arrowSet HomePage |arrowBookMark Us
right
lines

Global Publishers Tanzania- Uwazi » Articles for 16.11.2009

Tafuta  

Tembelea...

Kalenda

Gazeti la Ijumaa

Marafiki wetu

Habari Zilizopita

Soma Magazeti Yetu...

Gazeti la Risasi Mchanganyiko
Amani
Gazeti la Ijumaa Wikienda

Bongo Celebrities ...

 
Habari Zinazotamba Habari Mchanganyiko
» Aunt Ezekiel alivyopigika k ...
» ZITO LAIBUKA
» KIGOGO WA MURO NAYE KUKAMAT ...
» GLOBAL PUBLISHERS MUSIC PLA ...
» JERRY MURO AKOSWA RISASI
» Kigogo afanyiwa umafia
» JERRY: NASAKWA NIUAWE!
» HII KALI
» KIMBUNGA CHA BARAFU CHA ...
» Mramba, Yona kumtoa mgo ...
» Dalili 20 za mpenzi asi ...
» MWALIKO KWA WASOMAJI NA ...
» WATOTO WA MITAANI WAJIS ...
» Irene Uwoya:RAY NI KUWA ...

 

TIGO WAMWAGA ZAWADI

photos  
TIGO WAMWAGA ZAWADI
Kushoto ni Afisa Rasilimali Watu wa Tigo Bennett Kakorozya akikabidhi zawadi ya Laptop kwa mshindi wa PILI wa promosheni ya TIGO CHEMSHA BONGO HASSAN MOHAMED wa MBAGALA, katikati ni Tawonga Mpore Ofisa huduma za ziada Tigo na Afisa Uhusiano wa Tigo Jackson Mmbando wakishuhudia wakati wa hafla fupi ya makabidhiano iliyofanyika leo ofisi za Tigo makao makuu. kushiriki Mteja alitakiwa kutuma neno SWALI kwenda 15550 na kisha alianza kupokea maswali mbalimbali kutoka Tigo kwa mwezi mmoja uliopita.


TIGO WAMWAGA ZAWADI
Kulia ni Afisa Rasilimali Watu wa Tigo Bennett Kakorozya akikabidhi zawadi ya Plasma TV Inch 26 kwa mshindi wa kwanza wa promosheni ya TIGO CHEMSHA BONGO JAMAL JUMBE wa KINONDONI, katikati ni Tawonga Mpore Ofisa huduma za ziada Tigo na Afisa Uhusiano wa Tigo Jackson Mmbando wakishuhudia wakati wa hafla fupi ya makabidhiano iliyofanyika leo ofisi za Tigo makao makuu. kushiriki Mteja alitakiwa kutuma neno SWALI kwenda 15550 na kisha alianza kupokea maswali mbalimbali kutoka Tigo kwa mwezi mmoja uliopita.


TIGO CHEMSHABONGO WAKABIDHIWA ZAWDI ZAO.
WAWILI WATOKA MBAGALA


Tarehe 16 Novemba 2009, Kampuni ya simu za mkoni Tigo leo imekabidhi zawadi kwa washindi wa mchezo wa promosheni ya Tigo Bingwa iliyokuwa ikichezeshwa kwa kipindi mwezi mmoja uliopita. Zawadi zilizokuwa zikishindaniwa katika mchezo huo ni pamoja na 1Plasma TV 26 Inch-LCD mshindi wa Pili
    (16 November 2009)
Views: 78 | Maoni (1) | Soma Zaidi

 

'NIMELISHA WATU NYAMA YA MBWA KWA MIAKA 4'

uwazi  
'NIMELISHA WATU NYAMA YA MBWA KWA MIAKA 4'

Na Igenga Mtatiro, Tarime
JAMAA awliyefahamika kwa jina la Sinda Saidi mkazi wa Mtaa wa Saronge wilayani hapa, amenusurika kuuawa baada ya kubainika ana tabia ya kuwauzia watu nyama ya mbwa akidai kuwa ni ya mbuzi...
    (16 November 2009)
Views: 1914 | Maoni (9) | Soma Zaidi

 

Polisi alivyoua kwa risasi

uwazi  
Polisi alivyoua kwa risasi

Haruni Senchawa na Aziz Hashim
KISA cha tukio la askari polisi, PC Chediel George, wa Kituo cha Stakishari jijini Dar es Salaam kumuua kwa kumpiga risasi mfanyakazi wa Kampuni ya Mwananchi Communications Limited, George Jackson Demzee Nyanda (24), (pichani) kimetajwa...
    (16 November 2009)
Views: 1219 | Maoni (4) | Soma Zaidi

