arrowSet HomePage |arrowBookMark Us
right
lines

Global Publishers Tanzania- Uwazi » uwazi » MWANAFUNZI CHUO KIKUU ALIVYOUAWA

Tafuta  

Tembelea...

Kalenda

Gazeti la Ijumaa

Marafiki wetu

Habari Zilizopita

Soma Magazeti Yetu...

Gazeti la Risasi Mchanganyiko
Amani
Gazeti la Ijumaa Wikienda

Bongo Celebrities ...

 
Habari Zinazotamba Habari Mchanganyiko
» Aunt Ezekiel alivyopigika k ...
» ZITO LAIBUKA
» KIGOGO WA MURO NAYE KUKAMAT ...
» GLOBAL PUBLISHERS MUSIC PLA ...
» JERRY MURO AKOSWA RISASI
» Kigogo afanyiwa umafia
» JERRY: NASAKWA NIUAWE!
» Waliomzushia Amina msuk ...
» MVUA ZINAVYOKWAMISHA US ...
» We mama mbavu zangu..!
» VICKY AZIKWA NA GAUNI L ...
» Arsenal yaifyatua Slavi ...
» Lukuvi kukutana na wate ...
» UBUNIFU WA MATANGAZO!

MWANAFUNZI CHUO KIKUU ALIVYOUAWA

uwazi

Tukio hilo la kusikitisha lilitokea Jumamosi ya wiki iliyopita majira ya saa 3, usiku katika Hosteli ya wanafunzi ya Chuo Kikuu cha Dar es salaam iliyopo Mabibo wilayani Kinondoni jijini Dar es Salaam kwa kile kinachodaiwa kuwa ni wivu wa mapenzi.

Uwazi lilipotembelea eneo la tukio liliambiwa kwamba siku hiyo, kulikuwa na Bonanza la michezo lililoandaliwa na SPW (Student Partinership Worldwide) wakishirikiana na serikali ya wanafunzi chuoni hapo (DARUSO) ambalo lilianza saa 9 alasiri na kumalizika saa 3 usiku kwenye viwanja vya mpira vya Mabibo hosteli.

Aidha, taarifa hizo zilieleza kwamba muda mchache baada ya marehemu kutoka mazoezi ya kwaya ya Kanisa la Roman Catholic yaliyokuwa yakifanyika jirani na hosteli hizo, alipita kwenye tamasha hilo ingawa hakukaa kwa muda mrefu kabla ya kwenda kwenye chumba chake namba 250 kilichoko Block C kwa malengo ya kujipumzisha huku akiwaacha wenzake wakiendelea na chereko.

Habari hizo zilieleza kwamba mara marehemu alipofika chumbani alienda kuchukua chakula na maji ya kuoga na aliporejea alifuatwa na mpenzi wake huyo ambaye alimgongea kabla ya kumfungulia ingawa hakumruhusu aingie ndani kwani alisimama ukutani pembeni ya mlango ili kumsikiliza.

Taarifa kutoka eneo la tukio zinadai kuwa baada ya kuanza mazungumzo nje ya chumba cha marehemu, Mpenzi wake huyo alichomoa kisu mfukoni na kuanza kumchoma nacho na kumfanya aanguke sakafuni na kuvuja damu nyingi.
Kwa mujibu wa taarifa za uhakika kutoka kwa mashuhuda, marehemu alichomwa kisu mara tatu kwenye matiti hali iliyomfanya aanguke na kugaragara huku damu zikiwa zimetapakaa sakafuni (kama inavyoonekana pichani ukurasa wa mbele)

Taarifa zaidi zinasema, katika damu hizo zilizokuwa zikitambaa kwenye korido za hosteli hiyo, kulikutwa kisu kilichokuwa kimekatika katika vipande viwili (Kama inavyooneka pichani ukurasa wa mbele) hali iliyoashilia kuwa uchomaji wake ulikumbana na mfupa hivyo kukifanya kishindwe kuhimili hivyo kukatika.

