Kiongozi wa Stone Mayiyasika, Maluu Stonch, akionekana 'kutekwa' na muziki wa bendi yake ambayo imeelezwa na wadau kuwa ni 'tishio' kwa bendi nyingine nchini.
VIJANA TUPENDE SCOUT Scout ni kazi ya kujitolea inayofanywa na baadhi ya vijana, hasa wanafunzi wa shule mbali za msingi jijini Dar es salaam. Mafunzo wanayopewa vijana hao husaidia kuwajenga kimwili na kiakili. Pichani ni baadhi ya Scout walioshiriki hafla moja katika viwanja vya Mnazi Mmoja jijini Dar es Salaam hivi karibuni.
Muslims from around the world continued to celebrate the end of their annual pilgrimage. Thousands of animals have been slaughtered in different parts of the country to mark the holiday known as Eid-al-Adha.
This week, ministers of 13 Eastern African countries signed, in Nairobi, a joint political declaration endorsing the UNODC Eastern Africa programme for 2009-2012.
"In Eastern Africa, warning lights are flashing - we must respond immediately", warned UNODC Executive Director Antonio Maria Costa, speaking at the regional ministerial conference on "Promoting the Rule of Law and Human Security in Eastern Africa". He added that Eastern Africa is under threat from all sides: smuggling and piracy along its coast, trafficking through its airspace and across porous borders, and the spillover of threats from unstable neighbours.
This regional UNODC programme is based on three pillars: countering trafficking, organized crime and terrorism; fighting corruption and promoting justice and integrity; and improving health and human development. Such a comprehensive programme is urgently needed because Eastern Africa is vulnerable to drugs and crime due to conflict, poverty and a weak rule of law.
To read the full story, please click here: http://www.unodc.org/unodc/en/frontpage/2009/November/-eastern-africa_-ministers-endorse-unodc-regional-programme-.html?ref=emaileastafricaprbp
Sincerely,
A[b]dvocacy Section United Nations Office on Drugs and Crime Website: www.unodc.org
Waziri Mkuu, Mizengo Pinda akizungumza na viongozi wa wilaya na Halmashauri ya Monduli, Arusha kuhusu hali yaukame na njaa wilayani humo kwenye ukumbi wa Halmashauri hiyo Novemba 27, 2009. Kulia ni Waziri Mkuu Mstaafu na Mbunge wa Monduli, Edward Lowassa na katikati ni mkuu wilaya hiyo, Njowika Kasunga. (Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu)
Waziri Mkuu, Mizengo Pinda akikagua uzalishaji wa mbolea katika kiwanda cha Minjingu mkoani Manyara, Novemba 27, 2009. Wapili kushoto ni mkuu wa mkoa wa Manyara, Henry Shekifu na kulia ni Mkurugenzi Mkuu wa kiwanda hicho, Hans Tosky.
Bibi Udamahena Marisha wa kitongoji cha Almasi alikuwa ni mmoja wa wananchi wengi waliofika kwenye viwanja kiwanda cha mbolea cha Minjingu, Manyara kumsikiliza Waziri Mkuu, Mizengo Pinda wakati alipotembelea kiwanda hicho na kuwahutubia wananchi Novemba 27, 2009. (Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu
Wafanyakazi wawili wa kampuni ya Global Publishers & General Enterprises Ltd, wachapishaji wa magazeti pendwa ya Ijumaa, Uwazi, Amani, Championi, Risasi, Ijumaa Wikienda na wamiliki wa mtandao huu, Sara Lushu na Alice Mtaki, jana wametunukiwa Stashahada zao za Uhasibu (Advanced Diploma in Accountancy), katika Chuo Cha Usimamizi wa Fedha (IFM) jijini Dar es Salaam. Aliyewatunuku vyeti hivyo ni Waziri wa Fedha na Uchumi, Mustapha Mkulo, katika mahafali ya 35 yaliyofanyika kwenye viwanja vya Karimjee, ambapo zaidi ya wahitimu 2000 walitunukiwa vyeti, Stashahada na Shahada katika taaluma mbalimbali.
Mahafali hayo yalianza kwa maandamano maalumu yaliyoanzia chuo cha IFM , Barabara ya Shaaban Robert na kuishia Karimjee ambapo yalipambwa na Brass Band ya Jeshi la Wananchi Tanzania (JWTZ).
Wakionekana wenye nyuso za furaha ni wafanyakazi wa Global Publishers, Sara Lushu (kulia) na Alice Mtaki kabla ya kutunukiwa Stashahada zao.
Sara na Alice wakiungana na wahitimu wenzao katika zoezi la kuvaa kofia maalum kama ishara ya kutunukiwa Stashahada zao kwa pamoja.
Sara (mwenye joho na kofia) akifurahi na marafiki zake mara baada ya kutunukiwa Stashahada yake ya Uhasibu.
Baadhi ya vigogo wa chuo cha IFM, wakiongozwa na Waziri wa Fedha na Uchumi, Mustapha Nkuro (kulia) wakihitimisha hafla ya Mahafali hayo ya 35.
