Tembelea... |
 |
Kalenda |
 |

Marafiki wetu |
 |
Habari Zilizopita |
 |



|
|
 |
|
|
 |
 |
|
 |
Taarifa za kiuchunguzi ambazo zimethibitishwa na watu wa karibu wa pande zote mbili (ya Marehemu na Mtuhumiwa), zinaeleza kwamba, mtuhumiwa wa mauaji Masamba Musiba (27) ambaye pia ni mwanafunzi wa mwaka wa pili katika chuo hicho, alichukua uamuzi huo kufuatia kusononeshwa na uwepo wa kigogo wa TRA Makao Makuu ya jijini Dar es Salaam (jina halikupatikana) aliyekuwa akitembea na marehemu enzi za uhai wake.
Vyanzo vyetu hivyo vya habari ambavyo viko ndani ya Hosteli za Mabibo zinazomilikiwa na Chuo Kikuu cha Dar es Salaam, vinasema kwamba, kigogo huyo wa TRA alikua akifika mara kwa mara majira ya jioni akiwa kwenye gari lenye rangi ya bluu aina ya Toyota RAV 4 muundo wa kisasa (New Model) na kumpakia kisha kuondoka naye kusikojulikana.
Taarifa zaidi zinaeleza kuwa, kigogo huyo wa TRA alikua akifika na gari hilo lenye vioo vyeusi (tinted) kuanzia majira ya saa 2 jioni na wakati mwingine alikua akimuachia fedha za kukodi teksi kwa lengo la kumfuata anakokuwa na kurudi kesho yake.
“Huwa tulikuwa tunamuona huyo jamaa wa TRA akija hapa jioni na kuondoka naye.Lakini mara nyingine alikuwa akimwachia hela ya teksi na yeye kumfuata,” alisema mmoja wa wasichana walio jirani na kilichokuwa chumba cha Beatha.
Hata hivyo, chanzo kimoja cha habari kimeliambia Uwazi kuwa,Beatha (Marehemu) alianza kuwa na uhusiano na kigogo huyo baada ya kutokea mgogoro wa kimapenzi kati yake na Musiba.
Kimezidi kueleza kuwa, mgogoro huo ulisababishwa na Beatha kutoa kauli ya mwisho kwa mpenzi wake Musiba (mtuhumiwa) ikimtaka aache mara moja tabia ya ulevi na uvutaji bangi kupindukia aliyokuwa nayo ambapo mtuhumiwa alikubali kubadilika na kuahidi kutorudia tena ingawa siku chache baadaye alirejea katika tabia hiyo chafu hali iliyomuudhi Beatha na kusisitiza kuachana naye.
Habari zaidi zinasema kuwa, mtuhumiwa alikua akihisi vibaya pale Beatha alipoendeleza azma ya kusitisha penzi lao, hali iliyomfanya kuwa katika majaribu ya kujiua kwa kujitupa kutoka ghorofani kwenye Hosteli za Mabibo mara kwa mara ingawa ilishindikana baada ya kuokolewa na wanafunzi wenzake.
Baadhi ya waliokuwa marafiki wa marehemu enzi za uhai wake waliohojiwa na gazeti hili walisema kwamba, uhusiano baina ya wawili hao ulianza zamani ingawa hata hivyo matumizi ya vilevi halali na haramu yalikuwa yakitia doa raha ya penzi lao na ilifikia hatua ya Beatha kumpa muda wa kujirekebisha mpenzi wake huyo vinginevyo angesitisha mapezi.
Waliendelea kusema, baada ya Musiba (mtuhumiwa) kushindwa kutumia muda huo kujirekebisha, Beatha aliamua kuchukua maamuzi magumu ambayo yalihitimisha penzi lao na yeye kuhamisha mapenzi yake kwa kigogo huyo wa TRA ambaye imeelezwa kwamba anafedha ‘chafu’ zilizokuwa zikimpa kiburi marehemu.