Hata hivyo baada ya tukio hilo ambalo ilikuwa vigumu kushuhudiwa na wanafunzi kwani wengi wao walikuwa kwenye tamasha, muuaji alitoroka eneo la tukio kwa kukimbia hali iliyowashtua baadhi ya wasomi wachache waliokuwa vyumbani hivyo kuanza kumfukuza wakihisia ni mwizi huku wakipiga kelele zilizovuta hisia za watu wengi hivyo kukusanyika.

Katika hali ya kushangaza walimtambua kama mwanafunzi mwenzao ingawa hata hivyo hali aliyokuwa nayo ya hofu na kutweta iliwafanya wamkabe na kumrudisha alikotokea ndipo walipobaini kuwa amefanya mauaji hayo kisha kuanza kumpa kibano kikali ambacho kilimfanya ajeruhiwe na baadaye kutoa taarifa polisi ambao walifika na kumtia hatiani mtuhumiwa.

Aidha, taarifa Uwazi ilizozipata zinasema kwamba mahusiano kati ya wawili hao yalikuwa yamegubikwa na mgogoro mzito uliotokana na marehemu kusitisha uhusiano naye kiasi kwamba Masamba (mtuhumiwa wa mauaji) alikuwa haruhusiwi kuingia chumbani kwa marehemu kama ilivyokuwa zamani kabla ya kuhitilafiana.

Taarifa zilizidi kusema kwamba, wiki moja kabla ya tukio mtuhumiwa baada ya kuona marehemu haoneshi dalili za kurejesha uhusiano wa awali, alikusanya vitu vyake na kuviweka kwenye begi kabla kutaka kujirusha ghorofa ya tatu kwa lengo la kujiua ambapo aliwahiwa na mashuhuda na kuokolewa.

Baada ya tukio hilo la maujai kutokea hofu kubwa ilitanda maeneo ya hosteli huku baadhi ya wanafunzi wakienda kulala kwa ndugu zao walio karibu kwa kuhofia usalama wao.

Naye Kasonzo Sebastian, Katibu wa Kwaya ya Mtakatifu Filomena ya Mabibo Hostel ambaye alikuwa akiimba pamoja na marehemu alisema kwamba, wameshtushwa na kifo hicho na ni pigo kubwa kwa wanakwaya, waumini wa Kanisa la Roman Catholic, wanafunzi wenzake na watu wote kwa ujumla.

Sebastian alisema kwamba, marehemu alikuwa mshirika mzuri katika kwaya na isitoshe Jumapili ya Juni 31, mwaka huu, alienda kufanya kazi ya kuuza Kanda ya albamu yao ya kwanza iitwayo ‘Mbawa za Asubuhi’ shughuli aliyoifanya kwa uaminifu.

Katibu huyo aliendelea kusema kwamba, siku hiyo ya tukio marehemu alifika mapema saa 1:30 usiku katika mazoezi ya kwaya na ilipokaribia saa 3 za usiku wanakwaya waliagana na kila mmoja kuendelea na ratiba yake wakiwa na imani kwamba kesho yake Jumapili (Juzi) wangekuwa naye kuongoza ibada katika Kigango cha Boko, zoezi lililofanyika bila yeye kuwepo.

“Kwa kweli tulipopata taarifa juu ya tukio hilo hatukuamini hadi pale tulipofika katika chumba chake na kumuona akilia kwa maumivu makali ya majeraha yaliyotokana na kisu, Mungu ailaze roho ya marehemu Bertha mahali pema peponi, Amin,” alisema Sebastian kwa uchungu.

Naye Kamanda wa Polisi Mkoa wa Kipolisi wa Kinondoni Mark Kalunguyeye alithibitisha kutokea kwa tukio hilo na kuongeza kuwa mtuhumiwa anashikiliwa na jeshi la Polisi na jana (Jumatatu) alisomewa mashtaka katika mahakama ya wilaya ya Kinondoni huku mwili wa marehemu ukihifadhiwa katika hospitali ya Mwananyamala.

Makamu Mkuu wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam Profesa Rwekaza Mukandala alikaririwa akisema kuwa tukio kama hili halijawahi kutokea katika historia ya chuo hicho tangu kianzishwe na kuelezea masikitiko yake kwa familia ya wafiwa.

