Tembelea... |
 |
Kalenda |
 |

Marafiki wetu |
 |
Habari Zilizopita |
 |



Nani Yupo / Alikuwepo |
 |
|
|
 |
|
|
 |
 |
KESI YA LIYUMBA KUFUTWA!
|
photos |
|
 |
 Kesi inayomkabili aliyekuwa Mkurugenzi wa Utawala na Mipango wa Benki Kuu ya Tanzania (BoT) Amatus Liyumba na mwenzake Deus Kweka, katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu, leo imetakiwa kufutwa na Mawakili wao kwa mujibu wa kifungu cha sheria za nchi hii, kinachoutaka upande wa mashitaka kukamilisha upelelezi ndani ya siku 60, vinginevyo kesi hiyo kufutwa. Kesi hiyo ina zaidi ya siku 60 na upelelezi bado haujakamilika. Pichani (kushoto) Liyumba akirudishwa Mahabusu leo mchana mara baada ya kesi yake kuahirishwa mpaka Aprili 13, mwaka huu, itakapotajwa tena kabla ya kusikilizwa Aprili 25, mwaka huu. MAAFANDE WA 'DIFENDA' WAMVAMIA ‘SANGOMA’ ANAYEENDELEA KUTIBIA. Katibu Mwenezi wa Chama cha Waganga wa Jadi, Tiba asilia na Wakunga wa Jadi (CHAWATIATA), Bi. Fatuma Mwachengwa, akiwaelezea wanahabari kilio chao baada ya Askari Polisi, kumuingilia mmoja wao, Tandale Hill Top jijini Dar, wakitaka kumsomba kwa tuhuma za kuendelea kutibu.Hata hivyo Bi. Fatuma, ambaye aliongozana na uongozi wa kundi hilo walidai kuwa, Mganga huyo aliachiwa baada ya kuombwa shilingi laki 3 lakini akawapa laki moja. Waganga hao wanatarajia kulifikisha suala hilo kwa Kamishna wa Jeshi la Polisi Kanda Maalumu ya Dar es Salaam, Suleiman Kova, mara baada ya kulifanyia kazi. DAR SASA KAMA MAMTONI. Jiji la Dar es Salaam hatimaye limeanza kupata sura ya kuvutia kufuatia majengo marefu ya kupendeza kama linavyoonekana pichani, jengo hili liitwalo Benjamin Mkapa, lililopo Barabara ya Maktaba, maeneo ya Posta jijini. Jengo hili linalinganishwa na majengo ya mamtoni. PICHA: RICHARD BUKOS NA CHRISTOPHER LISSA /GPL.
Dear Guest you have enter our site without being Registered. We recommend to register to view more...
"Mgeni wetu unatakiwa Kuregista kupata Udaku Wote..."
|
|
 |
|