Hali bado ni tete kwa wakazi wa eneo la Mbagala Wilayani Temeke na katika Jiji la Dar es Salaam kwa ujumla, kufuatia tukio lililotokea jana la kulipuka kwa mabomu makubwa katika ghala la Jeshi la Wananchi Tanzania (JWTZ) na kusababisha maafa makubwa. Watu kumi wamethibitishwa kupoteza maisha hadi leo, wakiwemo askari 5 wa JWTZ - kwa mujibu wa taarifa ya Jeshi la Polisi Kanda maalumu ya Dar es Salaam. Asubuhi ya leo, mtandao huu ulishuhudia wananchi, wakihaha kuwasaka ndugu na jamaa zao hasa watoto ambao walipotea jana. Vituo vingi vya Polisi, Msalaba Mwekundu, kambi za kijeshi na Hospitali, hasa Wilayani Temeke, mamia ya watu walijazana kutambua ndugu zao, huku vilio na mayowe vikitawala.
Askari wa Jeshi la Wananchi, JKT, Polisi, Scouts, wauguzi na watoa huduma ya kwanza walionekana wakiendelea kutoa huduma kwa watoto katika vituo huku zoezi la utambuzi likiendelea katika kambi za Mbagala Kizuiani na JKT Mgulani na katika Hospitali ya Wilaya ya Temeke. Kwa ujumla, Mbagala bado inazizima ambapo asilimia kubwa ya wakazi wake hawakwenda kwenye shughuli za kawaida na badala yake walizidi kuzagaa mitaani kusaka ndugu zao. JWTZ imeweka kizuizi kwa waandishi wa habari wa kawaida kuingia eneo la tukio (kambini) ambapo wanaoruhusiwa ni waandishi wa habari wanajeshi tu.
Hawa ni baadhi tu ya watu wanaoishi karibu kabisa na kambi ambayo kulikuwa na ghala lililolipuka wakiwa wamehifadhiwa katika kambi ya JKT Mgulani baada ya kukosa mahali pa kuishi.
Wananchi wakijiandikisha kwa ajili ya kutambua ndugu zao katika kambi ya JKT Mgulani leo.
Hawa ni watoto waliokusanywa baada ya kushindwa kurejea makwao, wakipata kifungua kinywa katika kambi ya msalaba mwekundu Kizuiani leo asubuhi.
HAWA SIYO MAHABUSU: Wananchi wakiingia kwenye kwenye gari ambalo hubebea mahabusu ‘Karandinga’ katika kituo cha Polisi Kizuiani Mbagala kwa ajili ya kwenda kambi ya JKT Mgulani kutambua ndugu zao waliopotea asubuhi leo.
Scout akisaidia kumnywesha uji mtoto mwenye umri wa kati ya miaka miwili anayehifadhiwa katika kambi ya Msalaba mwekundu Kizuiani.
Mama huyu akilia baada ya kumkosa mwanaye katika kambi ya JKT Mgulani, ikiwa ni baada ya kuhangaika sana kumtafuta.
Mmoja wa skari wa JWTZ ambaye alijeruhiwa na mabomu akiwa nje ya kambi ya jeshi Mbagala akielekezwa jambo na askari mwenzie.
Mchaga na dili la pesa Jamaa mmoja wa kichaga alikuwa anasumbuliwa na uvimbe tumboni. Ndugu zake wakaamua kumpeleka hospitali, akatakiwa afanyiwe operesheni. Gharama za Matibabu zilitakiwa milioni mbili.Ndugu na jamaa wakahangishana wakapata pesa hizo kisha wakampatia Dokta ili amfanyie upasuaji ndugu yao. Ile ndugu wanaondoka tu hospitalini pale, mazungumzo kati ya mgonjwa na daktari yakawa hivi: Mgonjwa: Dokta nataka tufanye dili la pesa. Mimi naona huu uvimbe achana nao, nishone tu ili wakija wajue umenifanyia operesheni. Kwenye hizo milioni mbili chukua laki tano niachie moja na nusu , nipate za kunywea bia! Msingi wa biashara hawataki kunipatia ila pesa ya kunitibia wanatoa, huu si ujinga Dokta. Dokta akabaki ameduwaa...
Jiji la Dar es Salaam, jana (Jumatano) lilitikiswa na mabomu yaliyolipuka kimakosa kutoka ndani ya ghala la Jeshi la Wananchi wa Tanzania ‘JWTZ’ lililopo Mbagala Kizuiani na kuzua tafrani kubwa miongoni mwa wakazi wa eneo hilo. Mlipuko mkubwa na wa aina yake ulisikika kwa mara ya kwanza majira ya saa 5:30, asubuhi na kutikisa paa za nyumba sehemu mbalimbali za jiji, jambo lililowafanya watu watoke majumbani na maofisini wakiweweseka kwa hofu ya tukio hilo lisilo la kawaida...