MWANAFUNZI CHUO KIKUU ALIVYOUAWA

MWANAFUNZI CHUO KIKUU ALIVYOUAWA

MWANAFUNZI CHUO KIKUU ALIVYOUAWA


 (Votes #: 7)
    (9 June 2009)
Soma Zaidi: 7235 | Maoni Yako (44)

Udaku Mwingine

uwazi
 
  • SIRI YAFICHUKA
  • Denti aliyeuawa chuo kikuu, yadaiwa Chanzo ni simu
  • Kijana auawa akigombea demu
  • MUME AMCHINJA MKEWE CHUMBANI
  • Polisi alivyoua kwa risasi
  •    

    #1 Author: maua (9 June 2009 02:14)

    Mhhh Jmani sinema au ??
     
    fast    

    #2 Author: MJ (9 June 2009 02:22)

    inasikitisha sana,
    .............MAY GOD rest his soul in PEACE!!!!
     
    fast    

    #3 Author: SALAMA (9 June 2009 02:31)

    JAMANI UNYAMA HUU UTAISHA LINI?MASIKINI JAMANI HIVI KWA NINI MTU HAUFIKIRII KWANZA NA NDIO UCHUKUE UAMUZI DUH IMENISIKITISHA SANA HADI MACHOZI YAMENITOKA.NAWAPA POLE SANA WAZAZI WA MAREHEMU MOLA AWAPE MIONYO YA SUBIRA KWA KIPINDI HIKI KIGUMU NA CHA BILA KUTEGEMEA.
     
    fast    

    #4 Author: lu (9 June 2009 02:47)

    mungu ailaze roho ya marehemu mahala pema peponi...Ameeen
     
    fast    

    #5 Author: MapigoSaba (9 June 2009 02:50)

    Maelezo yangetosha si lazima kuonyesha picha ya kisu kilichotapakaa damu ya binadamu. Ubinadamu lazima lazima uheshimiwe na kuzingatiwa.
     
    fast    

    #6 Author: furaha (9 June 2009 03:04)

    kiukweli nimesikitika sana zaidi ya sana,
    siwezi elezea Mungu ailaze roho ya marehemu mahala pema peponi AMINA
     
    fast    

    #7 Author: mujydebubyz (9 June 2009 03:22)

    Mungu ailaze roho ya marehemu mahali pema peponi. Amina


    --------------------
     
    fast    

    #8 Author: miss Brazil (9 June 2009 04:14)

    Oh my God!i dont believe, i stayed on that domitory in 2005. I feel it as if am there. Mungu ailaze roho ya marehemu mahali pema peponi Amen.
     
    fast    

    #9 Author: steven rutamu (9 June 2009 04:36)

    Jamani jamani, ubinadamu unaisha sasa unyama ndo unatawala myoyo za watu, inasikisha sana kuona mambo kama haya yanatokea kwa watu ambao tunafikilia kuwa ni wasomi. Jee wale wa vijijini wanao waua vikongwe na albino itakuwaje. Mungu ailaze mahari pema roho ya marehemu.
     
    fast    

    #10 Author: mimi (9 June 2009 04:45)

    watu wanaosoma katika vyuo vyetu vikuu kwa sasa wengi ni vimeo. Vyuo vyetu sasa si vitovu vya uchochezi wa fikra sahihi
     
    fast    

    #11 Author: Thomas (9 June 2009 05:37)

    Jamani mapenzi hayo, ndiyo maana wenye hekima wanasema usiyachochee mpaka yaone vema yenyewe,

    hakuna kitu kinachoudhi kama mpenzi wako kulazimisha kuvunja uhusiano na wewe kisha anaendelea na mwingine, unajitahidi kumbembeleza hataki mimi pia ime nitokea.

    katika kipindi hicho mtu huwa unafikiria mengi sana ikiwepo wazo la kujiua na kuuwa Asante Yesu sikufika huko.

    inasikitisha zaidi kuona tunapoteza wasomi wawili huyu wa kike anaenda kuzimu sijui kama alikumbuka toka lkn ilikuwaje kwa mkristo awe na uhusiano wa kimapenzi pasipo ndoa?

