Mwenye fulana yenye mistari ni Katibu Mkuu wa timu ya Yanga Iman Madega. Kama hujamtazama kwa makini mtu aliye mbele yake aliyevaa shati lenye mikono mirefu unaweza kumdhania kuwa ni aliyekuwa Mkurugenzi wa Utawala na Fedha katika Benki Kuu ya Tanzania (BoT) Amatus Liyumba ambaye anasota mahabusu kwa takribani mwaka mmoja na nusu sasa. Picha hapo chini ni Amatus Liyumba (original) jaribu kuwafananisha na Pacha wake hapo juu. Amatus Liyumba (original), akitoka katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu
TUKO TAYARI KWA FIESTA ‘ONE LOVE’ Watangazaji na Ma-DJ wakali wanaopiga mzigo katika kituo cha Redio Clouds FM cha jijini Dar es Salaam, DJ B12 (kulia) na DJ-Mully B a.k.a Mully Bringbring wakiwa katika picha ya pamoja. Ma-DJ hao walisema kuwa wako tayari ‘kukimbiza’ wakati wa Bonanza kubwa la Fiesta ‘One Love’ linalotarajiwa kufunika ndani ya viwanja vya Chuo cha Posta Kijitonyama jijini Dar es Salaam, Jumamosi (Novemba 21) mwaka huu.
MLIMA KILIMANJARO WAHAMIA DAR Ukitazama kwa makini picha hii utaona kama vile kwa mbali unaona kilele cha Mlima Kilimanjaro. Hii ni moja ya mfano wa mlima huo iliyopo katika viunga vya jengo moja jipya lililopo kando ya Barabara ya Mandela, jijini Dar es Salaam.Mfano huu wa kilele umekuwa kivutio kikubwa kwa wapiti njia licha ya kuonekana kwa mbali ukiwa ndani ya uzio.
MASILIANO HOUSE HIYOO Ujenzi wa majumba makubwa na ya kisasa unazidi kuendelea jijini Dar es Salaam na kufanya mandhari ya jiji kubadilika sana na kuwa ya kuvutia. Pichani ni jengo kubwa la Mawasiliano House lililopo kando ya barabara ya Sam Nujoma likiwa limekamilika.
PHARMACY YA DAWA ZA ASILI Utafiti wa dawa za asili a.k.a Mitishamba, unaozidi kujipatia sifa nchini Tanzania, umepelekea kuibuka kwa maduka mengi makubwa yanayouza dawa za asili huku wateja kibao wakimiminika kununua dawa hizo. Pichani ni moja ya duka la dawa lililonaswa na mpiga picha wetu maeneo ya Tabata jijini Dar es salaam likiwa na dawa mbalimbali za mitishamba.
Ndege aina ya Boeing 727 inayosafirisha kombe hilo
KOMBE la Dunia la soka linawasili jijini Dar es Salaam leo saa 10:00 jioni likitokea Addis Ababa, Ethiopia na kupokelewa na viongozi wa serikali ya Tanzania kwenye Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere.
Waziri wa Habari, Utamaduni na Michezo, Kapteni George Mkuchika ndiye atapokea kombe hilo ambalo litapelekwa moja kwa moja kwenye Uwanja wa Taifa na kukabidhiwa kwa Rais Jakaya Kikwete.
Burudani zaidi pamoja na kupiga nalo picha vitafanyika siku ya Jumamosi.
The seventh edition of the Sauti za Busara music festival will take place in Zanzibar, 11-16 February 2010; admission is free to all EA Residents before 5pm. Sauti za Busara (Sounds of Wisdom) is an international festival celebrating East African music taking place around the second weekend of February each year in Zanzibar.
TUKIO la kusikitisha, kutisha na kuogopesha limetokea Dar es Salaam, ambapo mwanaume mmoja mkazi wa Mbagala Charambe Machinjioni, jijini, Sharifu Hassani Kondo (45), anadaiwa kumchoma visu hadi kumuua mkewe wa ndoa, Bi. Khadija Daudi (22), Amani lina ‘fulu’ data kutoka kwa ndugu, wazazi na watu wa karibu wa wanandoa hao...
