Haikutarajiwa, lakini ndivyo ilivyotokea usikuwa kuamkia leo ndani ya ukumbi wa Diamond Jubilee jijini Dar es Salaam ambapo kundi la muziki wa mwambao la Jahazi Modern Taarab ‘Wana wa nakshi nakshi’ waliposhindwa kurudia historia yao ya kujaza nyomi ukumbi huo na kujikuta ikizindua albamu yake mpya ya Daktari wa Mapenzi huku mashabiki wakiwa nusu.Hii ni kutokana na maasi yaliyofanywa na waliokuwa wasanii nyota wa kundi hilo ambao walianzisha kundi lao liitwalo Five Stars Modern Taaarab lenye upinzani mkali na Jahazi kwa sasa.
Mkurugenzi wa kundi la Jahazi , Mzee Yusuf akimpagawisha shabiki jukwaani wakati wa uzinduzi
Mtu mfupi huyu alikuwa kivutio ukumbini humo baada ya kujimwaga na kujiachia kwa raha zake huku akikatika nyonga katikati ya watu warefu hasa wanawake.
Baunsa huyu aliyekuwa akilinda usalama jukwaa kuu, alijikuta akisahau majukumu yake baada ya kuvamiwa na vimwana ambao walianza kumkatia mauno hadi akawa legelege wakati wa uzinduzi huo.
Ghafla ukumbi wa Diamond Jubilee uligeuka ulingo wa ndondi. Mabaunsa wakimdhibiti kijana ambaye alikuwa akitishia usalama ukumbini humo baada ya kulewa ‘nyapinyapi’na kuanza tabia ya ukorofi wa kupigana na kufurumisha matusi mazito.
Mwimbaji nyota wa bendi ya muziki wa dansi ya FM Academia ‘Wazee wa ngwasuma’ Jesus Katunzi, akitoa burudani usiku wa kuamkia leo katika Hoteli ya kisasa ya Johannesburg, iliyopo Sinza jijini Dar es Salaam.
Bingwa wa kuandaa nyama choma, ndizi na mapochopocho mengine katika hoteli ya Johannesburg Sinza, Daudi Tryphone akiwajibika kuwaandalia wateja ‘mnuso’ usiku wa kuamkia leo.
Duh!Wabongo bwana.Hebu mcheki huyu ‘ mama nanihi’ mzima aitwaye Sara ambaye alinaswa mitaa ya Sinza akiwa amekalia kwa pozi la kimitego kiti cha plastiki cha mtoto, huku mmiliki wa kiti hicho ‘dogo’ flani hivi akiwa presha juu kuhofia kiti chake hicho kuvunjika.
Ama kweli ajali haina kinga. Daladala linalopiga ‘ruti’ zake kati ya Mwenge na Kigogo lilinaswa likiwa limetumbukia katika mfereji wa barabara ya Kawawa jijini Dar es Salaam jana. Uzembe huchangia zaidi ajali za namna hii.
ALITAKA RUSHWA KUBWA Jamaa mmoja alikwenda nchini Kenya kwenda kutembea. Kwa bahati mbaya alikamatwa na askari wa nchi hiyo kwa kosa uzururaji. Jamaa huyo alikuwa na uwezo wa kifedha na aliona njia nyepesi ya kuachiwa huru ni kutoa rushwa. Hata hivyo askari alikataa hongo hiyo na kumpeleka kituoni na kumfungulia mashtaka mawili moja la kuzurula na pili kutaka kutoa rushwa. Mkuu wa kituo alimuuliza yule jamaa: Mkuu wa kituo: Ni kweli asemayo afande? Jamaa: Ni kweli lakini hakusema ukweli kuwa nimempa rushwa na kupokea, ila alitaka zaidi nikakataa na kuamua kunileta hapa. Mkuu wa kituo: Umempa kiasi gani? Jamaa alitamka kiasi cha pesa alizokuwa nazo yule askari na kumfanya aje juu lakini Mkuu wa kituo aliagiza askari apekuliwe na kukutwa na kiasi cha pesa alizosema yule jamaa. Pesa alirudishiwa yule Mtanzania huku askari akiwekwa ndani na jamaa akaachiwa na faida ya pesa za askari. Kweli mjini shule... (bonyeza soma zaidi kuendelea)
Kampuni ya Global Publishers & General Enterprises Ltd, wachapishaji wa magazeti pendwa ya Ijumaa, Risasi, Ijumaa Wikienda, Amani, Uwazi, Championi na wamiliki wa mtandao huu, leo imewamwakabidhi kitita cha jumla ya Shilingi Milioni 1.1 wanafunzi wa tano wa kidato cha nne kutoka shule ya Sekondari Tirav, iliyopo Yombo Machimbo, Temeke jijini Dar es Salaam ambao walifanya vizuri katika masomo yao mbalimbali. Makabidhiano hayo yamefanyika katika ofisi za kampuni hiyo zilizopo Bamaga, Mwenge mchana huu.
Mhariri Mkuu Mtendaji wa Global Publishers Ltd, Richard Manyota (kushoto) akimkabidhi kitita cha Sh. 500,000/ Omary Kabono ambaye ni mshindi wa masomo ya Historia, Uraia, Jiografia, Book Keeping na Biashara, ambapo kila somo alipewa laki moja.
Mpiga picha Mkuu wa Global Publishers Ltd, Richard Bukos (kushoto), ambaye pia ni mdau wa mtandao huu, akimkabidhi kitita cha Sh. 200,000/ , mwanafunzi Mwanahamis Mramba ambaye ni mshindi wa masomo mawili ya Kiswahili na English.
Msanifu kurasa wa Global Publoshers Ltd, George Alphonce “MC George’(kushoto) akimkabidhi, Kiumbe Mlile kiasi cha Sh. 200,000/ baada ya kushinda masomo ya Kemia na Baiolojia.
