arrowSet HomePage |arrowBookMark Us
right
lines

Global Publishers Tanzania- Uwazi » Articles for 04.02.2010

Tafuta  

Tembelea...

Kalenda

Gazeti la Ijumaa

Marafiki wetu

Habari Zilizopita

Soma Magazeti Yetu...

Gazeti la Risasi Mchanganyiko
Amani
Gazeti la Ijumaa Wikienda

Bongo Celebrities ...

 
Habari Zinazotamba Habari Mchanganyiko
» JE, UNGEPENDA KUPATA RAFIKI ...
» JIDE HOI
» MSHANGAO!
» Rais Kabila aomba wakafungw ...
» HUKUMU YA BABU SEYA!
» Waraka wa Papii watua kwa J ...
» Aunt Ezekiel alivyopigika k ...
» Chinjachinja ya Simba l ...
» Ungekuwa wewe, ungefany ...
» Washauriwa kutokimbilia ...
» Wakware wamezea mate ma ...
» WANAJESHI WAFUMANIANA
» Wanaigeria wa Miembeni ...
» Tusiyape nafasi mapenzi ...

 

KAGERA SUGAR YAWAGEUKIA YANGA

champion ijumaa  
Na Phillip Nkini, Bukoba
BAADA ya kuwa timu ya kwanza ‘kuifungisha breki ya pointi tatu’, Simba Sports Club, Kagera Sugar imejigamba kuwa timu zinazokutana nayo wakiwamo mabingwa watetezi Dar Young African wakae chonjo...
    (4 February 2010)
Views: 71 | Maoni (0) | Soma Zaidi

 

PHIRI: PIGA UA, SIMBA BINGWA

champion ijumaa  

PHIRI: PIGA UA, SIMBA BINGWA

Na Phillip Nkini, Bukoba
KOCHA Mkuu wa Simba Patrick Phiri amesema, ingawa wachezaji wake walilewa sifa alijua kuwa siku moja rekodi lazima itavunjwa, lakini amesisitiza nafasi waliyonayo, lazima watwae mabingwa wa Tanzania Bara msimu huu...
    (4 February 2010)
Views: 103 | Maoni (0) | Soma Zaidi

 

MRWANDA AMRUDISHA MWAIKIMBA VIETNAM

champion ijumaa  
Na Jozaka Bukuku
MSHAMBULIAJI wa Prisons ya Mbeya, Gaudence Mwaikimba amesema atarejea tena Vietnam kufanya majaribio ya kucheza soka la kulipwa licha ya kuishia Uwanja wa Ndege nchini humo hivi karibuni baada ya kuisha kwa muda wake wa kufanya hivyo...
    (4 February 2010)
Views: 72 | Maoni (0) | Soma Zaidi

 

KOCHA WA WANAJESHI AITAKA NAFASI YA MAXIMO

champion ijumaa  
Na John Joseph
KOCHA Mkuu wa JKT Ruvu inayomilikiwa na Jeshi la Kujenga Taifa, Charles Kilinda amesema licha ya kuwa bado Tanzania inahitaji changamoto ya kocha wa kigeni, anasubiri kutajwa kwa vigezo vya atakayeajiriwa kukikoa kikosi cha Taifa Stars ili aweze kujitosa katika nafasi hiyo ikiwa atakidhi vigezo...
    (4 February 2010)
Views: 22 | Maoni (0) | Soma Zaidi

 

SIMU YA KIGANJANI SI KICHAKA CHA UFUSKA

Mahaba  

SIMU YA KIGANJANI SI KICHAKA CHA UFUSKA

KAMA ilivyo ada tumekutana kwenye kona yetu ya mahaba kutaka kujuzana mawili matatu kuhusiana na mambo ya kila siku katika maisha yetu ya mapenzi...
    (4 February 2010)
Views: 113 | Maoni (0) | Soma Zaidi

 

My Black Chapter -29

hadithi za Shigongo  
Mtoto anazaliwa na jinsia mbili, anakua na kuwa msichana mrembo kupita kiasi lakini ana siri kubwa moyoni mwake. Huyu ni Maryjose ambaye baadaye anakuwa mpenzi wa David, mwanafunzi mwenzake. Hakukuwa na tendo la ndoa kati yao ingawa David alitaka litokee, hali hii ilimfanya awe na uhusiano wa siri na rafiki yake Maryjose aitwaye Alice.

Baadaye wazazi wa Maryjose wanapata ajali mbaya ya gari na kufariki, anaachiwa urithi wote ambao kwa mapenzi aliyonayo kwa David anautumia kumtibisha ugonjwa wa Saratani ya uboho wa mfupa aliotakiwa kutibiwa nchini Uingereza kwa kubadilisha Uboho na kuwekewa mwingine.

