Na Mwandishi Wetu KIUNGO Ahmed Jamal raia wa Kenya, amesema yuko tayari kutua Simba, lakini ametaka kitita cha dola 50,000 ili kujiunga na kikosi cha Msimbazi kwa ajili ya mzunguko wa pili...
Na Mwandishi Wetu HATUA ya mfadhili mkuu wa Yanga, Yusuf Manji kugoma kutoa kitita cha zaidi ya shilingi milioni 50 kwa ajili ya kumlipa mshambuliaji, Robert Jama Mba raia wa Cameroon, kimeifanya timu hiyo kushindwa kumuacha...
Na Khadija Mngwai MSHAMBULIAJI wa nyota wa Azam FC, John Boko amesema atafanya kila juhudi kuhakikisha kikosi cha timu hiyo kinatimiza adhima yake ya kucheza michuano ya Kimataifa iliyo chini ya Shirikisho la Soka Afrika (Caf), msimu ujao...
Na Samirah Phillip UONGOZI wa Klabu ya Manyema Rangers baada ya kumalizika kwa mzunguko wa kwanza wa Ligi Kuu ya Vodacom, wameelekeza nguvu zao kukinoa kikosi cha timu B kujiandaa na michuano ya Uhai inayotarajia kufanyika Novemba 29 jijini Dar es salaam...
Na Samirah Philip KOCHA Mkuu wa Mtibwa Sugar, Salum Mayanga amesema wataitumia mikiki ya Ligi Kuu ya Vodacom kufanya vizuri na kulibeba kwa mara ya pili mfululizo kombe la Tusker...
Samira Phillip na Leah Kweka KOCHA mkuu wa timu ya Taifa Taifa Stars, Mbrazil, Marcio Maximo amesema anawashukuru Rais wa Jamhuri ya Muungano ya Tanzania, Jakaya Kikwete na yule ya TFF, Leordegar Tenga kwa kuwa wanamuunga mkono katika maendeleo ya timu hiyo...
Na Khadija Mngwai MWENYEKITI wa Simba, Hassan Dalali amesema anajiamini kwa asilimia mia moja kuibuka na ushindi tena kwenye uchaguzi mkuu wa klabu hiyo utakaofanyika Desemba mwaka huu...
Na Mwandishi Wetu MMOJA wa wagombea katika Shirikisho la Mpira wa Kikapu Tanzania (TBF), Selemani Semunyu amesema iwapo atapata nafasi ya uongozi atajikita zaidi katika kusaka, kuibua na kuendeleza vipaji vya watoto katika mchezo huo...
Na Saleh Ally MFUNGAJI bora wa Ligi Kuu ya Vodacom msimu uliopita, Boniface Ambani amesema anatarajia kurejea Yanga ndani ya wiki hii kuzungumza na uongozi wa klabu hiyo na mwisho kuchukua malipo yake baada ya mkataba wake kuvunjwa...
Amepandishwa juu ya ghorofa lililo jirani kabisa na ukumbi wa Golden Jubilee akiwa na bunduki yake aina ya AK47 na mikanda ya risasi, hapo alipo ni umbali wa mita mia mbili mpaka mahali walipo majambazi, maaskari na wanajeshi wanaamini si rahisi kumlenga mtu kwa risasi na kumpata lakini Josia amewaomba wamwachie kazi hiyo yeye! Muda mfupi baadaye helkopta ilionekana ikishuka taratibu juu ya paa la ukumbi wa Golden Jubilee ambako majambazi wamesimama wakijiandaa kupanda ili waondoke.
Walichokiona maaskari waliokuwa chini wakiwa wamekata tamaa na kuamini kombe limeondoka, ni jambazi akidondoka juu ya paa la ukumbi, yeye ndiye alikuwa amebeba kombe, likaanza kuporomoka juu ya bati na kwenda moja kwa moja hadi chini! Wakaelewa tayari Josia alikwishaanza kazi yake, jambazi mwingine tena akajaribu kuishika kamba lakini yeye pia akadondoka chini na kulala juu ya paa, hivyo ndivyo ilivyotokea kwa majambazi wote kumi, hatimaye helkopta ikaamua kuondoka.
