Hasheem Thabeet wakati wa utambulisho wake kwenda Memphis Grizzlies mwaka jana
HASHEEM THABEET, Mtanzania aliyeko Marekani akicheza mpira wa kikapu katika ligi ya nchini humo (NBA) ameweka historia, japokuwa mambo hayamwendei kama anavyotaka...
Malkia wa Pop duniani Robyn Rihanna Fenty, ijumaa iliyopita aligeuka na kuwa mwalimu wa Muziki akimfundisha Mchekeshaji na Mtangazaji maarufu kutoka nchini Uingereza Alan Carr kucheza muziki wa Pop, wakati walipokuwa kwenye kipindi cha televisheni kiitwacho Chatty Man kinachorushwa na kituo cha televisheni cha British Tv
Rihanna akijaribu kumfundisha Mchekeshaji Alan Carr jinsi ya 'kudansi'
Beki wa Manchester City, Wyne Bridge (wa pili kushoto) akikataa kupeana mkono na nahodha wa Chelsea, John Terry (wa pili kulia) kabla ya mechi ya Ligi Kuu England kwenye uwanja wa Stamford Bridge, London jana. Bridge alilipa kisasi kwa Terry wakati Man City ilipoichabanga Chelsea mabao 4-2. John Terry alikuwa na mahusiano ya kimapenzi na Mpenzi wa kike wa Wyne Bridge.
Marehemu Balozi Daudi Mwakawago, enzi za uhai wake.
Rais Jakaya Mrisho Kikwete akiweka udongo katika kaburi la Marehemu Balozi Daudi Mwakawago wakati wa mazishi ya Mwanasiasa huyo mkongwe yaliyofanyika katika makaburi ya kisutu jijini Dar es Salaam jana.
Rais Kikwete kisalimiana na Katibu Mkuu wa Chama cha Wananchi CUF Seif Shariff Hamad wakati wa mazishi ya mwanasiasa mkongwe na mwanadiplomasia Marehemu Balozi Daudi Mwakawago yaliyofanyika katika makaburi ya Kisutu jijini Dar es Salaam jana jioni. Katikati ni Rais Mstaafu wa awamu ya tatu Mh. Benjamin William Mkapa.
Na GPL Ripota Baada ya wiki iliyopita, mrembo aliye kinara katika sanaa za maigizo, Irene Uwoya kumbwaga mwenzake Wema Sepetu kwa tofauti ya asilimia 14, sasa ndani ya nyumba, wameingia wazee wazima wa Hip Hop.
Hapa nawazungumzia mzee mzima Joh Makini a.k.a Mwamba wa Kaskazini na Rashid Makwilo a.k.a Chid Benz, ambao wanasababisha kwenye game ya Muziki wa Kizazi Kipya.
Hawa ni wakali ambao mchango wao unajulikana vyema katika sanaa hiyo hapo ya muziki wenye ladha za Kibongo.
Sasa tuambie kwa mtazamo wako, kwa jinsi ujuavyo kazi za wakali hawa, ni nani zaidi kati yao? Piga kura yako sasa, ili umwezeshe staa wako aibuke kidedea! Pamoja saaaaana wakubwaaaaaa!!!!
Bendi ya Diamond Musica ‘Moto mara tatu’, usiku wa kuamkia jana ilimtambulisha rasmi kwa mashabiki wake mwanamuziki maarufu, Mulezili Boyange a.k.a Mulemule FBI.
Uzinduzi huo uliofanyika ndani ya Ukumbi wa Vatican City Sinza, jijini Dar, umati mkubwa wa mashabiki ulifurika na kuleta matumaini ya kuwa ujio wa FBI unaweza kuinyanyua bendi hiyo na kuwa tishio.
Kabla ya Mulemele kutambulishwa, vimwana wa Diamond walipanda jukwaani kuonesha ‘mavituz’.
Mulemule FBI akipewa maua na mmoja wa mashabiki baada ya kutambulishwa kuongoza Jahazi la bendi hiyo mbele ya mashabiki.
Shabiki huyu mwenye chupa ya bia mkononi alikuwa bonge la kituko ukumbini, cheki alivyolowesha suruali.
Umati wa mashabiki ukiserebuka ukumbini katika uzinduzi huo.