    na huyo kaka ataishia jera maisha yake yote, ni huzuni sana.
    Pia liwe fundisho kwa wasomi wetu sikuhizi wasomi wanaongoza kwa kupenda ngono wanalala watu wa jinsia tofauti kwenye chumba kimoja

    Dunia inapita hii tubuni muokoke.
     
    fast    

    #12 Author: Nancy (9 June 2009 06:30)

    ooooh my God!inasikitisha sana!
    jamani wivu gani huo hata kama ndio mapenzi basi hayo ni too much,sasa alikuwa anaomba asamehewe akaamua aue that is not love na haikuwa solution!mpendanao muwe mnawaza b4 kutenda!poleni wanafamilia!Mungu ailaze roho yake pema peponi!Mhhhhh!
     
    fast    

    #13 Author: august.minja (9 June 2009 07:51)

    hatuna budi kumuomba mungu sana kwani dunia inapoelekea inatisha,tuungane pamoja katika hili tumwombee ndugu yetu betha alazwe mahala pema peponi Amin
     
    fast    

    #14 Author: Cherrie Mori (9 June 2009 08:30)

    Jamani mapenzi ni nini? Wengine wanaua in the name of love and other cherish life in the name of Love!
    Roho imeniuma sana kwa kitendo hiki pamoja na tukio la IFM!
    Huyo kaka wa UDSM na dada wa IFM mliyoyatenda yatawaandama mpaka kufa na pengine msiishi muda mrefu, hata msipofungwa ile guiltness ni adhabu tosha.
    Dada mwenyewe anaonekana alikuwa decent masikini, anyway let her rest in Peace, Amen
     
    fast    

    #15 Author: manka mushi (9 June 2009 08:50)

    mmh jamani huu ni unyama
     
    fast    

    #16 Author: dnice (9 June 2009 09:14)

    Wewe Thomas usihukumu usije ukahukumiwa, unaposema huyu wa kike anaenda kuzima wewe ni Mungu? Wewe ulipokuwa na uhusuano na kuachwa hadi ukafikia mengi ulikuwa na ndoa? Mungu wetu ni wa rehema si kama umfikiriavyo wewe. Huoni uchungu walionao wazazi na ndugu zake kwa kupoteza binti yao mpaka unadiriki kusema maneno hayo.Mwogepe Mungu na uwe na roho ya ubinadamu usilete maumivu yako ya kuachwa enzi hizo hapa. Hebu fikiri kama ni wewe uzae kwa uchungu, taabu zote za kulea mtoto, umsomeshe hadi chuo kikiuu then aje binadamu ambaye hakuwepo kwenye taabu zote ulizopitia za kumlea binti yako mpaka hapo alipo eti akatize maisha yake sababu ya wivu wa mapenzi. Inauma sana
     
    fast    

    #17 Author: Musa Kidichi (9 June 2009 09:27)

    inasikitisha sana,kwanza nawapa pole wote wafiwa ndg,jamaa na marafiki,Mungu ailaze roho ya marehemu mahali pema peponi ameni,pili kwa mshitakiwa nadhani inabidi ajue mshahara wa dhambi ni mauti na hasira ni hasara inabidi ufikiri kabla kutenda,hii inaonyesha bado watu hawajakomaa katika suala la mapenzi hadi inafikia hatua ya kutoana roho,mwaka jana ilitokea pia nchi fulani chuoni bweninii mwanaume kamuua girlfriend wake kwa kila kinachoitwa wivu,ndg zangu nawaasa tujaribu kuepyukana na wivu unaovuka mpk hadi kushindwa kuzuia nafsi zetu,kama anakupenda atakulinda haina haja kuumizana na kutoana roho mapenzi ni kitu kinachoitaji kuvumiliana na ugomvi.
     
