Global Publishers na The Atriums Hotel ni miongoni mwa kampuni zinzoshiriki katika Tamasha la nchi za Jahazi (ZIFF) mjini Zanzibar na banda la kampuni hiyo ni miongoni mwa mabanda kadhaa yaliyomo Ngome Kongwe kueleza shughuli zao. PICHA: IMELDA MTEMA/GPL ZANZIBAR
Bibi wa Kidosi akikatiza mitaa ya Kariakoo jijini Dar es Salaam na baiskeli yake yenye alama ya ‘Learner’ (Lena) (L) ambayo inaashiria kwamba anajifunza kuendesha baiskeli hiyo. Hata hivyo haikuweza kufahamika mara moja kama mama huyo alikuwa amekata leseni hiyo ya ‘Learner’ au ni mbwembwe tu.
ARRRROOO... SOONGA MBERRREEE Mgambo wa Jiji akimpeleka puta kijana aliyedaiwa kuwatapeli watu maeneo ya Posta ya Zamani jijini Dar es Salaam, kwa kujifanya anawauzia aina mpya ya mitego ya panya. Hata hivyo baadaye aligundulika kuwa tapeli, kwani mitego hiyo iligundulika kuwa feki.
HUU NI UNYAMA! Mkazi huyu wa jiji la Dar es Salaam (pichani) akiinuliwa na wasamaria wema baada ya kupoteza fahamu maeneo ya Posta Mpya leo mchana kwa kile kilichoelezwa kuwa alilishwa dawa za kulevya na watu wasiojulikana. Tathmini ya mambo aliyofanyiwa haikuweza kupatikana mara moja kutokana kushindwa kujieleza.
Kijana huyo akiwa amebebwa mgongoni kupelekwa sehemu ya usalama.
KWA MTAJI HUU TAKA ZITAISHA? Gari la kuzoa taka la kampuni ya Sincon Environment Ltd likiwa limezidiwa na mzigo wa takataka wakati zoezi la uzoaji taka katika Soko Kuu la Kariakoo jijini Dar es Salaam leo mchana.
WAKENYA NAO WAVUVI HARAMU! Wakenya watatu wanaokabiliwa na tuhuma za uvuvi haramu wakiwa na raia wengine wa kigeni wenye asili ya kichina wakisuburi hatma ya dhamana yao katika kesi ya uvuvi haramu inayowakabili katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu jijini Dar es Salaam leo asubuhi. Ishu ya dhamana bado haijafanikiwa. Kesi hiyo itatajwa tena mahakamani hapo Julai 15 mwaka huu. PICHA:RICHARD BUKOS NA CHRISTOPHER LISSA /GPL
If you are lucky enough to be anywhere near London's Southbank on Tuesday 7th July 2009 - you might like to catch the DVD launch of an award winning film about Bi Kidude. In two years since it’s début screening, our intimate portrait of Swahili legend Bi Kidude has won friends and awards around the world. It is at the National Film Theatre NFT2 at 6:20pm and will be introduced by director Andy Jones.
If you are lucky enough to hear BBC Radio 3 - then don't miss a special programme recorded during Sauti za Busara 2009 about SAMBA MAPANGALA. It will be broadcast on Saturday 4th July 2009 at 3pm (UK time) - and also available from their archive for a week. More details at [url=http://www.bbc.co.uk/radio3]www.bbc.co.uk/radio3
Mama mzazi wa Miss Tanzania 2006-07, Wema Isaac Sepetu, Mariam Sepetu amedaiwa kumuachisha kazi binti yake kwa Mkurugenzi wa Jumba la Dhahabu, Tuesday Kihangala ‘Mr. Chuzi’ kwa kile kilichoelezwa kuwa ni hofu ya kuwepo kwa harufu ya mapenzi baina ya wawili hao...
Jimama Monica Juma (35), Mkazi wa Simike, jijini Mbeya, limefumwa laivu geto kwa denti wa kidato cha pili katika Shule ya Sekondari ya Malezi aliyetajwa kwa jina moja la Henry (18), likiwa limejiachia kwa raha zake...
