Na Mwandishi Wetu OFISA mmoja wa Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi (jina kapuni) amedaiwa kutoa agizo la kuwataka polisi wasiwazuie wanadada wafanyao biashara ya kujiuza, maarufu kama ‘machangudoa’, eneo la Buruguni, Ilala, jijini Dar es Salaam...
Na Victor Bariety, Geita MENGI yanazidi kujitokeza kwenye sakata la mtoto Rebeka (3) ambaye anadaiwa kuibwa na watu wasiojulikana toka kwa mwanamke Mary Mathias na kuuzwa kwa shilingi 600,000 kwa Diana John na mumewe John Wambura wakazi wa wilayani Geita Mkoa wa Mwanza, baada ya baadhi ya wananchi wa eneo hilo kuongea kuhusiana na suala hilo na Uwazi...
SHAMBA letu kama halikutoa mavuno ya kutosha, jibu lilikuwa wazi: au limerogwa au ni amri ya Mungu. Watoto wetu walipokuwa wagonjwa daima jibu lilikuwa rahisi au wamerogwa au ni amri ya Mungu. Nyumba yetu ilipopigwa radi ikaanguka, jibu lilikuwa rahisi: au ni uchawi au amri ya Mungu...
Mpenzi msomaji, kijana Mohamed Geni mkazi wa Dumila Kilosa mkoani Morogoro ambaye katika safari yake ya maisha anadai amekumbana na mkasa wa kubambikiwa kesi ya kubaka na kujikuta akitupwa gerezani alikotakiwa kutumikia kifungo cha miaka 30, anaendelea mkasa uliomkuta uliosababishwa na wema aliomtendea dada mmoja aliyefika Dumila akitokea Singida na baadaye kudaiwa alimbaka. Ilikuwaje? Ungana na MWANDISHI WETU KULWA MWAIBALE katika mkasa huu wa kweli…
Baada ya Theresia kukiri mbele ya Albert na maneno yake kuwafikia wazazi wa kijana huyo waliokuwa nje ya wodi, kwamba ni yeye ndiye aliyehusika na vifo vya wanafunzi wote mbugani akijifanya Popo, hasira iliwashika wazazi wa Albert hasa mama yake, wakamchukua mtoto wao kwenda shuleni ambako waliwapasha wazazi waliofiwa juu ya habari hiyo.
Hasira zikawapanda wazazi hao, wakaondoka kuelekea hospitali alikolazwa Theresia, lengo lao likiwa ni kwenda kumuua! Wakati wanaondoka, Albert alikuwa amesinzia akiwa ndani ya gari, alipozinduka aliwakuta hawapo lakini baba yake pekee ndiye alikuwepo, wote wawili wakaondoka, Albert akiendesha mpaka hospitali.
Kumbe wazazi wenye hasira walipofika hospitali waliamuru wagonjwa wengine wote kutolewa nje ya wodi, akabaki Theresia peke yake, huyu ndiye wakaamua kuchoma wodi akiwa ndani na kuteketea! Wakati Albert na baba yake wanafika ndio wodi ilikuwa ikiendelea kuteketea, Albert akauliza mahali alipokuwa Theresia na kuambiwa alikuwemo ndani ya moto, moyo ukamuuma sana hasa baada ya kusikia wananchi wakishangilia kifo cha mchawi! Kabla hajafanya lolote alishtukia akishikwa na watu wawili, walikuwa ni baba na mama yake akiwa ametapakaa damu nyingi iliyovuja Theresia alipompiga na nguvu zake za uchawi, akaokolewa na Albert kwa maombi. Je, nini kitaendelea? SONGA NAYO…
MAPENZI yanataka elimu, lakini si wote wanaojielimisha namna ya kuwafanya wapenzi wao wajione kuwa ni salama na hivyo kuyafanya mapenzi yao kudumu kwa muda mrefu. Wanaume wa siku hizi wamekuwa hawafahamu ni vitu gani ambavyo wanawake wanapenda kuvipata kutoka kwao. Kushindwa kuwa na elimu hii, wanaume wengi wamejikua wakitumia ukali kuwatawala wake zao, jambo ambalo limekuwa likizidisha migogoro ya kimapenzi na hatimaye wapenzi huachana. Yafuatayo ni mambo muhimu ambayo wanawake hupenda watendewe na wapenzi wao...
KATIKA maisha yetu ya kila siku mara nyingi tunajikuta katika mazingira yanayotulazimu kufanya maamuzi magumu au kuchagua kitu katikati ya vitu vingi ambavyo vinatuchanganya akili. Wengi wetu kwa ugumu huu wamejikuta wakifanya maamuzi mabovu na chaguzi mbovu ambazo ama ziliwapa hasara au ziliharibu kabisa muelekeo au mustakabali wa maisha yao...
Tamasha la burudani la Fiesta mwaka huu ambalo lilipewa jina la ‘One Love’ limeacha bonge la stori kutokana na makamuzi yaliyofanywa na wasanii mbalimbali akiwemo mkali wa Hip Hop kutoka Marekani, Busta Rhymes.
Busta Rhymes (kulia) na mwanamuziki wake, Spliff Star.