 

MAAJABU SAME

uwazi  
MAAJABU SAME

Na Dege Masori, aliyekuwa Same
NYUMA ya pazia la maafa ya mlima wa mawe na udongo uliofunika Kitongoji cha Manka, kilichopo katika kijiji cha Goha, Kata ya Myamba, wilayani Same, Kilimanjaro na kusababisha vifo vya zaidi ya watu 24, kuna maajabu mengi, Uwazi linaandika...
    (16 November 2009)
Views: 2192 | Maoni (7) | Soma Zaidi

 

Nilibambikiwa kesi, nikafungwa miaka thelathini-3

Mikasa ya kusisimua  
Mpenzi msomaji, kijana Mohamed Geni mkazi wa Dumila Kilosa mkoani Morogoro ambaye katika safari yake ya maisha anadai amekumbana na mkasa wa kubambikiwa kesi ya kubaka ambayo hatoisahau iliyosababisha kukaa gerezani miaka 9 akitumikia kifungo bila hatia, anaendelea kusimulia alivyojikuta katika kifungo hicho baada ya kumsaidia dada mmoja aliyefika Dumila akitokea Singida na baadaye kudaiwa alimbaka. Ilikuwaje mpaka akajikuta akitupwa lupango ili atumikie kifungo cha miaka thelathini? Ungana na MWANDISHI WETU KULWA MWAIBALE katika mkasa huu wa kweli…
    (16 November 2009)
Views: 553 | Maoni (3) | Soma Zaidi

 

NYERERE AONYA TOKA KUZIMU-2

Pasua Jipu  
HUU ni ubinafsi mbaya sana. Ni kweli kwamba demokrasia haiwezi kudumu ikiwa wachache hawatakubali matakwa ya wengi. Lakini matakwa ya wengi hujulikana katika majadiliano au mazungumzo ya wazi wazi...
    (16 November 2009)
Views: 136 | Maoni (0) | Soma Zaidi

 

REVENGE OF THE DEAD -29

hadithi za Shigongo  
Theresia anamsimulia Albert kila kitu kilichotokea maishani mwake, namna alivyochukuliwa na mizimu na kupelekwa chini ya bahari ambako alipewa kazi ya kukusanya damu ambayo ni chakula cha mizimu hiyo! Jambo pekee ambalo hakulielezea vizuri ni namna alivyoua, kwani hali hiyo ilitokea bila yeye mwenyewe kujitambua lakini fahamu ziliporejea alikuta watu wamekufa na akatupiwa lawama kwa mauaji hayo.

Maongezi hayo yanasikiwa na wazazi waliokuwa nje ya chumba cha hospitali alimolazwa Theresia, walipoingia baadaye, mama yake Albert akiwa na hasira nyingi alianza kumfokea Theresia akimwita mchawi na kumwambia angezisambaza habari za uchawi wake kwa Zimbabwe nzima ili kila mtu aelewe ni nani aliyewaua watoto wa Zimbabwe.

Theresia anaruka kutoka kitandani na kupiga magoti mbele ya mama huyo akimbembeleza asifanye hivyo, Albert akamnyanyua na kumrudisha kitandani tena, yeye akiwa amechukua jukumu la kumbembeleza mama yake asichukue hatua aliyotaka kufanya, mama huyo hakusikia, alizidi kufoka. Je, nini kitaendelea? SONGA NAYO…
    (16 November 2009)
Views: 1041 | Maoni (4) | Soma Zaidi

 

Hatua 10 za kutambua penzi la kweli!-2

Mahaba  
Wanawake/wanaume wengi hawafahamu wanahitaji wapenzi wa aina gani, hivyo wanajikuta kama watu wanaoingia sokoni bila kujua wanataka kununua nini? Ndiyo maana wengi wameangukia kwa matapeli wa mapenzi, wakichezewa na kuumizwa moyo bure...
    (16 November 2009)
Views: 344 | Maoni (1) | Soma Zaidi

 

Jinsi ya kuujenga na kuukuza ujasiri wetu-2

Saikolojia na maisha  
UTAKUTA mwingine anaambiwa “umependeza” anajibu “eeh, nilijua leo mtasema nimependeza” au “hata mi najua, mke wangu kaniambia nimependeza”...
    (16 November 2009)
Views: 143 | Maoni (0) | Soma Zaidi

 

DAR NA USIKU WA VIPAJI VYA TAARABU

photos  
Kundi la Jahazi Modern Taarabu usiku wa kuamkia leo liliwashindanishwa mashabiki wake kuimba nyimbo za kundi hilo ambapo mashabiki 14 waliweza kuonesha vipaji vyao kwa kuiga sauti za waimbaji wa kundi hilo.