Tuanze somo letu la leo kwa kutafakari baadhi ya taarifa za kuhuzunisha, ambazo wengi wetu tunakutana nazo kila siku katika maisha yetu. “Kuanzia leo umefukuzwa kazi” “Nimeamua tuachane” “Baba yako mzazi amefariki leo asubuhi” “Mwanao amefariki katika ajali ya gari.” Bila shaka taarifa za aina hii zinahuzunisha na swali linabaki tufanyeje tunapokuwa na mawazo ya aina hii?...
Ni wiki nyingine tena tunakutana kupitia safu hii ambayo ni mahususi kwa kuandika makala mbalimbali zinazogusa maisha yetu ya kimapenzi. Wiki hii nitazungumzia mada ambayo imetokana na malalamiko mengi ambayo nimekuwa nikiyapata kutoka kwa baadhi ya wanawake wakielezea jinsi wanavyosumbuliwa na wanaume wakware, wengine wakidai wanataka kuwaoa, wengine wakieleza wazi kuwa wanataka kufanya nao mapenzi tu tena kwa ahadi ya malipo manono...
Mpenzi msomaji, kijana Beka aliyefundishwa uchawi huko Bububu Zanzibar anaendelea kusimulia mambo zaidi aliyokumbana nayo katika maisha yake. Wiki iliyopita nilielezea alivyochukuliwa kimiujiza na wachawi akiwa amelala na kupelekwa kuzimu kwa mtukufu Rusifa ambako aliwakuta babu yake wa Malawi na watu wengine waliokuwa na watoto wao ambao ni wafuasi wa Rusifa, wakipewa adhabu baada ya kumsaliti kwa kuamua kuokoka ambapo naye aliunganishwa nao. Wakiwa wanaunguzwa kwa moto kwenye shimo, walilia sana na kuomba wasamehewe ndipo walitolewa na kupelekwa mbele ya Rusifa. Je, Rusifa atawasamehe? Ungana na Mwandishi KULWA MWAIBALE katika kisa hiki cha kweli kilichomkuta kijana Beka…
Mariam anakuwa tayari kugombana na wazazi wake kwa ajili ya Tom, anaamua kuishi hotelini na Ramsey ambaye baadaye anamtaka kimapenzi jambo lililopingwa vikali na Mariam. Hata hivyo, baadaye anamkubalia lakini hakuwa tayari kufanya naye mapenzi, kitu kilichomuudhi sana Ramsey aliyeamua kumuacha na kurudi zake Morogoro.
Mariam akaamua kujiua, lakini kabla hajafanya hivyo anajikuta akijisikia mwenye dhambi sana kujitoa uhai wake. Akaamua kuahirisha, hapo ndipo alipoona umuhimu wa kwenda kwa wazazi wake ambao walimpokea kwa mikono miwili.
Akiwa nyumbani kwa wazazi wake, anapanga safari ya uongo ya kwenda kwa rafiki yake Clara, lakini ukweli ni kwamba alikuwa anakwenda Muhimbili. Huo ukawa ndiyo utaratibu wake wa kila siku, hadi siku alipoamua kusema ukweli mbele ya mama yake.
Mzozo mkubwa unaibuka lakini mwisho wake, Mariam anaamua kurudi nyumbani kwake Mbezi, anakuta nyumba chafu sana yenye mpangilio mbovu, anaweka vitu sawa na kufanya usafi kisha anaanza maisha upya huku jambo kubwa linalokuwa mbele yake likiwa ni kumhudumia Tom.
Miaka minne badaye, Tom anazinduka mbele ya Mariam, anamfukuza akimwambia aondoke kwani Mayasa akifika ingekuwa ugomvi! Kwa kifupi Tom amepoteza kumbukumbu kabisa, lakini baadaye anapata picha kwamba alivamiwa na majambazi usiku akiwa anarudi nyumbani. Tom anapooza kuanzia shingoni hadi miguuni, taarifa ambazo Mariam alipewa! Mariam hamwelezi Tom ukweli juu ya kifo cha mama yake. Kila anapomuuliza, anajaribu kumficha! Lilikuwa jambo gumu sana kumweleza Tom kwamba mama yake alifariki dunia, tena alizikwa na Halmashauri ya Jiji. Je, nini kitatokea? SONGA NAYO....