani na Championi, Eric James Shigongo, amemsambaratisha Mkurugenzi wa IPP, Reginal Mengi, baada ya timu yake ya Uwazi Giants kuichabanga timu ya mtani wake huyo kwa bao 10-0, katika mechi kali ndani ya Viwanja vya Sigara TCC Chang’ombe jijini Dar es Salaam juzi (Alhamis)....
Christopher Lissa na Richard Bukos Khadija Seleman ambaye ni mama mzazi wa Ramadhani Seleman ‘Rama mlawatu’ ambao kwa pamoja wanakabiliwa na shitaka la mauaji, ambapo Ramadhani alikamatwa maeneo ya Hospitali ya Taifa Muhimbili, Jijini Dar es Salaam akila kichwa cha mtoto, imeonekana ugali wa dona katika gereza la Segerea, umemkubali kutokana na mabadiliko makubwa aliyonayo kutoka uraiani hadi sehemu hiyo baada ya kuzidi kunenepeana ovyo tofauti na alivyoingia mahabusu....
Richard Bukos na Christopher Lissa Kesi iliyokuwa inamkabili aliyekuwa Mkurugenzi wa Utumishi na Utawala, Benki Kuu ya Tanzania (BoT), Amatus Liyumba na mwenzake, Deus Kweka jana (Ijumaa), iliingia hatua mpya baada ya kupatiwa Hakimu mwingine kufuatia Hakimu aliyekuwa akiindesha kesi hiyo Bi. Hadija Msongo, kujitoa katika kesi hiyo...
Umeibuka ugonjwa mpya katika Afrika Kusini mwa Jangwa la Sahara, ugonjwa huu unaitwa Chinese Encephalitis, ukienezwa na Mbu aitwaye AnophelenX, ni ugonjwa hatari ambao mpaka hivi sasa hauna tiba wala kinga na umekwishaua idadi ya watu elfu moja na mia mbili nchini Kongo. Taarifa ambazo CNN wametangaza muda mfupi uliopita ni kwamba tayari ugonjwa huo unavuka Ziwa Tanganyika kuingia Tanzania ambako unatarajiwa kuua idadi kubwa ya watu.
Hali hii imesababisha hofu kubwa na watu wengi wenye fedha zao wameanza kupanda ndege kuikimbia Tanzania wakiwaacha watu masikini wafe hii ni habari ya kusikitisha, hofu kubwa imetanda kila sehemu ya Tanzania. Jacob Steven ni mchumi wa Jiji la Dar es Salaam, mume wa Angela na wana mtoto mmoja mzuri aitwaye Natalia ambaye kila mtu aliyemwona anahisi atakuja kuchukua hata taji la Urembo wa dunia, familia yao ni yenye furaha.
Taarifa alizoziona kwenye runinga zimemshtua sana Jacob, naye anafikiria kuondoka nchini kwenda kujificha Uingereza mpaka hali itakapotulia. Ameamua kuandika barua ya kuomba likizo, alipoimaliza tayari ni saa kumi na moja jioni, saa za kazi umekwishakupita hawezi kuiwakilisha barua yake kwa bosi mpaka siku inayofuata.
Muda huo huo anapokea simu kutoka kwa mke wake Angela ambaye anampa taarifa kuwa mtoto wao Natalia ana homa kali! Taarifa hizi zinazidi kumchanganya Jacob ambaye mara moja anaamua kwenda nyumbani, huko wanamchukua mtoto na kumpeleka hospitali ya Dk. Pandya, bingwa wa matatizo ya watoto wadogo. Jambo la kwanza ambalo daktari huyo anafanya ni kumpima Natalia joto kabla hajaendelea na mambo mengine. Je, nini kitaendelea? SONGA NAYO…
Uwanja wa Huba ipo tena hewani na anayekuandalia safu hii namba moja ihusuyo mambo ya mapenzi ni mimi Joseph Shaluwa, nikikukaribisha kwa moyo mkunjufu ili kujifunza mbinu mpya za mapenzi.....