Mhariri wa gazeti la Ijumaa, Amran Kaima (kushoto) akimkabidhi Sh. 100,000/ Hysein Kangambili ambaye ni mshindi wa somo la Hesabu.
Wanafunzi hao wakiwa katika picha ya pamoja na mwalimu wao (watatu kushoto) wakifurahia ‘mahela’ yao.
KAMA HUYAJUI MAGAZETI YA GLOBAL PUBLISHERS LTD SOMA HAPA Picha: Christopher Lissa /GPL
Jiji lenye mastaa wengi, Dar es Salaam, Jumatano iliyopita lilitikisika na baadhi ya watu kusimamisha shughuli zao kwa muda, baada ya kusoma habari ya kihistoria, kuhusu mnyororo wa mapenzi wa mastaa kwa kuanzia kwa Wema Sepetu.
MKONGWE wa sanaa ya maigizo nchini ,Techla Mjata (Mama Mjata) amesema kuwa licha ya umri wake kuwa mkubwa, bado anaimudu vema fani hiyo na wakati mwingine anafanya vyema kushinda wale wanaoibuka sasa katika tasnia ya filamu...]
WAIMBAJI maarufu wa muziki wa Injili nchini, Upendo Nkone, Upendo na Amon Kilahiro, Victor Arone, Christina MwangÕonda na Joseph Nyuki watapanda jukwaa moja katika kumwombea afya njema Rais Jakaya Kikwete sambamba na uzinduzi wa Albamu ya Yesu ni Bwana na Tenda Wema ya muimbaji Margaret Somy...
Mshiriki wa shindano la kumsaka mkali wa Big Brother kutoka nchini Nigeria, Kelvin juzi alilazimisha kwa nguvu kumbusu bila mafanikio, Elizabet Gupta kama inavyoonekana pichani hali iliyopelekea binti huyo wa Kitanzania kumjia juu na kumzuaia asiendelee kumsogelea...
Mwenyekiti wa Serikali ya Mtaa wa Yangeyange, Kata ya Msongola, Ilala jijini Dar es Salaam kupitia tiketi ya Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), Bw. Colman Marwa Waisokera, anadaiwa kumjeruhi Muuguzi wa Zahanati ya eneo hilo, aliyetajwa kwa jina maarufu la Mama Marwa...
Baada ya vitisho vya kuuawa, Mkurugenzi wa African Stars Entertainment (ASET), inayomiliki Bendi ya Muziki wa Dansi ya African Stars ÔTwanga Pepeta InternationalÕ, Asha Baraka ÔThe Iron LadyÕ amesema, Ôhili nalo litapita tuÕ kufuatia kile alichodai ni kuandamwa na wabaya wake...
Hii ni hadithi yangu mpya, yenye mafundisho makubwa kwa watu waliofanya makosa na kuamini hawawezi kusamehewa! Pili kwa binadamu wengine ambao kazi yao kubwa ni kuhukumu na hawako tayari kusamehe, hawa huwahukumu hata watu waliokwishakufa! Ni vyema wakati mwingine kumwachia Mungu kazi yake. Nawakaribisheni muisome mwanzo mpaka mwisho, hakika hakuna atakayejuta kwamba alipoteza muda wake, kazi yangu mimi si kuburudisha tu bali kufundisha pia. ANZA NAYO...
Eflazia baada ya kutafuta dawa ya kuongezwa cheo anajikuta akiingia katika matatizo mengine kupaja ujauzito wa ndotoni. Nini kitaendelea TUWE PAMOJA...
Sueya baada ya kumtendea ubaya wifi yake na kushiriki katika mbinu za kumuondoa duniani mama Kiota kibao kinamgeukia na kujikuta amekuwa wendawazimu. Alipozinduka alijikuta kwa mganga akitibiwa bila kujua aliletwa lini na ugonjwa wake umechukua muda gani mpaka kurudiwa na akili timamu. Ili kutajua yote TUWE PAMOJA....
Hii ni Jumamosi nyingine tena tunakutana katika safu yetu nzuri kabisa ya kupeana elimu mahususi juu ya mambo ya mapenzi. Sina shaka wote mtakuwa wazima wa afya njema na mpo tayari kupata kitu kipya...
Dk. Clara ameamua kwenda porini kumsaka mume wake, lakini akiwa huko naye anaugua ugonjwa wa Chinese Encephalitis. Hataki kufia porini tena, anaingia ndani ya gari ili awahi Kinshansa, wakati anaingia barabarani, gari jingine linatokea upande wa pili na kumgonga! Akashuka mwanaume na kwenda kumkaba akiwa na hasira. Lakini mwanaume huyo alipiga kelele akisema ÒClaraaaaaa! Je, nini kitaendelea? SONGA NAYO...
Wachezaji wa timu ya Rasi kutoka Mbeya wenye (Jezi nyekundu) na wenzao wa Rasi ya Dar es salaam wenye (Jezi ya njano) wakiwania mpira kwenye uwanja wa Jamhuri Morogoro ambapo katika mchezo huo Rasi ya Mbeya waliibuka na ushindi wa bao 2-1.
Wachezaji hao walikuwa wakimenyana vikali katika michuano ya Idara na Wizara za serikali (SHIMIWI) inayoendelea mkoani Morogoro.
Georgia Gervase akimnyonyesha mtoto wake kabla ya kuingia uwanjani.
Georgia Gervase mchezaji wa timu ya Ras Kagera kutoka mkoani Kagera mwenye jezi iliyoandikwa GD akijarubu kumzuia mchezaji wa timu ya Rasi ya Mwanza ili asipeleke madhara katika lango la timu yake.