Katika jiji Dar es Salaam utakuta Bajaji nyingi zikisubiri abiria kwenye vituo vya usafiri, lakini kwa jiji la Tanga, Baskeli ndio utakuta zimejaa katika vituo mbalimbali zikisubiri abiria. Baskeli zikiwa zimepaki katika kituo kikuu cha mabasi mjini Tanga zikisibiri abiria, usafiri wa bakeli maarufu kwa jina la Bodaboda, zinabeba abiria kwa safari za mjini kati ya shilingi 200 hadi 500. hata wasiwasi.
Tamasha la Nchi za Jahazi (ZIFF) linalofanyika visiwani Zanzibar, limepamba moto, leo ikiwa ni siku yake ya 4. Burudani zinazendelea kutoka kwa wasanii mbalimbali, kama vile THT yenye wasanii mahiri kama Barnabas (pichani juu) anayetamba na wimbo wake wa Njia Panda pamoja na Mwasiti (pichani chini) ambaye alimchengua Mzungu mmoja na wimbo wake wa Nalivua Pendo na kupagawa kama anavyoonekana pichani chini.
MTIKISIKO mkubwa umelikumba eneo la Kongowe Mzinga, lililoko Kata ya Mbagala wilaya ya Temeke jijini Dar es Salaam ambapo watu wanaosadikiwa kuwa ni majambazi kwa siku kadhaa wamekuwa wakivamia maduka, kuteka watu na wamewaua kwa risasi raia wema wawili...
KWA mujibu wa maoni ya wasomaji wetu, kuna maamuzi mbalimbali yaliyofanywa na baadhi ya viongozi wetu kiasi cha kufikia hatua ya kulitia hasara taifa au kumuwekea doa kiongozi mwenyewe. Haya ni baadhi ya majina yaliyotajwa na wasomaji yakihusishwa na maamuzi hayo mabovu...
Askri Polisi wilayani Mag, mwenye namba F4152 aliyejulikana kwa jina moja la PC John amemuua kwa kumpiga risasi mahabusu mmoja aliyefahamika kwa jina la Salum Athumani (28) wakati akifikishwa...
Wadau mbalimbali wa sanaa za maigizo na vichekesho nchini, wameliponda Kundi la Vichekesho la Orijino Komedi kwa kudai limekufa kutokana na kushuka kiwango chake ikilinganishwa na hapo awali...
MENEJA wa Baa moja maarufu mjini Moshi, James John (33) maarufu kwa jina la Pendoo anadaiwa kufanyiwa umafia na kundi moja la vigogo (wafanyabiashara) ambao walimteka na kumpeleka nje ya mji umbali wa kilometa 15 kabla ya kumtesa na kumuua...
Wiki iliyopita nilianza kuongea juu ya namna ambavyo matumizi yetu mabaya ya tulichonacho yanaathiri maendeleo yetu na leo namalizia sehemu ya mwisho kabla sijaanza kuongea juu ya kichwa cha habari nilichokiandika hapo juu...
Nachukua nafasi hii kuwashukuru wasomaji wangu wote kwa kufuatilia hadithi yangu ya The Blood Deal (kazi ya damu) ambayo imemalizika wiki iliyopita, nawashukuru sana kwa kuendelea kuniunga mkono kwa miaka yote kumi ambayo nimekuwa nikiandika hadithi kwenye magazeti nami naahidi kuendelea kujitahidi kufanya kazi kwa nguvu na kutunga hadithi nzuri ambazo zitatoa mafundisho kwa watu badala ya kuendelea kuwaburudisha peke yake...
Hakuna kitu kibaya kama kumuua baba yako mzazi, tena baba ambaye walikutana na mama kwenye starehe ndipo wakapandikiza mbegu za uhai wangu. Binafsi nilifanya hivyo kwasababu ya ombi kutoka kwa mama yangu mzazi, mwanzoni nilikataa katu katu kumuua baba yangu lakini siku zilivyozidi kwenda nilijikuta nikishawishika kusitisha uhai wake...
Maadhimisho ya kupiga vita Madawa ya kulevya duniani yameadhimishwa Bongo na yamewahusisha vijana mbalimbali kwa kuwapima kama kweli hawatumii madawa hayo (Bangi na unga) pamoja na madawa mengine yanayoathiri maisha yao, hapa baadhi ya vijana wa Mwembe Yanga Temeke wakishiriki mchezo wa kukimbiza kuku na aliyemkamata ilikuwa ni zawadi yake.
