arrowSet HomePage |arrowBookMark Us
right
lines

Global Publishers Tanzania- Uwazi » ijumaa » JOYCE KIRIA: Nimekula uroda na wanaume wengi sana!

Tafuta  

Tembelea...

Kalenda

Gazeti la Ijumaa

Marafiki wetu

Habari Zilizopita

Soma Magazeti Yetu...

Gazeti la Risasi Mchanganyiko
Amani
Gazeti la Ijumaa Wikienda

Bongo Celebrities ...

 
Habari Zinazotamba Habari Mchanganyiko
» Aunt Ezekiel alivyopigika k ...
» ZITO LAIBUKA
» KIGOGO WA MURO NAYE KUKAMAT ...
» GLOBAL PUBLISHERS MUSIC PLA ...
» Aina 10 ya vyakula vinavyoo ...
» JERRY MURO AKOSWA RISASI
» Kigogo afanyiwa umafia
» Kasoro kubwa waliyonayo ...
» Mtumwa wa ngono (55)
» Machangudoa wa Kichina. ...
» Kauli za Martin Luther ...
» JINSI ILIVYOKUWA
» WABONGO WANATEGEMEA RAD ...
» NISAMEHE NILITELEZA, AS ...

JOYCE KIRIA: Nimekula uroda na wanaume wengi sana!

ijumaa

TQ: Nipo hapa kwa niaba ya wasomaji wa gazeti la Ijumaa ambao wanataka kujua maisha yako ndani na nje ya kazi. Bila kupoteza muda anza kwa kutueleza ni kitu gani hasa kilikufanya ukaamua kuingia katika fani ya utangazaji hasa ya kuchambua filamu za kibongo?

Joyce: (Akiwa makini) Napenda sanaa ya maigizo, lakini kila kukicha matatizo yamekuwa hayaishi kwenye filamu zetu, nikaona ni bora niingie niweze kuwakosoa na kuwapongeza waliofanya vizuri kama njia ya kuikuza.
TQ: Kazi yako ya utangazaji umewahi kuifanya nje ya Bongo?

Joyce: Zaidi ya Clouds Fm, Channel Ten na sasa EATV, sijavuka mipaka ya nchi yetu ingawa ni moja ya ndoto zangu za baadaye.
TQ: Nini mafanikio yako katika kazi yako?

Joyce: Mafanikio yapo ingawa siyo ya moja kwa moja. Kubwa zaidi ni kufahamiana na watu wa nyanja mbalimbali.
TQ: Unaweza kukumbuka idadi ya wanaume uliokuwa nao kabla ya kukutana na mumeo Dj Nelly?

Joyce: (Huku akicheka) Hapa lazima niseme ukweli...sikumbuki idadi kamili maana nimetembea na wanaume wengi sana! Uzuri wangu ndiyo unaowachanganya kwahiyo nikajikuta nikiwa na wanaume wengi sana, lakini baada ya kukutana na toto la Kihaya, Nelson Nkongo (Dj Nelly) nimetulia kwa raha zangu, maana ananipa kila ninachokihitaji.

TQ: Mh! Hujatulia wewe, enhee nini kilisababisha ukachaana na wapenzi wako wa nyuma?
Joyce: Unajua mimi nilikuwa natafuta mume wa kuishi naye, kwahiyo kila nilipogundua mtu ana nia ya kunitumia, niliachana naye haraka sana, ndiyo sababu nikawa na wanaume wengi.

TQ: Sasa wanaume wote hao jamani, hukukanyaga miwaya kweli?
Joyce: Nilikuwa makini sana, mara zote nilikuwa nikitumia kinga. Hata hivyo niliwahi kupima na kukuta nipo poa.

TQ: Unataka kuniambia baada ya kukutana na Dj Nelly mlipima?
Joyce: Kwakweli hapana, lakini najiamini maana sijawahi kutoka nje ya penzi letu, na hata yeye namuamini pia.

TQ: Kuna nyepesi zinasema kwamba, Dj Nelly alikuwa mume wa mtu na wewe uliingilia ndoa ya watu. Hilo unalizungumziaje?
Joyce: Hakuwa mume wa mtu bali alikuwa akiishi na mwanamke, lakini baada ya kuridhika na mimi ndiyo akaamua kunichukua jumla kwa ndoa halali ya Kanisani.

TQ: Sasa naomba kukuuliza swali la chumbani zaidi. Ni kitu gani ukifanyiwa na mpenzi wako faragha unajisikia raha zaidi?
Joyce: Mi’ napagawa zaidi na romance, hapo tu, ndipo panaponiacha hoi mtoto wa kike.

