arrowSet HomePage |arrowBookMark Us
right
lines

Global Publishers Tanzania- Uwazi » ijumaa wikienda » NDOA YA MSANII ALIYEKATWA MGUU: NI VILIO

Tafuta  

Tembelea...

Kalenda

Gazeti la Ijumaa

Marafiki wetu

Habari Zilizopita

Soma Magazeti Yetu...

Gazeti la Risasi Mchanganyiko
Amani
Gazeti la Ijumaa Wikienda

Bongo Celebrities ...

 
Habari Zinazotamba Habari Mchanganyiko
» Aunt Ezekiel alivyopigika k ...
» ZITO LAIBUKA
» KIGOGO WA MURO NAYE KUKAMAT ...
» GLOBAL PUBLISHERS MUSIC PLA ...
» JERRY MURO AKOSWA RISASI
» Kigogo afanyiwa umafia
» JERRY: NASAKWA NIUAWE!
» (Ni mdogo mno kufa) - 5 ...
» Maximo akiri...
» Juma Mbizo naye aitosa ...
» I am back from hell
» (Nitakufa kwa ajili ya ...
» MAMBO YAENDA YAKIONGEZE ...
» SAFARI NJEMA MHESHIMIWA

NDOA YA MSANII ALIYEKATWA MGUU: NI VILIO

ijumaa wikienda

NDOA YA MSANII ALIYEKATWA MGUU: NI VILIO

NDOA YA MSANII ALIYEKATWA MGUU: NI VILIO

NDOA YA MSANII ALIYEKATWA MGUU: NI VILIO

sherehe hiyo ilitawaliwa na vilio na majonzi, hasa pale Bibi harusi alipoingia kwenye eneo la wazi lililoandaliwa kwa shughuli hiyo akiwa amekaa kwenye baiskeli ya gurudumu (Wheel Chair).

Aidha, vilio vilisita baada ya kukaa kwenye kiti kilichoandaliwa ‘spesho’ kwa Bibi harusi, lakini vilianza tena baada ya maharusi hao kuimba wimbo kwa pamoja unaoelezea mapenzi yalivyo.

“Mke wangu sitakuacha, wewe ni mahabuba wangu, sitakuacha,” Sajuki aliimba wimbo huo. “Mume wangu unilinde, unipende, usiniache…,” Wastara naye alijibu na kusababisha vilio kutoka kwa wageni waalikwa. Aidha, yeye mwenyewe alishindwa kuendelea kuuimba wimbo huo na kujikuta akilia kwa uchungu mkubwa.

Habari zinasema wimbo huo pia waliuimba kwenye filamu ya Mboni ya Jicho Langu ambayo iliwashirikisha wote. Msanii wa kike wa filamu nchini, Aunt Ezekiel ambaye alikuwa miongoni mwa waalikwa, alishindwa kuvumilia na kuporomosha machozi huku akisema: “Kwa kweli kwa namna hii huwezi kuvumilia hata uwe na roho ya aina gani ni uchungu mno, lakini Sajuki ameonesha upendo wa ujasiri.” Ukumbi huo ulizidi kutawaliwa na simanzi ingawa na makofi kwa mbali, pale bwana harusi aliposhika ‘maiki’ na kuwatangazia waalikwa kuwa, Wastara ni mkewe wa maisha, kamwe hatomwacha.

“Nimesimama hapa kwa ajili ya kumhakikishia nyonga mkalia ini wangu (Wastara) kuwa mimi ni wake milele sitomuacha mpaka kifo,” alisikika Sajuki.
Baada ya Shamrashamra hizo, Sajuki alimbeba Wastara huku akicheza naye wimbo wa mwanamuziki wa Sauzi, Yvonne Machaka ‘Chakachaka’ uitwao ‘Mkomboti’ huku akielekea naye kwenye gari kwa ajili ya kuondoka. Tukio hilo lilisindikizwa na wasanii kibao kwa nyuma huku wakicheza mpaka maharusi hao walipopanda gari na kwenda kwenye Fungate lao Kigamboni, jijini Dar es Salaam.