...Jamaa wafurahia kuku wao na kutoka nduki
...mabinti nao hawakuachwa nyuma katika mbi za kuku
Ni kama anasema: nani kasema mboga hamna, cheki bonge la mjogoo huu, siamini kama siku ya leo na mimi narudi nyumbani na kitoweo cha kuitosheleza familia yangu, hata kama tuko kumi, lazima atatosha tu.
Waandaaji wa Tamasha la kupiga vita madawa ya kulebya wakitafakari jambo mara baada ya washiriki wa zoezi hilo kuondoka na kuku bila kuruhusiwa huku Afisa Elimu kata ya Tandika akishuhudia mtanange huo.
Afisa Elimu kata ya Tandika Bi. Beatrice Nyangu, Afisa Elimu kata ya Tandika, akiwashuhudia jinsi vijana wanavyopambana na upigaji vita nadawa ya kulevya katika viwanja vya Mwembe Yanga jijini Dar Es Salaam leo. PICHA NA ISMAIL MANG’OLA / GPL.
LAZIMA WATOKE WANANGU Produza wa Studio ya Bion 2 Records iliyopo Tabata Bima jijini Dar Es Salaam anayekwenda kwa jina la Kaju, akiwa katika harakati za kukamilisha moja ya kazi za wasanii wa kizazi kipya ambao wamekuwa wakifabyia kazi zao katika studio hiyo, Prodiza huyu ni mmoja wa maproduza wadogo kiumri kiliko maproduza wengine hapa nchini lakini uwezo alionao ni heshima.
UJENZI STENDI KUU YA SEGEREA Mmoja wa wafanyakazi wa kampuni ya ujenzi wakikarabati Stendi Kuu ya mabasi katika Kituo cha daladala Segerea, stendi hiyo inelekea ukingoni kukamilika ambapo magari yatakuwa yakitumia kwenda Ubungo bila kupitia Barabara ya Mandela ambako yataunganisha hadi Mbezi, Kibaha na kuendelea. Inaaminika kuwa usafiri huo utawasaidia kwa kiasi kikubwa wananchi wa maeneo hayo na kuondoa adha ya foleni za mara kwa mara.
ZAMANI WALIKUWA HAWAFUGIKI Licha ya kuwepo nguo aina ya Khanga, jina hilo limetokana na ndege hawa ambao wanarangi nzuri ambayo imezaa jina ya nguo ambayo ni nguo ya heshima. Zamani ndege hawa walikuwa hawafugiki kama ilivyo hivi sasa.
WE KAKA WEEE MBONA UNAJITAFUTIA MAKUU? Jamaa huyu hakika alitaka kujitafutia mambo makubwa, eti anakimbizana na Bajaj ili kuokota kipande cha Muhogo alichorushiwa na jamaa waliokuwa kwenye Canter, alikuwa akikimbia hovyo bila kuangalia usalama wake.
...Ameridhika na vipande vyake viwili vya muhogo…. PICHA NA ISMAIL MANG’OLA / GPL.
Katika gazeti letu la Ijumaa la Juni 25 – Julai 05 mwaka huu, tulikuwa na habari iliyokuwa ikizungumzia maisha ya wasanii wawili – wachekeshaji wa kikundi maarufu cha Orijino Komedi, Mpoki na Joti – ambapo maisha yao ya hapo nyuma yalikuwa ya dhiki, licha ya wao kuwa mstari wa mbele kuwashambulia na kuwadhalilisha watu ambao wanadai kwamba wamefilisika na “wanahangaika na dunia hivi sasa.”
Habari hiyo ina kichwa cha habari cha “Mpoki, Joti – Maisha yao enzi za Kufulia yaanikwa”. Neno “kufulia” limeingia katika msamiati wa mitaani, hususani kwa kuanzishwa na wasanii wa kikundi hichohicho likiwa na maana ya “kuishiwa, kufilisika au kutumia vibaya utajiri mtu aliokuwa nao”. Kwa ufahamisho tu, kundi hilo la wasanii linaundwa pia na
Na Imelda Mtema, Zanzibar Wakati Waislamu nchini wakiomboleza kifo cha Kaimu Mufti, Sheikh Suleiman Gorogosi, Mhadhiri Mwandamizi wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam, Profesa Haroub Othman naye amefariki dunia ghafla akiwa usingizini katika Hoteli ya Abuso, mjini Zanzibar usiku wa kuamkia jana.
Picha za mwisho alizopigwa marehemu Profesa Haroub (kushoto) na Mwandishi Wetu saa sita usiku wakati akiwa katika sherehe za uzinduzi wa ZIFF, ikiwa ni takriban saa sita kabla ya kifo chake. Hapa alikuwa akiongea na Profesa mwenzie ambaye ni Waziri wa Afya wa Kenya, Prof. Peter Anyang’ Nyongo.