Waliporejea nchini kutoka Uingereza, Maryjose alikuwa ameishiwa kabisa, hivyo kujikuta akiishi nyumbani kwao na David maeneo ya Mbagala jijini Dar es Salaam, haukupita muda mrefu sana akaugundua usaliti ambao David alikuwa anafanya na kukiri mwenyewe kuwa asingeweza kumuoa Maryjose sababu hakuwa msomi.

Kauli hii inamuumiza sana Maryjose, hasa alipofikiria ujinga alioufanya kwa sababu ya David! Anafikia uamuzi wa kumuua lakini akashindwa kutekeleza kitendo hicho na kutoroka nyumbani kwao, kwa muda mrefu akajificha katika Utawa na David na Alice wakaendeleza uhusiano wao wakiamini alishakufa!

Siku ya ndoa yao wanapanda ndani ya gari la bwana na bibi harusi na linalipuliwa kwa petroli, upelelezi ulipofanyika ulionyesha aliyelipua ni Maryjose na msako ukaanza kumtafuta bila mafanikio. Alice akafariki na David kupatwa na upofu, hata hivyo akaendelea na kazi za baba yake Alice kwenye kampuni yake ya Uwakili.

Maryjose anarejea nchini kutoka India akiitwa Sista Theresa na kukabidhiwa kituo cha watawa wa shirika la Mt. Francisca, watawa wasiotoka nje, kazi yao ikiwa ni kusali tu! Anajishughulisha sana na kazi ya kutoa misaada kwa jamii, hakuna anayemkumbuka lakini siku moja David na wafanyakazi wake walipokwenda kwenye ofisi yake kutoa msaada wa shilingi bilioni mbili zimsaidie, David aligundua kuwa sauti ya Sista Theresa ni ya Maryjose lakini sista alikana.

David bado anaendelea kufuatilia ukweli wa jambo hilo, tayari amekwishachukua mwandiko wa sista Theresa na kwenda kuulinganisha na barua za mtu aliyekuwa akimtumia kumwomba msamaha. Watu walioutazama mwandiko walimhakikishia kwamba ni wa mtu mmoja, akawa na uhakika kabisa sista Theresa ni Maryjose, neno pekee alilosema ni; NITAMPATA TU.
Je, nini kitaendelea? SONGA NAYO…
    (4 February 2010)
Views: 540 | Maoni (2) | Soma Zaidi

 

WAZAZI WAMFUNGIA MTOTO WAO KABATINI KWA MWAKA MZIMA

Habari mbalimbali  

WAZAZI WAMFUNGIA MTOTO WAO KABATINI KWA MWAKA MZIMA
Alfredo (kushoto) na Leticia Ines, wazazi wa mtoto huyo.

WAZAZI WAMFUNGIA MTOTO WAO KABATINI KWA MWAKA MZIMA
Hili ndilo kabati alimokuwa anaishi binti huyo.

WAZAZI wawili, Alfredo Ines na Leticia Ines wameshitakiwa kwa tuhuma za kumfungia mtoto wao kabatini kwa takribani mwaka mmoja....
    (4 February 2010)
Views: 778 | Maoni (1) | Soma Zaidi

 

THE COMMEDY ENTERTEINMENT

Videos  

Sit bak, rilakx! Ze Komedi in akshen laaiv!, injoi ze shoo
    (4 February 2010)
Views: 37 | Maoni (1) |

 

MPENDA WANYAMA AUAWA NA MBWA WAKE

Habari mbalimbali  

MPENDA WANYAMA AUAWA NA MBWA WAKE
Mmoja wa mbwa waliomshambulia “bwana” wao wakati akiwa katika bustani yake.

DAKTARI mmoja ambaye alishinda mapambano ya kisheria ya miaka minne ya kuwaokoa mbwa wake watatu wasikamatwe na kwenda kufungiwa mahali ambapo wasingeweza kutembea ovyo na kuwadhuru watu, ameuawa na mbwa haohao...
    (4 February 2010)
Views: 301 | Maoni (0) | Soma Zaidi

 

Muro aongeza utata

Habari mbalimbali  
Muro aongeza utata

Muro aongeza utata
HII NDIYO RISITI YA PINGU ANAZOMILIKI JERRY MURO

• Awasilisha risiti za pingu alizokamatwa nazo

SAKATA la mwandishi wa habari za uchunguzi, Jerry Muro, limeingia katika hatua mpya baada ya kubainika kuwa ana risiti za pingu ambazo polisi walimkamata nazo...
    (4 February 2010)
Views: 2199 | Maoni (23) | Soma Zaidi

 

SAKATA LA JERRY MURO NA CCJ NI MCHEZO WA MAFISADI KUONDOA UMMA KWENYE AGENDA ZA KITAIFA?