Binti maarufu jijini Dar es Salaam, aliyepata kushiriki mashindano ya kuwania Taji la Miss Tanzania 2005, Maureen Gislary amefumwa laivu tena akifanya mchezo mchafu yeye na msichana mwenzake aitwaye Cheshije Hamisi, kamera yetu imenasa ishu nzima...
Tom, kijana aliyesotea maisha, akiishi maisha ya dhiki na matatizo tupu, huku akishuhudia baba yake mzazi akifa mbele ya macho yake, tatizo kubwa likiwa ni fedha! Alikuwa fukara wa kutupwa, kama ufukara ungekuwa na harufu, basi Tom alikuwa ananuka ufukara, tena wenye harufu kali sana!
Pamoja na ufukara wake akatokea kumpenda mtoto wa kitajiri Mariam, ambaye wazazi wake walikuwa wakimkataza kabisa kuwa naye. Siku moja ambayo baba yake Tom alipozidiwa sana, Mariam huyo huyo ndiye aliyeiba gari la wazazi wake na kumkimbiza baba yake Tom hospitalini. Yote hayo ikiwa ni kwasababu alikuwa akimpenda sana.
Kwa bahati mbaya, wakati Mariam anarudi nyumbani anapata ajali inayomlaza kitandani kwa miaka kadhaa akiwa hajitambui kabla ya kupata nafuu na kurudi chuoni kuendelea na masomo. Hapo ndipo walipokutana kwa mara nyingine katika Ukumbi wa Nkurumah ambapo Tom alikuwa akitoa Semina ya Ujasiriamali. Machozi yanarejea tena katika maisha yake, hasa baada ya Tom kumtambulisha Mariam kwa mchumba wake mpya, Juliana.
Hata hivyo baada ya kushauriwa na Wataalamu wa Saikolojia, anaamua kukubaliana na hali halisi na kuendelea na maisha yake kama kawaida. Lakini katika hali ya kushangaza sana, siku ambayo Tom alipanga kufunga ndoa na Juliana, ndiyo siku anayomvalisha pete ya uchumba Mariam kabla ya kufunga naye ndoa wiki chache baadaye.
Uamuzi huo unasababishwa na mpenzi wake Juliana ambaye alitegemea kumuoa, kumfumania akimsaliti tena na rafiki yake kipenzi. Furaha kwa Mariam inakuwa ya msimu tu, kwani baadaye Tom anamletea Mariam mwanamke mwingine aliyeitwa Mayasa! Hapo ndipo mwanzo mpya wa machozi kwa Mariam.
Mariam ananyanyaswa, anateswa na kulazimishwa kulala chumba cha wageni, mambo yalivyomshinda akaamua kurudi nyumbani kwao, lakini kwa bahati mbaya akaanguka na kupoteza fahamu. Alipotibiwa na kupona, akawaomba wazazi wake waende kuzungumza na Tom, lakini walipoenda Tom na Mayasa, walifukuzwa kama mbwa!
Mariam anaamua uamuzi mpya, anakwenda kuishi kijijini Matombo, Morogoro, kwa bibi yake kwa nia ya kukaa mbali na Tom pamoja na vyombo vya habari. Hakutaka kusikia kabisa habari za Tom. Wakati hayo yote yakitokea, shetani wa pesa anamwingia Mayasa, anapanga mipango ya kumuua Tom ili aweze kurithi mali zote! Je, atafanikiwa? Vipi maisha ya Mariam huko kijijini Matombo? SONGA NAYO....
Inaweza ikawa ni mada ngumu kuikubali kutokana na sababu kadha wa kadha, lakini ukweli unabaki kuwa wanawake wamebainika kuwa na uwezo wa kuishi miaka mingi zaidi ya wanaume. Hii ni kwa mujibu wa tafiti nyingi zilizofanywa hivi karibuni ulimwenguni, ukiwemo ule ulioendeshwa na wanasayansi wa Chuo cha Liverpool John Moores (LJMU) nchini Uingereza...
Mpenzi msomaji, kijana Beka anaendelea kusimulia mkasa uliomkuta huko Bububu Zanzibar alikofundishwa uchawi. Wiki iliyopita nilielezea alivyomfanyia ndumba mrembo mmoja aliyekuwa akiutesa moyo wake ambaye kila alipomtongoza alimkataa kwa madai hakuwa na sifa za kuwa mpenzi wake. Kitendo hicho kilimuumiza sana Beka ndipo aliamua kutumia uchawi ambao ulizaa matunda kwani baada ya dada huyo aliyekuwa akiishi katika familia ya kilokole kuruka ndumba ambazo Beka alizichimbia ardhini kwenye mlango wa ofisi aliyokuwa akifanya kazi, mrembo huyo alipagwa na kwenda ofisini kwa Beka na kuonesha dalili za kumtaka kimapenzi.