Baadhi ya watu waliohudhuria harusi hiyo walisema kuwa, hawakutegemea kama Sajuki angemuoa Wastara, hasa baada ya kukatwa mguu na kwamba kwa tukio hilo ameonesha upendo wa hali ya juu. Wasanii waliohudhuria sherehe hiyo ya ndoa ni Steven Kanumba ‘Kanumba’, Vincent Kigosi ‘Ray’, Aunt Ezekiel, Emmanuel Mgaya ‘Masanja’, na Ahmed Olotu ‘Mzee Chilo.’ Wengine ni Hisan Muya ‘Tino’, Adam Kuambiana, William Mtitu ‘Mtitu’ na Hawa Mkama.

NDOA YA MSANII ALIYEKATWA MGUU: NI VILIO

NDOA YA MSANII ALIYEKATWA MGUU: NI VILIO

NDOA YA MSANII ALIYEKATWA MGUU: NI VILIO

NDOA YA MSANII ALIYEKATWA MGUU: NI VILIO

NDOA YA MSANII ALIYEKATWA MGUU: NI VILIO

NDOA YA MSANII ALIYEKATWA MGUU: NI VILIO

NDOA YA MSANII ALIYEKATWA MGUU: NI VILIO

PICHA:IMELDA MTEMA


 (Votes #: 9)
    (8 June 2009)
Soma Zaidi: 6800 | Maoni Yako (68)

Udaku Mwingine

ijumaa wikienda
 
  • Ndoa ya mkosi!
  • Msanii Sajuki, Mchumba wake wapata ajali mbaya
  • Ndoa ya Sajuki na Wastara: Visa Vyaanza
  • MASIKITIKO
  • Pigo la tatu... Wastara aanguka, apoteza fahamu
  •    

    #1 Author: Miriam (8 June 2009 02:03)

    Sajuki kweli wewe ni mwanaume umekamilika, hakuna anayeweza kufanya ulichofanya hasa nyie masupa staa ila angalia usipate tamaa baadaye ukamtesa mtoto wa watu na kama umeamua mpende kweli utabarikiwa, isiwe ni mwanzo tu.

    Nenda KCMC muweke mguu wa bandia atakuwa anavaa jisi na raba hakuna atakayejua atachechemea kidogo tu. mimi ninajua kwani nina mtoto wa ndugu yangu naye hana mguu ila wamempa wa bandia ukimwoma ghafla huwezi jua kama hana mguu. pole
     
    fast    

    #2 Author: njechellea (8 June 2009 02:04)

    Nakupongeza bwana harusi kwa upendo na ujasiri uliouonyesha,lakini kumbuka hiko ni kama kiapo, ukija kumuacha naamini mungu atakuadhibu.
     
    fast    

    #3 Author: Amna (8 June 2009 02:06)

    This is a true love
     
    fast    

    #4 Author: Eric Esron, Mg. (8 June 2009 02:10)

    poleni sana na hongera!Ndoa yenu iwe ya amani, furaha, upendo na uvumilivu! baraka tele....!!!
     
    fast    

    #5 Author: MapigoSaba (8 June 2009 02:15)

    Vema wameoana. Lakini hii ishu ndogo ukilinganisha na yule mwanamke wa kimarekani ambaye alikubali aolewe na mchumba wake ambaye sura yake yote iliharibiwa vibaya na kuakatika mikono kwa bomu vitani Iraq, jamaa alikuwa anatisha hata kwa kumtazama. Huyu dada kama ana fedha za kutosha aende nje apate mguu wa bandia ambao utafanana kabisa na mguu wake mwingine, na baada ya mazoezi atatembea wima kama awali bila kujua kuwa ni mlemavu.Mfano mzuri ni mkono bandia mh. Muzihiri. So global publisher hapa ndio pa kuosha jina lenu kwa kumsaidia huyu dada kuweza kutembea tena! pia kuikumbusha serikali na wadau kuleta huduma kama hizo hapa nchini.
     
    fast    

    #6 Author: promise (8 June 2009 02:16)