TQ: Halafu kuna tetesi mjini kwamba huo weupe wako ni wa dukani, nikimaanisha kwamba unajichubua. Hiyo nayo imekaaje?
Joyce: Naona maswali yamekuishia sasa...kifupi weupe wangu ni wa asili, kwaheri bro!


 (Votes #: 15)
    (19 June 2009)
Soma Zaidi: 8124 | Maoni Yako (31)

Udaku Mwingine

ijumaa
 
  • Madai ya Ray kutembea na Joyce Kiria... NI KIMBEMBE
  • NDOA YA JOYCE
  • MC UPANDE WA KULIA
  • Wasanii kula pilau na watoto yatima
  • Joyce Kiria aangalia ustaarabu mwingine
  •    

    #1 Author: Hadija (19 June 2009 04:00)

    Ni vizuri kusema ukweli kuwa umetembea na wanaume wengi ila sio sifa kujisifu kuwa wewe ni mzuri kwa hiyo unatoa hovyohovyo!! Acha hizo wewe mtoto!
     
    fast    

    #2 Author: saade (19 June 2009 09:02)

    hee we dada kweli mapepe ndio ujinadi kiasi hicho? usijisifu shangazi kama mzuri unasifiwa tu, si mpaka ujidani kiasi hicho huna haiba ya kike mweee uzuri si tija mama tabia ndio muhimu upo hapo
     
    fast    

    #3 Author: georgre (19 June 2009 09:51)

    sijui tukitumia kamusi ya kiswahili sanifu neno malaya litakuwa na maana gani,anyway hii ni sifa lakini ni sifa mbaya.bongo kazi kwelikweli!!
     
    fast    

    #4 Author: Master T (19 June 2009 09:51)

    Hukutulia wewe! hujui utamuumiza roho jamaa, unadhani ataamini kuwa umeeachana nao kweli?
    Mambo kama hayo ni bora kuambiwa tu.....ilikuwa hivi au vile kabla hujamuoa huyo bint...lakini siyo kutoka live kwa mhusika, mbaya mnooo! Kama mimi, itapunguza imani kwa kiasi fulani!
    Vipi jamii inakuonaje duh duh!!!! noma m2 wangu.
     
    fast    

    #5 Author: Bob Sambeke (19 June 2009 12:45)

    E Bwana We Mtoto Wa kike Ujatulia Kweli,Uoni utamuumiza Roho Mtoto wa kihaya? Kama Ulimwambia yeye b4 co mbaya lkn kam ulikuwa ujamwambia ni soo,Naungana na mdau hapo juu,Kwamba"Uzuri wa mwanamke co weupe au kuvutia bali ni tabia njema mbele ya jamii" Kwhyo jifunze dada ustaarabu!
     
    fast    

    #6 Author: MARK.MUSHI WA ITALY (19 June 2009 15:35)

    MBONA UJAMUULIZA NANI ALIYEMTOA USICHANA WAKE?BIG-UP MASTER T NI KWELI KABISA ATA NINGEKUWA MIMI,TUOMBE MUNGU TU IYO NDOA YENU IDUMU MAANA SIKUIZI UKO BONGO WATU WANAOJIITA MAPEDESHEE WAKO WENGI KWAIYO TAADHARI WATU WATAOMBA SITE,MIMI SIJAKUONA UMBO LAKO YA NI ADI CHINI NINGEKUONA UMBO LAKO ZIMA NINGEWEZA KUSEMA NI MZURI LAKINI SIKUJUI KWAIYO SIWEZI KUKUFAGILIA SAINGINE NI NUNGAEMBE?NITAJUAJE?ATA MIMI NAONA UWO WEUPE WAKE NI WA DUKANI,MTAFUTAJI MARK NDANI YA ITALY,
     
    fast    

    #7 Author: kimbula (19 June 2009 16:37)

    sijali uzuri wako, nashukuru umeacha. nafurahi Mmiliki wa The Utamu alivyokamatwa kama kuku tu! big up afandeee's
     
    fast    

    #8 Author: AYUB (19 June 2009 20:18)

    hapo kazi ipo jamaa kaoa mapepe huyo hajaachana nao atarudi yuu kukumbushia pindi atakapoanza kuchokana na jamaa nani hawajui dada zetu hawa kama alishavua chupi mara nyingi lazima atavua tena tuu
     
    fast    

    #9 Author: Poaz2 (19 June 2009 23:28)

