Sakata la kesi ya maharamia walionaswa na merini wakivua samaki aina ya Jodari katika kina kirefu ndani ya Bahari ya Hindi eneo la Tanzania kinyume cha sheria leo (Ijumaa) limechukua sura mpya baada ya Mhandisi Mkuu wa meli hiyo Cai Dong Li na Msaidizi wake, Chen Rui Hai kuachiwa na mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu na kurudi kwenye meli hiyo. Upande wa utetezi katika kesi hiyo uliomba wahandisi hao waachiwe kwa muda ili wakaikoe meli hiyo iliyoko katika hatari ya kuzama baada ya njia zake za kutolea maji yanayoingia kushindwa kufanya kazi baada ya kuzimwa baada ya watuhumiwa hao kukamatwa. Wahandisi hao watakaa melini humo mpaka kazi ya kutoa maji itakapomalizika ndipo watarudishwa tena mahabusu.
Baadhi ya maharamia wakisubiri kusomewa kesi inayowakabili
Baada ya kesi hiyo maharamia wengie walirudishwa rumande mpaka Machi 31 mwaka huu. PICHA: RICHARD BUKOS NA CHRISTOPHER LISSA
Mvua za rasharasha zilizonyesha kwa muda mfupi jijini Dar es Salaam leo, zimesababisha kuharibika kwa miundombinu na kusababisha baadhi ya watu kusitisha safari zao.
Pichani moja ya mitaa ya maeneo ya Posta Mpya jijini Dar, ukiwa umefungwa kufuatia maji kujaa na kutiririsha kinyesi.
Mtaro wa kinyesi ukiwa umezibuka eneo hilo maeneo ya Posta Mpya.
Wakazi wa Jiji wakivuka kwa taabu moja ya maeneo ya jiji kufuatia maji ya mvua kufurika barabarani. PICHA:RICHARD BUKOS NA CHRISTOPHER LISSA /GPL
Mama mzazi wa Miss Tanzania 2005-2006. Wema Isaac Sepetu, Mariam Sepetu amesema kuwa mwanaye amerudi nyumbani, amekuwa mtiifu kitabia na hata akili yake imenyooka...
MUDA mfupi baada ya mtangazaji mwenye jina kubwa nchini, Khadija Shaibu a.k.a Dida kukamatwa na kufanyiwa upekuzi akituhumiwa kumeza dawa za kulevya, Ijumaa limezinyaka za ndani...
Baada ya kuishi msituni muda mrefu na bibi Monica Lugembe, aliyekimbia kijijini kwake sababu ya tuhuma za uchawi, Dona anaamua kurejea jijini Dar es Salaam baada ya bibi huyo kufariki dunia na yeye peke yake akamzika. Ametembea kwa miguu umbali mrefu mno, ilikuwa safari ya siku mbili kutoka porini mpaka katikati ya jiji na kwenda moja kwa moja hadi eneo la Kivukoni ambako watoto wengi wa mtaani wanaishi!
Anachagua sehemu moja ufukweni na kulala mpaka asubuhi siku iliyofuata alipozinduka na kujikuta amelala karibu na kundi kubwa la watu wenye kelele, akagundua lilikuwa ni soko la samaki na hakuna mtu aliyeonekana kumjali! Je, nini kinaendelea? SONGA NAYO…
Kwanza namshukuru Mwenyezi Mungu kwa kuwa ni yeye ndiye aliyepanga tukutane tena leo katika safu yetu hii maridhawa ya Let’s Talk About Love. Hakika bila ya yeye sisi tusingekuwepo!...
HUENDA mshambuliaji wa Yanga na timu ya Taifa ya Kenya ‘Harambee Stars’, Boniface Ambani akazikosa Sh. Milioni 600 kutoka klabu ya Zhejian Greentown ya China...
BAO lililofungwa na Omari Matuta wa Mtibwa Sugar katika dakika ya 34 dhidi ya Simba mwishoni mwa wiki iliyopita, limezima kabisa mahesabu makali ya Kocha Patrick Phiri wa Wekundu hao wa Msimbazi ya kugusa michuano ya Kombe la Shirikisho mwakani...
Wakati mashabiki na wanachama wa Yanga wakiendelea kushangilia ubingwa wa Tanzania Bara walioupata mapema wiki hii katika Uwanja wa CCM Kirumba Mwanza mgongoni kwa 'watoto wao' Toto Afrika, Kocha Mkuu wa timu hiyo Professa Dusan Kondic amebadili mfumo wa uchezaji kwa kutoa 'promotioni' kwa wachezaji waliokuwa wanakaa benchi...
Vijana watatu, Edward, Paul na Adrian wanakutana shuleni na kukubaliana kwamba kwa pamoja watafanya kazi kwa kushirikiana mpaka waikomboe nchi yao kutoka mikononi mwa Wagandamizaji ambao pia ni Raia wa nchi ya ya Taiman. Wanatoka katika familia tofauti, Paul na Edward wanatoka familia tajiri ambako walifundishwa na wazazi wao kwamba ni lazima katika maisha watajirike na Adrian anatoka familia masikini ambako mama yake mjane alimfundisha kwamba kiini cha maovu yote ni kupenda fedha.
Walipomaliza Chuo Kikuu, Paul na Edward wanakuwa mawaziri na Adrian anakuwa Mhadhili wa Chuo Kikuu cha Taiman akiwa na mke wake Bernadetha, waliyekutana tangu enzi za sekondari! Cha kusikitisha zaidi, Edward ambaye hivi sasa ni Waziri wa Mambo ya nchi za nje ameanza kumtamani Bernadetha na anafanikiwa kumwingiza katika mtego wa mapenzi.
Ili kupata nafasi ya kufaidi mapenzi yao, unafanyika mchoro na Adrian anapata nafasi ya kwenda kusoma nje ya nchi, nafasi ambayo awali aliikataa kwa sababu hakutaka kumwacha mke wake lakini ni mke wake huyo huyo aliyemshawishi mpaka akakubali na kuondoka nchini kwa miezi tisa.
Amerejea bila mawasiliano, sababu mke wake alikuwa hampigii simu wala kumwandikia barua, ana wasiwasi kuna kitu kinaendelea! Nyumbani kwake anakuta gari aina ya Landcruiser limeegeshwa, lina namba za serikali! Akiwa hajapata jibu gari hilo linafanya nini nyumbani kwake usiku wa saa tano, anaamua kuzunguka nyuma ya nyumba yake na kuchungulia ndani, macho yake yanagongona na taswira za watu wawili wakifanya mapenzi kitandani kwake, hao ni Edward na Bernadetha, akiwa na hasira anarejea mlangoni na kuanza kugonga. Je, nini kitaendelea? SONGA NAYO...