Hata hivyo, ili kumalizia kumroga dada huyo, Beka alilazimika kwenda nyumbani anakoishi dada huyo usiku wa manane. Beka alipofika nyumbani kwa dada huyo akiwa na matunguri yake alishindwa kufanikisha kazi yake baada ya ndugu wa dada huyo ambao ni walokole kufanya maombi. Hata hivyo, kwa kushirikiana na mganga mwenzake aitwaye mzee Mohamed wanamua kufanya ndumba zaidi ili kumnasa msichana huyo. Je, watafanikiwa? Ungana na Mwandishi Wetu KULWA MWAIBALE katika mkasa huu wa kweli…
Kuachwa ni jambo linalotia uchungu usioelezeka katika mapenzi hasa pale wanaoachana mmoja anakuwa bado anampenda mwenzake kwa dhati. Wanaoachwa huku wanapenda hukonda kwa mawazo na wakati mwingine hutamani kufa kuliko kuishi bila wapenzi wao.
Wapenzi wengi huuliza “nifanyeje baada ya kuachwa au nitumie mbinu gani ili kurudiana na mpenzi wangu kwani siwezi kuishi bila yeye na kwamba bado namhitaji maishani.” Katika maswali haya wahusika hutaka kujua mambo mawili tofauti lakini yote yanatokana uchungu wa kuachwa.
Moja, ni namna gani wanaweza kufanya ili warudishe uhusiano na waliowaacha ili mioyo yao ipate tiba na pili wanawezaje kuepukana na uchungu wa kuachwa ambao huwakaa moyoni kiasi cha kuwatesa? Majibu ni kama ifuatavyo:
Dodoma Kampuni ya simu za mkononi ya tigo Tanzania kwa kushirikiana na shirika lisilo la kiserikali CODERT imetangaza ushirika maalum wa kuanzisha vikundi vya kuweka na kukopa kwa mfumo kwa mfumo wa kuweka hisa ndani ya kikundi ili kusaidia wananchi wa Tanzania kujikomboa kiuchumi na kuimarisha maisha yao kwa jumla kwenye jamii wanazoishi.
Kambi ya Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ), iliyoko Mbagal Kizuiani, inalipuka na nyumba zilizopo jirani na kambi hiyo zimeshika moto!! Habari kutoka kwenye eneo la tukio zinasema kuwa, mabomu hayo yalikuwa yamehifadhiwa kwenye ghala la silaha la kambi hiyo na yamekuwa yakiripuka kila baada ya sekendu chache na yanendelea kulipuka hadi wakati huu tunawaletea taarifa hii. Kishindo cha milipuko ya mabomu hayo, ambayo yameleta hofu kubwa katika jiji la Dar es salaam, hasa maeneo ya Mbagala, Mtoni kwa Azizi Ally na maeneo ya Temeke, kimekuwa kikisikika hadi maeneo ya Mwenge.
Kwa mujibu wa habari za Radio One, mtu mmoja hadi sasa ameripotiwa kufa katika kadhia hiyo ya aina yake baada ya bomu moja kuangukia ndani ya nyumba yake na kuiteketeza na kwa sasa barabara ya Kilwa imefungwa, magari kutoka Kongowe kuja Mbagala, yamezuiwa. Waandishi wetu wako eneo la tukio na tutawajia baadae na picha za tukio hili la kwanza na la aina yake kutokea nchini.
Maiti ya mwanaume anayekadiriwa kuwa na umri wa miaka kati ya 35 na 40, leo asubuhi imekutwa ikielea katika Mto Msimbazi karibu na daraja linalozitenganisha wilaya ya Ilala na Kinondoni jijini Dar es Salaam, maeneo ya Kigogo njia panda. Kufuatia tukio hilo wakazi wanaoishi jirani na eneo hilo walitoa taarifa Polisi ambao walifika na kuuchukua mwili huo kisha kwenda kuuhifadhi katika Hospitali ya Taifa ya Muhimbili wakati uchunguzi ukindelea. Mpaka mwili huo unaondolewa eneo hilo, hakuna aliyejitokeza kumtambua marehemu.
Mwili wa marehemu ukitolewa kutoka mtoni
Wasamaria kwa kushirikiana Askari kanzu wakiwa na mwili wa marehemu katika barabara ya Kawawa wakienda kuupakiza kwenye 'Difenda'
Na Waandishi Wetu Siku chache baada ya ‘kumwagana’ na Jumbe Yusuf Jumbe (aliyedaiwa kuwa ni mpenzie), Miss Tanzania 2006/07, Wema Isaac Sepetu amenaswa katika Hoteli ya Coral Beach, Masaki, jijini Dar es Salaam, akiwa na Mbunge ‘yanki’ wa Kigoma Kaskazini (CHADEMA), Zitto Zuber Kabwe, Risasi lina ‘ fulu muvi’.
ILIPOISHIA... Ikingi amempa lifti msichana aliyejitambulisha kwa jina la Jasmini. Walipofika Sinza ya Makaburini, anashangaa kumuona yule msichana akiwa barabarani, alipogeuza shingo yake upande wa pili, hakumuona. Ikingi akapiga kelele. Je, nini kitaendelea? Mwandishi Wetu JOSEPH SHALUWA anaendelea...