Sara (kulia) akiwa ametulia na rafiki yake
Mtangazaji nyota wa kipindi cha Njiapanda kinachorushwa na kituo cha Redio ya Watu (Clouds FM), Sebastian Ndege, ambaye katika mahafali hayo alitajwa kuwa miongoni mwa wanafunzi bora waliofanya vizuri zaidi katika masomo yao, akifurahia cheti maalum cha mwanafunzi bora kilichoambatana na zawadi lukuki zilizotolewa na chuo hicho. Mtandao huu unawatakiwa kila la kheri wahitimu wote.
Chanjo nyinyine zineweza kuleta madhara kuliko tiba kama ilivyokusudiwa. Binti wa miaka 26 huko Marekani amepatwa na ugongwa wa ajabu baada ya kudungwa chanjo ya Mafua ya Nguruwe, anaweza kusema na kufanya vitu vingine akiwa anakimbia au kutembea kinyume kinyume, lakini akisimama anaanza kutetemeka na hawezaikuongea vizuri. Madaktari wamebaki midomo wazi na wanasema tukio hilo huweza kutokea kwa mtu mmoja kati ya watu milioni moja. Video hii inaonesha hali halisi ya binti huyo, siyo mchezo wa kuigiza!!!!
TAASISI za dini nchini, FBOs zimetoa azimio la pamoja zikieleza kuwa nchi imekosa dira na kushauri rais apunguziwe mamlaka yake, ili kuweka uwiano wa maamuzi katika mihimili yote mitatu ya dola...
• Asema CHADEMA wako tayari kukaguliwa na Mkaguzi Mkuu MWENYEKITI wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), Freeman Mbowe, amesema inampasa mtu kuwa na akili za kiuendawazimu kufikiria kuwa viongozi wa juu wa chama hicho wanafuja fedha za ruzuku, kama inavyodaiwa na baadhi ya watu...
NIMEWATOA NJE WAKACHEZE MPIRA Ndege moja iliyokuwa imepakiwa vichaa kufika angani walianza kucheza mpira kasoro kichaa mmoja alikuwa kimya amekaa kwenye siti akiwaangalia wenzake. Baada ya kuona kero zimezidi alifungua mlango wa ndege na kuwatoa nje wenzake naye akarudi kukaa. Rubani baada ya kuona vurugu zimetulia alijua vichaa wametulia baada ya kuchoka kucheza mpira. Ndege ilipofika alipokuwa akiwapeleka alishangaa kumkuta kichaa mmoja amekaa kwenye kiti. Rubani: Wenzako wako wapi? Kichaa: Walikuwa wakinisumbua niliwatoa nje wakacheze mpira wao Rubani alibakia kichwa wazi asijue atajibu nini.
ALIFANANISHWA NA MUNGU Kulikuwa na jamaa watatu kila mmoja alitoa sifa yake ya kufanana na mtu maarufu duniani. Wa 1, mimi wananifananisha na Idd Amini Kwa sababu gani? Kutokana na umbile langu refu na rangi yangu nyeusi watu wananifananisha na Marehemu Idd Amini dada. Wa pili: Mimi na Osama bin Laden Kwa sababu gani? Kutokana na weupe wangu na ndevu nyingi hata jina langu limekufa siku hizi naitwa Osama Wa tatu ambaye alikuwa na umbile dogo kuliko wote. Mimi nafanishwa na Mungu Watu wote walishtuka na kumuona yule jamaa kama anamkufuru Mungu lakini aliwathibitishia kweli kuna mtu alimfananisha na Mungu. Najua hamuwezi kuamini kama mjuavyo mimi mwenzenu mpenda ulabu na vifungu haviniishi, kila nilipopelekwa polisi nilihukumiwa na hakimu mmoja siku moja baada ya kupanda kizimbani hakunihukumu bali alinieleza kuwa ameniachia huru na nisirudie kufanya tena makosa. Lakini kwa bahati mbaya nilikamatwa na kupandishwa kizimbani, na hakimu alikuwa yule yule wakati napanda alikuwa ameinama akiandika ripoti baada ya kuandika aliponyanyua macho akaniona na kushtuka huku akisema. Mungu wangu umerudi tena Bado tu hamjaamini kuwa niliitwa Mungu, jamaa alibakia wakitazama kutokana na mwenzao kushindwa kumuelewa hakimu alikuwa na maana gani na si kumfananisha na Mungu.
Na Mwandishi Wetu Mcheza filamu staa wa Bongo, Aunt Ezekiel Gryson amekumbana na saa kadhaa za kushikiliwa na maafande wa kituo cha Polisi, Oysterbay jijini Dar....
Mkali wa muziki wa Injili nchini a.k.a mama wa maadili, Bahati Bukuku anatarajiwa kulinogesha tamasha la uzinduzi wa albamu ya sita ya mkongwe wa miondoko hiyo Jennifer Mgendi inayokwenda kwa jina la Kiu ya Nafsi...
Mwanamuziki maarufu wa kundi la muziki wa mwambao Five Star, Khadija Yusuf amedai kuwa na shauku ya kufanya shoo ya pamoja na kundi la Jahazi Modern taarab lililochini ya Kaka yake Mzee Yusuf ili kuwadhihirishia kuwa wao kwa sasa ni moto wa kuotea mbali...