CHAMA cha Wananchi (CUF), leo kimefanya maandamano makubwa yenye lengo la kudai tume huru na ya haki ya chaguzi nchini. Maelfu ya wananchi, hususan wanachama wa CUF, walijitokeza kushiriki maandamano hayo ambayo yamelitikisa jiji la Dar es Salaam.
Maandamano hayo yalianzia Buguruni kupitia baraba za Uhuru, Bibi Titi, Lumumba na kuishia viwanja vya Kidongo Chekundu, Mtaa wa Lumumba ambapo Msajili wa Vyama vya Siasa nchini, John Tendwa, aliyapokea na kuyahutubia, sambamba na Mwenyekiti wa Taifa wa CUF, Profesa Ibrahimu Haruna Lipumba, Makamu Mwenyekiti, Juma Duni Haji na Katibu Mkuu, Self Sharif Hamad.
Polisi wakiwa katika mavazi maalum ya kutulizia ghasia pamoja na magari ya kumwaga maji ya kuwasha, maarufu kama ‘Vikojozi’, walitanda katika maeneo mbalimbali ya jiji ambamo maandamano hayo yalipita ili kuimarisha ulinzi.

Baadhi ya waandamaji wa CUF wakiwa eneo la Msimbazi Kariakoo.

Vikosi vya Polisi vikiimarisha ulinzi eneo la Mnazi Mmoja ambapo vurugu zilikuwa zinanukia baada ya waandamanaji kuwekewa kizuizi wasielekee eneo la Posta zilipo Ofisi za Msajili wa Vyama vya Siasa.

Magari ya kumwaga maji ya kuwasha (Vikojozi) yakiwa yamewekwa tayari eneo la Mnazi Mmoja kuthibiti ghasia zozote wakati wa maandamano hayo.

Moja ya mabango yaliyokuwa yamebebwa na waandamanaji hao.

Wafuasi wa CUF wakisikiliza kwa makini hotuba za viongozi wao.

Msajili wa Vyama vya Siasa nchini, John Tendwa (kulia), akiwa na Mwenyekiti wa CUF Taifa, Profesa Ibrahim Haruna Lipumba (katikati) na Maalim Self Hamad (kushoto )wakiwa katika mkutano wa chama hicho viwanja vya Kidongo Chekundu mara baada ya kupokea maandamano hayo.

Maalim Self (kushoto) akihutubia.

Profesa Lipumba akimkaribisha John Tendwa kuhutubia.

Tendwa akwaihutubia wafuasi wa CUF.

Kutoka kushoto ni Lipumba, Tendwa na Maalif Self wakiondoka katika viwanja hivyo baada ya mkutano kumalizika.

Mapaparazi wakiwa wameparamia mnara wa saa uliopo katika makutano ya barabara za Uhuru na Msimbazi ili kupata picha bora za maandamano hayo.

Mtoto wa wafuasi wa CUF akishiriki maandamano kwa kibaiskeli chake.
PICHA:CHRISTOPHER LISSA NA RICHARD BUKOS/GPL