    OH! mpaka raha mwenyezi mungu awape ndoa yenye furaha
    muishi na kusikizana Inshallah.
     
    fast    

    #7 Author: emmanuel (8 June 2009 02:19)

    good for the fox
     
    fast    

    #8 Author: Jane (8 June 2009 02:21)

    Hongereni maharusi siri nikama historia flani hivi na inatoa machozi kwakweli, but all the best maana mpaka kufikia hatua hiyo inaonyesha mna mapenzi ya kweli. Hujafa hujaumbika
     
    fast    

    #9 Author: Tanzomani (8 June 2009 02:21)

    Du! Adimu sana hii kwa maisha ya sasa, Hongereni sana na nawaombea ALLAH wape uvumilivu, mapenzi ya kweli na kizazi kilichobora kabisa, Ameen.
     
    fast    

    #10 Author: EMANUEL (8 June 2009 02:31)

    MUNGU NI MWEMA........
     
    fast    

    #11 Author: Lissa (8 June 2009 03:06)

    Hongera sana maharusi.
    Hongera sana Sajuki, umeonyesha ushujaa katika mapenzi
    Hili ndilo Penzi la kweli.
    Katika moyo wako unajua na unaamini unaweza lakini nakushauri mtangulize sana Allah. Umri bado mdogo sana hivyo yanaweza tokea mengi ya mabadiliko katika maisha.
    MUNGU AWABARIKI, AWAPE MOYO WA UPENDO ZAID, AWAPE AMANI KATIKA NYUMBA YENU, AWAJALIE RIZKI ZA HALALI, AWAJALIE UVUMILIVU NA FAMILIA, WATOTO WENYE KHERI NANYI INSHALLAH.
     
    fast    

    #12 Author: ju (8 June 2009 03:08)

    ongera sajuki huo ndio uwanaume
     
    fast    

    #13 Author: mwatima (8 June 2009 03:10)

    hengera sana samir na wastara mungu awazidishie imani na upendo ila mesikitika sana mpaka kujikuta machozi yananitoka lkn mungu mkubwa na ni mtihani lazima muukubali nawaombea maisha ya kudumu
     
    fast    

    #14 Author: SHIDA FRANK. (8 June 2009 03:19)

    Namuomba Mungu awatangulie katika maisha yenu. Mpendane daima mpaka kifo kiwatenganishe.
     
    fast    

    #15 Author: Rach! (8 June 2009 03:34)

    hongereni sana na Mungu azidi kuwalinda katika maisha yenu na awajalie kheri na fanaka! usijali dada wastara yote ni mipango ya mungu pia Mungu anakupenda sana thats'y umishuhudia siku ambayo ulikuwa unaingoja kwa hamu sana! pia sajuki big up sana kaka yangu umonyesha mfano kwa wanaume wengine kukubali mabadiliko yanapo tokea!Mungu akuzidishie ujasiri zaidi!!!!!!!!! ha ha ha ha ha ha!!! endeleeni kupendana sana tuu! wink wink
     
    fast    

    #16 Author: regina (8 June 2009 03:45)

    jamani hongereni na mungu awape nguvu muendelee kupendana hivyo hivyo. ila baadaye anaweza kupewa mguu wa bandia huo ukishapona.
     
    fast    

    #17 Author: kimavi (8 June 2009 04:08)

    jamani! so sad, mungu awabariki awape ustahamilivu na upendo wa kweli kutoka moyoni, nimehisi machozi jamani
     
    fast    

    #18 Author: Naira (8 June 2009 04:16)

    kila la kheri ktk ndoa yenu, mungu awaepushie vishawishi.
    Hongera Sajuki kwa kuonyesha mapenzi ya dhati Big Up Kaka
     
    fast    

    #19 Author: Monica Joel (8 June 2009 04:19)

    Mapenzi ndiyo hayo bwana,,, kaka hongera mwenyezi Mungu awajalie mema katika ndoa yenu na pia awabariki na watoto.
    Monica Joel
     
    fast    

    #20 Author: Dtv -Arusha (8 June 2009 04:21)