Kwa Josia kazi ilikuwa imemalizika, akashuka haraka hadi chini ambako alikimbia mpaka mbele ya ukumbi wa Golden Jubilee na kunyanyua mikono yake juu akiwaita maaskari wamsogelee, wakafanya hivyo, kwa pamoja wakaingia ndani ya ukumbi na kukuta maelfu ya watu wamelaliana! Hakuna jambazi aliyekuwepo.
Josia na Vivian wanapanda hadi darini lengo lao likiwa ni kupita sehemu ile ile waliyopitia majambazi kuingia ndani ya ukumbi, hapo Josia alisita na kumwacha Vivian atangulie kwanza, moyoni mwake alijua hapakuwa na tatizo lolote, majambazi walishakufa lakini Vivian alipotokeza nje tu mlio wa risasi ulisikika. Je, Vivian amekufa? Josia atafanya nini? SONGA NAYO..
Juu ni picha za matukio zinazoonesha miili ya watu waliopoteza maisha kwenye vurugu za kisiasa huko nchini Ufilipino
Ramani ya Ufilipino kuonesha eneo lililokumbwa na machafuko
AMPATUAN, UFILIPINO Rais wa Ufilipino, Gloria Arroyo ametangaza hali ya hatari kufuatia mauaji ya watu wapatao 46 katika machafuko ya kisiasa yaliyotokea nchini humo hivi karibuni.
Sehemu zilizotangazwa hali ya hatari kwa madhumuni ya kuwaruhusu askari polisi kuwatafuta wauaji ni majimbo mawili ya kisiwa cha Mindanao.
Waathirika wa mauaji hayo waliuawa wakati wakienda kujiandikisha kwa ajili ya uchaguzi mkuu unaotarajiwa kufanyika mwezi Mei, 2010. Hili ni miongoni mwa matukio mabaya ya vurugu za kabla ya uchaguzi kuwahi kutokea nchini Ufilipino.
Kumekuwa na taarifa nyingi za kuchanganya kuhusu idadi ya watu walionusurika katika maafa hayo. Jumatatu ya wiki hii iliripotiwa kuwa miili ya watu 22 iliokotwa kwenye mashimo visiwani humo lakini mpaka sasa inakadiriwa kuwa zaidi ya watu 46 wamepoteza maisha kutokana na vurugu hizo.
Imeelezwa kwamba idadi ya watu waliopoteza maisha inaweza kuongezeka zaidi endapo hali haitadhibitiwa mapema.
Kesi ya ufujaji wa mamilioni katika Benki Kuu ya Tanzania BoT inayomkabili aliyekuwa Mkurugenzi wa Utumishi Utawala na Fedha wa benki hiyo, Amatus Liyumba, leo imeendelea tena katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu kwa kusikilizwa.
Kesi hiyo imetolewa ushahidi na Mjumbe wa bodi ya benki kuu aliyekula kiapo kwa kujitambulisha kwa jina la Tatu Mwamba ‘hayupo kwenye mtandao kwa sababu maalum’, shahidi huyo pia ni Mhadhiri katika Idara ya Uchumi Chuo Kikuu cha Dar es Salaam, sambamba na cheo kingine alichokitaja mahakamani hapo kuwa ni Mwenyekiti wa Baraza Chuo cha Usimamizi wa Fedha (IFM), alipokuwa akielezea jinsi gani walivyokuwa wakifanya kazi katika jengo hilo la utawala.
JIKAZE KIUME MZEE HILI NALO LITAPITA Mtuhumiwa Liyumba akitoka katika sero ya mahabusu akipelekwa kizimbani kusikiliza shauri linalomkabili ambapo leo ilikuwa siku ya shahidi Tatu Mwamba kutoa ushahidi wake.
JELA KITU GANI BWANA!!! Mshitakiwa Liyumba akitembea kibabe kuelekea kizimbani huku akiwa chini ya ulinzi mkali wa ‘walezi wa watukutu’ yaani askari magereza.
PANDA NGAZI SHUKA MPAKA LINI? Mshitakiwa Liyumba akipandisha ngazi kuelekea kizimbani kusikiliza kesi yake katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu leo mishale ya saa nne asubuhi.
Steven Barker (kulia) aliyefungwa na mpenzi wake wa kike, Tracey Connelly (kushoto)
MMOJA wa watu watatu waliohukumiwa kifungo kutokana na kifo cha mtoto aitwaye Peter, leo atakata rufaa dhidi ya hukumu nyingine ya kumbaka mtoto wa kike aliyekuwa na umri wa miaka miwili...