    Kwa raha zako!! kwakweli mtoto ameumbika Author 1+4 hamana lolote wivu2 umewashika...Na hawa waandishi wamezidi umbea kiasi awape kweupee wazidi kuandika udaku!! masuali mengine yakiulizwa yawe na mipaka
     
    fast    

    #10 Author: SaLaMa (20 June 2009 00:57)

    duh haya makubwa tena kumbe kutembea na wanaume wengi ni sifa? joyce uzuri ni kusifiwa na si kujisifia bana naona unatafuta umaarufu kwa nguvu zote hivi mumeo akisikia unavyosema kuwa umetembea na wanaume wengi atajisikiaje? mie naona umejishushia heshima yako kwa kiasi fulani hata huyo mumeo atakuwa anamashaka sana na wewe.
     
    fast    

    #11 Author: JULLY (20 June 2009 06:27)

    kwa kweli unabona kujisifia subiri usifiwe
     
    fast    

    #12 Author: wifi mtu (20 June 2009 09:28)

    Mmh!! umetutia aibu wachaga wote wa Kibosho. Mtoto umetoka Kibosho leo hii umjua kujisifia sifa za kijinga namna hiyo, ungesubiri usifiwe mama. umeingia DAR kwa pupa jiji litakushinda lina wenyewe hili.
     
    fast    

    #13 Author: HAYA GIRL (21 June 2009 07:24)

    Joyce nakupa pole,Umewapa aibu wakwe zako waliokuzalia mumeo,Mama yako mzazi,Mumeo,wifi zako,Shemeji zako, kaka zako,wadogo zako na hata jamii nzima inayokuzunguka.Nilidhani una akili .Ni hayo tu.
     
    fast    

    #14 Author: KIMBI (21 June 2009 23:33)

    Nakusifu kwa kukiri umetembea na wengi ila sababu uliyotoa ya kuachana na wapenzi wako si za kweli. Binafsi hukuniacha bali nilikumwaga kutokana na tabia yako ya kutaka kujaribiwa na kila mwanaume.
     
    fast    

    #15 Author: Yoweri Museveni (22 June 2009 07:51)

    sio sifa nzuri kwa mtoto wa kike kutembea na wanaume wengi. Nadhani hii imesababishwa na malezi mabaya katika familia yako.
     
    fast    

    #16 Author: Kemmy (23 June 2009 02:41)

    jamani labda mi sijui kuangalia vizuri au macho yangu yana matatizo, naomba kujua huo uzuri wake uko wapi, ni hizo nywele kama kichaa wa nigeria au hayo macho kama ya mchina ambyo akicheka hayaonekani? au au ni huo mkorogo kama wa maimatha? tafadhari naomba nionyweshwe uzuri wake.
     
    fast    

    #17 Author: haji (24 June 2009 03:15)

    muogope mungu ambae ameumba vyote vilivyomo mbinguni na ardhini mola ambae ni mkali sana wa kuadhibu kwa wale watendao makosa kisha wakajinadi ulimwengu mzima kwa sifa za uzinifu hii si sifa isipokua unajipalia makaa rudi kwa mungu wako atakusamehe kwa yale uliyoyatenda kwa kukusudia nayale uliyoyatenda kwa kukosea
     
    fast    

    #18 Author: wa-michezo (25 June 2009 01:14)

    Duh, inasikitisha sana na kuhudhunisha sana kwa m2 kutoa mambo yako ya ndani kwenye jamii ,tena mambo ambayo yanaumiza familia ya upande wa mume na mume mwenyewe. Hivi huyu dada anatarajia wifi, shemeji ,wakwe zake n.k watakuwa wanatazama kwa mtazamo upi? kama co malaya, mwasherati, mzinzi na fisadi wa mapenzi, n.k.Tatizo huyu dada anaiga utamaduni wa nje ambao demu anaweza akadungwa na wa2 kibao maarufu na kujitangaza. cha muhimu acha ulibukeni dada kuna mambo mazuri ya kujisifia co hayo
     
    fast    

    #19 Author: Msema Kweli (25 June 2009 03:08)

    crying crying crying crying crying Nakupa pole wewe unajiita mume wa huyu kicheche wa Kibosho uliyenaye. Nakuhakikishia Dj Nelly, tabia haina dawa na muonja ASALI atarudia tuuuuuuuuuuu
     
    fast    

    #20 Author: Malangahe (25 June 2009 04:25)

    Kama umetembea na wanaume wengi sisi tufanye nini sasa,ushauri mrudie Mola ngoma itakuchomoa.
     
    fast    

    #21 Author: wifi mtu (25 June 2009 12:19)

    Yani namhurumia sanaDJ Nelly, sijui alibabaishwa na huo weupe wa dukani? Aibu aibu tupu.
     
