Chuo cha Usimamizi wa fedha cha IFM cha jijini Dar, kimeibuka kidedea katika Shindano la kumsaka mlimbwende wa Vyuo Vikuu nchini, Miss Higher Learning, baada ya Mwanafunzi wa chuo hicho, Betrice Lukindo, kutwaa taji hilo usiku wa kuamkia leo.
Wakati Betrice akibatizwa umalkia wa Vyuo Vikuu nchini, Linda Mzinga kutoka Chuo cha Ustawi wa Jamii, Kijitonyama amechukua nafasi ya pili na Doris Donatus kutoka Dar es Salaam Institute of Technology (DIT) akiibuka mshindi wa tatu.
Kwa ushindi huo, Magreth amepata tiketi ya moja kwa moja ya kujiunga na Kambi ya Miss Tanzania msimu huu, tayari kwa kuwania taji la Miss Tanzania, 2009/10.
Shindano hilo lilifanyika ndani ya viunga vya Karimjee katikati ya jiji la Dar es Salaam, lililosababishwa kwa udhamini mkubwa wa Mtandao wa simu za mkononi wa Vodacom, Global Publishers Ltd, Clouds FM, Ndege Insuarance, kinywaji cha Overmeer na wadhamini wengine kibao.

Miss Vodacom Higher Learning 2009/10, Betrice Lukindo (katikati) akiwa katika picha ya pozi na mshindi wa pili, Linda Mzinga (kulia) na kushoto ni Doris Donatus, mshindi wa tatu.

Hii ndiyo ilikuwa Top 5.

Majaji, kutoka kushoto ni Miss Tanzania mwaka juzi , Jokate Mwegelo, Mwenyekiti wa Kamati ya Miss Tanzania, Hashimu Lundenga ‘Anko’ na Miss Tz mwaka jana, Nasreen Mohamed, wakiwa makini kutazama warembo (hawapo pichani).

Warembo wakicheza staili ya Mugongo Mugongo jukwaani baada ya kupanda kwa mara ya kwanza.

Kundi la sanaa la International Youth Ferowship, likikonga nyoyo za wadau wa urembo kwa ngoma ya kichina kabla ya mrembo kutangazwa.

Wanenguaji wa bendi ya muziki wa dansi ya African Stars ‘Twanga Pepeta’ wakivamia jukwaa wakati wa shindano hilo.

Nani amesema wanenguaji siyo masister Duu? Hawa mamiss ila ni wanenguaji wa Twanga wakiwa chobingo wakijipodoa kwa ‘Mapouda’

Staa wa Kundi la ucheshi la Orijino Komed ‘Masanja Mkandamizaji” akiinama kukwepa kamera baada ya kubambwa ukumbini hapo akishuhudia mchuano mkali wa walimbwende hao.
PICHA:CHRISTOPHER LISSA/GPL