Katika mashabiki hao, walipatikana washindi watatu ambao watatoa burudani kwenye sherehe za miaka mitano ya kipindi cha Mitikisiko ya Pwani kinachorushwa hewani na kituo cha redio cha Times FM.

MLEMAVU MWENYE KIPAJI CHA MIPASHO
DAR NA USIKU WA VIPAJI VYA TAARABU
Shabiki mwenye ulemavu wa macho, Pili Salum (kulia) akionesha ujuzi wake wa kuiga nyimbo za kundi la Jahazi ambapo alifanikiwa kuingia kwenye tatu bora. Kushoto aliyemshikia kipaza sauti ni muimbaji wa kundi hilo, Miriam Amour.

UHONDO UNAPOKOLEA
DAR NA USIKU WA VIPAJI VYA TAARABU
Kundi la mashabiki likitimbwilika wakati, Bi. Pili akipagawisha.

‘MWANAUME MASHAUZI’
DAR NA USIKU WA VIPAJI VYA TAARABU
Mtoto wa kiume (kulia) kidomo cha tabasamu, kiuno cha kubinuka akiserebuka kimtindo katika shoo hiyo.

MRITHI WA HADIJA YUSUPH
DAR NA USIKU WA VIPAJI VYA TAARABU
Shabiki huyu aitwae Munira Juma, naye aliwapagawisha mashabiki kwa kuiga kibao kilichoimbwa na Khadija Yusuph enzi hizo kiitwacho ‘Mkuki kwa nguruwe’.

BADO NIPO NIPO
DAR NA USIKU WA VIPAJI VYA TAARABU
Mkongwe wa muziki wa dansi hapa nchini, Hassan Bitchuka, usiku wa kuamkia leo alinaswa na kamera yetu akiendelea kufanya makamuzi na bendi yake ya Mlimani Park Orchestra (Sikinde ngoma ya ukae) katika uwanja wake wa nyumbani, DDC Kariakoo ‘Old Trafford’, jijini Dar es Salaam.

‘NAMI BADO NAPAGAWISHA’
DAR NA USIKU WA VIPAJI VYA TAARABU
Mkali wa muziki wa dansi hapa Bongo, mzee wa enzi hizo, Maalim Muhidin Gurumo wa Msondo Music Band (kushoto), usiku wa kuamkia leo alinaswa ukumbi wa Africentre jijini Dar es Salaam akiendelea kupagawisha mashabiki katika onesho la bendi hiyo lililofanyika ukumbi huo jijini Dar es Salaam.

Kulia ni mmoja wa mashabiki wa bendi hiyo aliyeshindwa kuvumilia na kuamua kwenda kuchezea jukwaani, sambamba na mkongwe huyo.

PICHA ZOTE NA RICHARD BUKOS /GPL
    (16 November 2009)
Views: 197 | Maoni (1) |

 

HAPA NI JIKONI KWA BRAZAMENI DULLY SYKES, KARIBUNI SANA!

photos  
Wikiendi hii, mapaparazi wa mtandao huu walitua pande za Tabata Kimanga jijini Dar es Salaam nyumbani kwa msanii wa muziki wa kizazi kipya, Dully Sykes a.k.a Mr.Misifa. Bahati mbaya hawakuweza kumkuta lakini waliishia nje ambako walivutiwa na hali ya jiko lake pamoja na dishi la Runinga yake. Hebu cheki ilivyokuwa...

HAPA NI JIKONI  KWA  BRAZAMENI  DULLY SYKES, KARIBUNI SANA!
Huu ndio muonekano wa picha ya jiko la staa wetu Dully Sykes’ Handsome Boy’ ambaye picha yake inaonekana hapo juu

HAPA NI JIKONI  KWA  BRAZAMENI  DULLY SYKES, KARIBUNI SANA!
Hapa ni mahali anapotumia kupikia chakula chake.

HAPA NI JIKONI  KWA  BRAZAMENI  DULLY SYKES, KARIBUNI SANA!
Baada ya kula huhifadhi vyombo vyake juu ya kochi hili la ‘mbavu za mbwa’ bila kuviosha ambapo nzi hufanya tafrija kwenye makombo. Hapa ni baada ya kupata kifungua kinywa.

HAPA NI JIKONI  KWA  BRAZAMENI  DULLY SYKES, KARIBUNI SANA!
Hili ndio kabati lake la kuhifadhia vifaa vyote vya jikoni.

