Mabondia Rashid Matumla ‘Snake Boy’ na Joseph Marwa, kesho jioni wanatarajiwa kutwangana katika pambano lisilokuwa la ubingwa litakalofanyika Uwanja wa Uhuru jijini Dar es Salaam. Akizungumza na wanahabari katika Ukumbi wa Idara ya habari jijini Dar es Salaam leo, Mratibu wa pambano hilo, Ramadhani Uhadi alisema maandalizi yote ya mpambano huo yameshakamilika.
Promota wa mpambano huo Ramadhani Uhadi akiwainua mikono mabondia hao Joseph Marwa (kushoto) na Rashid Matumla wakati akiwatambulisha.
Rashid Matumla akipima Uzito kwaajili ya mpambano huo.
Joseph Marwa naye akipima uzito.
Jeseph Marwa (kushoto) na Rashid Matumla wakichimbiana mkwara kabla ya mpambano huo.
Matumla akimwaga majigambo mbele ya wanahabari (hawapo pichani).
Marwa naye alipopata nafasi aliyaponda majigambo ya Matumla na kujitapa kuwa yeye ndiye kidume na kusema kesho ndio kesho.
Marehemu Kawawa aliyefariki leo asubuhi saa 3:20 asubuhi, amehamishiwa hospitali ya jeshi la Wananchi ya Lugalo kwa ajili ya kuhifadhiwa wakati mipango ya mazishi ikifanywa na kusimamiwa na Serikali. Zifuatazo ni picha za tukio zima jinsi lilivyokuwa:
Mke wa marehemu, (aliyejifunga kilemba cheupe katikati) Bi Asina, akiusindikiza mwili wa mumewe Mzee Rashid Mfaume Kawawa.
Mama Salma Kikwete (wa pili kushoto mwenye kilemba) alikuwa miongoni mwa waombolezaji waliofika hospitalini hapo.
Huu ni msafara wa kutoka Hospitali ya Taifa Muhimbili kuelekea Hospitali ya Lugalo.
Kamishna mkuu wa kanda maalum ya Dar es Salaam, Suleiman Kova naye alikuwa miongoni mwa waombolezaji, ambapo alitumia nafasi hiyo kutangaza jinsi jeshi lake litakavyodhibiti usalama katika shamrashamra za kuukaribisha mwaka mpya 2010 usiku wa leo.
Picha: Musa mateja/GPL
Video mbili hapo chini, Mwili wa marehemu Mzee Kawawa ukitolewa Muhimbili tayari kupelekwa Hospitali ya Lugalo
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Jakaya Mrisho Kikwete, ametangaza siku saba za maombolezo kufuatia kifo cha aliyewahi kuwa Waziri Mkuu wa Tanzania Mzee Rashid Mfaume Kawawa, aliyefariki duania leo saa 3:20 asubuhi baada ya kusumbuliwa na ugonjwa wa kisukari kwa muda mrefu kwa muda huo bendera ya Taifa itapepea nusu mlingoti.
Rais alisema kuwa taratibu zote mazishi zitasimamiwa na serikali na atapewa heshima kwa muasisi wa kupigania uhuru wa Tanzania.
Msanii wa Bongo Flava anayejiita Beezy anayeiishi nchini Ujerumani, akimpaka Producer Marco Chali kwa madai ya kumzika milioni 1 za kibongo...msikilize mwenyewe.
Msanii wa Bongo Flava, anayejiita Wakazi anayeishi Chicago, Marekani, akimtetea Marco Chali kwa kumponda Weezy kuwa hajui kuimba vile vile..msikilize mwenywe.... kila mmoja katengeneza clip yake na kuiweka You Tube kila mtu aone na kusikia, hili ni bifu la kufungia mwaka, kazi kwenu wadau
Nyumba ya Gavana wa Benki kuu, Profesa Benno Ndulu
Gavana wa Benki Kuu, Profesa Benno Ndulu
WAKATI Wizara ya Fedha na Uchumi ikiwa katika uchunguzi wa gharama za ujenzi wa nyumba ya gavana wa BoT inayodaiwa kugharimu Sh1.4 bilioni, imebainika kuwa nyumba nyingine ya mmoja wa manaibu wake imegharimu Sh1.2 bilioni...
Picha hii ilipigwa Februari 27 mwaka huu, wakati Rais J.K akimpongeza Mzee Kawawa baada ya kuzindua kitabu chake uliofanyika katika viwanja vya Ikulu. Kitabu hicho kinachoelezea maisha ya Mzee Kawawa, kimeandikwa kwa ustadi wa hali ya juu chini ya usimamizi wa Profesa John Magoti, Mkuu wa Chuo cha Mwalimu Nyerere cha Kivukoni.
..hapa akitia saini kwenye moja ya vitabu vyake
Habari za kusikitisha za asubuhi ya leo zinasema kuwa Mzee Rashid Mfaume Kawawa, ambaye alizushiwa kifo jana, amefariki dunia leo asubuhi hii. Taarifa fupi ya Radio One Stereo iliyotolewa muda mfupi uliopita, imethibitisha kifo hicho. Mzee Rashid Kawawa, anafariki leo ikiwa ni siku ya mwisho kabisa ya kumaliza mwaka 2009 na anakufa akiwa na umri wa miaka 83. Mzee kawawa, ambaye pia alikuwa akijulikana kwa jina la Simba wa Vita, ndiye aliyekuwa Waziri Mkuu wa kwanza wa Awamu ya Kwanza wa Serikali chini ya hayati Baba wa Taifa, JK. Nyerere. MUNGU AILAZE ROHO YAKE PEPONI - AMIN!