Wakati mishemishe za Fiesta zikiendelea njemba ‘mwenye singlendi’ nyeupe ilibidi apigwe ‘Tanganyika Jack’ akituhumiwa kukwapua simu.
Mpiga picha Mkuu wa Global Publishers, Richard Bukos (kulia) akiwa ndani ya Fiesta; kushoto ni Msanii wa Mabaga Fresh, Chrisostoms Mwingira aka DJ Snox.
Mabaunsa wakiwadhibiti watu waliokuwa wakitaka kuvuka uzio wa kulikaribia jukwaa.
Busta akikamua.
Sir Juma Nature (katikati) akiwajibika na kundi lake la TMK Wanaume Halisi.
DJ Snox wa Mabaga Fresh (kulia) na msanii mwenzake wa kundi hilo Mkuu wa Maadui wakisindikiza Fiesta ‘One Love’.
Mkali wa Hip Hop kutoka Marekani, Spliff Star (kushoto), akihojiwa na Mwandishi Muandamizi na Mpiga Picha wa Global Pubishers, Christopher Lissa (mwenye begi).
DJ wa Busta Rhymes, Ice Cold, akimuandikia Lissa, E-mail yake na njia nyingine za kuwasiliana naye.
Ijumaa iliyopita msanii ‘The High Quality’ barani Afrika, Steven Charles Kanumba alitembelea ofisi za Kampuni ya Global Publishers and General Enterprises Ltd zilizopo Bamaga, Mwenge na kuongea na wafanyakazi.
Akiwa Global, Kanumba aliisifu kampuni hiyo inayozalisha magazeti ya Uwazi, Ijumaa, Amani, Risasi, Championi na Ijumaa Wikienda kwa kuandika habari za kweli zinazoelimisha, kuijenga jamii na kukosoa bila kumuonea mtu.
Steven Kanumba (kulia) akimsikiliza Mhariri Mtendaji wa Global Publishers, Richard Manyota (kushoto) ambaye alikuwa akiwafahamisha wafanyakazi wa kampuni hiyo kuhusu uwepo wa msanii huyo.
Steven Kanumba akizungumza na wafanyakazi wa Global Publishers (hawapo pichani)
Kanumba aliyevaa kofia nyeusi, akisikiliza maelezo ya jinsi ya kupanga gazeti kutoka kwa Msanifu Kurasa wa Global Publishers, George Alphonce ‘MC ’ aliyekaa. Wengine pichani ni Mhariri Mtendaji, Richard Manyota na Afisa Usambazaji, Gasper Mchele.
Kanumba (katikati) akihojiwa na mwandishi wa habari za michezo na burudani, Hemed Kisanda (kulia), kushoto ni mtaalamu wa kompyuta wa Global Publishers, Clarence Mulisa.
Rais Amani Abeid Karume, akipokea maandamano ya wananchi katika uwanja wa Demokrasia, Kibandamaiti, Mkoa wa Mjini Magharibi, Unguja, jana.
RAIS wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi, Amani Abeid Karume ameeleza kwa undani yaliyojiri katika mkutano kati yake na Katibu Mkuu wa Chama cha Wananchi (CUF), Maalim Seif Sharif Hamad na kumtaja kiongozi huyo wa CUF kuwa ni jasiri kutokana na uamuzi wake wa kwenda kuwatangazia wafuasi wake kwamba anamtambua kuwa ni Rais...
Wakazi wa Kijiji cha Mkunya, Wilaya ya Nachingwea mkoani Lindi, wakiwa na mabango yenye ujumbe mbalimbali.
Msafara wa Waziri Mkuu, Mizengo Pinda, juzi ulilazimika kusimama njiani baada ya wakazi wa kijiji cha Mkunya wilayani Newala, Mtwara, kuziba njia wakiwa na mabango huku bango kubwa likimwomba asimame na kuwasikiliza japo kwa dakika 10...
Na Waandishi Wetu Shoo ya Fiesta 2009 ilipambwa na vitu vingi, mojawapo likiwa ni tukio la warembo kumganda mwana-Hip Hop wa Marekani, Trevor Tahiem Smith Jr a.k.a Busta Rhymes huku kila mmoja akitaka aondoke naye...
Ni muimba kwaya Shinyanga! Ninavyomfahamu Johari alikuwa muimba kwaya Shinyanga, tena alikuwa kanisa moja na Kanumba (Steven). Mimi Edwin 0713-542446...
Na Hemed Kisanda Staa wa filamu ‘The High Quality’ barani Afrika, Steven Charles Kanumba ameamua kunena kuhusu uhusiano wa kimapenzi na nini hatma yake baada ya kuachana na Miss Tanzania 2006-07, Wema Isaac Sepetu ‘The History’...
Na Mwandishi Wetu Mwanamuziki aliyewahi kutamba enzi hizo kwenye muziki wa Bongo fleva, Happiness Thadei a.k.a Sister P (pichani), hivi karibuni alimuanika hadharani mchumba wake aliyemtaja kwa jina la HP huku akidai kuwa, ndiye anayetarajia kuishi naye katika maisha ya mume na mke...