    fast    

    #18 Author: mariana (9 June 2009 09:52)

    kwakweli nimeumia sn moyoni kwani kifo hakizoeleki kamwe, mwenyezi mungu awajaze nguvu wazazi wake pamoja na ndugu jamaa na marafiki wote wakumbuke kuwa sie sote ni wapita njia katika hii dunia hivyo kuondoka kwa Bertha iwe ni changamoto kwa sie tulobaki maana kila kiumbe kilichozaliwa kitakufa.
    kuna kufa kwa staili nyingi but tumshukuru mungu kwa yote maana yeye ndo mpangaji wa yote.Naomba sheria ikachukue mkondo wake juu ya hili kwani huyo kijana aonesha ni limbukeni wa mapenzi kwani wangapi wanafall in love wakiwa mashuleni na at the end wengine wanaoana na wengine wanaachana hawafanyi hivyo? ye ana wivu ulioje mpk aue? kila mtu kazaliwa na wivu but wake si wivu ni uuaji!!!! ingekuwa wivu na kama alimpenda kweli angembembeleza kwahali na mali ili wawe wote au angetimiza masharti aliyopewa ya kuacha bangi, pombe na sigara. sasa mwanaume gani utumie vilevi vyote hivyo? tutajenga familia au tutabomoa?
     
    fast    

    #19 Author: mrisho rajabu (9 June 2009 11:36)

    huyu muuaji lazima ni wa mara!!!! afu na nyie wadada wakimbieni hawa
     
    fast    

    #20 Author: Tchalewa Ndeki (9 June 2009 11:47)

    Nawaomba mabinti zetu walio katika vyuo mbalimbali hapa na nje ya nchi. Mapenzi ni asili, wawapo masomoni waangalie nani wakumpenda na pia wajue background ya hao wawapendao, familia zao, historia za familia zao, matukio takutisha yaliyowahi kutokea katika hizo familia wanakotoka hao wapenzi wao.
    Tumlaumu nani? Inauma sana, wazazi na Taifa waliwekezakatika Binti yetu huyu, na hata katika muuaji pia, anyway, tugange yajayo. Hili ni tukio mbaya la pili, Msanii wetu alisema LIFE IS NOT A REHEARSAL.
    Hayati sasa siwetu, nikusahau na kusonga mbele, tujivunze kwa hili pia.
     
    fast    

    #21 Author: Chissy (9 June 2009 12:27)

    Mapenzi na Elimu havichangamani hata siku moja. Kama wangezingatia kilichowapeleka chuoni, majonzi haya yasingekuwapo leo.
     
    fast    

    #22 Author: NOEL MSANJILA (9 June 2009 12:49)

    1]HUYU MAREHEMU ANASIKITISHA, [2]PAMOJA NA YOTE TUSIWE TUNAMFUNDISHA MUNGU KAZI,ETI MTU AKIFA TUSEME MUWEKE PEMA PEPONI. ACCORDING TO BIBLE BAADA YA MTU KUFA NI HUKUMU HATA UMUOMBEAJE MUNGU HABADILISHI YEYE HUANGALIA NENO LAKE SOMENI [WAEBRANIA 9;27]HUMU DUNIANI NI KAMA NDANI YA CHUMBA CHA MTIHANI UKISHATOKA NDANI YA CHUMBA CHA MTIHANI HUWEZI TENA KUBADILISHA MAJIBU ILA SUBIRI MATOKEO TU,NAOMBENI MUANZE KUELEWA HILO.WAOMBEE TU FARAJA NDUGU WA MAREHEMU MUNGU ATAISIKIA SALA YAKO SIO KUMWOMBEA MAREHEMU,AMEN.
     
    fast    

    #23 Author: mnyalu (9 June 2009 14:02)

    Naye auawe ndiyo9 dawa au mahakama ya wanyonge ipo.Roho ya marehem istarehe kwa amani Amina.