Marehemu Mzee Rashid Mfaume Kawawa enzi za uhai wake.
Rais Jakaya Kikwete akiwa kwenye hitma ya marehemu Mzee Rashid Mfaume Kawawa jana jijini Dar. Wengine ni Mtoto wa marehemu Kawawa (kulia) na kushoto ni Sheikh wa Mkoa wa Dar es salaam Sheikh Mussa Salum.
Baadhi ya viongozi mbalimbali waliohudhuria Arobaini ya Simba wa Vita Marehemu Mzee Rashid Mfaume Kawawa iliyofanyika jana jijini Dar es salaam.
Vijana wawili waliokamatwa na polisi wakifanya mapenzi na mbuzi katika mji wa Mbucuta uliopo katikati ya nchi ya Msumbiji, wamelazimishwa kufunga ndoa ya kimila na mbuzi huyo. Tukio hilo la aina yake limetokea baada ya vijana wawili ambao majina na umri wao haukufahamika mara moja kukamatwa wakimuingilia mbuzi kwa zamu...
Usiku wa kuamkia leo, Kamera yetu ilikuwa mtaani kama kawaida, ambapo mapaparazi wetu walijichanganya viwanja mbalimbali vya burudani kama Mtoni, Buguruni, Vatican Sinza, Mango Garden na Meridian Kinondoni. Matukio yaliyonaswa na kamera zetu ni kama ifuatavyo:
Ya kale dhahabu Wanamuziki wa bendi ya Vijana Jazz ‘Wanapambamoto’ wakiserebuka katika onesho la bendi hiyo lililofanyika usiku wa kuamkia leo katika ukumbi wa Kimboka Bar Buguruni.
Hapa kazi tu Wanenguaji wa bendi ya Akudo Impact wakionesha umahiri wao wa kunengua, katika onesho la bendi hiyo lililofanyika usiku wa kuamkia leo katika ukumbi wa Mango Garden, Kinondoni.
Kaka unauchapa usingizi abiria wanakupita Dereva Tax anayepaki katika kituo cha Mango Garden akiwa ameutwanga usingizi majira ya saa nane usiku, huku mwenzie akiwa amejikunyata akisubiri abiria. Mwanamke kujiweka Sop Sop Mnenguaji wa bendi ya Diamond Musica, Hawa Nassoro akijipodoa kabla ya kwenda kwenye uzinduzi wa bendi hiyo uliofanyika usiku wa kuamkia leo katika ukumbi wa Vatican Sinza jijini Jamani mambo ya Pwani hayooo!
Mwimbaji mahiri wa bendi ya taarabu ya Five Star, Jokha Kassim akiimba wimbo wa Babu Umefulia katika onesho la bendi hiyo lililofanyika katika ukumbi wa Equator uliopo Mtoni jijini Dar es Salaam.
*MREMA NAYE ATANGAZA RASMI KUMPIGIA KAMPENI KIKWETE 2010 MBUNGE wa Moshi Mjini (Chadema), Philemon Ndesamburo ameponda maelekezo ya Rais Jakaya Kikwete kwa wanasiasa kuhusu rushwa kwenye chaguzi akieleza kuwa msimamo wake huo hautekelezeki kwa kuwa CCM bila rushwa, haiwezi kushinda...
• Mufti aunda kamati kuwahamasisha nchi nzima VIJANA wa Kiislamu nchini wamehamasishwa kuchukua fomu za kugombea nafasi mbalimbali za uongozi nchini katika kipindi hiki cha kuelekea uchaguzi mkuu...
Na Mwandishi Wetu Madhara ya matumizi ya dawa za Kichina zinazotumika kuongeza na kupunguza maumbile ya viungo vya binadamu, yanazidi kuchukua nafasi mithili ya moto wa kifuu hapa Bongo, mbaya zaidi pale dozi yake inapokosewa na mtumiaji, Risasi Jumamosi linakupa kitu kamili...
Na Mwandishi Wetu Muimbaji wa muziki wa Injili Nchini anayetesa na albamu yake ya Ushindi, Kabula George amefanikiwa kuuteka Mkoa wa Mbeya kutokana na wakazi wa huko kuguswa ile mbaya na ujumbe wa nyimbo zake zilizojaa ishara na miujiza...