Theresia na Albert wameokolewa kutoka msituni wakiwa na maaskari wengine walioumwa na nyoka mwenye sumu ndani ya maji, kwa helikopta wakachukuliwa na kupelekwa mpaka hospitali ya Perirenyatwa ambako walilazwa na kuanza kupewa dawa ya kupambana na sumu ya nyoka! Siku chache baadaye Albert alirejewa na fahamu zake lakini Theresia aliendelea kubaki katika hali hiyo, matumaini ya yeye kupona yakazidi kupungua!
Kihistoria, Theresia ni mtoto wa aliyekuwa mfanyabiashara maarufu jijini Dar es Salaam, Steven Kunjumu ambaye alijihusisha na nguvu za giza katika utafutaji wa utajiri wake, akawa anaua watu na kuuza viungo vyao! Mwisho wa siku watu aliowaua wakaamua kulipa kisasi, hii ndiyo Revenge of the Dead! Kisasi hiki kikaanza na yeye Steven na mke wake, wakafa na kumwacha mtoto wao Theresia ambaye mizimu inaendelea kumtumia kuua watu ili ipate damu kama chakula chao. Je, nini kitaendelea? SONGA NAYO…
KATIKA kufanikiwa katika jambo lolote unahitaji walau mambo yafuatayo: 1. Kujua kile unachokitaka 2. Shauku ya hali ya juu ya kupata kile unachokihitaji. 3. Kuamini kwamba unaweza kukipata kile unachokihitaji, yaani kuuamini uwezo ulionao katika kuhakikisha unakipata unachokilenga. 4. Kuamini kuwa unastahili kukipata unachokihitaji. Namanisha kujiamini kuwa unathamani kabisa kukimiliki unachokitaka. Ujasiri ninaokwenda kuuzungumzia hapa unahusika moja kwa moja na jambo la tatu na la nne. Tuanze na jambo la tatu: Amini kwamba unaweza kukipata au kuwa nacho kile unachokihitaji...
KATIKA safari ya maisha, binadamu ukumbana na mitihani ya kila aina kwani wapo waliofiwa na watu wao muhimu kama watoto na wazazi, kuugua maradhi ya kutisha na kufilisika. Ukiacha hao, wapo ambao wamedhurumiwa mali na watu wengine na wapo ambao wanatumikia vifungo magerezani bila hatia yaani kwa kubambikiwa kesi za mauaji au makosa mengine.
Miongoni mwa watu wanaodai kukumbwa na kesi ya kubambikiwa ni kijana Mohamed A. Geni mkazi wa Dumila Wilaya ya Kilosa mkoani Morogoro.
Hebu ungana na Mwandishi Wetu katika mkasa uliomkuta kijana huyo ambaye anaanza kuelezea kilichomsibu na kujikuta akihukumiwa kifungo cha miaka 30 kwa kosa la kubaka lakini alitumikia miaka 9 tu na kuachiwa baada ya kubainika hakutenda kosa hilo…
TAASISI ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa Tanzania (TAKUKURU), imeendelea kulikomalia suala la wabunge wa Jamhuri ya Muungano kupokea posho mara mbili na kuwataka waheshimiwa hao kuiacha taasisi hiyo ifanye kazi yake kwa mujibu wa sheria...
Siku chache baada ya serikali kuchukua uendeshaji wa kituo kikuu cha mabasi ya mikoani na nchi jirani cha Ubungo jijini Dar es Salaam, hali ni shwari kabisa eneo hilo ambapo mapaparazi wetu walipatembelea mapema leo na kukuta shughuli za usafiri zikiendelea vyema kama inavyoonekana pichani. PICHA: CHRITOPHER LISSA NA RICHARD BUKOS /GPL
Bw. Nyelo Godwin kutoka kampuni ya Madini ya Euronets TZ Ltd, ambaye ni shahidi wa kwanza upande wa Serikali katika kesi ya ufisadi inayowakabili aliyekuwa Waziri wa Fedha, Basil Pesambili Mramba na aliyekuwa Waziri wa Nishati na Madini, Daniel Yona pamoja na aliyekuwa Katibu Mkuu wa Wizara ya Fedha, Grey Mgonja, ameanza kutoa ushahidi wake leo katika kesi hiyo inayounguruma katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu jijini Dar es Salaam. Kutoka kulia ni mshitakiwa wa kwanza katika kesi hiyo, Basil Pesambili Mramba, Daniel Yona na Grey Mgonja wakiwa katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu.