Katika kile kinachoonesha kuwa kigogo huyo wa TRA alikolea kwa penzi la Beatha, hivi karibuni alichukua likizo kazini kwake iliyompa wasaa wa kujivinjari mara kwa mara hivyo kuzidi kulifanya jina la Masamba kufutika kwenye mawazo ya Beatha kitendo kilichomkera na kuchukua uamuzi wa kinyama.
Mmoja wa Wanafunzi wa mwaka wa pili katika Chuo cha DUCE (hakutaka jina liandikwe) ambaye alidai kuwa rafiki wa Masamba, ameliambia Uwazi kuwa, migogoro baina ya wawili hao ilichukua sehemu kubwa ya muda wao wa masomo hali iliyosababisha warudi nyuma kitaaluma.
Musiba anakabiliwa na tuhuma ya kumuua mpenzi wake, Beatha kwa kumshambulia kwa kisu hivi karibuni nje ya chumba chake namba C 250 kilichoko Block C katika Hosteli za wanafunzi wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam (UDSM) mbapo kifo kilimpata wakati akikimbizwa hospitalini.
Kwa sasa mtuhumiwa amefunguliwa kesi ya mauaji iliyosomwa wiki iliyopita katika Mahakama ya Wilaya ya Kinondoni.
|
|
 |
 |
|
 |
 |
BADO NIKO HEWANI ATA MKINIPONDA VIPI,MIMI BADO NAULIZA HIVI-ENDAPO YULE ALIYEBAKA KAFUNGWA KIFUNGO CHA MAISHA JE SASA UYU ANAYEUWA ATACHUKULIWA ADHABU GANI 10YEARS ALAFU ATATOKA?KAMA NIIVYO MNANICHEKESHA SANA,SIJUWI SHERIA ZA UKO BONGO ZINASEMAJE LAKINI ZA APA ITALY UKIUWA KWA KUKUSUDIA YANI KWA MAKUSUDI KAMA ALIVYOFANYA MUSIBA-BASI UTAFUNGWA MIAKA30KISHA UTATOKALAKINI UMEUWA KWA BAATI MBAYA BILA KUKUSUDIA BASI UTAFUNGWA KWA MIAKA 10AU15KWISHA MCHEZO UMETOKA,ALIYEBAKA NI MIAKA15AU20JELA,WE MISS YOU PAPI KOCHA MTOTO WA MFALIME,NINA MAWAZO YA KUFUNGUA KITUO CHA KUSAIDIA YATIMA UKO BONGO,SIYO KUWALEA TU ATA WAPATE ELIMU BORA NA MAITAJI MUHIMU KAMA KUNA MTU MWENYE MAWAZO KAMA YANGU ANIANDIKIE,CHELSEAFORTE1@YAHOO.IT,AU ANIPIGIE,+393336989592,MTAFUTAJI MARK IN ITALY,YULE ALIYENIANDIKIA KUWA NIMTUMIE EURO3000ASINIANDIKIE TENA UYO NI TAPELI,WAZO LA LEO UKIWA NA MTOTO MMOJA ONGEZA MWINGINE,CIAO, |
|
|
 |
 |
#15 Author: easy (24 June 2009 03:19)
|
|
 |
 |
mpiluka nimekupata yaani huyo charlie anani -bore mpaka basi, yaani yeye kuishi Italy ni kama ameshafika peponi!kwanza hata vimaandishi vyake anavyotumia utajua nia kashamba fulani hivi!huyu si mchagga,anatumia hilo jina tu, wachagga hawana muda mchafu kama huo wa ku ji proud all of the time,,,,Mark will you stop blabbering,your sentiment is always irk me!your type of clueless life you'r living in Italy make you to belabor the name every time on you'r sentiments, am fed up for your evangelizing, will you find a college to back up your mind instead of the crappy job u'r doing there? |
|
|
 |
|
|
 |
Kura Yako / Poll |
 |
Habari Katika Picha |
|
 |

Nani Yupo / Alikuwepo |
 |
|