    Hongera sana Sajuki, mfano uliouonyesha ni mzuri wenye kuelewa watakuiga. Pole sana Wastara mumeo ameamua kukuonyesha upendo wake wa dhati, pia elewa muumba bado anakupenda nahuyo mumeo ndio changuo lake kwako. Ninawaombea mafanikio mwema.
     
    fast    

    #21 Author: Mtu mzima (8 June 2009 04:34)

    Mashallah! wamependeza M/mungu awape moyo wa Imani na ku mkumbuka na pia kuiheshimu ndoa yenu awajaliye mpate kizazi njema na chenye Upendo na kizazi chenye kumuheshimu na kumuogopa M/Mungu. AMIN

    yooote hiyo ni mitihani ndugu zangu yeyote yaweza mfika, msahau yaliopita mgange yajayo...
     
    fast    

    #22 Author: sofia (8 June 2009 04:38)

    Kwa kweli mmependeza sana, pia nampa hongera sajuki kuchukuwa uwamuzi wa kumuowa amefanya jambo ambalo linataka watu waige katika jamii,nawatakia maisha mema na upendo.Amiin
     
    fast    

    #23 Author: Poaz2 (8 June 2009 04:40)

    Hongera sana bwana na bibi harusi kwa upendo na ujasiri mlio uonyesha, huu ni mfano fika kwa waTanzania woote kwa ujumla. sina la kuongezea ila Wasia wangu wa soote hapa tukumbuke 'KAMA HUJAFA HUJAUMBIKA'
     
    fast    

    #24 Author: maua (8 June 2009 04:51)

    Mungu awajaalie jamani yaani roho imeniuma ..
     
    fast    

    #25 Author: JIMY (8 June 2009 05:12)

    ongera sana sajuki mungu atakuongoza kwa kila kitu na yote mungu ndiye aliye panga endelea kumpenda huyo ndiyo mkeo alali .usimtende kwani gods kwons.ongera sana kwa kufunga pingu za maisha.
     
    fast    

    #26 Author: miss brazil (8 June 2009 05:14)

    Hao lazima watakuwa wamelogwa si bure. Haiwezekani.

    Labda ama mwanamke au mwanaume au wote kuna mtu alimdanganya wataoana nae halafu akamshiti, sasa nae ndo kamwendea NGENDE.

    Loo. Binadamu sie jamani!
    sajuki usimwache mkeo wala kumnyanyasa, kwanza mkeo mzuri sana
     
    fast    

    #27 Author: vivian (8 June 2009 06:05)

    Mungu awatangulie ...........am so,so proud of you..Mungu ni mkubwa awawezeshe na kuwafanikisha katika kila jambo,,,,,,,kaka Sajuki mimi nakuomba uendelee kuwa na ujasiri na upendo huo ulionyesha kwa mkeo...Hongera sana bwana na bibi harusi
     
    fast    

    #28 Author: kojozi (8 June 2009 06:14)

    Kaka ongela kwa kumuonyesha mpenzi wako mapenzi ya kweli bwana awe nanyi milele.
     
    fast    

    #29 Author: Jas (8 June 2009 06:16)

    Watu wanapata changamoto ya majibu (+) ya UKIMWI na wanaoana vilevile sembuse kukosa mguu???

    Hongereni wanandugu ila mdhihirishe huo upendo wa keli na Mola awajaalie ndoa yenye kudumu na furaha.
     
    fast    

    #30 Author: beka unguja (8 June 2009 08:35)

    namshukuru Sajuki kwa jitihada zake alizonazo kwa msimamo wake mpaka wakfunga pingu za maisha tafadhali kaka Wastara ni mzur usimwashe milele
     
    fast    
    Back  <<  1 2 3  >>  Next Page

    Add comments

    Name:
    E-mail:

    Code:
    Include security image CAPCHA.
    to renew the code
    Enter Code:

     

    Kura Yako / Poll

    Habari Katika Picha


    Gazeti la Uwazi



    Nani Yupo / Alikuwepo


    Home Page | About Us | Regista | Picha | Bongo Celebrities | Maoni | Contact Us

     hit counter

    counters

    2008 © globalpublisherstz.com