    Hi noma hta shetani anasema hiyo ni dhambi kubwa washikaji kama demu kakumwaga pata pamba mawe endeleza makamuzi mpka utampata anaye kufaa halafu muonyeshee kuwa wewe ni babu K .Roho ya Dada wetu istarehe kwa amani Amina.
     
    fast    

    #24 Author: MARK.MUSHI WA ITALY (9 June 2009 14:59)

    AYA SASA HII MADA NDIYO NILIKUWA NAITAKAGA MIM I TOKA SIKU NYINGI,MIMI NAULIZA HIVI ENDAPO YULE ANAYEBAKA ANAFUNGWA KIFUNGO CHA MAISHA JE UYU ALIYEUWA ATAFUNGWA MIAKA MINGAPI?10?20?30?AU MIAKA 30 KISHA ANATOKA?WAKATI ALIYEBAKA AMEFUNGWA KIFUNGO CHA MAISHA APO HIPI NI KESI NZITO JAMANI?UYO ALIYEUWA NAYE AFUNGWE KIFUNGO CHA MAISHA ILI IWE FUNDISHO KWA WENGINE WATAKAOUWA,KAMA ILIVYOKUWA FUNDISHO KWA WALIOBAKA WE MISS YOU PAPI KOCHA SEWA,NAWAPA POLE NDUGU WA MAREHEMU,R.I.P.BERTHA WANAFUNZI WENZAKO WATAKUKUMBUKA DAIMA,
     
    fast    

    #25 Author: damassan (10 June 2009 01:49)

    mungu ailaze roho mahali pema.
     
    fast    

    #26 Author: Lili (10 June 2009 05:18)

    Yaani kwetu Tanzania siku hizi kunatisha sana, watu wamekuwa na roho mbaya, ujambazi nje nje,wasagaji mashoga yani kunatisha sana wajameni. natamani nieende likizo next month ila nikipata picha za ujambazi naogopa, sijui uongozi gani uje Tz iwe kama zamani.
     
    fast    

    #27 Author: Museveni (10 June 2009 06:36)

    Vyuo vikuu vya sasa vimejaza wanafunzi walevi,wavuta bangi,malaya,wezi,majambazi n.k,n.k. Huyu muuaji bila shaka ni kati ya wavutaji wa bangi, kwani mtu mwenye akili timamu hawezi kufanya kitendo kama hicho,ameiaibisha jamii nzima ya wasomi pale chuo kikuu,anastahili kunyongwa hadi kufa.
     
    fast    

    #28 Author: mamii (10 June 2009 08:06)

    ni kweli nakubaliana na Mrisho Rajabu checking family background is very important. lazima mtu anakuwa na vi-element vya family, kama vile hasira za kupindukia, ulevi ufuska, etc. After all watu wa mkoa wa Mara wana hasira za kuua
     
    fast    

    #29 Author: Jane (11 June 2009 04:14)

    Inasikitisha, muuaji naye anyongwe mpaka kufa bila huruma, dada yetu kapumzike kwa amani, wote ni njia moja.
    No. 26 Lili Tz itabaki kuwa nchi yako tu my friend, kukimbilia uingereza unaonyesha ni jinsi gani usivyokuwa shupavu wa kukabiliana na hali halisi ya nchi yako, mbona unamwacha kaka yako Hartman anapotea? Anitia aibu jijini kama ameshindwa kukua bongo mwambieni arudi Uingereza
     
    fast    

    #30 Author: jimmie (11 June 2009 04:35)

    jamani jamani,
    kwanza pole kwa wazazi wote 2, kwa wanafunzi wezake
    marehemu, nk.
    mm nimeskitika sana lakini huyu jamaa yu2 killer
    anapendwa na yy hapendeki then anajifanya m2 wa hasira,
    tusiwe ivo. msome jamani, msome mrudi kwenu.
    maamuzi ya mikumbo na hasira za kurithi ni mambo ya zamani hayo jamani.
    mbona cc wa2 wa mara 2po na 2meturia. hasira @ m2 anayo.
    asante,
    jimmie.
     
    fast    
    Back  <<  1 2  >>  Next Page

    Add comments

    Name:
    E-mail:

    Code:
    Include security image CAPCHA.
    to renew the code
    Enter Code:

     

    Kura Yako / Poll

    Habari Katika Picha


    Gazeti la Uwazi



    Nani Yupo / Alikuwepo


    Home Page | About Us | Regista | Picha | Bongo Celebrities | Maoni | Contact Us

     hit counter

    counters

    2008 © globalpublisherstz.com