KATIBU Mkuu wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), Dk .Wilbroad Slaa
KATIBU Mkuu wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), Dk .Wilbroad Slaa, amesema kuna haja kwa Rais Jakaya Kikwete, kuwaomba radhi Watanzania, kufutia kitendo cha serikali yake, kushindwa kutimiza ahadi ya kuibua ajira 1,000,000, kama alivyokuwa ameahidi katika kampeni zake za mwaka 2005...
Mkurugenzi mkuu wa asasi inayojishughulisha na maendeleo katika nchi za Afrika( FORDIA) Bubelwa Kaiza akitoa maelezo kuhusu taarifa ya utafiti wa mtazamo wa rushwa jijini Dar es Salaaam jana.
WAFANYAKAZI wa Shirika la Umeme Tanzania (Tanesco), askari polisi na wafanyakazi wa Mahakama, ndio wanaoongoza kwa rushwa nchini, utafiti uliofanywa na Mtandao wa Concern for Development Initiative in Africa (Fordia) umeonyesha...
Na Waandishi wetu Njemba mbili zilizojifanya Waandishi wa habari wa Kampuni ya Global Publishers zilizotajwa kwa majina ya Mick John Nyenza ‘Franco’ na Edward Mabula, Jumatatu wiki hii walitiwa mbaroni baada ya kunaswa wakiwa katika harakati za kutaka kulamba rushwa ya shilingi milioni 40 kutoka kwa kigogo mmoja wa kampuni ya simu za mkononi nchini (Jina tunaliminya) ..waandishi feki (mwenye shati la njano na shati jeupe) wakiwa chini ya ulinzi mkali mara baada ya kunaswa
Mwandishi Wetu na Mashirika ya Habari ya Kimataifa Wakati wananchi wengi Bongo wakiwa wamezoea kuona vibaka wa kiume wanaoibia watu wakikumbana na raia wenye hasira na kuwahukumu kwa moto, hivi karibuni mwanamke mmoja alistaajabisha watu baada ya kudakwa kama kibaka, hali iliyoashiria kuwa mwisho wa dunia unakaribia, Amani limeinyaka...
Na Mwandishi Wetu Leo ndiyo kikomo cha siku 365 za mwaka 2009, wengi wakitumbulia macho kesho ambapo mwaka mpya, 2010 unaanza, wengine kwa matumaini, wengine kwa kukata tamaa, Amani linakujuza zaidi...
Na George Kayala Nivigumu kuamini lakini ni kweli juu ya mambo yanayojitokeza kwa watu wanaoisikiliza albamu ya Ushindi ya mpakwa mafuta wa Mungu Kabula J.George ambayo imegeuka kuwa tiba kwa watu wenye matatizo sugu ambayo yameshindikana kutibiwa kwa madaktari bingwa na waganga wa kienyeji...
Mpenzi msomaji, kijana Kafumu aliyefundishwa uchawi na bibi yake, anaendelea kusimulia jinsi alivyosafiri na fisi akiwa na bibi yake hadi katika Bwawa la Kazima eneo ambalo wachawi wa Tabora hukutana na kufanya mambo yao lililopo karibu na kijiji cha Manoleo.
Anasema alipofika katika bwawa hilo alistaajabu kuwaona wachawi wa rika mbalimbali. Akiwa hapo bibi yake alimwambia ajichanganye kwenye kundi hilo la wachawi na kufuatilia kila kinachojiri. Akiwa amejichanganya babu mmoja alimfuata na kumbeba juu na kumwambia akiwa mkubwa atawasaidia watu wengi wenye matatizo kama alivyokuwa akifanya marehemu babu yake. Baadae babu huyo alimpeleka pembezoni mwa bwawa hilo alikowakuta akina bibi watatu, babu wawili,akina mama wawili na watoto wanne wa umri wake wakiwa wanachoma nyama na kula. Alipotakiwa kula nyama hiyo aligoma lakini baada ya kulazimishwa sana na kuambiwa kama angegoma kabisa angepoteza maisha alikubali. Nyama hiyo ni nyama gani na kwanini kama angekataa kula angekufa? Ungana na KULWA MWAIBALE katika mkasa huu wa kweli…
Nawashukuru watu wote ambao wamekuwa wakifuatalia somo hili toka tulipoanza wiki mbili zilizopita, naomba tuendelee tena wiki hii kuangali mambo mengine muhimu kuhusiana na aina za saikolojia na faida zake katika maisha yetu ya kila siku...
Kwanza nichukue fursa hii kumshukuru Mwenyezi Mungu mwingi wa rehema kwa kunijaalia kufikia siku ya leo nikiwa mzima bukheri wa afya. Nafanya hivyo nikiamini kwamba, wapo wengi waliotamani kuuona mwisho wa mwaka huu na mwanzo wa mwaka 2010 wakiwa wazima lakini kwa bahati mbaya leo hii wamelala kwenye nyumba za milele huku wengine wakiwa hoi mahospitalini wakisumbuliwa na maradhi mbalimbali...