Habari mbalimbali  
Nashukuru kwa michango ya wote kuhusu sakata la mwanahabari Jerry Muro na CCJ. Lakini kama sisi kama sehemu ya umma na kama sehemu ya wachangiaji wa masuala yanayohusu hatma ya nchi yetu na raia wake tunahitaji kwenda mbele zaidi na kufanya uchambuzi (kihabari tunaita News Analysis) ili kupata picha pana zaidi itakayotusaidia sisi na jamii nzima.

Katika uchambuzi kunaweza kuwepo maswali mengi. Mfuatiliaji wa masuala ya kitaifa
    (4 February 2010)
Views: 383 | Maoni (7) | Soma Zaidi

 

Maajabu ya Mungu ajali ya Tanga, mtoto wa miaka miwili atoka mzima

Habari mbalimbali  
Maajabu ya Mungu ajali ya Tanga, mtoto wa miaka miwili atoka mzima
Mtoto wa miaka miwili aliyenusurika katika ajali iliyotokea juzi na kuuwa watu 24 papohapo huku wengine 35 wakijeruhiwa

KATIKA kile kinachothibitisha maajabu ya Mungu, mtoto wa miaka miwili ametoka salama katika ajali iliyotokea juzi mkoani Tanga wakati mama yake mzazi anadaiwa kufariki dunia katika ajali hiyo....
    (4 February 2010)
Views: 326 | Maoni (0) | Soma Zaidi

 

KUELEKEA UCHAGUZI MKUU WA OKTOBA: Kikwete aanza kusafisha njia

Habari mbalimbali  
KUELEKEA UCHAGUZI MKUU WA OKTOBA: Kikwete aanza kusafisha njia
MWENYEKITI wa CCM Rais Jakaya Kikwete, leo anaanza ziara ndefu ya kutembelea na kuimarisha chama hicho kuanzia ngazi ya shina mkoani Dar es Salaam...
    (4 February 2010)
Views: 105 | Maoni (1) | Soma Zaidi

 

MAREHEMU IMRAN KULETWA LEO

photos  
Marehemu Imran Mtui, mtanzania aliyeuawa nchini India mapema wiki hii, anatarjiwa kurejeshwa nyumbani leo mida ya alasiri kwa ndege ya Shirika la Emirates. Marehemu, ambaye alikuwa masomoni nchini humo, mara baada ya kuwasili uwanja wa ndege, anatarajiwa kusafirishwa kwenda Marangu, Moshi kwa ajili ya maziko. Uchunguzi wa kifo chake bado unaendelea.
MAREHEMU IMRAN KULETWA LEO
Marehemu Imran Mtui

MAREHEMU IMRAN KULETWA LEO
Watanzania mbalimbali kutoka sehemu mbalimbali za india walifunga safari na kujumuika na watanzania wenzao katika kuomboleza msiba wa mtanzania mwenzao.
PICHA KWA HISANI YA HAKI NGOWI
    (4 February 2010)
Views: 96 | Maoni (0) |

 

RAIS WA NIGERIA ATAKIWA KUN'GOKA

Habari mbalimbali  

RAIS WA NIGERIA ATAKIWA KUN'GOKA
Rais wa Nigeria anayeugua, Umaru Yar'Adua

Kundi la wakuu wa vyombo vya habari limeonya kuwa Rais wa Nigeria anayeugua, Umaru Yar'Adua lazima akabidhi madaraka kwa makamu wake katika kipindi cha siku saba au ajiuzulu.

Wamiliki wa magazeti 17 na mashirika ya vyombo vya habari wamesema katika ujumbe wa pamoja kuwa Bw Yar'Adua lazima ashitakiwe kwa kutumia madaraka vibaya kama atashindwa kutekeleza matakwa yao.

Rais huyo anayeugua amekuwa katika hospitali moja ya Saudi Arabia tangu mwezi Novemba mwaka jana.
Kumekuwa na kesi kadhaa za kisheria zikihoji uwezo wa Rais kuongoza nchi akiwa amelazwa.

Katika kesi ya mwisho, mahakama kuu ilisema hakukuwa na kipengele chochote cha kikatiba kwa kiongozi yeyote wa mpito kuteuliwa.
    (4 February 2010)
Views: 21 | Maoni (0) |
Back  <<  1 2  >>  Next Page
 

Kura Yako / Poll

Habari Katika Picha


Author: admin


Gazeti la Uwazi


Nani Yupo / Alikuwepo


Home Page | About Us | Regista | Picha | Bongo Celebrities | Maoni | Contact Us

 hit counter

counters

2008 © globalpublisherstz.com