HAPA NI JIKONI  KWA  BRAZAMENI  DULLY SYKES, KARIBUNI SANA!
Ukishangaa ya Musa utaona ya Firauni.Hili ndiyo Dish ambalo 50 Cent wa Bongo, Dully Sykes hulitumia kwenye Runinga yake, ambalo ameligeuza kamba ya kuanikia nguo.

HAPA NI JIKONI  KWA  BRAZAMENI  DULLY SYKES, KARIBUNI SANA!
Pembeni ya nyumba ameegesha ‘ mkoko’ (gari) wake wa maana ambao hata hivyo ulikuwa na pancha katika tairi lake la mbele upande wa kulia.

PICHA:CHRISTOPHER LISSA NA ISMAIL MANG’OLA
    (16 November 2009)
Views: 1298 | Maoni (16) | Soma Zaidi

 

BINTI AMPA KICHAPO MAMA YAKE MZAZI WAKIGOMBEA MTOTO

photos  
Katika hali inayoonekana kuwa ni mmomonyoko wa maadili uliopitiliza , dada mmoja mkazi wa mtaa wa Mandala, Buguruni jijini Dar es Salaam ambaye jina lake halikufahamika mara moja, hivi karibuni amemshushia kichapo kikali mama yake mzazi anayekadiriwa kuwa na umri wa zaidi ya miaka 60 na kumuumiza vibaya.Chanzo cha tukio hilo la aina yake inaelezwa kuwa ni mvutano uliokuwepo kati ya binti huyo na mama yake kuhusu mtoto wa binti huyo.

Imeelezwa kuwa alikuwa akimtaka mwanae akatembee naye mitaani ambapo mama yake alikuwa akikataa kwa madai kuwa binti yake huyo ni kiruka njia na hastahili kuondoka na mtoto mdogo kutokana na tabia yake ya uzururaji. Binti huyo alianza kumshushia kipigo mama yake mzazi ambapo watu wenye hasira waliingilia kati na kuanza kumfunza adabu binti huyo kwa kumshushia kichapo kikali.


BINTI AMPA KICHAPO MAMA YAKE MZAZI WAKIGOMBEA MTOTO
Pichani, binti akiwa hoi kwa kipigo kutoka kwa watu wenye hasira

BINTI AMPA KICHAPO MAMA YAKE MZAZI WAKIGOMBEA MTOTO
Hapa akiangua kilio huku raia mmoja akimshika kinguvu ili apigwe picha

PICHA: CHRISTOPHER LISSA/GPL NA MDAU ALLY DAUDI
    (16 November 2009)
Views: 183 | Maoni (1) |

 

Wanafunzi Elimu ya Juu wageuka ombaomba

Habari mbalimbali  
WANAFUNZI katika vyuo vikuu kadhaa nchini wanadaiwa kuishi maisha ya kubahatisha kutokana na fedha wanazozitegemea kutoka Bodi ya Mikopo kutowafikia kwa wakati mwafaka...
    (16 November 2009)
Views: 341 | Maoni (1) | Soma Zaidi

 

MISELE YA MLALA NJE

photos  
MISELE YA MLALA NJE
Siku zote usalama ni jambo la muhimu sana katika maisha yetu, kutokana na kutambua hilo denti huyu ambaye hakufahamika jina lake wala shule anayosoma jijini Dar, aliamua kuuchapa usingizi juu ya benchi katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu. Lakini kama ingekuwa sehemu ingine isiyo salama, naamini asingethubutu kufanya hivyo kwa kuhofia ‘dungadunga.’


MISELE YA MLALA NJE
    (16 November 2009)
Views: 132 | Maoni (2) |

 

Rais Karume ataka CUF kupeleka majina ya wawakilishi

Habari mbalimbali  
Rais Karume ataka CUF kupeleka majina ya wawakilishi
Rais wa Zanzibar, Amani Abeid Karume

Rais wa Zanzibar, Amani Abeid Karume, amesema hakuna masharti waliyowekeana katika mazungumzo yake na Katibu Mkuu wa CUF, Maalim Seif Shariff Hamad, katika kumaliza mpasuko wa kisiasa wa Zanzibar...
    (16 November 2009)
Views: 507 | Maoni (1) | Soma Zaidi
Back  <<  1 2  >>  Next Page
 

Kura Yako / Poll

Habari Katika Picha


Author: admin


Gazeti la Uwazi



Nani Yupo / Alikuwepo


Home Page | About Us | Regista | Picha | Bongo Celebrities | Maoni | Contact Us

 hit counter

counters

2008 © globalpublisherstz.com