Mpambano wa kumtafuta mwanaume mkali zaidi Bongo 009 ‘The most handsome man Tanzania’ umeafanyika usiku wa kuamkia leo ndani ya Hoteli ya New Africa katikati ya Jiji la Dar es Salaam ambapo kijana Khalid Mohamed ameibuka kidedea kati ya vijana 11 waliokuwa wakichuana. Kwa maana hiyo jamaa atakamata Dola 1000 na kufanyiwa Shoping katika maduka ya Zizzou Fashion. Shindano hilo liliandaliwa na Angels Entertainment na kudhaminiwa na British Council, C2C ‘Mtu kwao’, I&R Identity, Ijumba Enterprises, Wapi na Michuzi Blog. NA HIVI NDIVYO WANAUME WA SHOKA WALIVYOCHUANA:

Khalid Mohamed ambaye alishinda akipita jukwaani na vazi la ubunifu

Mshindi wa pili Henry Mwinyi akionesha makeke yake jukwaani.

Mshindi wa tatu Ken Victor akikatiza jukwaani na vazi la ubunifu.

Hii ndiyo ilikuwa Top 3

Wanamitindo maarrufu nchini Mustapha Hassanali na Bi. Asia Idarus wakipeana ‘maks’ ukumbini muda mfupi kabla ya mapambano kuanza.

Majaji wa mpambano huo, (kutoka kushoto) Steven Kanumba, Christina Issabela na mshindi wa Big Brother Africa 2007, Richard, wakiumiza vichwa kutoa TOP 3.

Mashabiki wakiteta jambo wakati wakisubiri kutangazwa kwa Top 3
PICHA:CHRISTOPHER LISSA/GPL