Nimetoka kwenye mkutano wa Dr Edward Hoseah ambao umemalizika muda mchache uliopita katika ofisi za makao makuu ya TAKUKURU Upanga jijini Dar es Salaam.
Katika Mkutano huo, kwanza Dr Hoseah kaanza kwa kusema "Sijiuzulu ng'o, maana toka asubuhi ninapokea simu za watu wakiuliza kama nimejiuzulu tayari" hayo yalikuwa maneno yake wakati anaingia ukumbi wa mikutano kabla hata ya kusamiliana na wanahabari.
Dr Hoseah anasema "kuna nini mpaka wabunge waogope kuchunguzwa na TAKUKURU? kinachomshangaza ni kuwa hata sheria inayotekelezwa na TAKUKURU imepitishwa na bunge lenyewe tena na wabunge hao hao, iweje leo waanze kulalamika kuwa hawatendewi haki? haki wanayoitaka waheshimiwa wabunge ni ipi?" anahoji Hoseah.
Aidha anasema , barua ya bunge ya tarehe 26/02/2009 iliyokuwa imeelekezwa kwake, ilikitaka chombo chake kufanya uchunguzi ili kujiridhisha maana kulikuwa na minong'ono ya wabunge kulipwa posho mbili, huku wanalipwa na bunge pamoja na taasisi wanayokwenda kuitembelea!
Amewataka wabumge ambao wamekuwa na sifa kubwa ya kupinga vitendo vya kifisadi watoe ushirikiano ili chombo hicho kiweze kuwafanyia 'natural justice' maana katika detection tayari makachero wa TAKUKURU walishapata kila kitu kuhusu posho hizo mbili za wabunge.
Aidha amewataka wabunge ambao wanaona anafanya makosa kuwachunguza, wapige kura ya kutokuwa na imani naye, na yupo tayari kwa lolote litakalotokea, huku akijiganba kuwa TAKUKURU sio mwisho wa maisha yake hata kidogo, "there is life after PCCB" anasema Dr Hoseah. (NA MKINGA)
USHINDI wa wasanii watatu kutoka Nigeria, Zimbabwe na Namibia ambapo kila mmoja wao alishinda tuzo mbili katika mashindano ya tuzo bora za video za muziki kwa mwaka huu, yaani ‘2009 Channel O Music Video Awards’, zilidhihirisha nguvu kubwa waliyo nayo wasanii hao katika fani hiyo...
Day 54 on M-Net’s Big Brother Revolution and Nigerian superstar D’Banj surprises the housemates! Tune in to Big Brother Revolution on DStv channel 198 or 199 and for more information, log on to www.mnetafrica.com/bigbrother.
Matumainia ya kumalizika haraka kwa tatizo la mgawo wa umeme ulioikumba nchi kwa takriban mwezi sasa, yamefifia, baada ya mitambo ya kufua nishati hiyo inayomilikiwa na Kampuni ya Independent Power Tanzania Limited (IPTL), kushindwa kuwashwa jana, kama ilivyotangazwa awali na Waziri wa Nishati na Madini, William Ngeleja...
Baada ya mtangazaji Aboubakar Sadick kuibuka mshindi dhidi ya Abdallah Mwaipaya wiki iliyopita, sasa vumbi linatimka ndani ya Kundi la Orijino Komedi, ambapo wasanii Alex Chalamila ‘Mc Regan’ na mwenzake Isaya Mwakilasa ‘Wakuvanga’...
*Jiji waanza kukusanya ushuru wenyewe Halimashauri ya Jiji la Dar es Salaam imeanza rasmi kukusanya mapato katika kituo Kikuu cha Mabasi Ubungo (UBT) baada ya mkataba wa kampuni binafsi inayomilikiwa na familia ya mwanasiasa mkongwe, Kingunge Ngombale Mwiru, iliyokuwa ikifanya kazi hiyo kukatishwa...
WABUNGE wa Bunge la Tanzania wapo katika maombolezo, mwenzao, Sigifrid Ng’itu (55) ameaga dunia usiku wa kuamkia leo katika Hospitali ya Muhimbili, Dar es Salaam...