    fast    

    #22 Author: RAYUU (26 June 2009 04:06)

    kata nywele hizo ubaki na kipilipili chako au uzisuke na pia acha kupaka vipodozi ubaki natural ndio hapo ujisifie mzuri lakini si kujisifia uzuri wa dukani wakununu kila mtu akitaka atakuwa hivyo hivi wewe siuzishukuru make up hizo unauzuri gani wa kujisikia wewe? wazuri hauwaoni?
     
    fast    

    #23 Author: Davis (27 June 2009 05:58)

    Huyo dada anaonekana nimshamba wa mapenzi.pia sio mstaraabu kabisa wekutembea na wanaume yote hao hakafu unajua humu unajitangazia ili iweje?(Tukutokee na sisi au )

    Tena anaonekana ni Teja huyo mwanamke.na hiyo ndoa yake haina mwisho mzuri.hapo kaficha makucha yake tu na inaonekana mumewe akitoka anaenda kusuguliwa na masela mtaani.

    Namuonea huruma mshkaji Nelly
     
    fast    

    #24 Author: ediger (29 June 2009 05:26)

    amakweli mungu kazaraulika, mtu kama una akili huwezi kjisifu na mambo ya kipuuzi kiasi hicho' kwanza unatakiwa uone aibu ya kutembea na wanaume wengi kiasi hicho, hata mmeo ana kazi.mrudie mungu wako dada yangu.
    saade,
     
    fast    

    #25 Author: anyonymous (3 July 2009 00:17)

    Hivi wewe joyce kiria una akili kweli? kaka yako kiria wa kariakoo anajua hayo yote? unathubutu kujisifu kwa mambo ya aibu kama hayo> du nitampa pole kaka yako kweli huna akili.

    Na wewe unayesema kuhusu wachaga wa kibosho, mbona ndio makahaba wakubwa mjini hapa? washamba wanakurupuka na kuparamia mambo ya mjini wasioyajua vizuri, kiufupi wakibosho hamna lolote, ushamba umewajaa!
     
    fast    

    #26 Author: fatuma jafari (12 July 2009 10:02)

    Eeeh we dada mzuri anasifiwa na wala hajisifu, kama mzuri kaa watu watakusifia.

    mzuri anasifiwa na sio kujisifu
     
    fast    

    #27 Author: Junemary (15 July 2009 03:06)

    Heee we bint wafikiri umalaya sifa? shukuru mungu umempata Nelly kakuoa labda kuna ulilomfanyia akapagawa mhaya wa watu unless otherwise usingepata wa kukuoa mjini hapa coz kila mwanaume anajua utupu wako. kama kweli umeamua kuingia kwenye ndoa jaribu kutulia na kuongea kama mke wa mtu. kwa uzuri wala hautishi ni vipodozi vya shear illusion ndio vyakusitiri.poleeeeeee
     
    fast    

    #28 Author: assey (16 July 2009 06:10)

    kwanza kwa uzuri huna kihivyo ni wa kawaida saaaana. Pia shukuru mungu una vijisent kdg vya kugharamia vipodozi ili kujipendezesha. Kuwa na wanaume wengi co sifa, hujafundwa wewe. Mwanamke husemi yote tena hadharani? huna maadili hata kidogo huchagui la kusema. Huyo DJ wako bado hajapata mke sahihi. Polee wee!
     
    fast    

    #29 Author: mallya (21 July 2009 15:02)

    kweli malaya ni malaya tu hata km umfunge na kamba km kweli mwanamke wa kibantu atafikia hatua ya kujitangaza kwamba katembelea na wanaume wengi kuna nn tena naona ni mm u ndio nilyemkosa dah pole mama.

    rfwqgqwgf
     
    fast    

    #30 Author: shuwu (10 August 2009 04:20)

    in an nut shell malaya si malaya kama ana mtu, ambao aja mu omba vitu vyake..

    mean while please send me Joyce Kiria"s email or any other personal contacts, yani na jisikia nina mpendsa kinome!!!

    says Shuwu from Uganda kamapala
     
    fast    
    Back  <<  1 2  >>  Next Page

    Add comments

    Name:
    E-mail:

    Code:
    Include security image CAPCHA.
    to renew the code
    Enter Code:

     

    Kura Yako / Poll

    Habari Katika Picha


    Gazeti la Uwazi



    Nani Yupo / Alikuwepo


    Home Page | About Us | Regista | Picha | Bongo Celebrities | Maoni | Contact Us

     hit counter

    counters

    2008 © globalpublisherstz.com