Comedian ‘kiraka’ Bongo ndani ya Kundi la Orijino Komedi, Emmanueli Mgaya ‘Masanja MKandamizaji’, ameibuka na kudai anawamis kinoma flowers aliokuwa akikutana nao pale Club Maisha Masaki, jijini Dar es Slaam, ambayo iliteketea kwa moto hivi karibuni...
Nyota wa Pop na R&B toka pande za USA, Aliaune Badara Akon Thiam a.k.a Akon, ni mmoja wa staa barani Afrika watakaopiga shoo wakati wa ufunguzi wa michuano ya soka ya Kombe la Dunia huko Bondeni mapema mwakani...
Msanii wa Kizazi Kipya, Abrahamu Kasembe‘Dullayo’, mwisho wa wiki iliyopita alijikuta katika wakati mgumu baada ya kuchomwa visu na watuwasiojulikana alipokuwa akitoka Club ya Pop Life iliyoko Maeneo ya Uwanja wa Ndege, jijini Dar...
Taasisi za elimu ya juu nchini zinatajwa kuwa nambari wani kwa skendo za ngono zinazofanywa na ‘madenti’ ambao huishia kwa kuteketezana wao kwa wao, Amani lina ripoti kamili...
Maisha ya Kelvin kijana aliyepata mafanikio makubwa sana kwa kucheza soka kuliko Mtanzania mwingine yeyote katika historia kwani alifikia mpaka kuchezea klabu kubwa kama Liverpool ya Uingereza, yanaporomoka kwa kasi ya ajabu na kujikuta masikini wa kutupwa akiishi kwenye kibanda kidogo cha mwanamke aitwaye Regina, rafiki wa mama yake mzazi (Kokubanza)
Mambo haya yalianza akiwa kwenye kilele cha mafanikio, kwanza mama yake aliyekuwa akiishi naye nchini Uingereza aligundulika kuwa na Saratani ya damu na madaktari kusema angekufa baada ya miaka mitatu, jambo hili lilimfanya Kelvin akatishe mkataba wake wa mamilioni ya Paundi na kurejea nyumbani kumuuguza mama yake mpaka atakapokufa. Hakujua kwamba mama yake huyo huyo ndiye baadaye angemuuguza yeye!
Miaka miwili ilipopita, mama yake akijua alikuwa amebakiza mwaka mmoja tu wa kuishi, alimtaka Kelvin aoe ili amwone mjukuu wake kabla hajaondoka duniani! Wazo hili lilimfanya Kelvin amrejee msichana aliyemkatalia mapenzi kwa muda mrefu (Martina Weston) raia wa Uingereza, mtoto wa familia tajiri ya watengeneza mashine na karatasi za kuchapia magazeti ambaye alitegemewa kuwa mrithi wa utajiri wote baba yake akifa.
Wazazi wa Martina walikataa kabisa mtoto wao kuolewa Afrika, ndipo binti huyo akatoroka mpaka Entebbe ambako Kelvin alimpokea, mbele wakiwa njiani kuelekea Bukoba kabla hawajaondoka Kampala, gari lao liligongana uso kwa uso na lori kubwa, huo ndio ukawa mwisho wa kila kitu! Kelvin akapooza kuanzia shingoni mpaka miguuni, mama yake akaanza kumuuguza mpaka alipokufa wakiwa Beijing, China na kurejeshwa nyumbani kwa mazishi. Kelvin alilia mno, akiamini amebaki duniani peke yake.
Akajikuta mikononi mwa bibi Regina, rafiki mkubwa wa mama yake, ambaye alimchukua na kumpeleka kwenye kibanda chake kidogo cha nyasi, kufuatia nyumba yake kuungua kwa moto na kufilisika pale soko la Hisa la Uingereza ambako Kelvin aliwekeza fedha nyingi lilipoanguka na fedha zake zote kupotea! Mwanamke huyo alimsimulia historia ya maisha yake ambayo Kelvin hakuwahi kuisikia na kugundua kumbe mama yake hakuwa Mtanzania bali raia wa Rwanda, aliyeingia nchini mwaka 1959. Je, nini kinaendelea? SONGA NAYO…